Contributions by Hon. Dr. Wilson Charles Mahera (4 total)
Mpango Elekezi wa Maendeleo wa Muda Mrefu 2026/2027–2050/2051, Mapendekezo ya Mpango wa Nne wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2026/2027–2030/2031 na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2026/2027; na Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali Katika Muda wa Kati ya 2026/2027 hadi 2028/2029.
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa ili nami niweze kuchangia katika mpango huu. Kwanza kabisa nianze kumshukuru Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo kwa kazi nzuri na maandalizi mazuri ya hizi nyenzo kwa ajili ya kuenda kutekeleza Dira ya 2050. Nimshukuru pia Waziri wa Fedha naye kwa mipango mizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hapa, ninaanza kwa kuipongeza Serikali; tayari imekwishakuja na hizi nyenzo kama tatu kwa ajili ya utekelezaji wa Dira yetu ya 2050, ambapo Mpango Elekezi wa Muda Mrefu wa Maendeleo wa Miaka Ishirini wa Tano una dhima kwamba tunataka kuwa na Taifa ambalo lina uchumi jumuishi na Taifa linalojitegemea; ambapo kipato chake cha mtu mmoja mmoja kitakuwa dola 7,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili kuweza kuyafanya hayo inaonekana Wizara pamoja na Tume ya Mipango wamefanya kazi nzuri ya kufanya mapitio ya mipango ile mitatu iliyokuwepo kwa ajili ya Dira ya 2025 na wamebaini baadhi ya changamoto ambazo zilipelekea baadhi ya malengo kutokuweza kutimia. Moja ya hizo changamoto inaoneka ni kwamba kulikuwa na matumizi machache ya sayansi teknolojia na ubunifu, pia uzalishaji mdogo viwandani na kilimo pia kilichangia kwa kiasi kidogo; pia kulikuwa na tatizo la kutokuwepo na ajira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa vile tunataka kwenda kwenye Taifa ambalo linajitegemea kuna mambo mengi mazuri. Pia ilikuwa inaonekana kwamba kulikuwa na upungufu wa fedha katika kutekeleza baadhi ya mambo ambayo walikuwa wamepanga kuyafanya. Pamoja na hayo mafanikio yapo, lakini hatukufanikiwa kwa 100%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo mengi mazuri kabisa ambayo yako kwenye mipango na yameelekezwa. Changamoto inayokuja ni kwamba tunatakiwa tujitahidi sana kufanya kazi business as usual ili tutekeleze hayo ambayo tumeyaandika humu ili ndoto yetu iweze kutimia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kizuri ni kwamba pia wamekwenda kujifunza kwenye zile nchi ambazo ziko upper middle-income countries, nchi zenye uchumi wa kati hadhi ya juu na tayari wameona ni nini walichofanya mpaka wakafanikiwa. Kwa hiyo, kama Taifa ni lazima na sisi tuzingatie hizo core values ambazo tummeziona na pia ni lazima tuzingatie misingi waliyokuwa nayo na zile drivers.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kuna mengi tunakokwenda; moja ya mambo ambayo tunaya-aspire ni kwamba tunataka tuwe na Taifa la watu ambao ni educated na learned. Nitajikita tu kwenye suala la elimu, kwa sababu ili tuweze kufanikiwa kwa kweli ni lazima tuwekeze sana kwenye elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaipongeza Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwamba hata bajeti sasa itaongezeka, kutoka trilioni 7.31 hadi 8.19, lakini ninadhani bado inabidi kwa kweli tuongeze Bajeti ya Wizara ya Elimu. Hii ni kwa sababu mambo yote haya tunayokwenda kuyafanya wananchi lazima waelimishwe. Kuna ujuzi mbalimbali ambazo unatakiwa, hivyo ni lazima wananchi wasome waweze kuelimishwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapotaka kuwa na Taifa linalojitegemea tunaangalia; tangu mwaka 1974 wakati wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alielekeza; alikuwa na falsafa ya elimu ya kujitegemea ambapo hatukuweza kuwa nyenzo nzuri za kuweza kulitekeleza hilo hadi miaka ya 51 hapa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuja kuelekeza Wizara ya Elimu kupitia mitaala na ile mihtasari pamoja na maboresho ya sera na kuja na suala la elimu ya amali. Hii inaonekana itakuwa suluhisho katika kuchangia kuongeza pato la Taifa, lakini wananchi wa Tanzania kuweza kujiajiri wao wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo mengi Profesa Mhongo amesema asubuhi kuhusu namna watakavyokwenda kupata fedha. Ukiangalia kwenye suala la VETA; ametoa mfano wa kujifunza kwa Nchi za China na India. China kwa mfano wao kwa mwaka watu milioni 13 wanaingia kwenye shule hizi za vocations, na watu milioni 10 wana-graduate. Katika watu ambao sasa hivi wanakwenda kwenye kuchangia katika ajira kwenye viwanda na mijini wengi wao, zaidi ya 70% China wanatoka kwenye hizi vocations.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Tanzania kwa sasa ninachoweza kushauri kwamba kwenye Wizara ya Elimu hivi vyuo vya VETA ambavyo vipo kwa kweli awamu ya kwanza tumeshajenga bado kuna awamu ya pili; na ukitaka kuwa na elimu ya kujitegemea ni lazima ufanye practical zaidi. Kwa hiyo, tunatakiwa Tume ya Mipango kushirikiana na Wizara ya Elimu na Wizara ya Fedha tuwekeze fedha nyingi ili tuweze kukamilisha hivi vyuo. Vikamilike kwa hadhi ambayo inatakiwa pia tusomeshe watu wengi kwenye masuala haya ya vocations.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ikiwezekana pia; nimeona wakati wanafanya review kulikuwa na matumizi kidogo ya sayansi, teknolojia na ubunifu. Sasa tufanye kitu ambacho nadhani Tume ya Mipango iliwahi kusema ruleless prioritization. Ni lazima tuamue kwa makusudi kipaumbele kwamba, tuwekeze zaidi kwanza katika kuelimisha watu ili baadaye hawa watu ndiyo waje wachangie katika sekta nyingine hizo za nchi yetu ili kuweza kuleta mabadiliko. Kwa hiyo, ninashauri sana kwamba, tuwekeze huko. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia VETA hizi bado ni chache, tunatakiwa tuongeze idadi ya VETA, pia tuongeze programs nyingi na shule za sekondari za amali; tunamshukuru pia Mheshimiwa Rais; zimejengwa sasa hivi 103, lakini ninadhani bado zinahitajika; awamu ya kwanza ndiyo imekamilika. Ili tuwe na watu ambao watapata ujuzi unaohitajika ni lazima wafanye practical za kutosha. Kwa hiyo, tunaomba fedha ziongezwe tena Wizara ya Elimu ili kusudi awamu ya pili ya ujenzi wa hizo shule za amali uweze kuendelea. Karakana zikamilike ili kweli watu watakapotoka kwenye mfumo huo wa amali basi wawe na ujuzi mbalimbali ambao unahitajika. kwa hiyo, nilipenda nichangie hiyo kwenye sekta ya elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, twende zaidi tena mpaka kwenye vyuo. Tunamshukuru pia Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye mradi wake ule wa elimu ya juu kwa mageuzi, tuna kampasi kila mkoa. Tuzitumie zile campuses vizuri kwa ajili ya ujuzi mbalimbali katika particular areas huko zilipo hizo kampasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaona China kwa mfano wamejenga VETA kwa kushirikiana na Local Governments za huko. Kwa hiyo, hata hapa kwetu tuangalie, zile halmashauri ambazo zina uchumi mzuri basi Wizara ya Elimu au Tume ya Mipango iweze kushauri huko kwenye hizo halmashauri basi waanzishe hizo VETA kwa ajili ya kupata ujuzi unaohitajika kwenye hayo maeneo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija harakaharaka kwenye Sekta ya Afya kwa sababu tunataka tuwe na Taifa la watu ambao wana afya ya kutosha, ukiangalia kwenye Sekta ya Afya asilimia kubwa ya Watanzania wanatibiwa kwenye afya ngazi ya msingi. Kwa mfano 97% ya akinamama mwaka 2024 waliohudhuria kliniki walipata huduma katika vituo vilivyo chini ya Mamlaka ya Serikali za Mitaa (TAMISEMI). Vilevile, 93% waliojifungua Tanzania hapa walipata huduma hiyo kwenye vituo vya afya, lakini idadi kubwa ya akinamama zaidi ya 75% ya waliofanyiwa upasuaji kwa ajili ya kujifungua walifanya pia kwenye vituo vya afya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunakwenda kwenye suala la Bima ya Afya kwa Wote, lakini bado tuna-operate kwenye Sera ya Mwaka 2007. Ninadhani ile Sera nayo inabidi ifanyiwe mapitio kwa haraka kwa sababu kuna mabadiliko makubwa sana tangu ilipoanza mwaka 2007 mpaka sasa hivi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgawanyo wa fedha nao lazima uangalie. Hili suala lisiwe suala la Wizara moja, liwe ni suala la Kisekta. Ili tuweze kufanikiwa pia, ushauri wangu katika kutekeleza hii mipango ni lazima Wizara zikubali sasa kwamba tunakwenda kufanya kazi Kisekta zaidi badala ya kufanya kazi Kiwizara. Kwa sababu Wizara moja ikifanikiwa wakati Wizara nyingine hazijafanikiwa haina maana yoyote ile, lazima tushirikiane. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake ni kwamba, tukishirikiana hata mgawanyo wa fedha utakwenda kule ambako fedha zinahitajika kwa wakati muafaka. Kwa hiyo, hayo yalikuwa ni mawazo ambayo nilikuwa ninashauri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwa mfano fedha, labda ifikie mahali tuweke sheria au formula kabisa kwamba fedha lazima ziende kule ambako ndiko watu wanakozihitaji na wanakozitumia zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine walipofanya review ilionekana kwamba kulikuwa na poor linkage kati ya Vocational Education au Academic na industries. Sasa, tunashukuru Wizara ya Elimu tayari wamekuja na Mpango wa Industry Advisory Committee. Ninadhani hii tui-emulate kwenye maeneo yote ili tuweze kuhakikisha kwamba watu wetu wanakwenda huko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye viwanda tuweke pia mwongozo au kanuni ya kuwabana hawa watu ili wawe wanakubali internship, kwa sababu wakishaenda kule ndipo ambapo tayari ubunifu utafanyika na baadaye tunaweza kusoma kiteknolojia. (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa malizia.
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Ninaanza kushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Bunge la Bajeti, kama mtu wa tatu. Nikiwa natokea Jimbo la Butiama naomba kwanza nianze kwa kumpongeza Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kutupatia dira ambayo inatuwezesha kulipeleka Taifa hili katika Dira ile ya Mwaka 2050. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza Waziri Mkuu kwa utendaji kazi wake mzuri, viongozi wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI na wasaidizi wao pamoja na Katibu Mkuu. Ukiangalia Hotuba ya Waziri Mkuu, ya leo kwa kweli, ina mikakati mizuri ya kutuonesha kwamba tunakwenda kuitekeleza Dira hii ya Mwaka 2050 na hasa mpango wa maendeleo wa miaka minne ambao tayari dhima yake ni kukuza uchumi na kuzalisha ajira. Lengo kwa kweli, ni itakapofika Mwaka 2050 tuwe na Taifa la watu ambao wanajitegemea kwa hiyo, mambo mengi ya msingi yameelekezwa hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza pia, Rais kwa mambo yafuatayo; ukiangalia katika bajeti ya leo, hasa kipaumbele kinatolewa katika kuimarisha barabara za mijini na vijijini. Kwa hili pia, ninachukua nafasi hii kumpongeza Waziri Mkuu kwa kuielekeza Wizara ya Fedha kuimarisha upatikanaji wa fedha za Mfuko wa Barabara na kuelekeza zipelekwe moja kwa moja. Kwa hili ninaungana na Wabunge wenzangu waliotangulia kwamba, sasa angalau ile 30% ambayo ilikuwa inakwenda tena TANROADS halafu ndiyo ipelekwe TARURA sasa itaenda moja kwa moja TARURA na itawezesha utekelezaji wa barabara za TARURA kufanyika kwa umakini wa hali ya juu sana, kwa sababu, tatizo la TARURA, kama walivyosema watangulizi siyo kwamba, wana upungufu wa fedha bali fedha zilikuwa haziendi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaamini sasa kwa agizo hili kwa kweli, mambo yatakwenda kuwa mazuri zaidi na hii tumeona kabisa hata katika Hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Leo kuna baadhi ya barabara za kimkakati zinakwenda kujengwa, hasa barabara za kwenye majimbo, pamoja na madaraja yale 13 ikiwemo ile Barabara ya Suguti, Mkoa wa Mara kwa hiyo, ninapenda kuipongeza sana Serikali kwa hatua hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda pia,kuipongeza Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuunganisha Mkongo wa Taifa katika wilaya 120 kati ya wilaya 139, hii ni 86%. Sasa ninashauri hizi wilaya 19 ambazo zimesalia nazo zikamilishwe. Hii itasaidia katika kuongeza utekelezaji wa shughuli za Serikali za kidigitali na kuongeza mawasiliano inavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninachukua pia, nafasi hii kuipongeza Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na Hotuba ya Waziri Mkuu leo, hasa kwa kuendelea kujenga utekelezaji wa Sera ya Elimu ya Mwaka 2004, Toleo la 2023, ambapo mambo ya msingi yaliyoko mle ni pamoja na kuwapatia watoto wa kike elimu ya sayansi, teknolojia na ubunifu. Pia, lengo ni kuhakikisha kwamba, elimu ya amali inatolewa, lakini unaona shule 26 za wasichana zimejengwa kwenye kila mkoa na tayari shule saba zinajengwa, kwa ajili ya wavulana, lakini shule 103 za amali zimejengwa na kati ya hizo 29 ni zile za amali za ufundi na nyingine 74 siyo za ufundi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia pia, shule 158 zinatekeleza mkondo wa amali. Sasa ushauri wangu hapa ni kwamba, tujitahidi kuhakikisha kwamba, tunakamilisha majengo yale yanayohitajika pamoja na kuajiri walimu wa masuala haya ya amali, pamoja na kununua vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ili angalau mambo yaweze kwenda vizuri kwa sababu, hiyo ndiyo itakayokuwa njia pekee ya kusaidia kuhakikisha kwamba, ajira zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaipongeza pia, Serikali kwa kujenga VETA 64 ambazo zitasababisha kila wilaya iwe na VETA na ile moja ya Mkoa wa Songwe. Cha muhimu hapa ninachoshauri ni kwamba, tuongeze upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Pia, tuongeze kasi katika kuajiri Watumishi, ili angalau masuala ya amali vocational yaweze kufundishwa kwenye halmashauri zetu. Sasa tunazo VETA katika kila Wilaya, lakini ifikie mahali kwa sababu, tunayo VETA kila mkoa sasa twende kwenye VETA kila halmashauri, ili kila halmashauri iwe na mambo ya ufundi wanayofundisha kutokana na mazingira halisi ya huko.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda pia, kushauri kwamba, tuwekeze sana katika ajira za walimu wa sayansi na mambo ya hisabati. Tujenge lab kwenye hizi shule zetu za sekondari ambazo zimejengwa maana kuna juhudi kubwa sana ya ujenzi wa madarasa na maabara, hivyo vitu vikikamilika vitasaidia sana kuhakikisha kwamba, elimu inayotolewa ni ile ambayo itasababisha tuweze kufikia malengo ambayo tunayataka.