Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amosy William Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Barabara ya Ipole – Rungwa na Sikonge – Kipili kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. AMOSY W. MAGANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nimshukuru Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja tu la nyongeza. Kwa vile Barabara ya kutoka Ipole – Rungwa imekuwa kwenye ahadi ya Serikali kwa kipindi kirefu sasa na barabara hii imekuwa ni sehemu ya Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Je, Serikali haioni umuhimu kwamba sasa fedha zipatikane na barabara hiyo ianze kutengenezwa na impendeze Mwenyezi Mungu hii barabara ikamilike hata kabla ya mwaka 2030?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, niungane na Mheshimiwa Mbunge kwamba hii barabara imeshafanyiwa usanifu na kwa sisi kama Serikali imekuwa ni moja ya barabara kubwa na Barabara Kuu (Trunk Road) ndefu ambayo haijajengwa kwa kiwango cha lami. Tunavyoongea sasa hivi, Serikali inatafuta chanzo sahihi kwa maana ya kuijenga hiyo barabara kuanzia Ipole – Rungwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, atakubaliana nami, lakini kutoka Rungwa – Singida ambako tumeshaanza na kutoka Rungwa – Makongorosi ili kuiunga Tabora, Singida na Mkoa wa Mbeya kwa kiwango cha lami. Mpango upo mkubwa wa kutafuta chanzo cha uhakika ili kuikamilisha barabara hiyo. Ahsante.