MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itapeleka wataalamu na vifaa tiba kwa zahanati na vituo vya afya vilivyokamilika katika Jimbo la Hanang?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA, (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kupeleka vifaa tiba na madaktari katika hospitali zote nchini. Kwa hiyo, nimwelekeze Mkurugenzi wa Halmashauri ya Hanang, kuendelea kupeleka watumishi katika zahanati yetu hii na kuendelea kutoa huduma kwa mama zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.