Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fadhili Sandali Chilombe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Kazamoyo, Imani na Kilimani katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina swali moja lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika siku za hivi karibuni pamekuwa na ongezeko kubwa sana la watumiaji wako wa simu kwenye baadhi ya maeneo ndani ya Jimbo la Tunduru Kusini, hali hiyo imesababisha baadhi ya minara kuzidiwa na ubora wa mawasiliano kutoka kwenye minara hiyo kupungua.

(a) Je, Serikali haioni haja ya kwenda kufanya review, kwa maana ya mapitio kwenye baadhi ya minara ili kuangalia uwezekano wa ama kuongeza masafa au kujenga minara mingine karibu na maeneo hayo?

(b) Je, kama inakubaliana na mimi, kazi hiyo itaanza lini?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mhandisi Fadhili, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kufanya tathmini upya ni kweli baadhi ya minara kutokana na kuongezeka kwa watumiaji inakuwa inazidiwa. Kwa hiyo, nichukue fursa hii kupitia Bunge lako Tukufu kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, kumwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa TCRA kutuma wataalam katika maeneo ya Jimbo la Tunduru Kusini ili wafanye tathmini na kubaini changamoto hiyo haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Name

Cornel Lucas Magembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato Kaskazini

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Kazamoyo, Imani na Kilimani katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 2

MHE. CORNEL L. MAGEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nina swali moja la nyongeza. Kuna vijiji takribani vitano katika Jimbo la Chato Kaskazini, ambavyo ni Vijiji vya Mkungo, Nyakato, Buzirayombo, Itale na sehemu kubwa ya Ilyamchele. Vijiji hivi havipati mawasiliano kwa sababu hakuna mtandao na hii husababisha utoaji wa elimu hasa kwenye shule za msingi na Sekondari ambako sasa wanatumia TEHAMA wanafunzi wanashindwa kupata haki yao kama wanafunzi wengine. Je, Wizara ina mpango gani wa kwenda kuweka mtandao katika maeneo hayo? Ahsante sana.

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la ndugu Mheshimiwa Magembe, Mbunge wa Chato Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza katika jibu la swali la msingi, tunatambua changamoto ya mawasiliano nchi nzima na ninaamini kila Mbunge aliyemo katika jengo hili ana changamoto ya mawasiliano katika Jimbo lake kwenye sehemu moja au nyingine. Ndiyo maana sisi kama Wizara tunaandaa mkakati wa miaka mitano wa kuyafikia maeneo yote yenye changamo ya mawasiliano na tunaamini katika kipindi hiki cha miaka mitano, tutafika kila eneo kule ambako hakuna minara, tutajenga minara mipya, kule ambako minara imezidiwa, tutaiongezea nguvu ili kuhakikisha kwamba ifikapo mwaka 2030 changamoto ya mawasiliano katika Majimbo mbalimbali na hapa nchini iwe imepungua kwa kiasi kikubwa au tumeimaliza kabisa. (Makofi)

Name

Dr. Yahaya Esmail Nawanda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Kazamoyo, Imani na Kilimani katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. YAHYA E. NAWANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga minara katika Kata za Mtunguru, Mkwedu, Chilangala pamoja na Mikumbi? Ahsante. (Makofi)

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Nawanda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi Wizara inatekeleza Mradi wa Ujenzi wa Minara 280 katika bajeti hii na katika bajeti ijayo tutatekeleza tena mradi wa kujenga minara mingine 280 ambayo katika mradi huo Kata alizozitaja Mheshimiwa Mbunge nazo tutazipatia kipaumbele. (Makofi)

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Kazamoyo, Imani na Kilimani katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 4

MHE. HAIDERALI H. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Kata ya Mughunga, Ilongero Singida Vijijini? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Singida Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza kwenye jibu langu la swali la msingi, kwamba tumeandaa mkakati mahsusi wa miaka mitano wa kujenga minara mbalimbali nchini katika maeneo yote yenye changamoto ya mawasiliano. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mkakati huo na eneo lake hilo lenye changamoto pia tutalifikia.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Kazamoyo, Imani na Kilimani katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 5

