Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Kija Limbu Ntemi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katoro
Primary Question
MHE. ENG. KIJA L. NTEMI aliuliza:- Je, ni nani anayesimamia mikataba ya wenye leseni na wachimbaji wadogo wa madini wanaovumbua madini na mikataba hiyo ni ya muda gani?
Supplementary Question 1
MHE. ENG. KIJA L. NTEMI: Mheshimiwa Spika, ninamshukuru kwa majibu ya Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; ninapenda kufahamu huu mkataba utaanza lini, kwa sababu watu wameshaumizwa na wameshafungiwa mikataba ambayo inaonesha ni mkataba wa miezi minne, hauna malipo, lakini watu wamelipa fedha nyingi kwa ajili ya hii mikataba. Unafungiwa mkataba wa miezi minne kila duara moja inalipa shilingi milioni kumi kumi, zaidi ya maduara 100 watu wamelipa fedha.
Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, hawa watu waliolipishwa hizi fedha ndani ya miezi minne na miezi mitatu kuna uwezekano wa kurudishiwa fedha zao ili huu utaratibu utakapoenda kuanza, hawa watu wawe wamesharudishiwa fedha zao na utaratibu ufuatwe vizuri kwa sababu wameonewa na zile fedha wamelipa pasipo na utaratibu na hazina mfumo wowote.
SPIKA: Mheshimiwa maswali yako ni mawili tu.
MHE. ENG. KIJA L. NTEMI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Name
Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Longido
Answer
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la kwanza Engineer Kija, ninapenda kukujulisha kwamba kanuni hizi zilipotungwa au zilipofanyiwa marekebisho mwaka jana tukaweka kipengele kinachohakikisha kwamba hakuna mwenye leseni anayempangisha mchimbaji mdogo eneo bila kusainiana mkataba. Kwa hiyo, kwa sababu sheria haina tabia ya kurudi nyuma, siyo retrospective, kuanzia kanuni hii iliporekebishwa wote wanaoingia katika makubaliano mwenye leseni na anayetaka kupanga eneo lazima wa-comply.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, kiwango wanachowekeana ni maridhiano yao na sisi kama Wizara wakishasajili mkataba tunausimamia, yale yaliyopita wahenga wanasema si ndwele tugange yaliyopo na yajayo.
Mheshimiwa Spika, ninaomba kuwasilisha.
Name
Chacha Mwita Wambura
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Geita Mjini
Primary Question
MHE. ENG. KIJA L. NTEMI aliuliza:- Je, ni nani anayesimamia mikataba ya wenye leseni na wachimbaji wadogo wa madini wanaovumbua madini na mikataba hiyo ni ya muda gani?
Supplementary Question 2
MHE. CHACHA M. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kukushukuru kwa kunipa nafasi hii kwa ajili ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Nianze kwa kuipongeza Wizara ya Madini, ndugu yangu Mavunde kwa kazi kubwa ambayo anaifanya, lakini pamoja na hayo ninaomba kuuliza swali moja.
Mheshimiwa Spika, tunajua kabisa kwamba suala zima la double taxation limekuwa halikubaliki lakini kwenye Wizara hii ya Madini suala zima la mrabaha tumeona double taxation mara kadhaa ikifanyika. Kuna baadhi ya mikoa ambapo tuna-charge mara mbili. Mara moja tuna-charge wakati mchimbaji anavyokuwa anagawa mawe pia wakati mwingine mchimbaji huyu aki-process akipata dhahabu akifika kule sokoni tena anatozwa mrabaha. Je, Wizara imejipanga vipi au ina mpango gani kuhakikisha kwamba suala zima hili la double taxation tunaliondoa na huyu mchimbaji aende kulipa kodi moja kwa mara moja? (Makofi)
Name
Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Longido
Answer
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, ninapenda kulijulisha Bunge lako Tukufu kwamba kodi zilizoidhinishwa rasmi na Wizara ni kodi ya mrabaha, kodi ya ukaguzi wa leseni na ile ya service levy inayokwenda kwenye halmashauri. Hizi tozo anazoongelea Mheshimiwa ni tozo ambazo watu wanapotoa madini mgodini na wakati huo ni mawe tu, anayetoa mawe mgodini, anapoyapandisha pale siyo yeye anayepeleka sehemu ya kuchakata yale madini.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hakuna namna sisi tunaweza tukasubiri yaende mpaka kule mwisho wa eneo itakapotumika kuweza kuchaji. Kwa hiyo, anatozwa kwa asilimia ya mawe aliyogawa pale baada ya kutoa na yule anayekwenda kuchakata anawekewa kiwango ambacho kinalingana na zile tozo za Serikali.
Mheshimiwa Spika, tuko katika mpango wa kuhakikisha kwamba katika migodi yote uchenjuaji ufanyike palepale ili mawe yotozwe kodi ya Serikali baada ya kuwa yameshachakatwa.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved