Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timida Mpoki Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TIMIDA M. FYANDOMO aliuliza: - Je, hatua gani zimechukuliwa kulinda biashara na mitaji ya vijana dhidi ya ucheleweshaji wa malipo ya madeni ya wakandarasi?

Supplementary Question 1

MHE. TIMIDA M. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Waziri katika nchi za Umoja wa Ulaya, taasisi zinazofanya kazi na Serikali zinapaswa kufanya malipo ya madeni ndani ya siku 30, lakini pia riba hulipwa moja kwa moja endapo malipo yatacheleweshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali yangu ipo tayari kuandaa Prompt Payment Policy ya Taifa ili kuhakikisha wazabuni, wakandarasi, wafanyabiashara hususan vijana na SMEs wanalipwa ndani ya muda maalum unaotambulika kisheria ili kulinda mitaji ya vijana na wananchi wanaofanya biashara na Serikali? Ahsante. (Makofi)

Name

Laurent Deogratius Luswetula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nipongeze sana Mbunge wa Viti Maalum dada yangu Timida ambaye ni Mbaraza la Vijana wa Taifa kutokea Mkoa wa Mbeya kwa namna anavyoendelea kujenga hoja makini hapa Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikirejea kwenye swali la nyongeza, kwanza kabisa miongoni mwa vitu ambavyo hata Kamati yetu ya Bajeti imeweza kutushauri kama Wizara ya Fedha na kama Serikali imetushauri tuweze kupunguza angalau muda wa uhakiki wa madeni ya wazabuni na wakandarasi na watoa huduma mpaka kufikia siku 21.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na sisi tumeweza kupokea, lakini siku hizi 21 zinaweza zikapungua au kuongezeka kutokana na sababu kadhaa ikiwemo ukamilifu wa nyaraka, aina ya madeni lakini pia ushirikiano wa wadau kwa maana wadai pamoja na wadaiwa, lakini pia umri wa deni pamoja na wigo wa deni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Serikali, kama ambavyo nimejibu kwenye swali langu la msingi, tumeendelea kulipa madeni ya wazabuni, wakandarasi pamoja na watoa huduma na mpaka kufikia Februari, 2026 zaidi ya shilingi bilioni 477.6 ambazo tayari wakandarasi hawa na watoa wa huduma wamekwishalipwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya vipaumbele vikubwa vya Serikali katika bajeti yetu ya mwaka 2026/2027, tumetenga na tumekubaliana kuwa na mkakati wa kutenga shilingi bilioni 100 kila mwezi kwa ajili ya kulipa madeni ya wakandarasi, watoa huduma pamoja na wazabuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.

Name

Morris Joseph Makoi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Mjini

Primary Question

MHE. TIMIDA M. FYANDOMO aliuliza: - Je, hatua gani zimechukuliwa kulinda biashara na mitaji ya vijana dhidi ya ucheleweshaji wa malipo ya madeni ya wakandarasi?

Supplementary Question 2

MHE. MORRIS J. MAKOI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wakandarasi wa nchi hii wanadai fedha nyingi kama ambavyo ametamka Mheshimiwa Waziri, lakini wakandarasi wa ndani hawaruhusiwi kudai malipo yao pamoja na riba, kinyume na wakandarasi wa nje ambao hudai malipo ya madeni yao pamoja na riba.

Je, Waziri ana kauli gani kuhusiana na madeni ya wakandarasi wazawa wanaodai madeni yao pamoja na riba ili na wao wanufaike au waepuke hasara kama ambavyo wenzao wa nje wanavyoepuka?

Name

Laurent Deogratius Luswetula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA (MHE. LAURENT D. LUSWETULA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nikiri kama Serikali tumeendelea kulipa madeni yakiwemo madeni ya wakandarasi wa kigeni na madeni ya wakandarasi ambao ni wazawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyotangulia kusema kwenye swali langu la msingi, kwanza hakuna upendeleo wowote baina ya wakandarasi wa nje na wakandarasi wa ndani, kama Serikali tumekuwa tukishamaliza kufanya uhakiki wa madeni hayo tumekuwa tukilipa kwa wakati na hivyo Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini nipende kukuhakikishia kwamba kama Serikali tumejipanga kuhakikisha kwamba madeni yote ya wazawa na wa kigeni yanalipwa kwa wakati.