Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Questions from Hon. Ado Shaibu Ado (1 total)

MHE. ADO S. ADO aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga jengo jipya la Magereza Tunduru kwa kuwa jengo lililopo haliendani na mahitaji ya sasa?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Ado Shaibu Ado kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua hali ya uchakavu wa majengo katika magereza mengi hapa nchini likiwemo Gereza la Tunduru. Kwa sasa Serikali kupitia Jeshi la Magereza ina mpango wa ukarabati na upanuzi wa gereza hilo kwa awamu, ambapo tathmini ya uchakavu pamoja na michoro imekamilika na inatarajiwa kugharimu kiasi cha shilingi milioni 465 katika ukarabati na upanuzi huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Magereza itaendelea kutenga fedha kwenye bajeti kila mwaka pamoja na kutumia vyanzo vya ndani vya ubunifu ili kuhakikisha inatekeleza mpango mkakati wa ukarabati na ujenzi wa magereza nchini likiwemo Gereza la Tunduru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha.