Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hija Hassan Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwani

Primary Question

MHE. HIJA HASSAN HIJA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka vifaa tiba vya kutosha, hususan vifaa vya kujifungulia, katika hospitali zote nchini?

Supplementary Question 1

MHE. HIJA HASSAN HIJA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ninaomba nimuulize swali moja la nyongeza. Mwezi Novemba, Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara kwenye hospitali moja hapa Mjini Dodoma na wananchi, hususan wazazi, waliipongeza Serikali kwa huduma nzuri za matibabu na dawa, lakini walilalamikia ukosefu wa mabeseni na ndoo, kwa ajili ya wajawazito; Mheshimiwa Waziri Mkuu akaagiza jambo hili litatuliwe. Ninaomba kujua limefikia hatua gani?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. RAJAB S. JAFAR): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hija Hassan Hija. Tunakumbuka ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwenye kituo chetu, kile cha afya na akatoa maelekezo yale.

Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ndiyo maelekezo ya Serikali. Nami kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninawaelekeza Waganga Wakuu wote wa Mikoa, Waganga wote, ma-DMO wa Halmashauri na ma-MOI wetu waendelee kutekeleza majukumu hayo, waendelee kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa maana kwamba, sasa mambo ya kuwatoza hivyo vifaa kama mabeseni na ndoo visiwe vikwazo kwa mama zetu wanapokwenda kujifungua katika hospitali zetu

Name

Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HIJA HASSAN HIJA aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka vifaa tiba vya kutosha, hususan vifaa vya kujifungulia, katika hospitali zote nchini?

Supplementary Question 2

MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Spika, nimemsikiliza Mheshimiwa Waziri na amesema, Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo, lakini maelekezo haya mpaka tunavyozungumza huko kwenye vijiji wajawazito bado wanapeleka mabeseni wembe na mipira. Ninataka majibu ya Mheshimiwa Waziri kuanzia sasa, ni lini hii hali itakoma kwa wajawazito kwa sababu, Kigoma Kaskazini na maeneo mengine bado akinamama wanapeleka mabeseni na vifaa vingine? Ahsante.

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. RAJAB S. JAFAR): Mheshimiwa Spika, maelekezo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ni maelekezo ya Serikali. Ninarudia kwa kwamba, halmashauri zote nchini tunatoa wito kwa Wakurugenzi, Waganga Wakuu na ma-DMO watekeleze maagizo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa maana maagizo hayo ndiyo maagizo ya Serikali.