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke kwamba, kuna campus 14 zimejengwa katika mikoa yote kwa hiyo, Tanzania kwa sasa, mikoa yote, inakwenda kuwa na campus za vyuo vikuu. Nadhani ni wakati muafaka wa kutumia hizi campuses kuhakikisha kwamba, zinatoa fursa za kufundisha masomo haya ya innovations kwenye maeneo yetu ya Mikoa, ili kuweza kuhakikisha kwamba, watu wanapata ujuzi wa kuweza kujiajiri wao wenyewe, ili tuweze kuhakikisha tunapunguza tatizo la ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kuchukua nafasi hii pia, kuipongeza Serikali kwa kuhakikisha kwamba, katika kipindi cha mpaka Februari, 2026 zaidi ya shilingi bilioni 43.5 zimetolewa, kwa ajili ya kaya maskini. Pia, mikopo imetolewa kwa wanafunzi 3,179 wanaotoka katika kaya maskini na wanasoma katika vyuo vyetu; hilo ni jambo la kuipongeza Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ninashauri, kupitia TASAF, kama mnavyojua, malengo ya Mheshimiwa Rais sasa hivi ni kuhakikisha kwamba, Bima ya Afya kwa Wote inatumika. Sasa hili suala limeanza kutekelezwa, lakini linasimamiwa sana na Wizara ya Afya. Hivi karibuni walikuwa wanafanya ubainishaji wa kaya maskini ambazo zitanufaika na hili suala la Bima ya Afya kwa Wote, wanaokwenda ni watu wa NHIF, wakifika kule wanashirikiana na wale waratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninashauri kwamba, kwa sababu, zaidi ya 80% ya Watanzania wanatibiwa katika huduma ya afya ngazi za msingi, hapohapo ni TAMISEMI, nadhani ni vizuri tukaboresha ubainishaji wa wahusika watakaopata hii Bima ya Afya kwa Wote kwa kushirikiana na Watendaji na Wenyeviti wa Vijiji. Kwa maana nyingine ni kwamba, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI ishirikiane kwa karibu sana na Wizara ya Afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwenye suala la mikopo nadhani 10% hii, tunaishukuru tena Serikali kwa kuleta zile kanuni, imeboresha kanuni. Tunadhani ifike mahali fulani majiji nayo ya-graduate kusudi zile fedha ambazo wanapeleka kwenye vikundi wapeleke chache, nyingine wapeleke kwenye miradi ya maendeleo, ili Serikali iweze kuwa na uwezo wa kupeleka fedha kwenye halmashauri ambazo ni za hali ya chini. Huo nao ni ushauri ambao ninajaribu kuutoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, masuala ya fedha za mikopo ya madeni ya watumishi. Hapa napo tumeona kwamba, bado watumishi wengi sana wa halmashauri, Mamlaka za Serikali za Mitaa wanadai fedha. Kwa hiyo, tunashauri hapa Serikali, kwa kushirikiana na Mamlaka za Serikali za Mitaa, wajitahidi sana kadri inavyowezekana kutathmini haya madeni na kuyalipa kwa kadri inavyowezekana kwa haraka iwezekanavyo kwa sababu, tumeona hiyo ni changamoto ambayo ni kubwa kwa kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu matundu ya vyoo; ninadhani vilevile hii moja kwa ishirini na tano kwa wavulana na moja kwa ishirini kwa wasichana iangaliwe kati ya Wizara ya Elimu na Wizara ya TAMISEMI kusudi tuwe na uhalisia. Hii itasaidia kupunguza gharama hizi au kuonekana kwamba, tunadaiwa matundu mengi sana kumbe hali halisi ya Watanzania ni, labda tundu moja wanaweza wakatumia wanafunzi 30 au 40.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile madarasa; ifikie mahali hii one to forty nadhani bado ni requirement ya hali ya juu sana. Tuangalie, hiyo nayo itasaidia kupunguza upungufu mkubwa ambao unaonekana upo wa madarasa. Kwa hiyo, ninapenda kuchangia hayo na pia, kwa sababu tuna changamoto ya walimu kwenye masuala haya ya amali, ninaishauri Serikali iweze kuajiri watumishi zaidi na ikiwezekana waende kwenye Nchi za Ulaya Mashariki kupata walimu ambao watakuja kusaidia kufundisha kwenye masomo haya ya sayansi, teknolojia pamoja na amali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu masuala ya afya, hotuba inaonesha kwamba tutawekeza zaidi katika maboma ya zahanati, lakini zaidi ya akinamama waliofanyiwa upasuaji wanapojifungua, 75% wamejifungua kwa wamefanyiwa upasuaji katika vituo vya afya. Kwa hiyo, ninashauri kwamba bajeti hii tuwekeze sana katika ujenzi wa vituo vya afya badala ya kukamilisha maboma ya zahanati.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Ninaanza kushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia katika Bunge la Bajeti, kama mtu wa tatu. Nikiwa natokea Jimbo la Butiama naomba kwanza nianze kwa kumpongeza Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kutupatia dira ambayo inatuwezesha kulipeleka Taifa hili katika Dira ile ya Mwaka 2050. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ninampongeza Waziri Mkuu kwa utendaji kazi wake mzuri, viongozi wote wa Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI na wasaidizi wao pamoja na Katibu Mkuu. Ukiangalia Hotuba ya Waziri Mkuu, ya leo kwa kweli, ina mikakati mizuri ya kutuonesha kwamba tunakwenda kuitekeleza Dira hii ya Mwaka 2050 na hasa mpango wa maendeleo wa miaka minne ambao tayari dhima yake ni kukuza uchumi na kuzalisha ajira. Lengo kwa kweli, ni itakapofika Mwaka 2050 tuwe na Taifa la watu ambao wanajitegemea kwa hiyo, mambo mengi ya msingi yameelekezwa hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumpongeza pia, Rais kwa mambo yafuatayo; ukiangalia katika bajeti ya leo, hasa kipaumbele kinatolewa katika kuimarisha barabara za mijini na vijijini. Kwa hili pia, ninachukua nafasi hii kumpongeza Waziri Mkuu kwa kuielekeza Wizara ya Fedha kuimarisha upatikanaji wa fedha za Mfuko wa Barabara na kuelekeza zipelekwe moja kwa moja. Kwa hili ninaungana na Wabunge wenzangu waliotangulia kwamba, sasa angalau ile 30% ambayo ilikuwa inakwenda tena TANROADS halafu ndiyo ipelekwe TARURA sasa itaenda moja kwa moja TARURA na itawezesha utekelezaji wa barabara za TARURA kufanyika kwa umakini wa hali ya juu sana, kwa sababu, tatizo la TARURA, kama walivyosema watangulizi siyo kwamba, wana upungufu wa fedha bali fedha zilikuwa haziendi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaamini sasa kwa agizo hili kwa kweli, mambo yatakwenda kuwa mazuri zaidi na hii tumeona kabisa hata katika Hotuba ya Mheshimiwa Waziri. Leo kuna baadhi ya barabara za kimkakati zinakwenda kujengwa, hasa barabara za kwenye majimbo, pamoja na madaraja yale 13 ikiwemo ile Barabara ya Suguti, Mkoa wa Mara kwa hiyo, ninapenda kuipongeza sana Serikali kwa hatua hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda pia,kuipongeza Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuunganisha Mkongo wa Taifa katika wilaya 120 kati ya wilaya 139, hii ni 86%. Sasa ninashauri hizi wilaya 19 ambazo zimesalia nazo zikamilishwe. Hii itasaidia katika kuongeza utekelezaji wa shughuli za Serikali za kidigitali na kuongeza mawasiliano inavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninachukua pia, nafasi hii kuipongeza Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na Hotuba ya Waziri Mkuu leo, hasa kwa kuendelea kujenga utekelezaji wa Sera ya Elimu ya Mwaka 2004, Toleo la 2023, ambapo mambo ya msingi yaliyoko mle ni pamoja na kuwapatia watoto wa kike elimu ya sayansi, teknolojia na ubunifu. Pia, lengo ni kuhakikisha kwamba, elimu ya amali inatolewa, lakini unaona shule 26 za wasichana zimejengwa kwenye kila mkoa na tayari shule saba zinajengwa, kwa ajili ya wavulana, lakini shule 103 za amali zimejengwa na kati ya hizo 29 ni zile za amali za ufundi na nyingine 74 siyo za ufundi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia pia, shule 158 zinatekeleza mkondo wa amali. Sasa ushauri wangu hapa ni kwamba, tujitahidi kuhakikisha kwamba, tunakamilisha majengo yale yanayohitajika pamoja na kuajiri walimu wa masuala haya ya amali, pamoja na kununua vifaa vya kufundishia na kujifunzia, ili angalau mambo yaweze kwenda vizuri kwa sababu, hiyo ndiyo itakayokuwa njia pekee ya kusaidia kuhakikisha kwamba, ajira zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaipongeza pia, Serikali kwa kujenga VETA 64 ambazo zitasababisha kila wilaya iwe na VETA na ile moja ya Mkoa wa Songwe. Cha muhimu hapa ninachoshauri ni kwamba, tuongeze upatikanaji wa vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Pia, tuongeze kasi katika kuajiri Watumishi, ili angalau masuala ya amali vocational yaweze kufundishwa kwenye halmashauri zetu. Sasa tunazo VETA katika kila Wilaya, lakini ifikie mahali kwa sababu, tunayo VETA kila mkoa sasa twende kwenye VETA kila halmashauri, ili kila halmashauri iwe na mambo ya ufundi wanayofundisha kutokana na mazingira halisi ya huko.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda pia, kushauri kwamba, tuwekeze sana katika ajira za walimu wa sayansi na mambo ya hisabati. Tujenge lab kwenye hizi shule zetu za sekondari ambazo zimejengwa maana kuna juhudi kubwa sana ya ujenzi wa madarasa na maabara, hivyo vitu vikikamilika vitasaidia sana kuhakikisha kwamba, elimu inayotolewa ni ile ambayo itasababisha tuweze kufikia malengo ambayo tunayataka.
Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke kwamba, kuna campus 14 zimejengwa katika mikoa yote kwa hiyo, Tanzania kwa sasa, mikoa yote, inakwenda kuwa na campus za vyuo vikuu. Nadhani ni wakati muafaka wa kutumia hizi campuses kuhakikisha kwamba, zinatoa fursa za kufundisha masomo haya ya innovations kwenye maeneo yetu ya Mikoa, ili kuweza kuhakikisha kwamba, watu wanapata ujuzi wa kuweza kujiajiri wao wenyewe, ili tuweze kuhakikisha tunapunguza tatizo la ajira.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kuchukua nafasi hii pia, kuipongeza Serikali kwa kuhakikisha kwamba, katika kipindi cha mpaka Februari, 2026 zaidi ya shilingi bilioni 43.5 zimetolewa, kwa ajili ya kaya maskini. Pia, mikopo imetolewa kwa wanafunzi 3,179 wanaotoka katika kaya maskini na wanasoma katika vyuo vyetu; hilo ni jambo la kuipongeza Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ninashauri, kupitia TASAF, kama mnavyojua, malengo ya Mheshimiwa Rais sasa hivi ni kuhakikisha kwamba, Bima ya Afya kwa Wote inatumika. Sasa hili suala limeanza kutekelezwa, lakini linasimamiwa sana na Wizara ya Afya. Hivi karibuni walikuwa wanafanya ubainishaji wa kaya maskini ambazo zitanufaika na hili suala la Bima ya Afya kwa Wote, wanaokwenda ni watu wa NHIF, wakifika kule wanashirikiana na wale waratibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninashauri kwamba, kwa sababu, zaidi ya 80% ya Watanzania wanatibiwa katika huduma ya afya ngazi za msingi, hapohapo ni TAMISEMI, nadhani ni vizuri tukaboresha ubainishaji wa wahusika watakaopata hii Bima ya Afya kwa Wote kwa kushirikiana na Watendaji na Wenyeviti wa Vijiji. Kwa maana nyingine ni kwamba, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI ishirikiane kwa karibu sana na Wizara ya Afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwenye suala la mikopo nadhani 10% hii, tunaishukuru tena Serikali kwa kuleta zile kanuni, imeboresha kanuni. Tunadhani ifike mahali fulani majiji nayo ya-graduate kusudi zile fedha ambazo wanapeleka kwenye vikundi wapeleke chache, nyingine wapeleke kwenye miradi ya maendeleo, ili Serikali iweze kuwa na uwezo wa kupeleka fedha kwenye halmashauri ambazo ni za hali ya chini. Huo nao ni ushauri ambao ninajaribu kuutoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, masuala ya fedha za mikopo ya madeni ya watumishi. Hapa napo tumeona kwamba, bado watumishi wengi sana wa halmashauri, Mamlaka za Serikali za Mitaa wanadai fedha. Kwa hiyo, tunashauri hapa Serikali, kwa kushirikiana na Mamlaka za Serikali za Mitaa, wajitahidi sana kadri inavyowezekana kutathmini haya madeni na kuyalipa kwa kadri inavyowezekana kwa haraka iwezekanavyo kwa sababu, tumeona hiyo ni changamoto ambayo ni kubwa kwa kweli.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu matundu ya vyoo; ninadhani vilevile hii moja kwa ishirini na tano kwa wavulana na moja kwa ishirini kwa wasichana iangaliwe kati ya Wizara ya Elimu na Wizara ya TAMISEMI kusudi tuwe na uhalisia. Hii itasaidia kupunguza gharama hizi au kuonekana kwamba, tunadaiwa matundu mengi sana kumbe hali halisi ya Watanzania ni, labda tundu moja wanaweza wakatumia wanafunzi 30 au 40.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile madarasa; ifikie mahali hii one to forty nadhani bado ni requirement ya hali ya juu sana. Tuangalie, hiyo nayo itasaidia kupunguza upungufu mkubwa ambao unaonekana upo wa madarasa. Kwa hiyo, ninapenda kuchangia hayo na pia, kwa sababu tuna changamoto ya walimu kwenye masuala haya ya amali, ninaishauri Serikali iweze kuajiri watumishi zaidi na ikiwezekana waende kwenye Nchi za Ulaya Mashariki kupata walimu ambao watakuja kusaidia kufundisha kwenye masomo haya ya sayansi, teknolojia pamoja na amali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu masuala ya afya, hotuba inaonesha kwamba tutawekeza zaidi katika maboma ya zahanati, lakini zaidi ya akinamama waliofanyiwa upasuaji wanapojifungua, 75% wamejifungua kwa wamefanyiwa upasuaji katika vituo vya afya. Kwa hiyo, ninashauri kwamba bajeti hii tuwekeze sana katika ujenzi wa vituo vya afya badala ya kukamilisha maboma ya zahanati.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
Hotuba ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoitoa wakati wa Ufunguzi Rasmi wa Bunge la Kumi na Tatu, Tarehe 14 Novemba, 2025
MHE. DKT. WILSON C. MAHERA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kukushukuru kwa kunipatia fursa nami kuweza kuchangia katika mjadala huu wa leo. Kwa vile ni mara yangu ya kwanza kusimama hapa Bungeni ili kuweza kuchangia, ninaomba kwanza nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa baraka nyingi alizonipatia hadi kunifanya niwe Mbunge katika Jimbo la Butiama na kuwa Mbunge katika Bunge letu hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ninachukua nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ni Rais wetu na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na vikao vya juu kuniamini na kuniteua kwenda kugombea Ubunge katika Jimbo la Butiama na ninapenda pia wananchi wa Butiama kwa kura nyingi za kishindo ambazo walipatia CCM katika ngazi ya Urais. Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipata 98% katika Jimbo la Butiama nami nilifuatia kwa kupata 97%, lakini kata zote 18 ziko kwa tiketi ya CCM. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Butiama walikuwa wana sababu za kufanya hivyo. Butiama imeanzishwa mwaka 2013, lakini kwa muda mrefu kumekuwepo na changamoto kwenye baadhi ya miradi, lakini Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipoingia kwa muda wa miaka minne ameweza kutupatia zaidi ya shilingi bilioni 345. Haikuwa jambo dogo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, amefanya mambo mengi makubwa katika Sekta ya Afya. Tuna kata 18, lakini wakati anaingia tulikuwa na kata tatu na yeye katika kipindi chake pia tumepata kata tatu zenye vituo vya afya, lakini sasa hivi tumeongeza katika kipindi chake vituo sita vya afya, hilo siyo jambo dogo. Katika kipindi chake pia ameweza kujenga zahanati 14, shule nyingi za msingi mpya na za sekondari na madarasa, matundu ya vyoo na mabweni yamejengwa katika kipindi chake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sekta ya maji; tulikuwa tuna shida ya maji katika kata zote 18, kata mbili tu ndiyo zilikuwa zina uhakika wa kupata maji safi na salama, lakini katika kipindi chake kuna mradi wa maji wa shilingi bilioni 70.5 ambao tayari umeshakamilisha miundombinu ya msingi na unaenda kutupatia maji katika maeneo mbalimbali. Hata hivyo, kilichosalia sasa ni kutafuta fedha kwa ajili ya kuweka mtandao wa maji. Ninadhani hili Mheshimiwa Rais ameshaahidi. Tayari nimeongea na Waziri wa Maji; ameahidi kuna mradi wa usambazaji maji ambao ni wa thamani ya shilingi bilioni 4.8, ukipatikana huo wananchi wataweza kupata maji kwenye maeneo kama ya Kata ya Mirwa, Buhemba, Muliaza na Busegwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Butiama pia tumepata Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere chenye thamani ya shilingi bilioni 102. Hiki chuo kitaongeza thamani sana katika maisha ya wananchi wa Butiama katika masuala ya ajira za muda mfupi na ajira za muda mref,u lakini pia wananchi wa Butiama na hasa kanda ya ziwa wataweza kusoma kwa karibu sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kipindi chake hicho vilevile tumepata fedha shilingi bilioni 10.7 kwa ajili ya TARURA, shilingi bilioni 14.9 kwa ajili ya masuala ya TASAF. Hizo zote ni sababu za msingi ambazo zimepelekea Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kupata kura 98% kwenye Jimbo la Butiama. Katika siku zake 100 tayari Wilaya ya Butiama tumepata watumishi 80 wapya kati ya hao 80, 50 ni walimu wa shule za sekondari. Vilevile, tumepata watumishi 27 wa sekta ya afya, watumishi wawili kwenye Kilimo na Mifugo na mmoja upande wa Mipango. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye sekta ya nishati tuna vitongoji 160 ambavyo havina umeme, lakini katika siku zake 100 tayari vitongoji 51 vinakwenda kupata umeme, kwa hiyo vitongoji 119 vilivvyosalia maana yake ni kwamba kabla ya mwaka 2030 vitongoji vyote vitakuwa na umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo sasa, ninaomba sasa nijikite kwenye hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, hotuba ambayo imesheheni matumaini makubwa na mipango madhubuti ya kwenda kuibadilisha nchi yetu ya Tanzania. Ili uweze kuwa na maendeleo ni lazima wananchi wa nchi husika wapate elimu ya kutosha na hasa upande wa sayansi, teknolojia na uvumbuzi. Kwa hiyo, ukiangalia Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliielekeza Wizara ya Elimu kufanya mabadiliko ya kuboresha sera pamoja na mitaala ili kuweza kuweka mkazo zaidi katika elimu ya ujuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inakwenda kujibu hoja ya watu kumaliza elimu ya msingi au sekondari wanakuwa hawana ajira na hii katika sera na mitaala pia ilivyobadilishwa maana yake elimu ya lazima sasa ni miaka 10. Kwa hiyo, ina maana vijana wetu itakapofika mwaka 2030, tutakuwa na graduates wengi sana wa form four na form six.
Mheshimiwa Mwenyekiti, imeelekeza pia katika masuala ya elimu ujuzi ukiangalia kwenye hotuba yake ukurasa wa 19 anasema: katika kipindi cha miaka mitano anakwenda kuweka msisitizo zaidi katika utekelezaji wa elimu ujuzi. Pia, tunamshukuru Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kujenga VETA nyingi nchini Tanzania. Tunachokiomba kwa sasa ni kuhakikisha kwamba Serikali inatafuta fedha ili kukamilisha zile VETA 65 ambazo zinajengwa, lakini pia tupate fedha za kununua vifaa kwa ajili ya kujifunzia na kufundishia, ambapo sasa hivi kwa mtaala mpya ni kwamba elimu ni nyumbufu baadhi ya wanafunzi wanakwenda kwenye mikondo ya amali na wengine wanakwenda kwenye mikondo ya kawaida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuonesha kwamba sasa anakwenda kutatua tatizo la ajira nchini ameamua kujenga shule za sekondari 830 katika kipindi cha miaka minne iliyopita na kati ya hizo shule, shule 103 ni shule za amali na shule 29 ni shule za amali za kihandisi (technical schools) kama ulivyokuwa unasikia Moshi Technical School. Sababu tunakwenda kuwa nazo shule 29, hilo siyo jambo dogo. Kuna shule 74 za amali zisizo za kihandisi na shule 694 ni shule za sekondari za kata. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye hotuba hapa alisema anakwenda kuweka msisitizo zaidi katika masuala ya sayansi na hisabati na hasa kwa wasichana. Tayari Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshajenga shule 26 za wasichana katika mikoa yote 26. Hilo siyo jambo dogo, lakini na tayari shule za kikanda saba kwa ajili ya wavulana zinajengwa na anataka kujenga shule katika kila mkoa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa haya yote ukiyaangalia kwenye elimu ya ngazi ya awali, madarasa mengi ya awali, sekondari, msingi pamoja na vyuo vya kati yanajengwa kwenye nchi yetu. Sasa kwenye elimu ya juu napo amefanya mambo mengi makubwa ambayo kwa kweli watu wengi hawayafahamu, lakini ni makubwa sana. Kila mkoa kwa sasa unakwenda kuwa na kampasi za vyuo vikuu maarufu hapa nchini, hilo siyo jambo dogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo ni kampasi za vyuo kama vile vya Mzumbe, SUA, University of Dar es Salaam na Arusha Institute of Accounts kwenye mikoa 15. Hivi vyuo vitaongeza fursa kwa vijana wetu ambao watakwenda kusoma kwenye hivi vyuo lakini pia ni fursa kwa ajili ya ajira ndogondogo na zitatumika pia kuandaa vijana ambao watakwenda kuwa walimu katika shule zetu za amali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa sababu anasisitiza elimu ya ujuzi kuna mradi mkubwa wa US Dollar milioni 90 kwa ajili ya kukuza ujuzi katika nchi za Afrika Mashariki. Hapa vinajengwa vituo vinne vya umahiri ambavyo kwa Kiingereza inaitwa centre of excellence. Ukiangalia pale Dar es Salaam, Institute of Technology kuna kituo cha umahiri kwa ajili ya mafunzo ya TEHAMA na hii maana yake ni maandalizi kwa ajili ya kwenda, watu wetu kwenda kujifunza masuala ya akili unde.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapohapo kwenye kampasi hiyo, kwenye Taasisi ya Dar es Salaam kuna chuo kipo Mwanza ambapo watu watafundishwa mafunzo ya umahiri kwa ajili ya uchakataji wa ngozi. Pale Arusha Technical College kuna Kituo cha Umahiri kule Kikuletwa ambacho hiki kina focus katika masuala ya utafiti wa nishati jadidifu, ambavyo vyote hivi vinakwenda kuandaa vijana wetu ambao watasoma kwenye shule za amali kuweza kubobea katika masuala ya ujuzi ili kuweza kuibadilisha nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa kifupi ninataka kusema haya anayoyafanya Dkt. Samaia Suluhu Hassan, kwa sababau kama nchi ili kuweza kuendelea lazima tujiulize tulikuwa wapi, tuko wapi na tunakwenda wapi? Mwanzoni kabisa tulitangaza kwamba tuna maadui watatu: maradhi, ujinga na umaskini na njia ya kupambana na umaskini ni kuwasomesha vijana. Kwa hiyo, ukiangalia fursa zote hizi maana yake vijana wetu wa Kitanzania wengi sasa hivi wakae mkao wa kusoma na mkao wa kupata ujuzi mbalimbali wa kuweza kujiajiri wao wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ili haya yaweze kufanikiwa tunatakiwa kuwa na amani na utulivu katika nchi yetu. Hayo mageuzi makubwa ambayo yamefanyika sasa hivi katika utekelezaji wa sera na miataala mipya yanahitaji fedha nyingi sana, ndiyo maana kwa muda mrefu tangu mwaka 1974 tulipokuwa tuna falsafa ya elimu ya kujitegemea wengi tulishindwa kutekeleza hilo kwa sababu ya gharama kuwa kubwa sana, lakini Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alithubutu na amedhamiria kuibadilisha nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, ninaomba sasa niunge mkono hoja ya Serikali, ahsante sana. (Makofi)