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa na mimi nafasi ya swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itajenga minara ya mawasiliano katika Kata za Kitwai na Naberera Wilayani Simanjiro?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye mkakati wetu wa miaka mitano wa kuhakikisha kwamba nchi hii yote inapata mawasiliano, tutajenga minara, kama nilivyosema, katika maeneo mbalimbali ili kuyafikia maeneo yote yenye changamoto. Yale ambayo yana minara, lakini hayana mawasiliano ya kutosha au yana changamoto tutaiongezea nguvu. Kwenye eneo lake hili la Simanjiro ambalo hakuna minara ndani ya hiki kipindi cha miaka mitano tuna uhakika tutakuwa tumefika na tumejenga minara kwa ajili ya kuondoa changamoto hiyo.

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Kazamoyo, Imani na Kilimani katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 6

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuna baadhi ya maeneo, hasa katika Jimbo la Nanyumbu, minara ipo lakini wananchi wanahitaji huduma zaidi ya ule mnara wa mawasiliano. Je, Serikali haiko tayari kuwashauri wawekezaji wengine wakatumia ule mnara mmoja ili kurahisisha upatikanaji wa mawasiliano wa maeneo yote?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari kampuni za simu zinachangia baadhi ya minara katika baadhi ya maeneo; mnara mmoja kampuni mbili ama matatu zinaweka vifaa vyao vya mawasiliano. Kwa hiyo nichukue nafasi hii pia kumwelekeza Mkurugenzi Mkuu wa TCRA kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kulifanyia kazi suala hili ili hiyo minara kama ina changamoto au imezidiwa, basi waangalie uwezekano wa kuwasiliana na kampuni ili waongezewe nguvu. Kama kuna uwezekano mwingine pia basi kampuni ziruhusiwe kuwekeza zaidi kwenye mnara huo ili kampuni mbili ama tatu yaweze kutoa huduma kwa kutumia mnara mmoja. Zoezi hilo litafanyika kwenye baadhi ya maeneo.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. ENG. FADHILI S. CHILOMBE aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga mnara wa mawasiliano katika Vijiji vya Kazamoyo, Imani na Kilimani katika Jimbo la Tunduru Kusini?

Supplementary Question 7

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Tarime Vijijini lipo mpakani mwa Kenya. Kwa hiyo Kata za Susuni, Mwema, Sirari, Nyanungu, Gwitiryo tunapata mawasiliano kutoka Kenya; lakini vilevile maeneo kama Mrito kwenye mgodi pale wa dhahabu, Gorong’a karibu na Hifadhi ya Serengeti hakuna mawasiliano kabisa. Nimeuliza swali hili miaka mitano imepita sasa ninaomba Serikali iniambie. Je, ni kwa nini wananchi wa maeneo hayo wanapata shida ya mawasiliano mpaka leo? Ahsante.

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru kwa kupata nafasi na nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Niombe kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Waitara. Tunatambua changamoto iliyopo uhafifu wa mawasiliano hasa katika maeneo ya mipakani ikiwemo Sirari, Tarime pamoja na maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine, kama Serikali tunaendelea kufanyia kazi kuhakikisha tunaongeza nguvu katika minara iliyopo katika maeneo ya mipakani; na sasa katika awamu yetu ya kumi na moja eneo hilo litakuwa la kipaumbele ikiwemo maeneo yanayopita SGR, lakini pia maeneo ya barabara kuu pamoja na maeneo ya mipakani kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto kubwa ambayo imekuwa ikitukabili unajikuta mkifanya adjustment katika maeneo ya minara katika maeneo ya mipakani baada ya muda nchi za wenzetu pia wamekuwa wakifanya adjustments. Kwa hiyo unajikuta unarekebisha hali leo baada ya muda unajikuta pia changamoto inaendelea kurudi pale pale na inakuwa inapelekea masuala ya roaming na kusoma minara mingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, tutaendelea kufanya ukaguzi na usimamizi zaidi mara kwa mara ili kuhakikisha kwamba kutakuwa na adjustment ili kuhakikisha wananchi wetu wanapata mitandao kutoka mawasiliano ya Tanzania pekee. Ninakushukuru.