Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. TIMOTH G. ANYOSISYE aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga kingo za zege za Mto Mbezi ili kuzuia kusombwa kwa nyumba na kusababisha maafa?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, hivi karibuni katika Mto Kikafu, lile daraja, kumekuwa kukitokea ajali nyingi na kusababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji wa Barabara ya Moshi – Arusha, lakini barabara pekee ambayo ni ya mchepuko na ya mbadala ni Bomang’ombe - Chekimaji TPC, ambayo inajengwa kilometa 3.5. Je, ni lini sasa Serikali italeta fedha ya kumaliza barabara hii ili iweze kujengwa kwa kiwango cha lami na taa juu? Ahsante.

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO): Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Barabara ya Bomang’ombe - Chekimaji TPC. Kama ambavyo imeanishwa kwenye mipango yetu, Serikali itatenga fedha, kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii, kilometa 3.5, kwa kiwango cha lami mara tu baada ya fedha hizi kupatikana.