Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Hija Hassan Hija
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kiwani
Primary Question
MHE. HIJA HASSAN HIJA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka vifaa tiba vya kutosha, hususan vifaa vya kujifungulia, katika hospitali zote nchini?
Supplementary Question 1
MHE. HIJA HASSAN HIJA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninaomba nimuulize swali moja la nyongeza. Mwezi Novemba, Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara kwenye hospitali moja hapa Mjini Dodoma na wananchi, hususan wazazi, waliipongeza Serikali kwa huduma nzuri za matibabu na dawa, lakini walilalamikia ukosefu wa mabeseni na ndoo, kwa ajili ya wajawazito; Mheshimiwa Waziri Mkuu akaagiza jambo hili litatuliwe. Ninaomba kujua limefikia hatua gani?
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. RAJAB S. JAFAR): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hija Hassan Hija. Tunakumbuka ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwenye kituo chetu, kile cha afya na akatoa maelekezo yale.
Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ndiyo maelekezo ya Serikali. Nami kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninawaelekeza Waganga Wakuu wote wa Mikoa, Waganga wote, ma-DMO wa Halmashauri na ma-MOI wetu waendelee kutekeleza majukumu hayo, waendelee kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa maana kwamba, sasa mambo ya kuwatoza hivyo vifaa kama mabeseni na ndoo visiwe vikwazo kwa mama zetu wanapokwenda kujifungua katika hospitali zetu
Name
Kiza Hussein Mayeye
Sex
Female
Party
CUF
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HIJA HASSAN HIJA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka vifaa tiba vya kutosha, hususan vifaa vya kujifungulia, katika hospitali zote nchini?
Supplementary Question 2
MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Spika, nimemsikiliza Mheshimiwa Waziri na amesema, Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo, lakini maelekezo haya mpaka tunavyozungumza huko kwenye vijiji wajawazito bado wanapeleka mabeseni wembe na mipira. Ninataka majibu ya Mheshimiwa Waziri kuanzia sasa, ni lini hii hali itakoma kwa wajawazito kwa sababu, Kigoma Kaskazini na maeneo mengine bado akinamama wanapeleka mabeseni na vifaa vingine? Ahsante.
Name
Dr. Jafar Rajab Seif
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busanda
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. RAJAB S. JAFAR): Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ni maelekezo ya Serikali. Ninarudia kwa kwamba, halmashauri zote nchini tunatoa wito kwa Wakurugenzi, Waganga Wakuu na ma-DMO watekeleze maagizo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa maana maagizo hayo ndiyo maagizo ya Serikali.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved