Answers to supplementary Questions by Hon. David Mwakiposa Kihenzile (159 total)
MHE. SALIM MUSSA OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali yenye kutia matumaini, lakini nimuulize swali la nyongeza.
Je, haoni kama ipo sababu ya kuweza kuweka kipaumbele au Wizara yake iko tayari kutoa kipaumbele kwa hili jambo ili kuweza kutatuliwa kwa haraka sana, kwa sababu Wapemba wanalaghaiwa na issue hii imekuwa kubwa sana. Sasa hivi ili Wapemba waweze kukupa dua ili uweze kutoboa katika mikeka ijayo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Salim Mussa Omar kwamba Serikali inafahamu na inatambua uzito mkubwa na umuhimu wa kupeleka ndege hiyo Pemba na ndiyo maana imeshaanza mchakato. Alichokifanya ni kutukumbusha, nasi tutajitahidi kuongeza kasi zaidi ili angalau ndugu zetu Wapemba waweze kusafiri kama inavyotakiwa. (Makofi)
MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Waziri, swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amesema kwamba uko mdaki mmoja utafungwa katika eneo la Azam Sea Link, tunataka kujua, ni lini mdaki huu utakwenda kufungwa ili kuondoa adha kwa wananchi wanaotumia eneo hili?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa vilevile Mheshimiwa Waziri amesema kwenye bajeti ya mwaka huu, wametenga fedha kwa ajili ya kununua midaki mingine. Je, ni midaki mingapi itakwenda kunuliwa kwa ajili ya eneo la Azam Sea Link ili kuendelea kuboresha eneo hili? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza kuhusu lini, ni ndani ya Mwaka huu wa Fedha 2023/2024.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu ni midaki mingapi itajengwa kwenye eneo hili ni kwamba hakuna mpango wa kuongeza kwenye eneo la Azam Link kwa sababu tayari umeshapatikana mmoja na kama kutakuwa na uhitaji tutakwenda kwenye maeneo mengine yenye uhitaji mkubwa.
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA : Mheshimiwa Spika, ahsante sana na nashukuru kwa majibu mazuri ila nina maswali mawili.
Je, ni kwa nini Serikali haifanyi utafiti wa suala la bei wa safari za ndege za ndani ya nchi kutokana na bei hizo kuwa kubwa sana, kwa mfano Dodoma - Dar es Salaam 200,000 na zaidi mpaka 500,000 kwa safari ya mara moja?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Serikali haioni hatari ya kupoteza soko la ndani endapo yakajitokeza mashirika mengine yakafanya biashara hii kwa mfano Flight-Link inafanya safari hiyo kwa dola 180 sawa na shilingi 450,000 kwa safari ya kwenda na kurudi Dodoma - Dar es Salaam na ni fixed. Kwa nini hamuoni mfanye bidii ili kuliokoa Shirika la Ndege Tanzania lisije likazama? Kwa nini hamjiongezi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Asha Abdullah Juma kama alivyoeleza.
Mheshimiwa Spika, moja kuhusu tafiti, Shirika letu kwanza, mashirika ya ndege sio moja yako mengi kama alivyosema Mheshimiwa Spika, lakini kwa kuwa amegusia kwenye ATCL specific, ni kwamba tafiti zinafanyika lakini kwa kuwa jukumu la Bunge ni kushauri Serikali tutaongeza pengine utafiti zaidi ili kwenda sambamba na hoja yake.
Mheshimiwa Spika, kuhusu hoja namba mbili ya kwamba je, hatuoni hatari ya kupoteza soko, nadhani ni jambo ambalo pia linazungumzika kupitia utafiti huo ambao tunaenda nao ambao ameusema kama alivyoshauri tutaendelea kujipima, lakini kwa sasa hivi ATCL haijapoteza soko kwa sababu ipo kwenye ushindani na viwango vilivyowekwa ni kwa mujibu wa ushindani kama nilivyosema kwenye jibu la msingi. (Makofi)
MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, nini mpango wa Serikali kuhakikisha kwamba tunapata ndege za moja kwa moja kutoka Dodoma kwenda Kilimanjaro na Arusha au muda mfupi wa kuunganisha kwa kupitia Dar es Salaam?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, tumepokea ushauri wa Mheshimiwa Priscus Tarimo kuhusiana na kuanzisha route inayokwenda Kilimanjaro, nafikiri Serikali itakapokuwa tayari basi ataweza kuarifiwa. (Makofi)
MHE. ASYA SHARIF OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Serikali nashukuru kwa majibu mazuri, lakini nina swali moja la nyongeza.
Je, Serikali ina mkakati gani wa chuo hichi cha usafirishaji kuongeza wanafunzi wa kigeni? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asya kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Chuo cha Usafirishaji ambacho kiko pale Dar es Salaam kina wanafunzi 14,464 na katika wanafunzi hao asilimia 99.2 ni wanafunzi wa Kitanzania na asilimia 0.8 ni wanafunzi wa nje.
Mheshimiwa Spika, chuo kimeendelea na programu mbalimbali za kuhakikisha kinaongeza wanafunzi wengi kama ambavyo imeulizwa na Mheshimiwa Mbunge ikiwa ni kwa ajili ya kuhakikisha tunaongeza forex, lakini pia kwa ajili ya kuongeza experience kwa wanafunzi wetu.
Mheshimiwa Spika, programu mbalimbali zimefanyika katika chuo hicho ikiwa ni pamoja na kushirikiana na Balozi zetu za nje kukitangaza chuo chetu kimataifa. Vile vile tumeshiriki katika mikutano mbalimbali mingine imefanyika Nchini Rwanda kwa ajili ya kuongeza na kutangaza chuo chetu.
Mheshimiwa Spika, kama hilo halitoshi, chuo chetu kwa sasa kinaandaa mkutano mkubwa tarehe 18 mpaka tarehe 20 mwezi ujao ambao ni First International Conference on Transport and Logistics and Management ili kuleta wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi kuhakikisha kwamba pengine tunaweza kujitangaza zaidi na kupata wanafunzi wengi zaidi, ahsante.
MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri yenye kutia moyo. Pia, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nyasa na jirani zao tunapenda kushukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay. Baada ya hapo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay itakuwa ni kubwa na ya kisasa na itahitaji mzigo mkubwa kwa ajili ya kuhudumia Tanzania pamoja na nchi za jirani. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha sasa reli ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay inajengwa ili kuhakikisha kwamba bandari hii inatumika kiukamilifu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay inategemeana sana mizigo yake na bandari ndogondogo zilizopo Kando ya Ziwa Nyasa. Bandari kama Liuli, Njambe, Lipingu na kule Manda katika Wilaya ya Ludewa. Nini mpango wa Serikali kuboresha bandari hizi ili ziweze kusaidia na kuhakikisha kwamba mizigo yote inachukuliwa vizuri?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, kwanza kwa niaba ya Serikali nipokee pongezi za dhati za Mheshimiwa Manyanya kwa sababu ni kwa muda mrefu Wananchi wa Ruvuma na mikoa ya jirani wamekuwa wakitamani kuona bandari hii inafanyiwa uboreshaji na tayari Serikali ya Awamu ya Sita imeshaanza utekelezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake pili anauliza kuhusu bandari ndogondogo kama za Liuli, Njambe na maeneo mengine. Hizi bandari zote zimejumuishwa katika mpango kabambe ambao ni The Updated National Proposed Master Plan 2022/2023 mpaka 2026/2027 ambazo zipo kwenye mpango wa kuboreshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la kwanza ambalo ndio swali kubwa linaulizwa na Wabunge karibu wote wa Nyanda za Juu Kusini pamoja na Kusini. Kwamba ni lini sasa reli ya SGR ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay itaanza kujengwa na pengine reli hii wengine wanakwenda mbele zaidi wanataka kufahamu kuunganisha mpaka Liganga na Mchuchuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine nieleze kwa ufupi tu kwamba, Serikali inao mpango kwamba inatambua umuhimu na ukubwa wa mradi huu wa SGR ya Southern Corridor ambao ndani yake una miradi zaidi ya sita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja reli hii ikijengwa ya kilometa 1,000 kutoka Mtwara kwenda mpaka Mbamba Bay kwenda mpaka Liganga na Mchuchuma utawezesha kusafirisha makaa ya mawe ambapo Mungu ametujalia zaidi ya metric tons milioni 400 na yaligundulika zaidi ya miaka pengine mia moja iliyopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili itatusaidia makaa ya mawe yale yakishatengenezwa yataanza kuzalisha umeme zaidi ya megawati 600; nusu yake yakayeyushe chuma pale Liganga, nusu yake yaingie kwenye Gridi ya Taifa lakini kama haitoshi meli hii pia inakwenda kutoa ajira na inakwenda kutoa pia chuma ambacho kinakwenda kutengenezea magari na vitu mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi mnafahamu Watanzania kwamba kwa sehemu kubwa zaidi ya asilimia 100 tunaagiza chuma kutoka nje jambo ambalo linachukua fedha zetu nyingi zaidi. Hivyo basi, Serikali kwa kutumbua umuhimu huo mkubwa; moja, imeshaanza kutengeneza uboreshaji mkubwa wa Bandari ya Mtwara ili mzigo upatikane kwa wingi zaidi; lakini pili, inaongeza bandari nyingine ya pili ya kisiwa mgao ili bidhaa chafu zote kwa maana ya makaa ya mawe, simenti na kadhalika ipitie pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ipo kwenye mpango wa kuhuisha stadi iliyofanyika miaka ya nyuma kwa maana ya kutafuta mshauri mwelekezi kuhuisha ile reli ili tuweze kujua mahitaji yake ni yapi. Mara tu baada ya kukamiliisha tunategemea kuanza kuijenga kwa mfumo wa PPP na hatimaye tunaamini likikamilika hili ni moja kati ya mambo ambayo Mheshimiwa Rais wetu anayapigania na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu atakayakamilisha na hivyo kwenda kufufua uchumi wetu kwa kiasi kikubwa zaidi.
MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ukanda wa Ziwa Tanganyika yaani Mkoa wa Kigoma, Rukwa na Katavi tumesubiri kwa muda mrefu ukarabati wa meli ya MV Liemba. Je, ni lini Serikali itakamilisha ukarabati wa meli ya MV Liemba ili kunusuru usafiri huo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali ya awamu ya sita imejipambanua katika kutenda. MV Liemba ni kiungio kubwa la Ziwa Tanganyika na wananchi wote wanaotumia ziwa hilo. Tumekwishasaini mkataba mwaka jana mwezi Novemba na ndani ya mwaka mmoja tutakuwa tumeshakamilisha ukarabati na ili Wananchi wa Kigoma na maeneo jirani wasubiri kwa hamu tunakwenda kukamilisha meli yao.
MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna agenda ya Mtwara Corridor na tunapozungumza Mtwara Corridor tunazungumza bandari, tunazungumza Airport pia tunazungumza reli ya Liganga na Mchuchuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umekuwa ni wimbo toka mwaka 2020 mpaka leo hii Serikali kila ikija hapa wanasema ipo kwenye mpango. Tunataka sasa tufahamu ni lini sasa ujenzi wa reli hii ya Liganga na Mchuchuma.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, nafikiri Mheshimiwa Mtenga anataka kupata pengine ufafanuzi wa ziada. Nimekwishasema na naomba nirejee. Tulishaanza SGR ya kutoka Dar es Salaam kwenda mpaka Isaka, tumekwishaenda na SGR kutoka Dar es Salaam tumekwenda mpaka Kigoma sasa tunakwenda mpaka Msongati Burundi. Awamu inayofuatia Serikali ya Awamu ya Sita imejipambanua na imejiwekea malengo ya kwenda SGR Kusini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe mashaka uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita unakwenda kujenga reli ya SGR ya kusini ambayo ni Mtwara Corridor kama nilivyosema. Hii inakwenda kuungana pamoja na uboreshaji mkubwa wa Airport kama nilivyosema sambamba na uboreshaji mkubwa wa maeneo ambayo nimeyaeleza pale awali, kwa hiyo, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge.
MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kujenga meli kwa ajili ya abiria na mizigo katika Ziwa Tanganyika ili kutatua changamoto ya usafiri katika Mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa. Je, ujenzi huo utatekelezwa lini?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, siyo tu meli ya mizigo na abiria kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge. Serikali imesaini tayari mkataba, tumeanza kujenga kiwanda cha kutengeneza meli nyingi nyingi katika Ziwa Tanganyika. Ambapo kiwanda hicho kitahusika na kutengeneza meli za mizigo na abiria na kukarabati zilizopo, hili linakwenda sambamba na uboreshaji mkubwa wa meli ambazo zipo za akina Mwongozo, Sangala pamoja na kina Liemba kama ilivyoulizwa na Mheshimiwa Sylvia pale awali.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza niwapongeze Serikali kwa kujenga reli ya kisasa ambayo ya SGR kutoka Makutupora Tabora. Reli ile mpaka sasa hivi wamefukua makaburi ya watu wa Igalula, watu wa Goweko, Tula hamjawalipa mpaka leo. Je, ni lini mtawalipa fedha ambazo mliwarudishia msiba mpaka leo hamjawalipa kwa sababu reli inataka ipite?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, hii hoja ya Mheshimiwa Venant naomba niichukue tuifatilie halafu tuifanyie kazi baada ya kupata taarifa zake za kina.
MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari ya Tanga ilifanya vizuri sana miaka ya 1980 na sababu kubwa ilikuliwa ni uwepo wa viwanda vingi ambavyo asilimia 90 sasa vimeshakufa. Kwa kuwa, meli kubwa na nyingi haziwezi kwenda mahali ambako zitapeleka tu mzigo bila kuchukua, yaani ile exchange of containers hakuna meli kubwa ambayo itakwenda bila kukutana na hali hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, tunamini kabisa bandari ndiyo uti wa mgongo wa Taifa hili; Je, Wizara hii ya Uchukuzi haioni haja ya kushirikiana kwa karibu na Wizara zingine kuhakikisha kwamba meli kubwa zinakuja kwa kufufua viwanda ambavyo Tanga vimekufa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Bandari ya Mwambani ilipangwa kuendeshwa kwa ubia lakini kikwazo ilikuwa ni Sheria ya Ubia ambayo sasa imekwishafanyiwa marekebisho. Sasa Serikali itueleze wazi, mpaka sasa imeshachukua hatua gani kuhakikisha mpango ule wa kuendesha Bandari ya Mwambani kwa ubia unatekelezeka?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Eng. Mwanaisha kwa kazi yake kubwa anayofanya ya kufuatilia mchakato wa miundombinu katika Mkoa wa Tanga. Serikali imeshaanza kufanya mambo mengi katika eneo hilo, mojawapo ni ukarabati wa hiyo Bandari ya Tanga lakini pia uwepo wa fursa kama bomba la mafuta ni hatua muhimu kwenye kuelekea Tanga kuwa eneo muhimu sana la kiuwekezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza kama je, tuko tayari kushirikiana na Wizara nyingine, ni kweli, tuko tayari kushirikiana na sekta nyingine ikiwemo Wizara ya Viwanda na Biashara kuhakikisha kwamba viwanda vilivyokuwa vimefungwa na vimefanya vizuri miaka ya 1990 na huko nyuma vinafufuliwa ili angalau bandari hiyo iweze kupata mizigo. Mojawapo ya mambo ambayo tunayafanya ni pamoja na kufufua pia uwanja wa ndege wa Tanga ili ndege kubwa na za kati ziweze pengine kuanza kutumia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ameuliza kuhusu Bandari ya Mwambani, kwenye mpango wetu mkakati wa mwaka 2045 hiyo ni moja kati ya maeneo ambayo tunatazama kwa jicho la karibu zaidi. Kwa sasa hivi, moja tumeshakamilisha mabadiliko ya sheria ya PPP na hivyo tunakaribisha mtu yeyote anayetaka kuja kushirikiana nasi katika kuendeleza bandari hiyo ili kwa pamoja tuweze kuhakikisha kwamba Bandari ya Mwambani inafanya vizuri zaidi. Ahsante. (Makofi)
MHE. PROF. PALAMAGAMBA J. A. M. KABUDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo yanatia moyo wa kuanza kufufuliwa kwa reli hii muhimu kwa uchumi wa Tanzania. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Moja, ningependa kujua ni lini hasa mchakato wote huu utakamilika (timeframe) ili wananchi wa Kilosa lakini Wananchi wa Mikumi na wananchi wa Kilombero wajue ni lini reli hii itaanza kukarabatiwa?
Swali langu la Pili la nyongeza; kwa kuzingatia kwamba Mji wa Kilosa sasa utaunganisha reli tatu, yaani reli ya sasa ya MGR, reli ya SGR na kwa sababu kutoka Kilosa mpaka Kidatu inaanza reli ya TAZARA Kidatu mpaka Mlimba. Maana yake sasa Mji wa Kilosa utaunganisha reli tatu.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuifanya sasa Kilosa kuwa ndiyo logistic hub kubwa katika nchi yetu inayounganisha reli hizi tatu, ukichukua reli ya TAZARA ina uwezo mpaka wa kufika Zimbabwe, Zambia, Afrika ya Kusini na Namibia ili mizigo katika reli hizi iweze kuhamishwa na makontena kwa urahisi katika Mji wa Kilosa ambao sasa una stesheni kubwa mbili ya MGR na SGR na uwezo wa kuungana na reli ya TAZARA. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Profesa kwa sababu swali lake linagusa sehemu kubwa sana ya maeneo ya Mashariki na Kati mwa Tanzania. Kwa kuwa reli hii ilikuwa ni muhimu sana miaka ya nyuma kwa nchi za SADC kuanzia nchi za South Africa mpaka Uganda, Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Jemedari Dkt. Samia Suluhu Hassan inao mkakati madhubuti wa kufanyia kazi jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza ni lini, jibu ni Mwaka huu wa Fedha 2023/2024, tumekwishaanza mchakato wa kimanunuzi na pengine ifikapo mwezi Februari tayari tutakuwa kwenye hatua kubwa zaidi.
Swali la pili anauliza ni upi mkakati wa Serikali wa kuifanya Kilosa kuwa logistic hub, kwa sababu tayari reli ya MGR, SGR na TAZARA zinaungana, kwanza nataka kumhakikishie kupitia SGR na MGR, tutajenga kituo kikubwa cha mizigo katika eneo hilo la Kilosa na tayari tumeshaanza upembuzi yakinifu katika kuhakikisha tunatimiza jambo hilo na hivyo kuifanya Kilosa kuwa ni Logistic hub kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameuliza hapo awali kwenye swali lake la nyongeza.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa kuna malalamiko kwamba hata kazi ndogo ndogo kama za usafi, kufyeka na ulinzi, mkandarasi anatoa wafanyakazi maeneo ya mbali badala ya maeneo ya Seke, Malampaka na Malya. Je, Serikali inamshauri nini mkandarasi huyu?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa pia kuna malalamiko kwamba mkandarasi ambaye ndiyo mwajiri hapeleki au anapeleka michango kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kwa kusuasua, je Serikali inasemaje juu ya malalmiko haya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki.
Mheshimiwa Spika, la kwanza, amezungumzia kuhusiana na watu wengi kutoka nje ya eneo la mradi. Moja, nimetoa takwimu ya watu ambao wameajiriwa kutoka kwenye eneo hilo katika Mkoa wake wa Shinyanga.
Pili, nimkumbushe tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi huu ni wa Kitaifa. Hata hivyo, Serikali itaendelea kumsimamiwa na kumsisitiza kwamba, anatafuta kwanza wafanyakazi kwenye eneo husika kabla hajepeleka kipaumbele kwenye maeneo mengine ya nje ya eneo husika.
Mheshimiwa Spika, hoja yake pili ni kuhusiana na michango ya NSSF, kwamba pengine mkandarasi anasuasua. Tunafahamu Sheria ya NSSF (The National Social Security Act) Revised ya 2018 Cap. 50, inamtaka mkandarasi au mwajiri kuhakikisha kwamba anapeleka makato hayo NSSF mapema iwezekanavyo.
Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba kuna changamoto kubwa sana kwenye upande wa mkandarasi huyu kwa sasa. Tayari tumeshaanza vikao kupitia wenzetu Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa ajili ya kukaa naye na kuweka commitment, mara tu anapolipwa fedha aweze kupeleka michango hiyo kwenye Mifuko ya Hifadhi za Jamii. Pia, aweze kuwalipa na wazabuni mbalimbali wa ndani. (Makofi)
SPIKA: Mheshimiwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, naona umesimama.
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana na namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, napenda tu kuongezea kwenye kile kipengele cha mkandarasi kutopeleka michango kwenye Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).
Mheshimiwa Spika, nakiri kweli kuna madai ambayo mkandarasi anadaiwa na Mfuko umekuwa ukifatilia madai hayo na kuna makubaliano ambayo NSSF imeweka na mkandarasi ambapo tunataka madeni haya yakamilike ndani ya mwaka mmoja.
Mheshimiwa Spika, nimesimama pia kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, kuna utaratibu ambao umewekwa kati ya NSSF na mkandarasi kwa wale ambao wanatakiwa kulipwa mafao yao sasa, kuna utaratibu maalum wa fedha zao kupatikana ili wasiathirike na malipo hayo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba, kama Wizara ambayo tunasimamia mifuko ya hifadhi ya jamii, tutahakikisha kwamba madeni haya tunayafatilia ili haki za wafanyakazi zisipotee. Ahsante sana.
MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri yenye kutia moyo. Pia, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nyasa na jirani zao tunapenda kushukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay. Baada ya hapo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay itakuwa ni kubwa na ya kisasa na itahitaji mzigo mkubwa kwa ajili ya kuhudumia Tanzania pamoja na nchi za jirani. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha sasa reli ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay inajengwa ili kuhakikisha kwamba bandari hii inatumika kiukamilifu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay inategemeana sana mizigo yake na bandari ndogondogo zilizopo Kando ya Ziwa Nyasa. Bandari kama Liuli, Njambe, Lipingu na kule Manda katika Wilaya ya Ludewa. Nini mpango wa Serikali kuboresha bandari hizi ili ziweze kusaidia na kuhakikisha kwamba mizigo yote inachukuliwa vizuri?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, kwanza kwa niaba ya Serikali nipokee pongezi za dhati za Mheshimiwa Manyanya kwa sababu ni kwa muda mrefu Wananchi wa Ruvuma na mikoa ya jirani wamekuwa wakitamani kuona bandari hii inafanyiwa uboreshaji na tayari Serikali ya Awamu ya Sita imeshaanza utekelezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake pili anauliza kuhusu bandari ndogondogo kama za Liuli, Njambe na maeneo mengine. Hizi bandari zote zimejumuishwa katika mpango kabambe ambao ni The Updated National Proposed Master Plan 2022/2023 mpaka 2026/2027 ambazo zipo kwenye mpango wa kuboreshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la kwanza ambalo ndio swali kubwa linaulizwa na Wabunge karibu wote wa Nyanda za Juu Kusini pamoja na Kusini. Kwamba ni lini sasa reli ya SGR ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay itaanza kujengwa na pengine reli hii wengine wanakwenda mbele zaidi wanataka kufahamu kuunganisha mpaka Liganga na Mchuchuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine nieleze kwa ufupi tu kwamba, Serikali inao mpango kwamba inatambua umuhimu na ukubwa wa mradi huu wa SGR ya Southern Corridor ambao ndani yake una miradi zaidi ya sita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja reli hii ikijengwa ya kilometa 1,000 kutoka Mtwara kwenda mpaka Mbamba Bay kwenda mpaka Liganga na Mchuchuma utawezesha kusafirisha makaa ya mawe ambapo Mungu ametujalia zaidi ya metric tons milioni 400 na yaligundulika zaidi ya miaka pengine mia moja iliyopita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili itatusaidia makaa ya mawe yale yakishatengenezwa yataanza kuzalisha umeme zaidi ya megawati 600; nusu yake yakayeyushe chuma pale Liganga, nusu yake yaingie kwenye Gridi ya Taifa lakini kama haitoshi meli hii pia inakwenda kutoa ajira na inakwenda kutoa pia chuma ambacho kinakwenda kutengenezea magari na vitu mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi mnafahamu Watanzania kwamba kwa sehemu kubwa zaidi ya asilimia 100 tunaagiza chuma kutoka nje jambo ambalo linachukua fedha zetu nyingi zaidi. Hivyo basi, Serikali kwa kutumbua umuhimu huo mkubwa; moja, imeshaanza kutengeneza uboreshaji mkubwa wa Bandari ya Mtwara ili mzigo upatikane kwa wingi zaidi; lakini pili, inaongeza bandari nyingine ya pili ya kisiwa mgao ili bidhaa chafu zote kwa maana ya makaa ya mawe, simenti na kadhalika ipitie pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ipo kwenye mpango wa kuhuisha stadi iliyofanyika miaka ya nyuma kwa maana ya kutafuta mshauri mwelekezi kuhuisha ile reli ili tuweze kujua mahitaji yake ni yapi. Mara tu baada ya kukamiliisha tunategemea kuanza kuijenga kwa mfumo wa PPP na hatimaye tunaamini likikamilika hili ni moja kati ya mambo ambayo Mheshimiwa Rais wetu anayapigania na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu atakayakamilisha na hivyo kwenda kufufua uchumi wetu kwa kiasi kikubwa zaidi.
MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ukanda wa Ziwa Tanganyika yaani Mkoa wa Kigoma, Rukwa na Katavi tumesubiri kwa muda mrefu ukarabati wa meli ya MV Liemba. Je, ni lini Serikali itakamilisha ukarabati wa meli ya MV Liemba ili kunusuru usafiri huo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali ya awamu ya sita imejipambanua katika kutenda. MV Liemba ni kiungio kubwa la Ziwa Tanganyika na wananchi wote wanaotumia ziwa hilo. Tumekwishasaini mkataba mwaka jana mwezi Novemba na ndani ya mwaka mmoja tutakuwa tumeshakamilisha ukarabati na ili Wananchi wa Kigoma na maeneo jirani wasubiri kwa hamu tunakwenda kukamilisha meli yao.
MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna agenda ya Mtwara Corridor na tunapozungumza Mtwara Corridor tunazungumza bandari, tunazungumza Airport pia tunazungumza reli ya Liganga na Mchuchuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umekuwa ni wimbo toka mwaka 2020 mpaka leo hii Serikali kila ikija hapa wanasema ipo kwenye mpango. Tunataka sasa tufahamu ni lini sasa ujenzi wa reli hii ya Liganga na Mchuchuma.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, nafikiri Mheshimiwa Mtenga anataka kupata pengine ufafanuzi wa ziada. Nimekwishasema na naomba nirejee. Tulishaanza SGR ya kutoka Dar es Salaam kwenda mpaka Isaka, tumekwishaenda na SGR kutoka Dar es Salaam tumekwenda mpaka Kigoma sasa tunakwenda mpaka Msongati Burundi. Awamu inayofuatia Serikali ya Awamu ya Sita imejipambanua na imejiwekea malengo ya kwenda SGR Kusini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe mashaka uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita unakwenda kujenga reli ya SGR ya kusini ambayo ni Mtwara Corridor kama nilivyosema. Hii inakwenda kuungana pamoja na uboreshaji mkubwa wa Airport kama nilivyosema sambamba na uboreshaji mkubwa wa maeneo ambayo nimeyaeleza pale awali, kwa hiyo, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge.
MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kujenga meli kwa ajili ya abiria na mizigo katika Ziwa Tanganyika ili kutatua changamoto ya usafiri katika Mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa. Je, ujenzi huo utatekelezwa lini?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, siyo tu meli ya mizigo na abiria kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge. Serikali imesaini tayari mkataba, tumeanza kujenga kiwanda cha kutengeneza meli nyingi nyingi katika Ziwa Tanganyika. Ambapo kiwanda hicho kitahusika na kutengeneza meli za mizigo na abiria na kukarabati zilizopo, hili linakwenda sambamba na uboreshaji mkubwa wa meli ambazo zipo za akina Mwongozo, Sangala pamoja na kina Liemba kama ilivyoulizwa na Mheshimiwa Sylvia pale awali.
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza niwapongeze Serikali kwa kujenga reli ya kisasa ambayo ya SGR kutoka Makutupora Tabora. Reli ile mpaka sasa hivi wamefukua makaburi ya watu wa Igalula, watu wa Goweko, Tula hamjawalipa mpaka leo. Je, ni lini mtawalipa fedha ambazo mliwarudishia msiba mpaka leo hamjawalipa kwa sababu reli inataka ipite?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, hii hoja ya Mheshimiwa Venant naomba niichukue tuifatilie halafu tuifanyie kazi baada ya kupata taarifa zake za kina.
MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali na nina maswali mawili ya nyongeza. Mchakato wa uboreshaji na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege Kilwa Masoko ni wa muda mrefu sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; nataka Mheshimiwa Naibu Waziri, awahakikishie Watanzania, Wanakilwa na Bunge hili, je, mpango wa Serikali wa uboreshaji na upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kilwa Masoko bado uko pale pale?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Mheshimiwa Naibu Waziri amefika Kilwa Masoko mara kadhaa. Alifika mwezi Juni akiwa Mwenyekiti wa Kamati na akafika mwezi Agosti akiwa Naibu Waziri katika Sekta hii ya Uchukuzi na alikuja mahususi kwa ajili ya masuala haya ya kiwanja cha ndege.
Mheshimiwa Naibu Spika, pale kuna changamoto kadhaa, kwa wananchi wangu hawa 438 mpaka sasa bado hawajalipwa fidia. Je, yuko tayari sasa baada ya Bunge hili kwenda Kilwa Masoko akiambatana nami ili kwenda kusikiliza kero za hawa wananchi wangu 438?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. DAVID M. KIHENZILE): Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimpe uhakika Mheshimiwa Mbunge wa Kilwa Kusini kwamba, Serikali ya Awamu ya Sita inayo dhamira ya dhati ya kuboresha Uwanja wa Ndege wa Kilwa Masoko. Pia, hiyo inakwenda sambamba na uwekezaji mkubwa unaofanyika pale wa kujenga bandari kubwa kwa ajili ya uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namhakikishia kwamba mpango wa Serikali uko pale pale, mara baada ya wenzetu wa Wizara ya Fedha kukamilisha taratibu za ndani, fidia hiyo kwa wananchi hao itaanza kulipwa. Hilo moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili anauliza je, niko tayari kuambatana naye baada ya kumaliza Bunge hili. Amekiri mwenyewe nilikwenda pale pamoja na wenzangu nikiwa Mwenyekiti wa Kamati Kilimo na Mifugo. Vile vile, nimekwenda hapo juzi kukagua bandari hiyo na uwanja huo. Niko tayari kwenda pamoja naye ili tukawape uhakika wananchi hao ambao wanamwamini Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ili waendelee kujenga imani naye.
MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri mwenyewe kwamba, upembuzi yakinifu utakamilika Desemba, je, ni lini ujenzi utaanza rasmi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; je, ujenzi huo utazingatia kwa kiasi gani kuweka vifaa vya kisasa ili abiria wasikaguliwe na mbwa kama inavyofanyika sasa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. DAVID M. KIHENZILE): Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumhakikishia Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan kama nilivyosema hapo awali. Hatua ya kwanza ambayo Serikali inafanya ni kufanya uthamini au upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambao utaweza kutusaidia kujua nini kinapaswa kufanyika. Pia, mara baada ya kukamilisha hatua hiyo, hatua itakayofuatia itakuwa ni kuanza kufikiria au kuanza mchakato kwa ajili ya ujenzi. Kwa sababu, Serikali imeendelea kufanya maboresho makubwa sana kwenye bandari zetu nchini ikiongozwa na Bandari yetu kubwa ya pale Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, namba mbili; kama nilivyojibu swali la kwanza, katika usanifu huu unaoendelea kwa ajili ya ghati letu jipya la Dar es Salaam, utaambatana pamoja na ufungaji wa mashine ya ukaguzi wa kisasa ambao utatumia teknolojia ya kisasa ya ukaguzi kwa ajili ya abiria na mizigo.
MHE. AMINA ALI MZEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha Sheria za Utumishi zinaendana na mradi wa reli?
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali inatuhakikishiaje vijana wengi wanaendelea kupata ajira nchini? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Wizara ya Uchukuzi na Serikali kwa ujumla itaendelea kusisitiza na kusimamia sheria zote zilizowekwa kama nilivyotaja pale awali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kama nilivyoeleza, tunatambua na kuthamini ujuzi mkubwa walioupata vijana katika ujenzi wa reli inayoendelea. Pengine nitumie nafasi hii pia kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba Taifa letu linaweza kuwa miongoni mwa mataifa ya awali ambayo yatakuwa na vijana wengi wenye uwezo mkubwa wa kujenga reli. Kwa sababu kama unavyofahamu, katika takribani kilometa 72,000 za reli iliyojengwa barani Afrika, zaidi ya nusu inajengwa Tanzania. Hivyo tunakwenda kuwa na manpower kubwa ya vijana wenye uwezo, uzoefu na ustadi mkubwa. Hivyo uzoefu na uwezo huo tutauthamini na kuhakikisha tunautumia ndani ya nchi yetu na hata wakati mwingine kuwa-recommend kwenye maeneo ya nje ya nchi yetu.
MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kwa mujibu wa matokeo ya sensa ya mwaka jana, 2023, inaonesha dhahiri kwamba ni zaidi ya vijana 1,800,000 kila mwaka wanaingia kwenye soko la ajira. Je, Serikali ina mkakati gani mahususi inayoweza kuonekana ya kuweza kuhakikisha kwamba hao vijana wanaendelea kupata ajira?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Sita inatambua umuhimu wa ajira kwa vijana na imefanya mambo mengi. Ajira mbalimbali zimeendelea kutangazwa Serikalini, kwenye taasisi zake na kadhalika, hiyo ni moja. Pili, tumeendelea kuvutia uwekezaji mkubwa kwenye Taifa letu. Katika kipindi kifupi kilichopita, wawekezaji wameongezeka zaidi na miradi imefunguliwa. Tatu, miradi yetu, kwa mfano ya sekta hii kama nilivyoeleza, kwa upande wa reli kuanzia Dar es Salaam mpaka Isaka, kutoka Tabora mpaka Kigoma na Kigoma mpaka Msongati, pia tunakwenda kujenga reli inayotoka Mtwara mpaka Mbamba Bay, Liganga na Mchuchuma, kote huko tunaenda kuajiri vijana wa Kitanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba tunapunguza gap la ajira nchini.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa inaonekana katika hizo sheria alizosema za LATRA, watu wa bajaji na bodaboda hawamo kwenye hizo sheria, je, ni lini Serikali itatunga sheria za kuwalinda watu wa bodaboda na bajaji?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Katika nchi yetu tuna uhaba mkubwa sana wa ajira na hasa kwa vijana wetu wote wa darasa la saba, certificate, diploma mpaka degree, wote wamejiajiri kwenye bajaji na bodaboda, lakini kuna kodi nyingi sana katika sekta hii, na hasa kodi ya TRA na kodi ya parking; ni lini Serikali itafikiria namna ya kuwaondolea kodi ya TRA ambayo ni shilingi 120,000/= na kodi ya parking?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tupokee kama ushauri maswali mawili ya Mheshimiwa Mwita Getere, anamezungumzia kuhusu pengine kuboresha na kutazama sheria zetu ikiwa ni sambamba na suala la kodi ambayo kwa maelezo yake inawakwamisha vijana wetu. Tumepokea kama ushauri, tutapitia mchakato wa kawaida halafu tutaweza kufanyia kazi kulingana na uhitaji wa wakati huu.
MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Moja ya nchi ambazo zimefanikiwa sana katika usimamizi wa biashara ya bodaboda ni nchi ya Rwanda. Je, Serikali ipo tayari kuwatuma maafisa wake kwenda kujifunza ni namna gani biashara hii inaweza ikadhibitiwa vizuri ili wananchi wangu pale Kinondoni waweze wakafaidika na utaratibu huo mpya? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ametoa ushauri mzuri, lakini pia huwa napenda kuwakumbusha Waheshimiwa Wabunge na viongozi, tunapofanya comparison ni vizuri tukatazama pia na mazingira halisi. Ukiangalia ukubwa wa nchi ya Rwanda ni takribani square meter 27,000, wakati Tanzania ina 904,500. Jiji la Dar es Salaam ni kubwa zaidi, lakini hata hivyo tunapokea ushauri wake, tunajifunza tuone wenzetu wamefanyaje? Ahsante sana. (Makofi)
MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Nini kauli ya Serikali kuhusu usalama wa usafiri wa bodaboda kupakia abiria zaidi ya mmoja tena bila kuvaa helment?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatoa kauli wasafiri wote wa vyombo vya moto nchini, iwe bodaboda, iwe bajaji, na kadhalika, kuzingatia sheria pamoja na usalama kwa ajili yao wenyewe ikiwa ni sambamba na abiria wanaowabeba. (Makofi)
MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nipate faraja kidogo kwa majibu ya Serikali kwamba hatua iliyofikiwa sasa hivi ni kwamba tayari daftari lipo kwa Mthamini Mkuu Hazina kwa maana ya Wizara ya Fedha. Wananchi hawa wamekuwa wakiathirika kwa muda mrefu tangu 2013 walikuwa ni 144, ukafanyika tena uthamini 2023 wakafikia wananchi 438. Hivi tunavyozungumza wananchi wangu hawa 438, hawana makazi kutokana na kushindwa kuziendeleza nyumba zao kwa kusubiri taratibu za Serikali. Hali ni tete kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kutokana na ukweli kwamba tumeshakaa na Mheshimiwa Waziri pamoja na Wizara ya Fedha na kukubaliana kwamba, wananchi hao walipwe haraka iwezekanavyo. Je, ni nini kauli ya Serikali kulipa wananchi hawa fidia ndani ya kipindi kifupi kijacho kabla hawajaendelea kuathirika? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; Uwanja wa Ndege wa Kilwa Masoko ni moingoni mwa viwanja 12 ambavyo tuliviingiza katika mpango wa miaka mitano wa kuboresha na kupanua. Faraja tuliyonayo pale Kilwa Masoko tunajenga Bandari ya Uvuvi. Kufuatia ujenzi wa Bandari ya Uvuvi, umuhimu mkubwa wa kuimarisha kiwanja hiki upo na uhitaji mkubwa utahitajika huko mbele ya safari. Je, ni lini sasa Serikali baada ya kulipa wananchi wangu ndani ya muda mfupi, itaanza ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Kilwa Masoko? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Ally Kassinge kwa ufuatiliaji makini wa Kiwanja hiki cha Ndege. Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa Kiwanja cha Ndege cha Kilwa Masoko. Moja, ameeleza vizuri sana, Serikali imewekeza bilioni 268 kwa ajili ya ujenzi wa bandari kubwa katika Ukanda wetu wa East Africa, Bandari ya Uvuvi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia tunao Mradi mkubwa sana wa Gesi wa Mkoa wa Lindi. Hivyo, kiwanja hiki ni muhimu sana siyo tu kwa wananchi wa Lindi na ukanda huo, lakini kwa Taifa letu. Hivyo nimhakikishie Mbunge kwamba, Serikali kauli yake imeshafanya uthamini hatua ya kwanza na ya pili na mpaka wamefika wananchi karibu 454 ambao tunategemea kuwalipa karibu 6,200,000,000. Naomba Mbunge apokee kauli ya Serikali ninayoenda kuitamka sasa. Serikali italipa fidia wananchi hao, mara tu itakapokamilisha hatua za ndani na itaanza hatua za ujenzi mara moja.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri mwenye pesa kasimama.
NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi hii. Naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri mwenzangu kwa majibu yake mazuri, pia nimpongeze sana muuliza swali. Muuliza swali amehusisha Wizara ya Fedha. Ni kweli suala hili tunalitambua na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wake kule Kilwa, wawe na amani kabisa fedha hiyo italipwa kwa wakati. (Makofi)
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana, na pia napongeza kwa majibu haya ya Serikali. Naomba kupata ufafanuzi kwa maswali mawili. Moja, nilitaka kujua kwa sababu uchumi wa watu wa kwenye ukanda huu wa bahari hususan Pemba, Unguja, Tanga, Mtwara na Lindi wanategemea sana upatikanaji wa usafiri wa baharini. Ni lini fedha hizi zitapatikana ili kwenda kufanikisha upatikanaji wa Meli hiyo?
Mheshimiwa Naibu Spika, mbili; kwa kuwa Ilani ya CCM inahimiza zaidi kwenye ushirikiano baina ya taasisi ambazo siyo za Muungano, ni maeneo yapi ya ushirikiano ambayo Kampuni hii ya Meli ya Tanzania inashirikiana na Shirika la Meli la Zanzibar? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bakar, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, moja, kuhusu ni lini mchakato utakamilika wa upembuzi yakinifu, tumeshaingiza kwenye bajeti katika mwaka huu wa fedha 2023/2024. Tunategemea kabla hatujakamilisha mwaka huu, tutakuwa tumeshakamilisha upembuzi yakinifu kwa kujua lini, kiasi gani, na kwa namna gani pengine inapaswa ifanyike?
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ameuliza swali kuhusu ushirikiano kati ya Kampuni ya Meli ya Tanzania (ATCL) pamoja na ile ya SHIPCO (Shirika la Meli la Zanzibar). Tumeshaanza katika hatua za awali ushirikiano kati ya pande hizi mbili na yapo maeneo makuu matatu ambayo tunaweza kuyatazama katika hatua za kuanzia. Moja, tunaangalia ushirikiano katika taarifa na wataalam; pili, tunaangalia uwezo na kuwajengea uwezo wataalam wetu katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabaharia, TEHAMA, mipango, utafiti, rasilimali watu pamoja na masoko; tatu, tutaongeza zaidi kwenye eneo la kubadilishana uzoefu katika pande zote mbili.
MHE. JOSEPHAT. S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya kutia matumaini kutoka Serikalini, naomba niulize maswali mawili kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, juu ya efficiency ya TAZARA ni suala ambalo hatuna ubishani kama Taifa na hasa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, juu ya ufanyaji kazi bora wa TAZARA. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba ukarabati unafanyika na mtaji unawekwa ili TAZARA iweze kufanya kazi kwa jinsi ambavyo tunatarajia? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa Serikali imefanya uwekezaji mkubwa na hivi tunavyoongea tayari imeshafanya upanuzi katika Bandari ya Kasanga, na lami imeshajengwa mpaka kufika Kasanga, je, Serikali haioni kwamba ni wakati muafaka wa kuishirikisha sekta binafsi ili kuhakikisha kwamba kutoka Kasanga kwenda DRC na kui- decongest Bandari ya Dar es Salaam; na bahati nzuri Mheshimiwa Naibu Waziri anajua tuna makubaliano mazuri na DRC, ni wakati muafaka wa kufanya extension ili tuweze ku-decongest bandari yetu?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, TAZARA ni reli muhimu kwa uchumi wa Taifa letu. Sisi sote tunafahamu tangu ilipoanza kujengwa na kuanza kutumika mwaka 1976 kwa Sheria ya Bunge Na. 23 ya mwaka 1975 yenye urefu wa kilometa 1,860. Pia, sisi Watanzania tuna faida kubwa zaidi kwa sababu asilimia 52 ya reli hiyo ambayo ni 975 iko Tanzania na wenzetu ni 885.
Mheshimiwa Spika, ilipokuwa inatengenezwa wakati huo, ilikuwa imelenga kubeba mzigo wa tani milioni tano, lakini karibu miaka yote hiyo, hatukuwahi kufikia ufanisi huu, ni miaka michache tulifikia asilimia 24. Mamlaka za nchi kwa maana ya Tanzania, Zambia pamoja na wenzetu Wachina, baada ya kuitazama reli hii ndefu kabisa barani Afrika ambayo ina madaraja karibu 318, ina mahandaki karibia 22 na makaravati karibu 2,229, wakasema ipo haja ya kuanza kuitafakari upya.
Mheshimiwa Spika, hii inakwenda sambamba na uboreshaji mkubwa tunaoufanya pale bandarini. Tayari Rais wetu na Marais hawa wawili wako kwenye mazungumzo. Tunategemea ukarabati mkubwa sana kwenye miundombinu pamoja na vitendea kazi unaweza ukaanza kufanywa mwaka huu 2024 ili kuiboresha bandari hiyo.
Mheshimiwa Spika, kwenye hoja ya pili aliyoisema ya PPP, tunatambua ni hoja yake ya muda mrefu Mheshimiwa Mbunge, anajenga hoja kwamba kutoka Kaprimposhi mpaka kule Lubumbashi ni Kilometa 1,000 wakati kutoka kutoka pale Kasanga - Mlilo ukivuka ng’ambo ni kilometa 400.
Mheshimiwa Spika, tumepokea ushauri wake, tutaufikisha Serikalini ili tuuchakate kama tunavyochakata mambo mengine ili tuone namna gani tunakwenda kuutekeleza, ahsante.
MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Ni lini Serikali itajenga reli kutoka Bandari ya Mtwara kuja Tunduru – Namtumbo - Songea, pale Matomondo - Mbinga mpaka Mbamba Bay? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, tayari tuko kwenye hatua ya kuhuisha design hiyo ya southern corridor kwa maana ya kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay mpaka Liganga na Mchuchuma. Itakapokuwa tayari, nafikiri Serikali itaanza kutekeleza mara moja.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kupewa nafasi. Kwa kuwa kuna ushindani mkubwa wa Lobito Corridor, je, Serikali ina mkakati gani wa haraka kuhakikisha miundombinu ya TAZARA inakuwa katika kiwango cha SGR?
Mheshimiwa Spika, nashukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, katika majibu ya nyongeza nimezungumza mpango wa Serikali wa kuiboresha vizuri sana TAZARA, ambapo tayari viongozi wetu wameshaanza mazungumzo na yatakapokuwa tayari tutaanza kuyatekeleza mwaka huu wa 2024.
MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Ni kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa ikiahidi ujenzi wa Reli kutoka Tanga – Arusha – Loliondo – Mugumu hadi Musoma, lakini ni miaka sasa imepita. Napenda kujua nini kauli ya Serikali kuhusiana na ujenzi wa hiyo reli?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge hoja hii aliyoizungumza ya Tanga – Arusha na Musoma baada ya hapa tupate muda wa kuijadili halafu tuweze kupata majibu kamili.
MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, inasemekana kwamba Kampuni inayomilikiwa na Serikali ya Uchina imeshatoa pendekezo la ukarabati wa reli husika kwa thamani ya shilingi trilioni 2.5 na majadiliano yalianza na Serikali ya Zambia kupitia Waziri mwenye dhamana kama wewe. Hiyo imekuwa reported na gazeti la Citizen la tarehe 10 Februari, 2024. Serikali mnatuambiaje kuhusiana na hili? Hayo unayoyasema ndiyo kampuni inayomilikiwa na Serikali ya China?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, mazungumzo yanaendelea na kwa kuwa hatujafika hatua ya mwisho, itakuwa ni mapema sana kuanza kuzungumzia gharama na hatua tuliyofikia. Namuomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira, yakishakamilika taarifa hizi ni za wazi, basi ataweza kufahamu pengine ni mkandarasi gani anayefanya kazi hiyo.
SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri kwa sababu swali hili limekuwa likijirejea mara kwa mara na hili swali alilouliza Mheshimiwa Msongozi na umejibu hapa kwamba 2024 nafikiri ulikusudia kusema 2024/2025. Sasa ni muhimu ili 2024/2025 linahusu hii ya TAZARA au inahusu ile ya Mheshimiwa Jacqueline aliyouliza ile ya kuanzia Mtwara mpaka Mbamba Bay. Hii 2024/2025 inahusu ipi kati ya hizi mbili?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, mwaka huu 2024 nilichokizungumzia ni uboreshaji wa Bandari ya TAZARA kutoka Dar es salaam mpaka Kapirimposhi kilomita 1860 hii Reli ya TAZARA kutoka Dar es salaam mpaka Kapirimposhi huu ndio uboreshaji tunaozungumza kwamba mazungumzo yanaendelea kati ya nchi hizi tatu na tunategemea mwaka huu pengine tuanze utekelezaji wake.
SPIKA: Sawa umerejea tena 2024, ukisema 2024 maana yake ni mwaka huu wa fedha ule unaokuja unaitwa 2024/2025 wewe unakusudia kusema upi 2023/2024 au 2024/2025?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nilikusudia kusema kwa maana kuanzia Januari hii mpaka Desemba hapa katikati tutakuwa tumefikia hatua nzuri ya utekelezaji.
MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri juu ya mradi huu wa ujenzi wa reli kutoka Mtwara hadi huko Mbamba Bay. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, rai yangu kwa Serikali, kwa kuwa mmeamua ku-engage private partnership kushiriki katika mradi huu, mimi nawapongeza sana na naiomba Serikali iongeze jitihada ili reli hii iweze kufunguliwa na iwe mkombozi kwa wananchi wa Kusini hasa usafirishaji wa makaa ya mawe kutoka Liganga, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mhata kwa kutoa pongezi, wachache sana wakitendewa mambo mema wanasimama na kushukuru. Kwa hiyo nakushukuru sana Mheshimiwa Mhata kwa kuwa na moyo wa shukrani ambao utazidishiwa yaliyo mema zaidi. (Makofi)
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haioni umuhimu wa kutengeneza baadhi ya mabehewa kuweka mfumo wa ubaridi (cold room) katika reli ya TAZARA ili tuweze kusafirisha parachichi zetu na mazao ya mboga mboga yamfikie mlaji wa mwisho yakiwa na ubora? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana dada yangu Mheshimiwa Mgaya kwa sababu ni mdau mkubwa sana wa reli ya TAZARA na tukubali ukweli kwamba kwa sasa katika reli yetu na mabehewa yaliyopo hatuna cold rooms, lakini kila mtu anafahamu umuhimu wa ukuwaji wa sekta ya parachichi katika mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa unyenyekevu mkubwa Wizara tunapokea ushauri huu na tunapokwenda kwenye hatua ya pili ya maboresho makubwa ya reli yetu kutoka Dar es Salaam mpaka Kapiri Mposhi tutaona namna ya kuweza kuweka hicho alichokizungumza cha cold room.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Serikali imeboresha miundombinu ya Bandari ya Tanga kiasi kwamba shehena zimeongezeka, lakini reli ya kutoka Tanga kwenda Dar es Salaam na kutoka Tanga kwenda Arusha bado ni chakavu sana, je, kuna mpango wowote wa kuboresha reli hii ili sasa shehena hii iweze kutoka kwa urahisi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Shangazi, Mbunge wa Mlalo na Katibu wa Bunge la CCM kwa swali lake kubwa na zuri la maslahi ya watu wa Tanzania na watu wa Kaskazini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inao mpango mzuri na kabambe kwa sababu inatambua umuhimu wa upande wa Kaskazini kwanza kwenye utalii, kilimo pamoja na sekta nyingine, hivyo katika mwaka wa fedha 2023/2024 tumeshafanya kazi kubwa, tulishasaini mkataba wa kununua materials za kukarabati reli inayotoka Tanga kuelekea mpaka Arusha kilometa 533.
Kwa hiyo, mara baada ya kusaini mkataba huo katika mwaka wa fedha huu unaofuatia tunakwenda kuanza kutoa reli iliyokuwepo, tunataka tuweke reli nzito ambayo itakuwa na capacity ya ratilika 80 kwa yard, iliyokuwepo ilikuwa 45 kwa yard.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii reli iliyopo sasa hivi speed inayokwenda treni ni karibu speed ya 15 - 20 kwa saa moja, hivyo inawachukuwa muda mrefu sana kufika kwenye destination inayotakiwa. Tukifanya maboresho haya speed itaongezeka mpaka 75, kwa hiyo muda kama ilikuwa ni saa 12 tutakuwa tunatumia saa karibu nne. Kwa hiyo, habari njema hii kwa watu wa Kaskazini, Tanga na Watanzania kwa ujumla juu ya maboresho makubwa ya reli ya Kaskazini. (Makofi)
MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Wizara ya Uchukuzi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Mlimba usafiri wa reli ya TAZARA ndiyo usafiri unaotegemewa, sasa lini mpango wa Serikali katika kuboresha reli hii ikiendana sambamba na kuongeza mabehewa na route za safari ya reli hii kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, reli ya TAZARA kama inavyofahamika ilijengwa miaka 1975 baina ya Serikali tatu, China, Tanzania na Zambia na kipindi chote hicho designed capacity ilikuwa ni metric tons milioni tano, lakini kutokana na ubovu wa miundombinu hatukufikia lengo. Habari njema kutoka kwa daktari wa maendeleo Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania amefanya kikao na Waziri wa Zambia pamoja na Rais wa China, hivi ninavyozungumza tupo kwenye hatua za mwisho za majadiliano, reli nzima inakwenda kufumuliwa upya. Moja, kuongeza uwezo wa reli wa kubeba mzigo, lakini pili tutaongeza mabehewa pamoja na vichwa vya kutosha ya mizigo na abiria. Kwa hiyo, Wana-Mlimba na watumiaji wote wa reli hii inayotoka Dar es Salaam mpaka Kapiri Mposhi kilometa 1,860 waendelee kusubiri habari hii njema ambayo inakuja kwa Watanzania wote. (Makofi)
MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Napenda kuiuliza Serikali, ni sababu zipi ambazo zimefanya wabadili uamuzi wa awali ambapo ilikuwa wanatoa eneo la meta 700 kutoka kwenye njia ya kurukia ndege na sasa wanachukua eneo lote mpaka nje ya milima upande wa pili ambapo hapahitajiki kwa upanuzi wa Uwanja wa Ndege? Hilo ni swali la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naishukuru pia Serikali kwamba zoezi la uthamini limeanza na lilipangwa kufanyika kwa siku 55, mpaka sasa hivi siku 38 zimekamilika, ni mitaa miwili tu ambayo imefikiwa ambayo ni Mtaa wa Bulyanhulu na Shibula bado mitaa mitatu; mtaa wa Kihili, Monze na Nyamwilolelwa. Je, ni lini kazi hiyo itakamilika kwa mitaa yote mitano ili wananchi waweze kupata haki yao?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kuhusiana na eneo ambalo awali lilikuwa limepangwa, lakini baada ya tathmini ya kina na tukiangalia kwamba Serikali ina mpango mkubwa wa kufanya Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuwa wa Kimataifa, vipo vigezo mbalimbali, kimojawapo ni usalama. Tathmini ya kiusalama ilipofanyika, ilidhihirika kwamba ni muhimu na ni lazima wananchi wa eneo lote lile wapishe ili tuweze kuwa na uwanja ambao siyo tu ni mkubwa, lakini pia unakidhi takwa la kisheria pamoja na la ukubwa kwa maana ya kiusalama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, kuhusiana na muda. Pendekezo la Mkoa kupitia Mkuu wa Mkoa la kuwatoa wananchi katika eneo lile kwa sababu za kiusalama lilipokamilika lilibidi liwasilishwe Serikalini na baada ya kupata idhini, tayari uongozi wa Mkoa pamoja na Kamishna wa Ardhi wa Mkoa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege wameshaanza mchakato kwa ajili ya uthamini. Mara tu tutakapokamilisha, tutaanza zoezi la kulipa.
MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeshaanza mchakato wa kuwalipa fidia wananchi wanaopisha upanuzi wa uwanja wa Moshi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wale wanaostahili tumeshaanza kuwalipa na wengine tumeshawalipa, lakini kuna wananchi waliovamia ambao hawatastahili kulipwa katika eneo hilo.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Fidia imekuwa ikicheleweshwa sana kwa muda mrefu kwa hawa wanaopisha upanuzi wa viwanja na mmekuwa mkiahidi mtalipa riba, mfano pale Uwanja wa Manyara - Karatu. Je, ni lini mtalipa hizo riba? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, malipo ya fidia katika viwanja vyote nchini ikiwemo Kiwanja cha Manyara yatalipwa kwa kuzingatia sheria na taratibu za ulipaji fidia Serikalini.
MHE. MARTHA N. GWAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza: Je, ni lini Serikali italipa fidia kwa wananchi waliopisha maeneo yao kwa ajili ya ujenzi wa SGR, ambao ni wananchi wa Halmashauri ya Itigi na wananchi wa Halmashauri ya Manyoni?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Ni lini Serikali italipa Service Levy kutokana na ujenzi wa reli ya SGR kwa hizi Halmashauri ambazo zimepitiwa na reli hii; Halmashauri ya Itigi na Halmashauri ya Manyoni? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia malipo hayo, nataka nimjulishe kwamba mfumo wa utoaji wa ardhi katika eneo hilo umekuwa ukienda sambamba na kulipa fidia. Maeneo ambayo hayajalipwa fidia kwa sasa ni yale maeneo ambayo tuna uchimbaji wa malighafi ya ujenzi ikiwa ni pamoja na Tambukareli, Centre pamoja na Milembela. Maeneo hayo yataendelea kulipwa kulingana na hatua za uthamini zitakapokamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusiana na Service Levy kwa Halmashauri zote mbili kwa maana ya Itigi pamoja na hiyo nyingine ya Manyoni, tulifanya vikao mwaka jana, 2021 kati ya TRC pamoja na Halmashauri zote mbili, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake baada ya kukubaliana ikaonekana kwamba pengine inatakiwa waanze kulipwa shilingi 1,500,000,000 kwa kila Halmashauri moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyozungumza, tayari wameshalipwa shilingi 214,000,000 kila mmoja na malipo mengine yataendelea kufanyika kulingana na jinsi tutakavyokuwa tumechimba zile material. (Makofi)
MH. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza; kwa kuwa nchi iko katika ushindani wa kibiashara baina ya mataifa mengine, je, Serikali haioni umuhimu wa kuharakisha mchakato?
Mheshimiwa Spika, swali langu namba mbili, kutokana na changamoto kubwa ya msongamano wa malori ndani ya mpaka wa Mji wa Tunduma ambayo yanavuka mpaka nataka kujua hatua zilizofikiwa mpaka sasa katika kujenga kituo cha maegesho cha muda ili kuepusha changamoto ya mlundikano wa magari makubwa. Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Fiyao, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza kuhusu kuharakisha mchakato, Serikali inaendelea kufanya kazi hiyo ya kuharakisha kama nilivyosema, bila kuathiri taratibu ambazo zimewekwa ikiwa ni pamoja na kufanya huo uthamini na baadaye kulipa fidia katika mwaka wa fedha ambao unafuatia.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kuondoa msongamano, hii imekuwa ni changamoto kubwa na ndiyo maana Serikali imefanya mambo mawili makubwa kwa sasa kama unavyofahamu. La kwanza, tayari tumeshakaa kama nchi mbili, Zambia na Tanzania. Hii ilikuwa ni maamuzi yaliyofikiwa na viongozi wakuu wa nchi kupitia ziara ya Rais wetu alipokwenda Zambia ili tuondoe vikwazo vyote vilivyopo mpakani.
Mheshimiwa Spika, tunaamini suluhu hii ni ya kudumu zaidi pengine kuliko kuweka kipande pembeni pale Tunduma. Pia, Serikali inaendelea na mchakato mkubwa wa kuboresha reli yetu hii yote ili mzigo mkubwa zaidi uweze kubebwa kupitia Reli ya TAZARA kutoka Tanzania mpaka Kapiri Mposhi, Zambia.
MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Tabora, Wilaya ya Manispaa, Kata ya Ifucha waliahidiwa kujengewa bandari kavu kwenye mkutano wa hadhara alipokuja Mheshimiwa Waziri Mbarawa; na mpaka sasa hivi Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imeshalipa fidia ya heka 600 katika Kata ya Ifucha, je, Serikali inatupa status gani wananchi wa Mkoa wa Tabora ili kusubiri kwa hamu ujengaji wa bandari kavu katika mkoa wetu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Mbunge, dada yangu Munde kwa kuweza kukumbushia jambo hili. Nimhakikishie kwamba Mheshimiwa Waziri ameshanituma katika Bunge hili niende Tabora kwa ajili ya kuona sehemu hiyo ili kuendelea kupanga namna bora ya kufanya kuendana na jambo hilo.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali ilishakuwa na makubaliano ya awali kuchukua eneo ambalo siyo zaidi ya ndani ya meta 700 kulipa fidia na sasa inaonekana itakwenda zaidi ya kata tano zikiwemo Kata za Shibula pamoja na Bulyanhulu na wakazi zaidi ya 1,400, je, Serikali haioni kuchukua eneo lote hili kwa wakati mmoja kutaathiri maisha ya baadhi ya wananchi ambao wako nje kabisa ya eneo la uwanja wa ndege?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Serikali kwa kuanza ujenzi wa jengo la abiria, ni lini mkakati wa Serikali kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Mwanza na wenyewe unakuwa moja ya viwanja vya Kimataifa hapa nchini? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la pili kisha nirudi swali la kwanza.
Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita inatambua umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuufanya wa Kimataifa na tayari mambo kadhaa yameanza kufanyika. La kwanza, tuko kwenye hatua za ndani za documentation. Ili uwanja uweze kuwa wa Kimataifa, kuna taratibu za kisheria ambazo lazima zizingatiwe.
Mheshimiwa Spika, la pili, ni pamoja na kuondoa wavamizi wapatao 1,000 katika uwanja huu ili waweze kupisha kiwanja hicho kiweze kuwa salama. Pale kuna milima na maeneo mbalimbali ambayo wananchi wamevamia. Kwa hiyo, huwezi kukifanya cha kimataifa wakati huo huo usalama wa kiwanja uko mashakani.
Mheshimiwa Spika, la tatu, tunafanya kazi ya uboreshaji wa miundombinu. Kama unavyofahamu, tarehe 28 mwezi huu Waziri wetu Mheshimiwa Mbarawa alikwenda kushuhudia ujenzi wa jengo la abiria. Iko mikakati mingi, lakini nimetaja mitatu ya kuufanya uwanja huu kuwa wa kimataifa.
Mheshimiwa Spika, sasa nikirudi kwenye swali lake la kwanza, nafikiri litakuwa limeshajibiwa na hoja hii ya pili, kwa sababu hatuwezi kuacha eneo ambalo nimeshalisema pale juu, kwa sababu tu tunataka tuufanye uwanja wa kiamataifa. Kwa hiyo, lazima watu wapishe ili tuweze kuupa hadhi inayostahili, ahsante.
MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, Serikali kwa kuchelewa kulipa pesa ya wananchi zaidi ya miaka mitano sasa, haioni kwamba imerudisha nyuma maendeleo ya wananchi hao kwa kukosa sehemu za kulima? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, naomba kauli thabiti ya Serikali, je, ni lini wananchi hawa wa Nachingwea wataipata pesa yao?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba tuna viwanja takribani 15 nchi nzima ambavyo tunafanya uhakiki na hatua mbalimbali za utwaaji wa ardhi ili kuweza kufanya maendelezo makubwa ya viwanja vya ndege. Hilo moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ningependa kujibu maswali yake kwa umoja wake. Tunafahamu umuhimu mkubwa wa Uwanja wa Ndege wa Nachingwea, siyo tu kwa ajili ya korosho, madini ambayo yamegundulika na LNG, lakini pia kwa ajili ya mazao kama ufuta na kadhalika. Hivyo basi, Serikali kwa maana ya kutoa kauli thabiti, inaliarifu Bunge lako Tukufu kwamba tunao mpango wa kujenga uwanja huu na ndiyo maana sasa tulifanya uhakiki kwa wale wananchi 116. Awali ilikuwa tuwalipe shilingi bilioni 3.5, lakini baada ya kufanya uhakiki na ongezeko la gharama ya mazao, tukapata ni shilingi bilioni 3.4 – 3.5. Hii yote ni dhamira ya Serikali katika kuona kwamba wananchi hao wanakamilishiwa mradi wao. Hivyo basi, tunaendelea na taratibu mbalimbali za Serikalini, tukikamilisha tutaweza kuanza ujenzi huo. Ahsante.
MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Uwanja wa Ndege wa Musoma, watu wanadai fidia sasa ni zaidi ya miaka mitatu ambayo ni fedha isiyopungua bilioni 3.9. Hakuna biashara inayoendelea kwa kuwa wanategemea wapate fidia ili waendelee na maisha yao. Je, ni lini sasa hawa watu watalipwa fidia ili waweze kuendelea kuondoka pale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu madai mbalimbali ya Uwanja wa Ndege wa Musoma na hivi juzi Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuwa hapo na alitoa maelekezo kwa sisi wasaidizi wake Serikalini tukamilishe haraka iwezekanavyo. Tupo kwenye hatua mbalimbali hususan za mwisho kwa wenzetu Wizara ya Fedha. Mara watakapokamilisha tutakwenda kulipa mara moja, kwa sababu tunafahamu umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Musoma kwa maana ya madini pamoja na vitu mbalimbali ambavyo viko pale. Ahsante.
MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naishukuru Serikali kwa kutupa shilingi bilioni 11 kwa ajili ya kulipa fidia kwa wananchi wale waliokuwa Uwanja wa Ndege wa KIA ili waweze kuondoka. Hata hivyo, kumejitokeza changamoto ndogondogo, baadhi ya wananchi kufanyiwa tathmini ndogo tofauti na hali halisi na baadhi yao kusahaulika. Changamoto hiyo Mheshimiwa Makamu wa Rais aliiagiza Wizara ya Uchukuzi iifanyie kazi. Je, ni lini sasa Serikali itamaliza changamoto hii ikiwa ni pamoja na kurudia tathmini kwa wale ambao walifanyiwa tathmini ambayo siyo sahihi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanya uhakiki kwa baadhi ya waliolalamika kwamba walipunjwa malipo yao katika Uwanja wa KIA, lakini kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge ameleta hoja hiyo, tuko tayari kama kuna malalamiko mengine, kuyapitia upya ili waweze kupata stahiki zao. (Makofi)
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Wananchi wa Wilaya ya Kyerwa na Karagwe ambao kwa muda mrefu waliambiwa wasiendeleze maeneo ambayo yako karibu na barabara ambazo ni Barabara kutokea Omugakorongo kwenda mpaka Murongo zikiathiri Kata za Kibale, Bugara na maeneo mengine. Je, ni lini sasa fidia hizo zitatoka ili wapishe hayo maeneo ya uendelezaji wa barabara kwa sababu wameshindwa kuendelea na maendeleo au kufanya chochote kwa sababu ni issue ya muda mrefu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema kwenye maelezo wakati namjibu mwenye swali la msingi, tupo kwenye hatua mbalimbali za utwaaji wa ardhi, tuna viwanja 15 nchini kote. Pamoja na hoja aliyoisema Mheshimiwa Mbunge, tunaichukua tuifanyie tathmini na tutaona namna bora ya kuonana naye ili kuweza kuzifanyia kazi hoja za wananchi hao.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini wananchi wanaopisha upanuzi wa Uwanja wa Manyara watalipwa fidia?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa hatua tuliyopo ni uandaaji wa taarifa ya uthamini, mara tutakapokamilisha, tutawalipa fidia.
MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Moja ni kwamba, tangu mkataba wa ukarabati umefanywa mwaka 2023 mpaka leo kipande cha Tabora - Kigoma chenye urefu wa kilometa 411 hakuna kazi yoyote mpaka sasa inayoendelea. Haijafanyika kazi yoyote na bajeti ya mwaka 2023 na mwaka 2022 mmekuwa mkitenga fedha kwa ajili ya ukarabati na hakuna kazi inayoendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kwamba, mliongeza mabehewa katika reli hiyo ili kuongeza safari za train kutoka tatu kwa wiki mpaka nne kwa wiki, na mpaka leo bado safari ni tatu na mabehewa yaliyoongezeka yapo na ya ukarabati yapo lakini hakuna kinachoendelea. Nini mpango wa Serikali kwenye jambo hili?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda kwa kukubali majibu ya Serikali ambayo tumeyatoa na kimsingi katika swali lake la kwanza la nyongeza anaweka mkazo kwamba dhamira hii ya Serikali ambayo imeonekana inafaa mpaka tumefika hatua ya kupitisha na hatimaye kusaini mkataba pengine angependa kuona ianze mara moja.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumepokea ushauri huu na tunaendelea kujipanga kuhakikisha katika muda ambao tumeusema, basi ukarabati huu tunauanza mara moja kwa ajili ya kusaidia wanakigoma.
Mheshimiwa Naibu Spika, hii inakwenda sambamba na kwenda kutazama hii habari ya route ambayo amezungumza pamoja na kuongeza mabehewa, lakini bado hatujaanza route, tumelipokea, nashukuru sana.
MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, naishukuru Serikali kwamba imeona umuhimu wa uwanja ule kwa sababu ni uwanja ambao ulitumika kukomboa nchi za Kusini mwa Afrika na ule ni miongoni mwa viwanja hivyo. Kwa hiyo, nataka kujua kama Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kwenda Newala ili kuona hali ya uwanja ule?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili ni kwamba, ni zaidi ya miezi mitatu sasa imepita tangu mkataba wa jengo la abiria kwenye uwanja wa Mtwara usainiwe, lakini mkandarasi hajalipwa advance payment ili ujenzi huo uanze. Je, ni lini Serikali italipa advance payment ili ujenzi wa jengo la abiria katika uwanja wa Mtwara uanze kujengwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Serikali napokea shukurani, na ninaomba shukrani hizi ziende kwa Rais wetu mpendwa ambaye anajenga viwanja takribani nchi nzima. Pia, niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwa ajili ya kutembelea eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili amezungumza kuhusiana na jengo la abiria Mtwara. Serikali katika awamu ya kwanza imefanya kazi kubwa ya kujenga runway katika uwanja wa Mtwara, kuweka taa za barabarani, maegesho, na kadhalika. katika hatua ya pili Serikali imeshasaini mkataba wa takribani shilingi bilioni 67 ambapo tunajenga jengo la abiria, control tower, jengo la zimamoto, hali ya hewa, na kadhalika. Vilevile, hivi ninavyozungumza tayari mkandarasi amekabidhiwa site na ujenzi unaanza mara moja.
MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, suala hili nimelizungumza hapa Bungeni hii ni mara ya saba, ikiwa maswali ya msingi matatu, ya nyongeza mawili na nimechangia mara moja. Mheshimiwa Waziri wa Fedha wakati anahitimisha Mpango na Bajeti wa mwaka 2024/2025 alizungumza masuala ya fidia kuwa yatakuwa kipaumbele. Mwaka wa fedha umeanza na hii ni robo ya kwanza: -
(a) Je, ni lini wananchi wangu hawa watalipwa fedha hizi kiasi cha shilingi bilioni 6.2?
(b) Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari baada ya Bunge hili aambatane na mimi kwenda Kilwa Masoko ili tukakutane na wananchi wangu hawa tukawape majibu ya Serikali yenye matumaini?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, kwa swali la pili, mara tu baada ya Bunge niko tayari niongozane na Mheshimiwa Mbunge twende huko.
Mheshimiwa Spika, swali lake la kwanza, kwamba ni lini; ni mwaka huu wa fedha 2024/2025.
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza; je, ni lini Serikali itaongeza viti mwendo vya umeme katika viwanja vyetu vya ndege na stesheni zetu, hasa SGR kwa kuwahudumia watu wenye mahitaji maalum?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa tumeshuhudia watu wenye mahitaji maalum wanapata shida sana wakisafiri hasa kwenye stesheni zetu za SGR. Je, ni lini Serikali itatoa mafunzo maalum kwa wahudumiaji wa watu hawa wanaposafiri katika stesheni zetu za SGR na viwanja vya ndege na vituo vya mabasi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyopigania haki ya watu wenye mahitaji maalumu katika viwanja vyetu katika SGR, treni na usafiri mwingine wa mabasi. Serikali inayo nia na imekuwa ikifanya hivyo. Kama ambavyo nimesema kwenye swali la msingi, ujenzi wowote unaojengwa katika viwanja vyote unazingatia watu wenye mahitaji maalum.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, tayari tuna vitimwendo vya umeme ambavyo vinasimamiwa na watoa huduma katika maeneo mbalimbali ikiwemo Swissport na wengine. Pia, hata kwenye upande wa SGR au hata kwenye ndege unapokwenda kupanda usafiri huu wako watu wenye mafunzo, si tu pale unapokuwa unapanda lakini pia wapo na madaktari pamoja na fani mbalimbali katika afya ambao kama kutakuwa na changamoto yoyote wako tayari kwa ajili ya kuja kuhudumia.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, tunapokea ushauri wake. Tutaendelea kuongeza ubora katika viwanja vyetu kulingana na mahitaji ya watu wenye mahitaji maalum hatua kwa hatua.
MHE. TASKA R. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza tunaishukuru Serikali kwa ujenzi wa bandari. Swali la kwanza; kwa kuwa bandari imeshakamilika na kwa kuwa ujenzi wa reli hii unakwenda kuunganisha Nchi yetu ya Tanzania na Nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, pia inakwenda kutoa fursa kwa wananchi wa Tanzania hususan wananchi wa Mkoa wa Katavi kufanya biashara na Nchi ya Congo. Je, Serikali ina mkakati gani wa kupata fedha kuharakisha ujenzi wa reli hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa upembuzi yakinifu umeshakamilika wa kilometa 321 kutoka Kaliua Mpanda hadi Kalema kwa ajili ya ujenzi wa reli hii, lakini katika ujenzi huo kuna wananchi ambao watapisha ujenzi wa reli hii. Je, ni lini wananchi wanaopisha ujenzi wa reli hii watalipwa fidia yao?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama utaridhia kabla sijajibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Taska Mbogo, ninaomba nitumie nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa tukio kubwa linaloendelea sasa hivi Nchini China, ambapo yeye pamoja na Marais wenzake, Rais wa China pamoja na Mheshimiwa Rais wa Zambia, wamesaini hati ya makubaliano ya kuboresha reli yetu ya TAZARA. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa Bungeni mara kadhaa hoja hii imeulizwa kila wakati, ni lini TAZARA itaboreshwa, leo hati maalum ya makubaliano imesainiwa ili kuifumua TAZARA iweze kubeba mzigo na kufungua biashara kati ya nchi yetu na Nchi za Congo na nchi ya Zambia na sote tunafahamu tuna potential ya mzigo wa ten million metric tons Congo pamoja na seven million metric tons upande wa Zambia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nikirudi kwenye swali la Mheshimiwa Taska Mbogo, namba moja anauliza mkakati wa kupata fedha. Serikali ya Tanzania imejitambulisha kwamba ndiyo Serikali inayoongoza Barani Afrika kwa kuwa na agenda maalum kwenye reli, ndiyo maana tunajenga reli ndefu kuliko reli nyingine yoyote katika Bara letu na duniani tukiwa ni nchi ya tano. Ninamwomba Mheshimiwa Mbogo pamoja na Waheshimiwa Wabunge wengine wa mikoa hiyo wavumilie kidogo, tupo kwenye kipande cha saba sasa kwa maana kutoka Dar es Salaam mpaka Mwanza wakandarasi wapo site tayari na kutoka Tabora mpaka Kigoma wapo site tayari na kutoka Kigoma Uvinza kuelekea mpaka Burundi tupo kwenye hatua za kumpata mkandarasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Mbogo avumilie, tukimaliza hapa tutarudi kwenye vipande vingine vinavyoendelea ikiwa ni pamoja na kwake Kaliua - Mpanda, pamoja cha Mtwara Corridor ambacho najua Wabunge wa Mtwara lazima wangeuliza, leo pamoja na kutoka Rusumo kwenda mpaka Kigali na kutoka Tanga, Arusha na Musoma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hoja ya pili, Serikali hii inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, inajali wananchi wake. Nimhakikishie pale itakapobainika kunahitaji fidia wananchi hawa kwa mujibu wa taratibu na sheria za nchi yetu watapewa fidia zao. (Makofi)
MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wilaya ya Kahama imekuwa ndiyo kitovu cha kibiashara kwa Mkoa wa Shinyanga, lakini pia na Mikoa ya Kanda ya Ziwa na Nchi hizi za Maziwa Makuu. Kwa nini Serikali isitenge japo fedha kidogo ili kuukarabati uwanja huu ambao ni wa kiwango cha moramu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Manispaa ya Kahama imekuwa ikikusanya fedha nyingi zaidi ya shilingi bilioni 13 mpaka shilingi bilioni 15 kwa mwaka. Kwa nini Serikali isitoe kibali sasa kwa Manispaa hii ya Kahama angalau uwanja huu uwekwe kwa kiwango cha lami pamoja na miundombinu yetu ili kuondoa adha wanayoipata wasafirishaji?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Cherehani kwa ufuatiliaji wake wa karibu wa Uwanja wa Ndege wa Kahama lakini hata ule wa Shinyanga. Pili, napenda kumwarifu Mheshimiwa Cherehani pamoja na Waheshimiwa Wabunge kwa ujumla kwamba katika kipindi ambacho Serikali imewahi kutenga fedha nyingi kuliko wakati mwingine wowote, ni sasa. Hivi ninavyozungumza, takribani Shilingi trilioni moja zinajenga viwanja vya ndege karibu vyote kwenye nchi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, moja, tumepokea ushauri wake mzuri kwa ajili ya kuweka moramu ili uwanja huu uendelee kutumika zaidi na ikizingatiwa ni jengo la ubia ambalo limejengwa na wenzetu wa Madini. Pili, namwomba pia awe na subira kidogo, tutakapokamilisha Uwanja wa Ndege wa Shinyanga, tutapima mahitaji makubwa yaliyopo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kahama halafu tuone ni hatua ipi ambayo inahitajika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, izingatiwe kwamba, tunapozungumza hapa hata maeneo mengine kwenye viwanja vya mikoa, kuna mahitaji makubwa ya fidia pamoja na viwanja hivyo vifanyiwe maboresho. Kwa hiyo, watupe muda kidogo, baada ya hapo tutaona cha kufanya kama Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, nampongeza kwa sababu amekuja na mawazo ya kimapinduzi. Anazungumza juu ya Halmashauri ya Kahama kwamba ni halmashauri kubwa ambayo inakusanya mabilioni ya pesa na anaomba kibali kwamba pengine waruhusiwe kufanya ukarabati. Kimsingi Serikali hii ya Awamu ya Sita inaunga mkono jitihada za halmashauri na Waheshimiwa Madiwani wa aina yake katika kuiunga mkono Serikali kusaidia maboresho mbalimbali ya viwanja vya ndege.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yetu chini ya Mheshimiwa Waziri Mbarawa pamoja na Mamlaka yetu ya Viwanja vya Ndege haitakuwa kikwazo, bali itakuwa msaada katika kurahisisha azma yenu hiyo kutokana na umuhimu mkubwa ambao mmeuona endapo mtatenga fedha kwa ajili ya kufanya maboresho.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Mara ni mkoa wenye historia katika nchi hii, kwani anatoka Muasisi wa Taifa letu Baba Julius Kambarage Nyerere. Tumeona mkiwa mnamuenzi kwa matembezi na kwa vitu mbalimbali. Sisi watu wa Mkoa wa Mara, moja ya kumuenzi Baba wa Taifa ni kuhakikisha mnakamilisha Uwanja wa Ndege wa Musoma kwa kiwango cha lami. Ni lini mtatenga fedha za kutosha kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Musoma unakamilika? Wabunge tumechoka kushukia Mwanza.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Ester Bulaya kwa swali lake ambalo ameuliza kwa umakini mkubwa. Serikali hii ya Awamu ya Sita inatambua, inazingatia na inafahamu umuhimu wa Baba wa Taifa. Pia inatumbua umuhimu wa viwanja vya ndege nchi hii, ndiyo maana pamoja na viwanja vyote nilivyosema vinaendelea kujengwa na kukarabatiwa, Uwanja wa Ndege wa Musoma upo, umeshatengewa fedha na unajengwa. Hivi ninavyozungumza, upo 60%. Labda ninachoweza kumhakikishia, ni kuiagiza mamlaka inayosimamia iharakishe ujenzi huo ukamilike ili uweze kuanza kutumika.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ya kutia matumaini, naomba kuuliza. Swali la kwanza; je, Serikali au Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kutaja kiwango kilichotengwa kwa ajili ya kuanza kazi hii ya kufunga taa katika Kiwanja cha Ndege cha Mafia? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa Uwanja wa Ndege wa Mafia licha ya kwamba hauna taa lakini una uwezo wa kuruhusu ndege kubwa kutua na kwa kuwa Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye Shirika letu la Ndege ATCL. Je, ni lini Shirika la ATCL litaanza safari ya kwenda Mafia ili kuwawezesha watalii hasa kipindi cha Mwezi wa Kumi mpaka wa Tatu ambapo utalii wa samaki mkubwa anayepatikana kwenye nchi sita tu hapa duniani aina ya samaki potwe?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa jinsi anavyojenga hoja kuhusiana na Uwanja wa Ndege wa Mafia na nimhakikishie swali lake la pili kwamba tumeshaanza tathmini ya kina kufahamu mahitaji na habari za kutosha kuhusiana na Uwanja wa Mafia na tukikamilisha tutapeleka Ndege ya ATCL.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza kuhusiana na habari aliyozungumza, kwanza nimkumbushe Serikali inafahamu umuhimu mkubwa sana wa Kiwanja cha Ndege cha Mafia kilichojengwa miaka mingi iliyopita kuanzia wakati wa mkoloni na tumefanya kazi kubwa pale. Tulirekebisha runway tukajenga ambayo ina urefu wa mita 1,500 na upana wa mita 30, tukaongeza eneo la kuegesha ndege kiasi kwamba ndege sita ndogo Caravan C208 zinaweza kutua pale. Kama hiyo haitoshi, tunapozungumza hapa tunafanya usanifu kwa ajili ya kuongeza jengo la abiria ili liwe na uwezo wa kubeba abiria zaidi kwa sababu jengo lililopo linabeba abiria 50.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, katika mwaka huu wa fedha nimeshamtamkia, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia inao mpango na inakwenda kuweka taa za kuongozea ndege katika kiwanja hicho. Atupe muda tu tutakwenda kukamilisha.
MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Naibu Spika, Uwanja wa Ndege wa Kahama unapokea watu zaidi ya 200 kwa siku. Je, Serikali ina mpango gani wa kuupanua na kuujenga kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Uwanja wa Kahama ni moja ya viwanja muhimu kwa Taifa letu na kwa kushirikiana na wadau tumeshajenga jengo la abiria zuri sana. Tuko kwenye hatua za tathmini ili kuhakikisha kwamba tunajenga njia kwa ajili ya kuruka na kutua ndege.
MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Waziri ametueleza kwamba Uwanja wa Ndege wa Kahama uko kwenye process, sasa ni lini wakati wanasubiri mchakato huo wataanza kuleta safari za Ndege za ATCL ambazo zitatua Kahama? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ameleta kama ushauri, tumepokea.
MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; Meli ya MV Victoria husafirisha abiria kwa madaraja matatu, daraja la tatu, daraja la pili na daraja la kwanza. Mimi nilisafiri na meli hiyo kupitia daraja la kwanza, nikalala usingizi nilipoamka saa saba badala ya watu wawili nilikuta tupo watu sita. Sasa napenda kujua ni taratibu gani zinatumika ili hao watu wa TASAC au kama ni Marine Service wanahakikisha usalama wa abiria kwa kufuata taratibu zilizowekwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; huko nyuma Afisa Kazi wa Mkoa alikuwa katika daraja la kwanza kwenye meli, alifuatwa ndani ya meli, akachukuliwa na akatupwa ndani ya maji akafariki. Je, Marine Service au kama ni TASAC sasa wako tayari kuweka ulinzi thabiti ndani ya meli kuhakikisha kwamba kunakuwa na usalama wa kutosha hasa ule usiku mkuu maana hii meli inasafiri usiku ndani ya maji? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpe pole Mheshimiwa Mbunge kama alivyoeleza kwa aliyoyasema Bungeni, lakini nimhakikishie na nitumie nafasi hii kutoa maelekezo maalum kwa Wakala wa Meli pamoja na TASAC kuhakikisha kwamba wanadumisha ulinzi na usalama kwa abiria kwa vyombo vyote majini siyo tu Ziwa Victoria na maeneo mengine yote ikiwemo Ziwa Tanganyika, Ziwa Nyasa na kwingineko kote.
MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa ujenzi wa bandari kavu ilikuwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Tatu Hayati Mheshimiwa Mkapa na kwa kuwa Serikali imesema haijakidhi vigezo, je, Serikali iko tayari kwenda kuwaelezea wananchi ili sasa wazo hilo lifutwe kwenye mawazo yao kwa sababu walikuwa wanasubiria?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, lengo hasa ilikuwa kuongeza uchumi kupitia shughuli za usafirishaji wa mizigo hasa kutoka Bandari ya Mtwara na kupitia Daraja la Mtambaswala lile la Umoja, je, Serikali inafikiria shughuli gani sasa ili kuweka shughuli mbadala katika lengo la awali?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mhata na Mheshimiwa Hokororo kwa maana ya swali lao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, unapojenga bandari kavu vipo vitu unavyovitazama na kikubwa tunaangalia shehena na ndio maana kwa sasa hivi ninapozungumza, Serikali ya Awamu ya Sita inajenga reli kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma, inaunganisha mpaka Burundi, lakini pia inajenga reli kuelekea Mwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ushoroba huu kilometa 2,300 tunajenga Bandari Kavu ya Kurasini, Bandari Kavu ya hapa Ihumwa - Dodoma, Bandari Kavu ya Fela kule Mwanza na Katosho, Kigoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hatua ya pili tukishatoka kwenye upande huu wa central corridor kwa maana ya CSGR Serikali inaendelea na mchakato kwa ajili ya kujenga reli ya kusini inayotoka kwenye bandari yetu ya Mtwara pamoja na Kisiwa Mgao, inaunganisha kwenda Liganga na Mchuchuma ambako kuna madini pamoja na makaa ya mawe, lakini inakwenda mpaka Mbamba Bay ambayo tayari ninavyozungumza mjenzi wa Bandari ya Bamba Bay yupo site. Sasa hii Bandari Kavu ya Nang’omba itakuwa ni bandari muhimu tukishafika hatua hiyo ili tutoe mzigo bandari tuupeleke Msumbiji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutauingiza katika mchakato huu wa southern corridor kuhakikisha kwamba na yenyewe inakuwa sehemu ya mradi wetu wa reli hiyo.
MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Je, Serikali inajua faida zitakazopatikana kutokana na ujenzi wa njia ya reli ya mwendokasi kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay Wilayani Nyasa? (Makofi)
(b) Je, ni kwa nini Serikali inachelewesha kuanza ujenzi wa njia ya reli ya mwendokasi kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kama nilivyosema kwenye swali la msingi, kwanza nianze kumshukuru Mheshimiwa Msongozi kwa sababu yeye pamoja na Wabunge wengi ambao nina uhakika watasimama tu kwa ajili ya kuhoji swali hili, wamekuwa wakihitaji kwa muda mrefu kuona SGR inajengwa kutoka upande wa Southern Corridor na Serikali inafahamu umuhimu wa jambo hili. Unapozungumza SGR ya Kusini lazima ufungamanishe Liganga na Mchuchuma pamoja na Bandari. Nini Serikali imefanya mpaka sasa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya kwanza tumekwishalipa fidia mwaka jana wananchi 1,142 takribani shilingi bilioni 15.4. Hii ni commitment ya juu kabisa ya kuona jinsi ambavyo tunataka jambo hili likamilike mapema iwezekanavyo. Hatua ya pili tumekwishaanza ujenzi wa bandari ya Mbamba Bay na hivi ninavyozungumza tupo hatua za mwishoni kuanza kujenga Bandari ya Kisiwa Mgao – Mtwara. Kwa sababu unapozungumza reli hiyo lazima uzungumzie namna ya kusafirisha chuma pamoja na makaa ya mawe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya tatu tunaboresha viwanja vya ndege kuanzia Njombe ambayo tupo kwenye usanifu wa kina lakini Mtwara pamoja na Lindi ambayo tunajenga pia kingine kipya. Kama nilivyosema hata katika bajeti hii tumetenga takribani milioni 702 yote hiyo ni kuelekea kuhakikisha kwamba tunafanya jambo hilo linakamilika mapema iwezekanavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hatua nyingine ambayo tunaifanya tunapojenga Reli ya SGR kutoka Dar es Salaam - Mwanza mpaka Kigoma takribani kilometa 2,102 hiyo ni kuonesha utayari wa Serikali katika kujenga Reli ya SGR Kusini. Kwa sababu unaanza hatua ya kwanza unamaliza hatua ya pili halafu unakwenda hatua zingine ambazo zinafuatia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyozungumza tayari tumejenga 2,102 reli kwa maana kama nchi na inakuwa ni nchi ya tano. Kwa hiyo, tukijenga na kilometa 1,000 na Mtwara Corridor 1,000 tutakuwa na 3,000 kama na mia tatu au na mia nne. Hivyo, tutakuwa ni nchi ya tatu duniani kwa kujenga reli ndefu zaidi na kwa nchi ya kwanza kwa nchi zinazoendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, faida zake kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge. Tuna faida nyingi ambazo tunazipata tukifanikiwa kujenga Reli ya Kusini kama nilivyosema Reli ya Kusini inafungamanishwa pamoja na Liganga na Mchuchuma ambayo Liganga na Mchumchuma tuna madini ya Vanadian, takribani pengine asilimia 0.4 kila mzigo unaopata pale ndani. Tuna vanadian na titanian ambayo inatengenezea engine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili inatusaidia kwenda kupata umeme megawatt 600 ambayo takribani 250 inakwenda kuyeyusha chuma na 350 inakwenda kuingia kwenye Gridi ya Taifa, nchi yetu ina changamoto ya umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi reli hii itatusaidia sasa kuchukua malighafi zile zote kwa maana ya Mchuchuma yale makaa ya mawe kusafirisha, kuyatoa pale yale yalipo kuyapeleka duniani yanapohitajika kwa wingi zaidi sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo taifa letu litapata fedha nyingi zaidi. Kama haitoshi pia itatuwezesha kufungamanisha nchi yetu kwenye viwanda, takribani milioni 2.9 ya chuma tutazalisha kwa mwaka wakati sisi mahitaji yetu tunakalibia milioni moja. Hivyo, basi niendelee kumuomba Mheshimiwa Mbunge, nafahamu yeye ni mkulima na angependa kujua faida kubwa ambazo zinapatikana kusafirisha mazao mbalimbali kwenye ukanda wa Kusini kupeleka nchi jirani na nchi za mbali kupitia reli hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niendelee kumuomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira wakati Serikali inakamilisha mchakato huu na hatimaye tutaenda kuanza ujenzi huo.
MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naomba kuipongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri juu ya mradi huu wa ujenzi wa reli kutoka Mtwara hadi huko Mbamba Bay. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, rai yangu kwa Serikali, kwa kuwa mmeamua ku-engage private partnership kushiriki katika mradi huu, mimi nawapongeza sana na naiomba Serikali iongeze jitihada ili reli hii iweze kufunguliwa na iwe mkombozi kwa wananchi wa Kusini hasa usafirishaji wa makaa ya mawe kutoka Liganga, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mhata kwa kutoa pongezi, wachache sana wakitendewa mambo mema wanasimama na kushukuru. Kwa hiyo nakushukuru sana Mheshimiwa Mhata kwa kuwa na moyo wa shukrani ambao utazidishiwa yaliyo mema zaidi. (Makofi)
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali haioni umuhimu wa kutengeneza baadhi ya mabehewa kuweka mfumo wa ubaridi (cold room) katika reli ya TAZARA ili tuweze kusafirisha parachichi zetu na mazao ya mboga mboga yamfikie mlaji wa mwisho yakiwa na ubora? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana dada yangu Mheshimiwa Mgaya kwa sababu ni mdau mkubwa sana wa reli ya TAZARA na tukubali ukweli kwamba kwa sasa katika reli yetu na mabehewa yaliyopo hatuna cold rooms, lakini kila mtu anafahamu umuhimu wa ukuwaji wa sekta ya parachichi katika mikoa ya Mbeya, Njombe, Iringa na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa unyenyekevu mkubwa Wizara tunapokea ushauri huu na tunapokwenda kwenye hatua ya pili ya maboresho makubwa ya reli yetu kutoka Dar es Salaam mpaka Kapiri Mposhi tutaona namna ya kuweza kuweka hicho alichokizungumza cha cold room.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Serikali imeboresha miundombinu ya Bandari ya Tanga kiasi kwamba shehena zimeongezeka, lakini reli ya kutoka Tanga kwenda Dar es Salaam na kutoka Tanga kwenda Arusha bado ni chakavu sana, je, kuna mpango wowote wa kuboresha reli hii ili sasa shehena hii iweze kutoka kwa urahisi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Shangazi, Mbunge wa Mlalo na Katibu wa Bunge la CCM kwa swali lake kubwa na zuri la maslahi ya watu wa Tanzania na watu wa Kaskazini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inao mpango mzuri na kabambe kwa sababu inatambua umuhimu wa upande wa Kaskazini kwanza kwenye utalii, kilimo pamoja na sekta nyingine, hivyo katika mwaka wa fedha 2023/2024 tumeshafanya kazi kubwa, tulishasaini mkataba wa kununua materials za kukarabati reli inayotoka Tanga kuelekea mpaka Arusha kilometa 533.
Kwa hiyo, mara baada ya kusaini mkataba huo katika mwaka wa fedha huu unaofuatia tunakwenda kuanza kutoa reli iliyokuwepo, tunataka tuweke reli nzito ambayo itakuwa na capacity ya ratilika 80 kwa yard, iliyokuwepo ilikuwa 45 kwa yard.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii reli iliyopo sasa hivi speed inayokwenda treni ni karibu speed ya 15 - 20 kwa saa moja, hivyo inawachukuwa muda mrefu sana kufika kwenye destination inayotakiwa. Tukifanya maboresho haya speed itaongezeka mpaka 75, kwa hiyo muda kama ilikuwa ni saa 12 tutakuwa tunatumia saa karibu nne. Kwa hiyo, habari njema hii kwa watu wa Kaskazini, Tanga na Watanzania kwa ujumla juu ya maboresho makubwa ya reli ya Kaskazini. (Makofi)
MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, pamoja na kazi nzuri inayofanywa na Wizara ya Uchukuzi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Mlimba usafiri wa reli ya TAZARA ndiyo usafiri unaotegemewa, sasa lini mpango wa Serikali katika kuboresha reli hii ikiendana sambamba na kuongeza mabehewa na route za safari ya reli hii kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, reli ya TAZARA kama inavyofahamika ilijengwa miaka 1975 baina ya Serikali tatu, China, Tanzania na Zambia na kipindi chote hicho designed capacity ilikuwa ni metric tons milioni tano, lakini kutokana na ubovu wa miundombinu hatukufikia lengo. Habari njema kutoka kwa daktari wa maendeleo Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Tanzania amefanya kikao na Waziri wa Zambia pamoja na Rais wa China, hivi ninavyozungumza tupo kwenye hatua za mwisho za majadiliano, reli nzima inakwenda kufumuliwa upya. Moja, kuongeza uwezo wa reli wa kubeba mzigo, lakini pili tutaongeza mabehewa pamoja na vichwa vya kutosha ya mizigo na abiria. Kwa hiyo, Wana-Mlimba na watumiaji wote wa reli hii inayotoka Dar es Salaam mpaka Kapiri Mposhi kilometa 1,860 waendelee kusubiri habari hii njema ambayo inakuja kwa Watanzania wote. (Makofi)
MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri mimi kwanza naipongeza Mamlaka ya Hali ya Hewa inafanya kazi nzuri sana ya kutoa tahadhari ya hali ya hewa ya nchi yetu na tahadhari ambazo ni za ukweli kwa asilimia kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa taarifa za hali ya hewa zinatolewa mapema sana, lakini Serikali haichukui hatua za mapema matokeo yake kunatokea madhara makubwa sana kama vile inaponyesha mvua kubwa katika maeneo mbalimbali. Je, mamlaka zinazohusika zina mpango gani sasa wa kuhakikisha wanafanyia kazi taarifa za hali ya hewa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa tumeshuhudia kunyesha kwa mvua kubwa katika maeneo na kusababisha mafuriko kama vile ya Rufiji, Kibiti, Kilwa, Lindi na Arusha - King’ori kulitokea mvua kubwa, madaraja yakavunjika mpaka gari la wanafunzi likaingia kwenye daraja.
Je, Serikali imejipanga vipi sasa kutoa taarifa pale inapotokea mvua inanyesha angalau kusimamisha masomo kwa wanafunzi wa shule za msingi na nursery school? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninamshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kutoa pongezi kwa Mamlaka yetu ya Hali ya Hewa kwa kazi kubwa ambayo wanafanya na hii ni kutokana na uwekezaji mkubwa sana ambao Serikali imefanya katika kuiwezesha mamlaka hii itoe taarifa sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, amezungumza kuhusu kufanyia kazi, Mamlaka ya Hali ya Hewa ina jukumu kubwa la kuangaza, kukusanya, kuchakata pamoja na kuhifadhi na kusambaza taarifa za hali ya hewa na mara baada ya kukamilisha jukumu hilo la kwanza, jukumu la pili ambalo linafanyika sasa ni namna gani taarifa hizo zinakwenda kuwafikia wananchi mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri tunayo sheria ya mwaka 2006 ambayo ni Sheria yetu ya TMA inaipa mamlaka kufanya kazi hiyo, lakini pia tuna Sheria ya Maafa Namba 6 ya mwaka 2022 ambayo kimsingi inatoa nafasi kwa Kamati zetu za Maafa mbalimbali nchi nzima. Mara baada ya kupokea taarifa za TMA, kuhakikisha kwamba zinasambazwa na kufikishwa katika maeneo mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo Serikali kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali imeendelea kutoa elimu mbalimbali kwa wananchi kupitia vyombo vya habari, kuimarisha mifumo yetu ya tahadhari pamoja na kujenga uwezo wa watendaji ili kuhakikisha kwamba taarifa zinakuwa sahihi, lakini pia zinafika kwa wananchi wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru pia kwa swali lake la pili juu ya ushauri alioutoa kwamba pengine inapotolewa taarifa hizo za hali ya hewa pengine kutakuwa labda na kimbunga na kadhalika, ni vyema shule zikafungwa. Ushauri huu ni mzuri na sisi kama Serikali tumeupokea, tutaenda kuuchakata na kuufanyia kazi hatua kwa hatua. (Makofi)
MHE. BAKAR HAMAD BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru, ni kweli kwamba Mamlaka yetu ya Hali ya Hewa inafanya kazi nzuri hivi sasa kutokana na uwekezaji mkubwa ambao Mheshimiwa Rais ameuwekeza, lakini kumekuwa na changamoto kwa wadau na taasisi mbalimbali zinazotumia taarifa hizi, kuchelewesha malipo kwa mamlaka yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni ipi kauli ya Serikali kuhusiana na taasisi hizi ambazo zinachelewesha malipo baada ya kutumia taarifa za hali ya hewa ili taarifa zetu za hali ya hewa ziendelee kuwa endelevu na bora zaidi? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru Mheshimiwa Bakar kwa swali lake la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninatumia nafasi hii kuomba taasisi mbalimbali ambazo kimsingi ni wanufaika wa taasisi hii au taarifa za taasisi hii ili waweze kulipa ndani ya muda kwa ajili ya kusaidia mamlaka yetu ipate fedha na kuongeza uwezo zaidi, iweze kutengeneza au kuandaa taarifa zingine sahihi zaidi kuliko pengine livyokuwa hapo mwanzoni. (Makofi)
MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza namshukuru Waziri wangu wa Miundombinu kwa majibu yake mazuri aliyoyatoa sasa hivi, yana kina ndani yake. Kama ingelikuwa sitaki kumwuliza swali lingine, basi ilikuwa mimi niseme basi, maana nimeridhika nalo, lakini nina swali moja dogo la nyongeza nimpe Waziri wangu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Serikali imejenga meli Maziwa Makuu, je, ni lini itajenga meli ya baharini kwa ajili ya abiria na mizigo ikiwemo kwenda Zanzibar? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, kwanza Serikali inamiliki meli pamoja na Serikali ya China kwa hisa ya 50% kwa 50%, ambayo ilijengwa mwaka 1967. Kwa sasa kutokana na umuhimu mkubwa wa usafiri kwenye Mwambao wa Pwani, kwa maana ya Malindi, Comoro, Tanga, Pwani, Zanzibar na maeneo mengine, Serikali ipo kwenye hatua ya upembuzi yakinifu katika mwaka huu wa fedha 2023/2024 ili kufahamu gharama, wahitaji na fursa zilizopo katika bahari yetu, hatimaye kuweza kuanza kununua meli hizo.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Wananchi wa Mkoa wa Geita wanategemea Bandari ya Mwanza na Bukoba. Sasa Mkoa wa Geita unakua na unajitegemea; tunalo eneo zuri kabisa la bandari ambayo haijaboreshwa ya Nkome ambayo ingetumika kushusha mizigo kutoka Kenya na Uganda. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiboresha Bandari ya Nkome ili wananchi wa Mkoa wa Geita tuweze kuitumia kushusha mizigo yetu kutoka nje? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, tayari Serikali inafanya maboresho makubwa kwenye Ziwa Victoria kwa namna mbili; moja, tunajenga Bandari ya North Mwanza, Bandari ya Kemondo na Bandari ya Bukoba pamoja na kununua meli mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, baada ya kukamilisha hatua hiyo, tutakwenda kwenye hatua ya pili ya kutazama maeneo mengine kulingana na uhitaji wake ambayo ni pamoja na eneo la Nkome ambalo Mheshimiwa Mbunge ameulizia.
MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote ninashukuru sana kwa hatua iliyofikiwa na maelezo ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyatoa. Kwa namna ya pekee tunashukuru sana Mheshimiwa Rais kwa sababu hii ilikuwa ni ahadi aliyoitoa kwa Wana-Njombe alipotutembelea mwaka 2021.
Mheshimiwa Naibu Spika, nina swali moja la nyongeza. Kwa vile Mji wa Njombe unakua kwa haraka na sasa mapendekezo ya kuwa manispaa yana ngoja maamuzi ya Serikali na kwa vile pressure ya ardhi katika Mji wa Njombe ni kubwa sana, eneo hilo lipo katikati kabisa ya mji. Je, Serikali inaweza kufikiria kulirudisha eneo hilo kwa halmashauri yetu ya mji ili tuweze sasa kufanya matumizi mengine ambayo ni ya muhimu sana kwa shughuli za kijamii? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Deo Mwanyika kwa ufuatiliaji wake wa karibu wa Uwanja wa Ndege wa Njombe ambao kama nilivyoeleza ni muhimu sana kwa maslahi ya mkoa huo na maeneo ya nyanda za juu kusini kwa ujumla. Pili, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa Mnyaa nipokee shukrani alizozitoa kwa Serikali ya Awamu ya Sita ambayo inaahidi na kutekeleza. Hoja yake ya mwisho amezungumzia kuhusiana na kuomba eneo hilo ambapo tutakapohamisha uwanja kama lingeweza kutumika kwa ajili ya maslahi ya wananchi wa Njombe.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka jana Bunge lako Tukufu lilipitisha Sheria Namba 108 ya mwaka 2024 ambayo pamoja na mambo mengine imetoa mwongozo wa namna ya kufanya uendelezaji wa rasilimali za viwanja vya ndege nchini. Hivyo, mara baada utakapokamilisha uhamishaji wa kiwanja hicho Mamlaka ya Viwanja vya Ndege itaweka mfumo mzuri wa kukaribisha wawekezaji wa ndani na wa nje ikiwemo mwananchi mmoja mmoja pamoja na halmashauri hivyo, nitamwomba na yeye Mheshimiwa Mwanyika pamoja na halmashauri muda ukifika basi waweze kuchangamkia fursa hiyo ili kuendeleza eneo hilo kwa maslahi ya wananchi na nchi yetu.
MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Uwanja wa Ndege wa Bukoba unaweza uka-accommodate ndege ndogo, lakini tuna abiria wengi sana. Ni lini sasa Serikali itajenga uwanja mkubwa na wa kisasa wa kimataifa wa Bukoba? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa Mkoa wa Kagera kuwa na uwanja mkubwa ambao utaweza kuendana na mahitaji ya sasa. Awali tulipanga kufanya maboresho katika uwanja ule uliopo ikiwa ni pamoja na kujenga jengo la kuongozea ndege pamoja na kuweka taa, lakini baada ya kubaini umuhimu mkubwa Serikali imeanza mchakato wa kutafuta eneo lingine. Tayari eneo limeshapatikana tumeanza taratibu za awali ili kujenga uwanja mkubwa ambao utakuwa ni wa kisasa na utaweza kusaidia shughuli mbalimbali za Mkoa wa Kagera na wilaya zake.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Uwanja wa Ndege wa Musoma umekuwa ukipewa ahadi kwa muda mrefu kukamilika kwa kiwango cha lami na kama mnavyojua Mkoa wa Mara ni mkoa ambao umeshiriki katika harakati za nchi hii, anakotokea Baba wa Taifa, ili kumuenzi ni lini watakamilisha Uwanja wa Ndege wa Musoma kwa kiwango cha lami? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa Uwanja wa Ndege wa Musoma siyo tu kama alivyozungumza Mheshimiwa Mbunge kwa maana kama kumuenzi Baba wa Taifa, lakini pia huko ndiko kuna utalii kwa wingi lakini shughuli za madini pamoja na shughuli za uvuvi. Hivyo basi, ninataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunaendelea na mchakato wa kukamilisha taratibu za ndani kwa maana ya kuwalipa wakandarasi ili ujenzi huo sasa uweze kuendelea na ninakuhakikishia kwamba utakamilika na utakwenda kuwanufaisha wananchi wa mkoa huo.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru sana kwa majibu mazuri ya kuanza kutenga fedha ya kutengeneza hii barabara kwa sababu imekuwa ya muda mrefu. Hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; je, lini Barabara ya Mahenge – Liwale – Nachingwea mpaka Masasi ambayo ina umuhimu kwa sababu inaunganisha mikoa mitatu ambayo ni Mkoa wa Morogoro, Mkoa wa Lindi na Mkoa wa Mtwara itaanza kujengwa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; swali hili la pili huwa ninaliuliza mara kwa mara humu Bungeni, lakini bado sijapata majibu sawasawa ni kipande cha Kilosa – Mikumi na kipande cha Turiani - Mziha ni lini vitaanza kujengwa ili kusudi kuunganisha Barabara ya kutoka Tanga kwenda mpaka Morogoro na kwenda kwenye Mikoa ya Kusini? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Mahenge – Liwale - Masasi ni barabara ambayo kwa sasa kimsingi haipo, lakini tulitenga katika mwaka huu wa bajeti na nimelijibu kama siyo jana ni juzi hili swali kwamba sisi kama Wizara tumeshatenga fedha kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu wa hiyo Barabara. Nilisema pia ninaendelea kusema kwamba, kwa kuwa ni barabara yote inapita kwenye Mbuga ya Selous kwa maana ya Mwalimu Nyerere tuna wadau wengi ambao tunashirikiana nao ili kufanya usanifu wa barabara hiyo kabla hatujaanza kuijenga. Kwa hiyo, sisi kama Wizara tumeshatenga fedha na taratibu zimeshaanza ya kufanya upembuzi yakinifu na kuona uwezekano wa kuijenga barabara ambayo itaunganisha Mikoa ya Kusini na Morogoro.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la pili kuhusu Barabara ya Kilosa - Mikumi. Barabara ya Kilosa - Mikumi itakuwa ndiyo mwendelezo wa barabara ambayo ndiyo iliulizwa kwenye swali la msingi kutokea Songea – Ifakara kuja Mikumi, lakini watu hawa wanapokuja huku wangependa wapitie kuja Kilosa kwa ajili ya kuja Dodoma. Tayari Barabara hii imeshafanyiwa usanifu na tumeshaanza kujenga kwa awamu. Kwa mfano, kutoka Dumila mpaka Kilosa tayari na sasa hivi tunatafuta fedha ya kujenga Kilosa kuja Mikumi ili sasa tuweze kuunganisha Mikumi na Kilosa kwa kiwango cha lami. (Makofi)
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya Serikali ya kujenga kipande cha Barabara ya lami kilometa 10 kutoka Waso kwenda Loliondo Wilaya ya Ngorongoro, Mkoa wa Arusha lakini mpaka sasa ahadi hii haijatekelezwa. Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi hii kwa wananchi wa Ngorongoro? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli usanifu ulishakamilika na maelekezo yalishatoka kutoka kwa Makamu wa Rais kwamba barabara hiyo ijengwe na tumeshakamilisha taratibu zote. Kwa hiyo, sasa hivi tunatafuta fedha kumlipa mkandarasi malipo ya awali ili kipande hicho cha kilometa kumi kiweze kujengwa. Ahsante.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami kilometa 22 za Barabara ya Isyonje Kikondo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya kutoka Isyonje kwenda Kikondo aliyoitaja ni barabara ambayo inaunganisha Mkoa wa Mbeya na Mkoa wa Njombe na haiishii Kikondo; kimsingi inakwenda Makete. Katika barabara hii barabara yote yenye kilometa karibu 96.4 imeshafanyiwa usanifu, na tumeshaanza kuijenga kwa kiwango cha lami.
Mhesimiwa Naibu Spika, Serikali tuliamua tujenge eneo ambalo ni korofi (eneo la katikati) ni eneo la Kitulo kwenda Iniho katika ile Mbuga ya Kitulo. Kwa hiyo, tumeshaanza na mkandarasi yuko site. Wakati tunatafuta fedha ya kukamilisha vipande vingine kwa Mkoa wa Mbeya na upande wa kutokea Makete. Ahsante.
MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Kolandoto kwenda Mhunze ambayo ni Makao Makuu ya Wilaya ya Kishapu ni barabara ambayo ipo katika mpango wa bajeti ya mwaka huu ambao tunakwenda kuumaliza na katika Bunge liliopita nilipata majibu ya Serikali kwamba barabara hiyo inaenda kutangazwa na kimsingi imo kwenye bajeti hii. Sasa nataka nipate majibu ya Serikali ni lini sasa barabara hii inaenda kutangazwa na kuanza kutekelezwa? Ninakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumepanga iko kwenye utaratibu wa kuanza kujengwa hiyo barabara ambayo ni sehemu ya barabara zetu kuu katika nchi yetu. Tunachosubiri sasa hivi ni kuitangaza hiyo barabara kama tulivyokuwa tumeipanga kwenye mpango wa bajeti ya mwaka huu wa fedha.
MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa hii barabara inayotoka Namtumbo kupita Malinyi mpaka Ifakara Serikali imetwambia itajengwa kwa awamu. Je, kwa wakati huu inaweza ikatufungulia kusafirishia wakati inajengwa kwa kiwango cha lami basi angalau tuwe tunapita kuitumia njia hiyo kwa kiwango hicho cha changarawe?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara ilikuwa imetangazwa yote. Kwa hiyo, tulitegemea mkandarasi ambaye angekuwepo angeweza kuwa anaifanyia matengenezo. Baada ya kufanya utaratibu tumeshawaagiza Mameneja wa Mikoa ya Ruvuma na Morogoro kuhakikisha kwamba kile kipande ambacho kitajengwa ataendelea na mkandarasi, lakini vipande vilivyobaki ma-regional managers wa-TANROAD wahakikishe kwamba wanazikarabati kupita kipindi chote cha mwaka. Kwa hiyo, kwa kiwango hicho cha changarawe kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge wa Namtumbo.
MHE. JOSEPHINEN J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali itajenga Barabara ya kutoka Kitanga – Kigadye – Helushingo - Nyarugusu mpaka Makere kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa barabara hii ya mpakani kati ya Tanzania na Burundi inafanyiwa usanifu, lakini kilichofanyika kwa sasa ni kuunganisha kwanza Wilaya ya Kasulu na Wilaya ya kibondo ambapo Daraja lililokuwa la Malagarasi ndilo linahamishiwa pale na mkandarasi yuko site. Sasa wakati tunajiandaa kutafuta fedha baada ya kukamilisha usanifu kuweza kuijenga kwa kiwango cha lami na hasa tukizingatia hilo eneo ndiko kuna shamba kubwa na kiwanda kikubwa cha miwa, pia ni barabara ya mpakani.
MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na nishukuru kwa majibu ya Serikali. Hata hivyo, nisikitike tu kwamba majibu haya yamekuwa kila siku yakitia faraja kwamba zitaanza, zitaanza kwa sababu hii ni mara ya tatu nauliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mara ya kwanza walisema wanasubiri ndege ikija. Ikaja ile ndege, lakini hawakubadilisha route, imekuja nyingine hawakubadilisha na leo wanasema mpaka Desemba, 2025.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tukumbuke kwamba Uwanja wa Ndege wa Mwanza ni lango la Miji ya Maziwa Makuu na Makau Makuu sasa hivi Dodoma. Ili kurahisisha pia mawasiliano, hawaoni kama ni usumbufu wa watu kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam halafu wanakuja Dodoma wakati Mwanza pia ni Mji ambao ni wa pili kwa ukuaji wa uchumi na unazalisha sana na abiria wengi wanatoka Kanda ya Ziwa? Swali langu la kwanza; ni lini kwa uhakika usafiri huo utaanza? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; tunayo mashirika mengi ya binafsi ya ndege yakiwemo haya ya AURIC ana ndege ndogo na wanaweza kuwa pia na ndege kubwa; tunayo Coastal line na tunayo pia Precision. Je, Serikali haioni ni muda muafaka sasa wa kuzungumza nao ili waweze kuwa na ndege kubwa zitakazoweza kufanya kazi hiyo kama tulivyoomba, Mwanza – Dodoma, Dodoma - Arusha, Dodoma – Mbeya na mambo mengine kama hayo ili kukuza uchumi wa Taifa hili katika usafiri wa anga? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Dkt. Mabula kwa ufuatiliaji wake kwenye upande wa ATCL, lakini nimhakikishie kwamba, Serikali hii imefanya jitihada kubwa sana ya kuongeza au kuboresha usafiri nchini. Sote ni mashahidi, miaka tisa nyuma tulikuwa na ndege moja tu. Serikali imenunua ndege zimefika 16 ikiwemo ndege ya mizigo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji ni makubwa. Hivi ninavyozungumza hapa, tunaboresha viwanja vya ndege ambavyo havijakamilika karibu nchi nzima. Vitakapokamilika nina uhakika Wabunge wa maeneo hayo nao watakuwa wakisimama hapa wanahitaji ndege. Kwa hiyo, nichukue ushauri wake wa pili alioutoa Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa mashirika binafsi yote yanayo-operate, yaliyopo ndani ya nchi yetu pamoja na nje ya nchi yetu ili kutazama fursa ambayo Serikali imewekeza kwenye kujenga miundombinu ya viwanja vya ndege karibu kila mkoa, waone namna gani wanaweza kuleta ndege zao ili kuboresha usafiri, lakini na wao watafanya biashara.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itapeleka usafiri wa ndege kuanzia Dodoma – Tabora mpaka Kigoma? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inamhakikishia Mheshimiwa Genzabuke na Wabunge wote itapeleka ndege katika maeneo mbalimbali nchini baada ya kukamilisha manunuzi kulingana na upatikanaji wa fedha.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kuhusu swali nililouliza bado narudi kwa Serikali kuiuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kutokana na kwamba Uwanja wa Ndege wa Urambo upo katikati ya Mji na umuhimu wake kwa ajili ya dharura ya ndege kutua pale na kadhalika, kweli Serikali yetu ilivyo makini inaweza kushindwa kuweka uzio ili kuutunza uwanja wenyewe lakini pia kwa ajili ya usalama wa wananchi? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, kwa jinsi ilivyo makini Wizara ya Uchukuzi, kweli imeshindwa kuweka watu wa kufanya usafi ili na sisi mji wetu upendeze? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, kupitia Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa Mbarawa nimpongeze sana Mheshimiwa Mama yetu Sitta kwa ufuatiliaji mkubwa anaoufanya wa shughuli za maendeleo katika eneo lake na pia, kwa kutambua kwamba Serikali hii ni makini. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Mama yetu Sitta kwamba Serikali kama nilivyosema ni makini na inao mpango huo, lakini atupe muda tu kama nilivyokuwa nimeeleza kwenye jibu la msingi.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na jambo la pili la usafi. Ninamwelekeza Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege kupitia timu yake waende kwenye eneo hilo na waendeleze programu ya kufanya usafi ili uwanja huo uweze kuwa msafi. (Makofi)
MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, Mtwara ni Mji ambao unakua na tukilinganisha tupo mpakani mwa Msumbiji na Comoro. Ni lini Serikali itatujengea meli kwa jili ya kuendelea na suala letu la kibiashara Mtwara - Comoro na Mtwara – Mozambique. Ahsante sana. (Makofi)
SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, sijamsikia vizuri, anazungumzia meli siyo?
MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, ninazungumzia meli.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, okay. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Mtenga anavyofuatilia maendeleo katika Jimbo lake. Serikali inajenga meli mbalimbali katika Maziwa Makuu na hivi mwezi uliopita imekamilisha mpango wa kumkabidhi msanifu. Tumeshaanza usanifu wa kina na upembuzi yakinifu kwenye Bahari ya Hindi ili tuanze kujenga meli ambayo itakuwa inafanya shughuli zake kwenye Mwambao wa Bahari Hindi ikiwemo Mtwara, Lindi, Tanga, Zanzibar na maeneo mengine yote ambayo yanapakana na Bahari hiyo.
MHE. PRISCUS J. TARIMO: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana. Ni lini Serikali itakamilisha ukarabati wa Uwanja wa Ndege wa Moshi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimshukuru Mheshimiwa Tarimo kwa ufatiliaji na yeye ni shahidi tulikuwa wote kutembelea uwanja huo hivi majuzi kwenye eneo hilo. Tunaendelea na taratibu mbalimbali za ndani ili kuweza kumlipa Mkandarasi aweze kuendelea na hatimaye akamilishe ujenzi wa uwanja huo wa Moshi ambao ni muhimu sana kwa maslahi ya nchi yetu. (Makofi)
MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, Uwanja wa Ndege wa Iringa umewekewa uzio na una usalama wa kutosha, lakini ndani ya ule uwanja kuna Shule ya Msingi inayotumika. Je, watatusaidiaje ili kuondoa watoto mle ndani kwa sababu ndege kubwa zimeanza kushuka pale?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Iringa Mjini kwa ufuatiliaji wake makini wa Uwanja wetu wa Iringa. Ninataka nimhakikishie kwamba taratibu mbalimbali zinaendelea kufanyika ili kuhakikisha jambo hilo linafanyika kwa kuzingatia sheria na taratibu za nchi yetu.
MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Wilaya ya Muleba ina visiwa vingi na tumekuwa tukitegemea Meli ya Clarious kutoa huduma ambayo si salama kwa kipindi hiki. Swali la kwanza; je, Serikali ina mpango gani wa kutupatia vyombo salama na imara kwa ajili ya kuhudumia watu wetu wa Muleba?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Mheshimiwa Waziri Mkuu alipotembelea Wilaya ya Muleba mwaka juzi alitoa maelekezo TPA kujenga bandari ndogo ya Katembe Magarini. Je, lini TPA ina mpango wa kutekeleza hilo agizo? Ninashukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Kikoyo pamoja na Mheshimiwa Mwijage kwa sababu wamekuwa ni Waheshimiwa wanaofuatilia kwa ukaribu sana maboresho makubwa sana ya kibandari katika ziwa letu, Ziwa Victoria ambayo ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, ninapenda kumfahamisha Mheshimiwa Kikoyo kwamba Serikali imefanya mambo mengi katika Ziwa Victoria ili kuimarisha usalama na kuhakikisha kwamba usafiri unaokuwepo unakuwa ni wa uhakika. Kwa awali ninapenda kumhakikishia na kumweleza kwamba tayari Serikali imefanya maboresho ya kujenga bandari tatu ikiwemo Bandari ya North Mwanza, Bandari ya Kemondo na Bandari ya Bukoba. Bandari ya Kemondo imekamilika North Mwanza pamoja na Bukoba zinaendelea. Hiyo ni hatua ya kwanza ya kuhakikisha kwamba usafiri kwenye ziwa hilo unakuwa ni wa uhakika na wenye usalama.
Mheshimiwa Spika, pili, Serikali imechukua jukumu kubwa ya kujenga vituo mbalimbali vya uokoaji katika Ziwa Victoria. Vingine vimejengwa Sengerema, vingine Victoria pale, kwa maana ya Mwanza na Geita na maeneo mengine. Aidha, tayari Serikali imetenga fedha za kutosha na tupo kwenye hatua za mwisho wa kujenga meli kubwa MV Mwanza Hapa Kazi Tu ambayo tunategemea itakamilika siyo muda mrefu kuanzia sasa. Itakapokamilika hiyo itakuwa imaimarisha usafiri wa uhakika kati ya Mwanza, Bukoba kwa maana ya Mkoa wa Kagera, pamoja na maeneo kama Port Belly na maeneo mengine ambayo yanazunguka kwenye ziwa hilo.
Mheshimiwa Spika, ukija kwenye hoja yake ya visiwa vile vya kawaida alivyovisema ikiwa ni pamoja na vilivyopo katika eneo la Muleba, tayari Serikali inatambua umuhimu wa meli hiyo kuwepo, ambayo ni ya Serengeti. Tumekwishaanza utaratibu wa kuainisha mahitaji, kwa sababu meli hii ilisimama 2019 lengo letu tutazame mahitaji ni kiasi gani tuikarabati na ianze kufanya kazi ambayo itakwenda kwenye visiwa vidogovidogo ikiwa ni pamoja na ambavyo Mheshimiwa Kikoyo amevisema.
Mheshimiwa Spika, pamoja na hilo tayari meli ya mizigo ya ML Wimbi ambayo ambayo yeye anaifahamu ambayo inabeba mizigo midogomidogo, ikiwemo bidhaa za dukani pamoja na dagaa na vitu vingine vingine iko mwishoni ikikamilika itakwenda pia kwenye eneo hilo la Muleba kwa ajili ya kuhakikisha tunawasaidia wananchi wetu hao.
Mheshimiwa Spika, swali lake la pili amezungumzia kuhusu agizo la Mheshimiwa Waziri Mkuu. Wizara yetu inatekeleza maelekezo ya viongozi wakuu wote kwa msisitizo na uzito unaostahili, ikiwa ni pamoja na maelekezo ya Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mheshimiwa Waziri Mkuu, pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Spika, na kwa kuanzia tayari tumeshaanza mchakato kwa ajili ya kuhakikisha tunatazama namna ya kuweka kwenye bajeti ijayo. Hata hivyo ikumbukwe kwamba nchi hii ina bandari 693, uwezo wa Serikali kuanza kuzijenga zote kwa wakati mmoja hauwezekani. Tunaanza kidogo na tumeshaanza kurasimisha mpaka mwaka 2021 tulikuwa tumerasimisha bandari 80 na Mheshimiwa Dkt. Samia suluhu Hassan amekwenda kwa kasi kubwa zaidi zimeongezeka zaidi ya bandari 50. Hivyo nimuombe awe na subira tutajitahidi hatua kwa hatua na kwake tutamfikia tena. Ahsante.
MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, lini ujenzi wa Bandari ya nchi Kavu ya Gungu Mjini Kigoma utaanza kwa sababu Serikali imekuwa ikiahidi kwa muda mrefu sasa?
SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu kwa kifupi.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, samahani nilikuwa sijasikia bandari gani?
SPIKA: Bandari kavu.
MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, bandari ya nchi kavu Gungu Mjini Kigoma.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, Serikali kwa Kigoma inafanya mpango wa kujenga bandari kavu iliyopo Kigoma mjini ili kuunganisha kati ya nchi yetu na nchi jirani. Hii aliyoitaja ninaomba nichukue na tuanze kulifanyia kazi kulingana na mahitaji sambamba na uwepo wa fedha.
SPIKA: Mheshimiwa Kavejuru hiyo uliyoitaja iko jimbo gani?
MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, iko Jimbo la Kigoma Mjini na tayari Serikali ilikwishaweka fensi kwa muda mrefu na ilipa fidia wananchi waliokuwa wanaishi pale wakaondoka kabisa kwa muda mrefu, zaidi ya miaka 10 sasa; na pana fensi. Sasa kwa muda mrefu wananchi wa Kigoma wamekuwa wakisubiri ujenzi wa bandari hiyo ya nchi kavu mpaka sasa hivi hakuna kitu kinachoendelea.
SPIKA: Haya ahsante sana. Sasa umepata ufafanuzi Mheshimiwa Naibu Waziri ni hiyohiyo ya mjini uliyoijibia, ndiyo hiyohiyo na yeye anayoiulizia ahsante sana.
MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninashukuru sana na kuipongeza Serikali kwa kuwa juhudi za kujenga uwanja wa ndege ndani ya Wilaya ya Misenyi ambayo ulikuwa ni wa Omukajunguti ni za muda mrefu, lakini Serikali kama inavyosema kupitia Kamati maalumu iliweza kubaini eneo lingine ambalo ni karibu na eneo la awali la Omukajunguti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; wananchi ambao walikuwa katika maeneo ya Omukajunguti walisimamishwa kufanya shughuli za uendelezaji na za kiuchumi katika maeneo yao kwa muda mrefu na kimsingi walikuwa wameshafanyiwa na tathmini kulipwa fidia kupisha ujenzi wa uwanja wa ndege. Sasa, ni nini tamko la Serikali kwa wananchi hao kuhusiana na maeneo yao ili waweze kuyaendeleza katika shughuli zao za kiuchumi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa eneo la Kihabajwa linakaribiana na maeneo yanayomilikiwa na wananchi lakini mengine yanamilikiwa na Serikali zetu za vijiji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni nini mkakati wa Wizara yetu ya Uchukuzi kushirikiana na Wizara ya Ardhi na uongozi wa Mkoa na Wilaya ya Misenyi kuhakikisha kwamba tunafanya mipango miji vizuri kupima maeneo hayo, ili kuweza kuwa na maeneo ambayo yamepimwa ili kuleta kivutio pindi uwanja wa ndege utakapojengwa na maeneo ambayo yanazunguka uwanja huo yawe na yenyewe yana hadhi kama uwanja huu utakavyojengwa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, kwa maelezo yake mazuri aliyoyatoa ya kuipongeza Serikali yetu kwa jitihada ambazo tunazifanya, lakini ninampongeza kwa sababu ya uhamasishaji mkubwa ambao amekwishaanza kuufanya ikiwa ni pamoja na kuwaanda wananchi juu ya mradi mkubwa wa kiwanja cha ndege utakaojengwa katika eneo la Kihabajwa ambao haujawahi kutokea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kazi nzuri ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye baada ya kuona umuhimu wa mkoa huo kiuchumi pamoja na sekta nyingine akaelekeza Wizara yetu kwamba, uwanja mnaotaka kuendelea kuuboresha hapana, ninataka ujengwe uwanja mkubwa utakaoendana na mahitaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lake la kwanza alilouliza, je wananchi wanaruhusiwa kuendeleza maeneo yao? Jibu ni ndiyo, kwa kuwa tayari tumeshakubaliana kwamba tutakwenda kujenga Kiwanja cha Ndege cha Kihabajwa, maana yake hili eneo la awali halitatumika tena kwa ajili ya jambo hili. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lake la pili anauliza mpango wa Serikali. Ninapenda kumhakikishia na bahati nzuri nami nimekwenda eneo hilo nilikuwa na yeye mwenyewe na anafahamu kidogo. Sema hapa ninataka nchi nzima iweze kufahamu, tayari Serikali yetu kupitia Wizara ya Uchukuzi, ikishirikiana na Ofisi ya Mkoa kupitia Mamlaka yetu ya Viwanja vya Ndege, imekwishawasiliana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kuanza mpango wa upimaji ili kuweza kuboresha eneo hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo ni nini? Moja, ni kuhakikisha kwamba maeneo jirani na uwanja wa ndege yanakuwa na mandhari mazuri; lakini pili, kuvutia uwekezaji. Wote tunafahamu uwanja huu hautaishia kunufaisha watu wa Kagera tu, hata nchi jirani zitakwenda kuutumia uwanja huo. (Makofi)
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ni lini ujenzi wa uwanja wa ndege wa Musoma utakamilika kwa maana ya run way pamoja na jengo la abiria ili kuweza kuanza kutumika na kukuza uchumi wa Mara kupitia utalii, biashara, pamoja na kurahisisha usafiri na usafirishaji? Ninakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Matiko kwa sababu anavyokimbizana kufuatilia uwanja wa ndege wa Musoma, siyo muda mrefu atamkaribia mpaka Mbunge wa Jimbo la pale mjini jinsi anavyohangaikia usiku na mchana kuona kwamba uwanja huu unakamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie, kutokana na umuhimu mkubwa wa utalii, madini na maeneo mengine, Serikali iliamua kufanya maboresho ya uwanja wa Musoma na hivi ninavyozungumza umevuka asilimia 58 na mjenzi yupo site anaendelea na kazi baada ya kusimama kwa muda mrefu kidogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, ninamwomba aendelee kuwa na subira, Serikali ambayo imekwishaanza kujenga inakwenda kukamilisha uwanja huo wa Musoma. (Makofi)
MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa Manyara Airport ili kuongeza utalii katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro na Manyara National Park?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Awack kama alivyoliuliza. Anaulizia kuhusu uwanja wa ndege, ninafikiri anaongelea wa mkoa maana pale kuna viwanja viwili. Kama anazungumzia wa mkoa, tupo kwenye hatua za utoaji wa ardhi, tutakapozikamilisha Serikali itaanza kufanya taratibu za ujenzi. Kama anazungumzia ule wa utalii kwa maana ule wa Lake Manyara, tayari tumeshampata mkandarasi, tupo kwenye hatua za mobilization na ujenzi utaanza mara moja. (Makofi)
MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwanza ninachukua nafasi hii kuipongeza Serikali pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri. Nauliza Serikali, imewalipa wananchi 226 kati ya wananchi 1,800. Je, Serikali ina mpango gani kuwamalizia hawa wengine maana wapo kwenye hali mbaya na kuna mvua kubwa zinazonyesha? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajibu kwa kifupi lakini moyo usio na shukrani hukausha mema yote. Ninampongeza Mheshimiwa Bonnah kwa kuweza kufuatilia na kupongeza Serikali hii kwa sababu jambo hili lilikwama kuanzia miaka ya 1990 ambapo wananchi zaidi ya 1,528 walikuwa wanadai. Tumekwishalipa shilingi bilioni 20 na siyo muda mrefu tutakwenda kulipa tena. Hii ni jitihada za Mheshimiwa Rais wetu na ninaamini kwa kuwa wameshaanza kulipa na hata waliobakia hao atakwenda kukamilisha. (Makofi)
MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi hii. Kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya ujenzi wa uwanja wa ndege Mkoa wa Njombe na Mheshimiwa Naibu Waziri alikuja kwenye cave akaona lile eneo. Wananchi wetu wa Makambako, Njombe Mjini, Lupembe, kuna wafanyabiashara wengi sana, hata Mwenyekiti Mheshimiwa Deo Mwanyika ili apande ndege mpaka aende Mkoa wa Songwe au aje Mkoa wa Iringa, ni lini uwanja wa ndege Mkoa wa Njombe atajengwa sasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilifikiri utaniambia nijibu kwa ufupi, lakini naona hujazungumzia hilo. Wewe na Mheshimiwa Swalle pamoja na Wabunge wote wa Mkoa wa Njombe, mmelifuatilia jambo hili kwa ukaribu sana na Serikali inatambua umuhimu wa uwanja wa ndege wa Njombe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali tulikuwa na mpango kwa ajili ya kukarabati ule uliopo, lakini baada ya kuona eneo ni dogo na mipango ni mikubwa, Serikali ikaona ni lazima ibadilishe uwanja ijenge uwanja mkubwa pengine wenye hadhi sawa na uwanja wa Songwe. Hii kwa sababu gani? Kwa sababu, kwanza unaweza kuona Mkoa wa Njombe ndiyo una maghala makubwa ya chakula ya NFRA. Mbili, tunao Mradi wa Liganga na Mchuchuma ambao tukikamilisha ujenzi wa reli ya kusini, uwanja ule ndiyo utakuwa jirani kwa ajili ya kufikisha watu mbalimbali kwenye eneo lile. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, uwanja huo pia utakuwa na faida kubwa kwa kilimo cha parachichi pamoja na mazao mbalimbali, lakini pia yapo maeneo jirani ikiwa ni pamoja na Chimala ambapo pia kuna madini mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua umuhimu wa uwanja huu, nimesema wiki iliyopita ninaomba nirejee tena, tumeshampata mkandarasi anaitwa Intercontinental Technocrats ambaye anafanya uhuwishaji, upembuzi yakinifu ili kuweza kujua gharama na mahitaji ya uwanja huo yatakuwaje. Hatimaye tukishamaliza hatua hiyo tutatangaza na tutampata mjenzi ajenge uwanja kama ambavyo yeye mwenyewe amekuwa akihitaji kwa muda mrefu. (Makofi)
MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakushukuru na pia naishukuru Serikali kwa majibu mazuri. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa umuhimu wa Mji wa Kwala ambao una bandari kavu, una kongani kubwa ya viwanda, una Mji wa Magindu unakua kwa kasi, Mji wa Chalinze unakua kwa kasi. Je, Serikali haioni sasa ni muda sahihi wa kujenga kituo cha treni ya SGR, mahali ambapo treni zinapishana ili wananchi wa maeneo hayo wanaotaka kuingia kwenye Mji la Kwala waingie kirahisi na kupata huduma zinazostahili? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Bandari Kavu ya Kwala kazi yake ni kupokea mizigo inayotoka kwenye bandari zingine na inayoingia pale kwa njia ya treni. Je, ni nini mkakati wa Serikali wa kuiunganisha Bandari ya Kwala na Bandari ya Bagamoyo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mwakamo kwa maswali yake ya msingi ambayo ameendelea kuyafuatilia na jinsi ambavyo anatusaidia kama sekta kuona umuhimu mkubwa wa eneo la Kwala pamoja na Bagamoyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nimhakikishie kwamba, tayari Serikali imekwishaona umuhimu mkubwa wa kuunganisha Bandari ya Kwala pamoja na reli zote tatu, kwa maana ya Meter Gauge ya TAZARA pamoja na Meter Gauge ya TRC, Cape Gauge ya TAZARA na SGR. Tayari kituo kimeshawekwa pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kilometa 1.3 ya reli ya meter gauge imeshaunganishwa na katika eneo hilo husika. Hivyo, basi tutaendelea kufanya hivyo ili kuhakikisha kwamba eneo hili la Bagamoyo, eneo hili la Pwani ambalo ni kongani ya viwanda na linakwenda kuwa na uchumi mkubwa, linakuwa linaunganishwa moja kwa moja na reli hii ili kutoa mizigo sehemu moja kupeleka mizigo sehemu nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yake ya pili ni kuhusiana na bandari ya Bagamoyo namna gani inaweza kuunganishwa pamoja na Kwala. Moja, nimfahamishe Mheshimiwa Mbunge, jinsi ambavyo Serikali imefanya kazi kubwa kuendelea kuboresha bandari nchini na hii inafanyika kwa sababu ya potential ya mizigo mingi iliyopo katika nchi jirani, ambapo ni muhimu tuboreshe bandari zetu ili tuweze kufikia masoko ya nchi zote zinazotuzunguka ikiwa ni pamoja na central corridor, nchi za kusini, kanda ya ziwa na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutekeleza hilo pamoja na maboresho ya bandari zetu mbalimbali ambayo tumefanya ikiwemo Bandari ya Dar es Salaam, Bandari ya Mtwara, Tanga pamoja na bandari zilizopo katika Maziwa ya Tanganyika na Nyasa, Serikali imeona umuhimu wa Bandari ya Bagamoyo kwa sababu pamoja na kazi hiyo kubwa meli kubwa za maximum zinazoweza kutua katika bandari zetu ikiwemo Dar es Salaam ni za mita 320.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, Bandari ya Bagamoyo ndiyo yenye uwezo mkubwa ya kuweza kupokea meli kubwa zaidi kwenda mpaka mita 400. Katika kutimiza hilo Serikali ina mpango wa kuunganisha Bandari ya Bagamoyo, Kwala na Bandari Kavu ya Kwala ili mizigo inayotoka sehemu mbalimbali duniani, ikitua pale Bagamoyo iweze kuunganisha moja kwa moja Kwala na kwenda sehemu mbalimbali inakohitajika ndani ya nchi yetu na nje ya nchi yetu.
MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ninalo swali moja la nyongeza. Kwa kuwa Uwanja wa Ndege wa Mpanda uko katika eneo zuri la kimkakati, kwa maana ya uchumi mpana ikiwa ni jirani na nchi ya DR-Congo. Serikali inasema nini kwa maana ya kuweka kwenye mipango yake uboreshaji wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda, ikiwa ni pamoja na miruko na mituo sambamba na ujenzi huo wa mnara wa mawasiliano? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, kulingana na uhitaji wa mara kwa mara, Serikali imeendelea kujenga minara ya ndege katika maeneo mbalimbali hapa nchini, ikiwa ni pamoja na Viwanja vya Julius Nyerere, KIA, Arusha, Dodoma, Mwanza, Iringa, Tabora, Tanga, Mtwara, Songea na maeneo mengine, lakini kulingana na uhitaji mkubwa minara mbalimbali inajengwa kwa sababu ikiwa ni pamoja na Shinyanga, Sumbawanga, Kigoma, Tabora, Msalato na Iringa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo yako maeneo mengine ambayo tutaanza ujenzi sio muda mrefu, ikiwa ni pamoja na Tanga, Mtwara, Kigoma, Lindi na Lake Manyara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, kama anavyofahamu Mheshimiwa Mbunge, Serikali imetumia fedha bilioni 1.4 katika Kiwanja cha Mpanda ambapo tumejenga runway, tumejenga jengo la abiria, tumejenga jengo la zimamoto na bado control tower.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge ambao ametimiza jukumu lake la msingi la Kibunge ambalo ni kuishauri na kuisimamia Serikali na kwamba ushauri wake na hoja yake, itafanyiwa kazi kulingana na mahitaji, kama ambavyo nimeainisha hapo juu ikiwemo ni pamoja na miruko ya ndege, ratiba maalum zilizoko, tukiona inafaa kwa wakati husika tutalifanyia kazi.
MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili. Swali la kwanza; je, Serikali inatambua hasa umuhimu na uwezo wa reli ya Kusini katika uchumi wa nchi yetu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa, katika majibu ya msingi amesema itajengwa kwa utaratibu wa PPP, utaratibu huu unapohusisha uwekezaji wa ujenzi wa reli na uendeshaji ninaamini itachukua muda mrefu. Hapa ninaomba nitoe ushauri, ninaishauri Serikali yangu sikivu ifikirie upya badala ya kusubiri ubia ione namna ambavyo itajenga reli ya kusini yenyewe, halafu mwekezaji aje kufanya uendeshaji. Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wa Mheshimiwa Mbunge umepokelewa kwa sababu ni jukumu la Bunge kuishauri Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la kwanza ni kwamba, Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa reli ya Kusini, hii inatokana na ukweli kwamba upande wa Kusini kwa maana kutoka Mbamba Bay mpaka Mtwara na matawi yake kuna fursa kubwa ikiwemo uwepo wa makaa ya mawe zaidi ya tani milioni 426, kuwepo kwa ikiwemo vanadium, titanium, lithium pamoja na kwenye eneo la Dangote zaidi ya tani milioni 232 za simenti. Pia umuhimu wa reli hiyo ndiyo unakwenda kuongeza matumizi makubwa ya Bandari yetu ya Mtwara ambayo Serikali imeweka pesa za kutosha pamoja na Mbamba Bay.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunatambua kwamba tukifanikiwa kuanzisha reli hiyo itaweza kusaidia madini ambayo nimeyataja na hivyo Serikali kupunguza kuagiza madini kutoka nje na chuma kutoka nje. Pamoja na umuhimu huo napenda nimhakikishie Mheshimiwa muuliza swali Mheshimiwa Hokororo kwamba Serikali imeshafanya mambo mengi sana ili kutambua na kuthamini umuhimu wa reli hiyo. Kwanza tumeshaanza maboresho mbalimbali ya bandari tatu, moja hivi ninavyozungumza ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay umekwishaanza na zaidi ya bilioni 80 Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan amezielekeza pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, tumefanya maboresho makubwa Bandari ya Mtwara kwa kuweka zaidi ya bilioni 157. Tatu, kwa sababu tunajua sehemu kubwa ya malighafi zitakazotoka pande wa Liganga na Mchuchuma itakuwa ni pamoja na bidhaa chafu au makaa ya mawe tunajenga bandari mpya ya Kisiwamgao ambapo zaidi ya bilioni 835 zimeelekezwa kwenye bandari mpya kabisa hii yote inadhihirisha na kuthibitisha namna ambavyo Serikali hii ya awamu ya sita inatambua umuhimu wa bandari hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumekwishalipa fidia pia kwa zaidi ya wananchi 1000 waliopo kwenye eneo la Liganga na Mchuchuma ili kupisha maeneo yale yote hiyo inaonyesha ni kwa namna gani Serikali inatambua jambo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaanza kufanya jambo la kwanza tunakuja la pili. Tumeshaanza kujenga reli ya kati kutoka Dar es Salaam mpaka Mwanza mpaka Kigoma na mpaka nje ya nchi ambayo inagharimu zaidi ya dola bilioni 12, zaidi ya takribani trilioni 30 hii inamaanisha nini? Inamaanisha utayari wa Serikali sasa ya Awamu ya Sita kuamua kuwekeza kwenye upande wa reli especially SGR.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapoanza maboresho makubwa kwenye reli yetu ya Kusini kwa maana ya TAZARA yote hiyo inaonyesha kwamba nchi yetu imeamua kufanya uchumi wake kuwa uchumi na uchukuzi, kwa hiyo nimtoe mashaka nimuombe aendelee kuwa na subira wakati Serikali inakamilisha mambo ambayo imeshaanza kuyafanya na siyo muda mrefu neema ipo mlangoni, watu wa kusini wajiandae Serikali itaanza kujenga reli hiyo. (Makofi)
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, Nyanda za Juu Kusini ni wakulima wakubwa wa zao la parachichi na horticulture kwa ujumla. Je, ni lini Serikali itaweka mfumo wa cold-room katika baadhi ya mabehewa katika Reli ya TAZARA ili kuhakikisha kwamba wakulima wakubwa wa mazao hayo wanasafirisha mazao hayo kufika Dar es Salaam kwa ajili ya kupeleka nje ya nchi yakiwa na ubora? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Mgaya, kama lilivyoulizwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Zambia pamoja na China ilijenga Reli ya TAZARA yenye urefu wa kilomita 860. Kwa sasa reli hiyo iliyojengwa ilikuwa na uwezo wa kubeba tani milioni tano, lakini kutokana na sababu mbalimbali hatukuweza kufikia hata 30% ya lengo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tayari tumeshaanza maboresho mbalimbali kwa ajili ya kuboresha reli yetu hiyo ya TAZARA, hivyo ninachukua ushauri wake Mheshimiwa Mbunge tuone namna ya kutazama, siyo tu kuweka cold room kwa ajili ya mazao ya parachichi ambayo yapo Mkoa wa Njombe, lakini kuangalia chain nzima katika njia nzima kuanzia inapotokea Kapiri Mposhi mpaka Dar es Salaam ili iweze kuwa sehemu ya kuchechemua uchumi wa maeneo ambapo reli hiyo inapita.
MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Mwanzoni kulikuwa na mpango wa kujenga reli kutoka Tanga – Arusha kuelekea Musoma na sasa, badala yake mpango huo umebadilika kwamba, reli inapita Simiyu. Je, ni lini sasa mchakato huo wa ujenzi wa reli hiyo ya kwenda Musoma utaanza?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninapenda kumjibu Mheshimiwa Manyinyi, swali lake alilouliza; Mpango wa Serikali ni kuunganisha Bandari yetu ya Tanga na Mikoa ya Kaskazini kwenda mpaka Ziwa Tanganyika. Mpango huo upo, hatujali sana imepita wapi, lakini tunaangalia kiuchumi ni wapi ipite na kadhalika. Kwa mfano, katika njia hiyo kuna madini mbalimbali, ikiwa ni pamoja na magadi soda, Engaruka kuna madini kule Dutwa, nickel na kadhalika. Kwa hiyo, njia specific pengine naweza nisizungumzie hapa, lakini kwa maana ya mpango huo ambao Serikali inao itakwenda kujenga baada ya hatua za awali kukamilika, ikiwa ni pamoja na usanifu wa kina.
MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Kwanza naomba nitumie nafasi hii kuipongeza sana Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi kwa ujenzi mkubwa sana wa bandari wa zaidi ya shilingi bilioni 49, na kwa zaidi ya miaka miwili, sasa umekamilika pamoja na kwamba haujaanza kufanya kazi. Sasa nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, mosi, pamoja na mikakati hii mizuri ambayo Serikali inayo, na bandari hizi zitakapokamilika kwa upande wa DRC lakini itakuwa ni bandari tu zimekamilika, ipo haja ya kupatikana barabara kutoka Bandari ya Moba mpaka kufika Lubumbashi ambako Watanzania wengi ndiko soko wanakolitegemea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri ni shahidi, alipofanya kikao na Country Manager wa TPA pale Lubumbashi na Ubalozi wetu mdogo, walimthibitishia umuhimu wa hii barabara. Je, ni upi mkakati wa kuanza ujenzi wa barabara kutoka Moba mpaka Lubumbashi ili kuiunganisha nchi yetu ya Tanzania moja kwa moja na DRC bila kupitia nchi ya Zambia? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa tunatambua jitihada hizi ambazo zinafanywa na Serikali zinaweza zikachukua muda mrefu kwa sababu ni uwekezaji mkubwa, na bado mpaka sasa hivi wafanyabiashara kulifikia Soko la Lubumbashi ambao ni miongoni mwa miji mikubwa ambayo inawapatia Watanzania wengi pesa, bado wanapitia changamoto kubwa na kadhia kubwa wanapopitia nchi ya Zambia kutokana na vita ya uchumi iliyopo kwa sababu kila mtu analiangalia Soko la DRC. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni ipi hatua madhubiti ya Wizara hii ya Uchukuzi kwa kushirikiana na Wizara nyingine kukaa chini kuendelea kutatua changamoto za wafanyabiashara wanaoliendea Soko la Lubumbashi ambazo wanapitia kwenye nchi ya Zambia? Ni upi mkakati wa haraka na dharura ili Watanzania wasiendelee kuumia? Ahsante (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wetu wa Uchukuzi, natumia nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Sichalwe kwa jinsi anavyofuatilia. Mheshimiwa Sichalwe ni moja ya wadau muhimu wanaofuatilia sana namna ambavyo Serikali inaweza ku-access Soko la Kongo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba nchi yetu imebarikiwa kuzungukwa na nchi nyingi zisizo na bandari, na upande wa Zambia tuna zaidi ya mzigo wa tani milioni saba, na upande wa Kongo zaidi ya mzigo wa tani milioni 10 na nchi nyinginezo. Hata hivyo, bado hatujafikia inavyotakiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kumpa pongezi hizo, naomba nijibu maswali yake mawili ya nyongeza ambayo ameyauliza kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja, ameuliza habari ya suala la barabara kutoka Moba kwenda Lubumbashi. Huu ni ushauri anaoutoa mara kwa mara, nasi Serikalini tumeshaupokea na tumeshaanza kuandaa taarifa ya wataalamu ili kutazama fursa zilizopo na mchakato mzima wa namna ya kufikia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tunaendelea na hilo, ukizingatia swali lake la msingi aliuliza ni kwa nini Serikali ilianza kujenga Karema wakati upande wa pili hatujaanza pengine kupatumia, Serikali kwa kushirikiana na wenzetu wa Kongo tayari tumeshaanza kufanya utilization ya bandari hizi mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyozungumza, ukienda pale Kongo upande wa Katanga eneo la Manono, tuna madini mengi ya lithium na copper ambapo ujenzi wa barabara kilometa 450 kutoka kule Manono – Katanga – Kalemie umeshaanza sambamba na usanifu wa awali ili hapo baadaye tuweze kujenga SGR.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kwa miaka mingi sana Bandari ya Kalemie ilikuwa haitumiki na imekuwa ni kilio cha Wabunge wengi sana wanaotumia Ziwa Tanganyika. Tayari ujenzi huo umeanza kama nilivyozungumza na wenzetu wa Kongo kwa kutumia mwekezaji wanajenga Bandari ya New Kalemie.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hilo peke yake haliishii hapo. Ili kuona Serikali imetambua umuhimu wa fursa zilizopo katika Ziwa Tanganyika, inakwenda sambamba na ujenzi wa meli nne ili wawekezaji hao waweze kusafirisha mzigo wa lithium na copper na madini mengine kutoka kule Katanga kuja hapa kwetu, kwenda mpaka Bahari ya Hindi ambapo tunaanza na meli nne.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tayari wameshaanza kujenga meli ya kwanza tarehe 1/4/2025 na meli nyingine nne zitakuwa zimekamilika ndani ya miaka hii miwili. Tunategemea mzigo zaidi ya metric tons 1,500,000 katika mwaka wa kwanza utaanza kupitishwa. Kwa hiyo, nampongeza sana Mheshimiwa kwa kufuatilia jambo hili na nimeona nitoe kwa ufafanuzi mkubwa zaidi ili aweze kupata picha hiyo kubwa zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, nakubaliana na changamoto zilizopo kwenye upande wa madereva wetu wanapotoka hapa kwenda upande wa Kongo kupitia upande wa Zambia. Changamoto hizo zinaendelea kushughulikiwa kwa kushirikiana na nchi hizi mbili kidiplomasia kwa lengo la kuboresha biashara hiyo ili sisi sote kwa sababu wao ni wanufaika na sisi ni wanufaika na maeneo mengine tuweze kunufaika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mkakati wetu mzuri na wa kudumu zaidi ni kutazama namna ya kuweza kufikia nchi specific kupitia Ziwa Tanganyika kama ambavyo nimeeleza kwenye maelezo ya awali, ahsante.
MHE. MAULID SALEH ALI: Mheshimiwa Spika, nishukuru kwa majibu mazuri ya Serikali; nitauliza swali moja. Kutokana kwa kuhamasika kwa wananchi kutumia usafiri wa treni ya SGR. Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza route zake kutoka Dodoma – Dar es Salaam?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, ninamshukuru Mheshimiwa Maulid Saleh Ali, kwa swali lake la nyongeza. Ninakubaliana naye kwamba tangu usafiri wa treni ya SGR ulipoanzishwa mwamko umekuwa ni mkubwa sana kwa Watanzania, wamefurahia huduma hii na mahitaji yameongezeka zaidi. Kutokana na hali hiyo tayari hivi ninavyozungumza timu ya wataalam imeshaanza kufanya kazi ili kuchambua na kutazama mahitaji halisi ili hatimaye sasa tuweze kufikiria tuanzishe route pengine ziwe lini. Kwa sababu ukiangalia weekend mahitaji yanakuwa makubwa zaidi kuliko katikati ya wiki; kwa hiyo wataalam wanafanya kazi yao.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Maulid na Waheshimiwa Wabunge wengi ambao kimsingi wamekuwa wakifuatilia jambo hili, timu hiyo itakapokamilika tayari Mheshimiwa Waziri wetu, Mheshimiwa Mbarawa ameelekeza kwamba kazi hiyo ianze mara moja, route hizo ziongezwe. Jambo jema na zuri ni kwamba tayari Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, alikwishatupatia fedha na vitendea kazi vipo vya kutosha; kwa hiyo tunaamini kwamba kazi hiyo inakwenda vizuri zaidi. (Makofi)
MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa reli ya SGR kutoka Jijini Dar es Salaam, kupitia Lindi na Mtwara hadi Mbamba Bay? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, samahani, kutoka Dar es Salaam?
SPIKA: Kutoka Dar es Salaam, kupitia Mtwara mpaka Mbamba Bay.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mheshimiwa Ndulane kwa swali lake zuri. Kwa sasa Serikali haijaanza upembuzi yakinifu wala usanifu wa kina kuhusiana na reli kutoka Dar es Salaam kwenda Lindi. Hata hivyo, kwa kutambua umuhimu mkubwa wa reli ya kusini, yaani kutoka Mtwara Port kwenda mpaka Mbamba Bay kupitia matawi ya Liganga na Mchuchuma tayari tumeshakamilisha study.
Mheshimiwa Spika, sasa hivi Serikali ipo kwenye hatua ya utafutaji wa fedha ili kuweza kuunganisha kipande hicho kiweze kujengwa kwa njia ya SGR; na kutokana na umuhimu mkubwa wa makaa ya mawe ambayo tuna zaidi ya makaa ya mawe zaidi ya metric tons milioni 428, tuna chuma cha kutosha, lakini pia ni kutekeleza maoni ya waasisi wa nchi zetu hizi za Malawi, Tanzania pamoja na Msumbiji katika kuhakikisha kwamba tunaziunganisha kupitia Ziwa Nyasa na Bahari ya Hindi.
MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itaanza ile ahadi yake ya kutengeneza reli ya SGR kutoka Dar es Salaam kwenda Kilimanjaro? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa swali lake Mheshimiwa Shally Raymond. Ni kweli kabisa kwamba Serikali inao mpango wa kujenga reli ya kisasa SGR inayounganisha Tanga kwenda mpaka Arusha kuunganisha mpaka Musoma na hii ni kutokana na uwepo wa madini ya kutosha ya nickel kule Dutwa, madini ya magadisoda kule Engaruka pamoja na kule Minjingu.
Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii pia kueleza pia vizuri. Reli hii ya kisasa ni gharama kubwa sana kuijenga, kwa hiyo unapoamua kufanya maamuzi ya kujenga lazima uwe na uhakika na mzigo uliopo. Kipande hiki tayari tumeshajiridhisha mzigo upo wa kutosha. Kwa sasa tumeshakamilisha study tupo kwenye hatua za utafutaji wa fedha ili tukikamilisha tuweze kuanza kujenga. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tunajenga kilometa 2,300 kwa sasa hivi. Tuna kutoka Dar es Salaam mpaka Mwanza, tuna kutoka Tabora mpaka Kigoma na tumeanza kutoka Uvinza mpaka Burundi. Hivyo sio rahisi tukafanya mambo yote kwa wakati mmoja, hizi kilometa 2,300 hakuna nchi Barani Afrika imewahi hata kufikiria na hivyo inaifanya nchi yetu na kumfanya Dkt. Samia, kuwa ndiye Rais, kinara wa reli ya kisasa Barani Afrika. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, reli hii ya kisasa anayoijenga Dkt. Samia, inamfanya kuwa ndiye Rais, kinara wa ujenzi wa reli ya kisasa Barani Afrika na kumfanya kuwa wa tano duniani. Niwaombe Waheshimiwa Wabunge, tuvumilie amalize kazi hii ambayo ameshaianza ili baadaye tuweze kuanza na sehemu hizo zingine ambazo kimsingi wamekuwa wakizihitaji.
MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, David Kihenzile nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kufuatia changamoto za usafirishaji na ukuaji wa uchumi katika maeneo ya ukanda wa bahari ikiwemo Mafia, Bagamoyo, Kibiti na Mkuranga, ni upi sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha inaboresha bandari za maeneo hayo na kujenga meli zake? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; nipende sana kuipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea na mkakati wa kujenga miradi mikubwa ya kimkakati. Swali langu ninataka kujua, ni upi mpango wa Serikali kuhakikisha vijana wanaopata ajira zile ambazo zisizo na ujuzi (unskilled labour) kutoka katika maeneo hayo ya miradi kwamba wanazingatiwa vijana kutoka katika maeneo hayo yenye miradi husika? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nitumie nafasi hii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma kwa jinsi ambavyo amekuwa mfuatiliaji wa miradi mikubwa na hata ya kawaida katika Mkoa wa Pwani ikiwemo ya sekta yetu ya uchukuzi hususan pale Mafia, bandari na maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, nimhakikishie Mheshimiwa Hawa Mchafu Chakoma kwamba Serikali imeamua kuifanya sekta ya uchukuzi kama mishipa kwa kuitambua kwamba ni mishipa ya damu katika Taifa letu. Hivyo basi, inafanya maboresho ya bandari mbalimbali nchi nzima pamoja na kujenga meli katika maziwa makuu yote na sasa ninapozungumza kwa upande wa swali lake la msingi Bandari za Mafia, Mkuranga pamoja na Bagamoyo ya zamani, tayari tumeshapewa idhini na Serikali kupitia Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan. Hivyo, tunaweka kwenye mpango wa mwaka wa fedha 2025/2026 tuanze maandalizi ya kuzijenga bandari hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii inakwenda sambamba na kuanza kujenga meli. Tarehe 8 Machi TASHICO (Kampuni yetu ya Meli Tanzania) ilisaini mkataba wa kuanza usanifu wa kina kwa ajili ya kutazama fursa zilizopo katika mwambao wa Bahari ya Hindi. Lengo ni nini? Ni kutazama biashara iliyopo. Tunao mpango kama Serikali kuona kwamba tunaimarisha usafiri wa nchi jirani kama vile Visiwa Comoro, Madagascar, Shelisheli pamoja na maeneo kama vile Mtwara, Tanga, Lindi na kadhalika. Hivyo, tutakapokamilisha usanifu huo tutakwenda hatua ya pili ya kuanza kujenga meli hizo kulingana na mahitaji na kujua fursa ambazo ziko pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ameuliza kuhusiana na vijana waliopo katika maeneo hayo wapewe kipaumbele. Kwanza, swali hili limekuwa likiulizwa sana hapa Bungeni. Ninapenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kwamba nchi hii ni yetu sote. Ni haki ya kila Mtanzania kuajiriwa mahali popote bila kujali kuna mradi au hakuna mradi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazingatia pia kwamba, kodi zinazojenga miradi hiyo ni kwa Watanzania wote. Aliyekuwepo Iringa analipa kodi katika mradi uliokuwepo mkoa mwingine. Hivyo basi, ninapenda kuwataarifu Waheshimiwa Wabunge kwamba tuendelee kutoa fursa kwa vijana wetu nchi nzima wafanye kazi popote. Aidha, tukubaliane pia yako maeneo ambayo vijana hawapendelei sana kufanya kazi zile ambazo ni unskilled. Hivyo, hata mjenzi angependa kwenda kutafuta sehemu ambapo vijana wako tayari kufanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijahitimisha nitoe rai pia kwa kutambua umuhimu kwamba mradi unapotekelezwa kwenye eneo fulani ni vyema vijana wa eneo wakapewa kipaumbele zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaagiza wakandarasi waliopo kwenye sekta yetu ya uchukuzi watazame pamoja na kuchukua maeneo nchi nzima ya nchi hii lakini pia watazame katika eneo mradi uliopo ili wapewe kipaumbele vijana wa eneo hilo.
MHE. MAIMUNA A. PATHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itaboresha Uwanja wa Ndege wa Kilwa na Nachingwea, ukizingatia kwamba Uwanja wa Ndege wa Nachingwea umetumika sana katika ukombozi wa Bara la Afrika? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru Mheshimiwa Pathan kwa swali lake la nyongeza. Serikali inao mpango wa kuboresha viwanja vyote katika nchi hii na katika viwanja alivyovitaja kwa sasa hivi tupo kwenye hatua za awali kwa ajili ya kulipa fidia. Tukimaliza fidia pamoja na kutwaa maeneo tutakwenda kwenye hatua ya pili kwa ajili ya kuviendeleza.
MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Je, ni lini safari za ndege za kutoka Dodoma kwenda Mbeya zitaanza, ukizingatia Mbeya kuna abiria wengi sana? Unapokwenda Mbeya mpaka uende Dar es Salaam ndiyo uende Mbeya.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza dada yangu Mheshimiwa Suma Fyandomo kwa swali lake aliloliuliza la kufuatilia safari za ndege Mkoani Mbeya. Ni kweli Mkoani Mbeya kuna abiria wengi na ndege hazitoshi, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Suma kwamba siyo Mbeya tu, kutokana na kazi kubwa ambayo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameifanya ya kujenga viwanja vingi mahitaji ya ndege yameongezeka zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tungesema kila Mbunge asimame karibu Wabunge zaidi ya 20 wangeweza kusimama ili tuongeze ndege kwenye maneo yao. Hata hivyo, kutokana na umuhimu huo mkubwa katika mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali imepanga kununua ndege nyingine mpya za masafa marefu na mafupi pamoja na ndege ya mizigo. Tunategemea kwamba kadiri muda utakavyozidi kuongezeka ndivyo tutaendelea kuboresha na kupeleka ndege kwenye maeneo mbalimbali ya nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine kabla sijamaliza kujibu swali lake ninapenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba viko viwanja hivi ninavyoongea zaidi ya vitano ambavyo vinafanyiwa maboresho vikikamilika navyo vitahitaji ndege. Kwa hiyo, Mheshimiwa Suma na Wabunge wote waendelee kutuvumilia wakati Serikali inaendelea kutafuta suluhu ya kudumu ya jambo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na mwisho niziombe sekta binafsi kwa maana private operators wa hizi ndege watazame fursa zilizopo Mkoani Mbeya na maeneo mengine kwa sababu siyo lazima kupeleka ndege za Serikali. Tunazo kampuni nyingi, hebu zichangamkie fursa hiyo.
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mbuga ya Serengeti ni kati ya mbuga kubwa na maarufu kwa Afrika ambapo watalii mbalimbali kutoka duniani hupenda kutembelea lakini kwa sasa hivi the only entry point its either watue Kilimanjaro au Arusha ndio waweze kuja Serengeti au watue Kenya waweze kupitia Tarime na kwenda Serengeti kitu ambacho kinakuwa kinawa-discourage at a time. Nikataka kujua ni lini Uwanja wa Serengeti utaanza kujengwa ili sasa watalii hawa waweze kuja moja kwa moja na kuongeza uchumi wa nchi yetu? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Matiko kwa hoja yake ya Serengeti. Hata wiki iliyopita nilikuwa ninazungumza na viongozi wa CCM wa Mkoa wa Mara, kilio chao kikubwa ni hichohicho. Ninapenda kumhakikishia Mheshimiwa Matiko kwamba Serikali inao mpango wa dhati na imeshaweka kwenye Bajeti ya 2025/2026 kuanza mchakato wa ujenzi wa Kiwanja cha Ndege Serengeti.
MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Uwanja wa Moshi utakamilika? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Uwanja wa Moshi tunaufahamu ni uwanja wa kihistoria katika Taifa letu. Serikali kwa kutambua umuhimu huo mkubwa ilishaanza ujenzi na hivi ninavyozungumza iko zaidi ya 50%. Nimwombe Mheshimiwa Shally Raymond atupe muda kidogo wakati tunaendelea kufuatilia taratibu za malipo zikamilike ili mkandarasi aendelee kulipwa na hatimaye aweze kukabidhi uwanja.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imerejea mpango wake wa ujenzi wa Bandari Bagamoyo na kwa kuwa wapo wananchi ambao waliahidiwa ardhi katika Kata ya Zinga; na kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri aliwahi kujibu na kukubali ombi langu la kutembelea Kata ya Zinga ili awasikilize wananchi wa maeneo yale hususan wa Mlingotini. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari kutekeleza ahadi yake ili awasikilize wale wananchi ambao waliahidiwa kupata ardhi mbadala kwa ajili ya eneo ambalo limetengwa kujengwa Bandari ya Bagamoyo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, niko tayari na Mheshimiwa Mbunge dada yangu Mheshimiwa Subira Mgalu, baada ya kutoka hapa tupange ziara twende Lindi tukazungumze na wananchi hao ili kuwaelewesha umuhimu na mawanda mapana ya Bandari yetu ya Bagamoyo Mbegani. Kwa sababu Taifa tayari sasa limeshaona fursa hiyo na tuko tayari kwa ajili ya kuanza uendelezaji wake.
MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; tulikwenda pale Itungi na Mheshimiwa Naibu Waziri tukaiona ile Meli ya MV-Songea bado iko vizuri sana. Je, lini Serikali itatoa fedha ili meli ile ikarabatiwe na kuweza kusaidia usafiri wa wananchi wa Ziwa Nyasa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; wananchi wa Ziwa Nyasa, Ludewa ina kata nane wanatumia usafiri wa maboti ambayo mengine hayana usalama kwa sababu ratiba ya meli ni mara moja kwa mwezi. Je, nini maelekezo ya Serikali ili kusaidia wananchi wale waweze kusafiri kwa usalama mkubwa ndani ya Ziwa Nyasa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza sana Mheshimiwa Kamonga kwa ufuatiliaji wake mkubwa wa usafiri katika Ziwa Nyasa. Ni kweli mimi na yeye tulikwenda pamoja na Wabunge wengine ambao wanapakana na Ziwa Nyasa tulifanya ziara katika Ziwa hilo tukatambua fursa zilizopo na changamoto ambazo zinawakumba wananchi hao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, miongoni mwa mambo ambayo Waheshimiwa Wabunge waliishauri Serikali ikiwa ni kutimiza jukumu lao la msingi la kuishauri na kuisimamia Serikali, ilikuwa ni kuomba Meli ya MV Songea irejeshwe kwa sababu ni mbovu na imesimama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kusikia kilio chao Serikali makini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan, ilifanya maamuzi katika mwaka wa fedha 2025/2026 wa kurejesha meli hiyo. Tumetenga bilioni 4.0 na katika mwaka wa fedha 2025/2026 tunakwenda kukarabati meli hiyo kwa sababu kwanza, ilivyotengenezwa inaendana na hali halisi ya Ziwa Nyasa kwa sababu inaweza kustahimili mawimbi pia inatumia mafuta kidogo na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, amezungumza kuhusu ratiba. Kwanza, nimpe pole kwa sababu kuna changamoto pale Kyela ya mafuriko na hivi navyozungumza tunapata changamoto kubwa ya kupata vitendea kazi kama mafuta na vitu vingine. Hivyo, usafiri ni kama vile umesitishwa. Lakini mara baada ya hali itakapotengemaa naielekeza Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) irejeshe ratiba zake angalau mara mbili badala ya kufanya mara moja kwa mwezi.
MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, niishukuru Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utayari najua kwa maana ya Bandari ya Karema imejengwa kuna meli nne zinaendelea kujengwa kuna barabara ya lami inapelekwa Karema huo wote ni utayari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; Serikali inasema nini katika kufungamanisha Uwanja wa Ndege wa Mpanda na fursa nyingine zilizopo kama utalii na Soko la Kongo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; nini mkakati wa Serikali katika kusaidia Uwanja wa Ndege wa Mpanda kupata miruko iwe ni kutoka ATCL au makampuni mengine binafsi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Mheshimiwa Kapufi, kwa maswali yake ya nyongeza mawili na nimpongeze kwa anavyofuatilia kwa karibu sana maendeleo ya mkoa wake na kipekee jimbo lake, lakini zaidi alivyotambua kazi kubwa ambayo Serikali imeshaanza kufanya katika eneo hilo la Mkoa wa Katavi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali inatambua umuhimu mkubwa wa Mkoa wa Katavi pamoja na uwepo wa kuboresha ule Uwanja wa Ndege wa Mpanda na hii ni kutokana na ukweli kwamba, Katavi:
(i) Kuna utalii na sote ni mashahidi;
(ii) Madini ya kutosha;
(iii) Mazao ya kutosha;
(iv) Serikali inavyozungumza hivi inakamilisha ujenzi, maboresho ya reli ya kutoka Kaliuwa mpaka Mpanda na inaanza maandalizi mwaka wa fedha ujao 2025/2026 kujenga reli ya mita gauge kutoka pale Mpanda kwenda mpaka Kalema;
(v) Tayari tunajenga barabara ya lami kutoka pale Mpanda kwenda mpaka Karema; na
(vi) Tunajenga meli mbalimbali kwenye Ziwa Tanganyika yote haya na mengine ambayo sijayataja yanadhihirisha na kuthibitisha umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali tayari ninavyozungumza hapa imefanya makubwa katika Uwanja wa Mpanda. Kwanza, tumeshatengeneza na kukamilisha runway yenye urefu wa mita 2000. Pili, tayari tumejenga jengo la abiria la 1.4 bilioni na linatumika hivi navyoongea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Kapufi akubali kwamba, jitihada hizi zinadhirisha na kuthibitisha dhamira ya dhati ya Daktari Samia Suluhu Hassan kuthamini na kutambua Mkoa wa Katavi. Hivyo basi, ninaomba nichukue jambo lake la taa za kuongozea ndege tuendelee kutazama huko mbeleni kadiri tukipata fedha tutaweza kujitahidi kuhakikisha kwamba, uwanja huu unakuwa na taa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taa hizo pia kama nilivyosema kwenye swali la msingi zinategemeana sana na miruko, ninaomba nitumie nafasi hii kuzishauri na kuziomba kampuni mbalimbali za ndege nchini zilizo nchini na nje ya nchi kutazama fursa zilizopo katika Mkoa wa Katavi. Abiria wapo wa kutosha hebu tuongeze ndege, tukishaongeza ndege tutakuwa na miruko, tukiwa na miruko tuta-justify hata umuhimu wa kwenda kuweka taa za usiku kwa sababu ndege zitakuwa zipo za kutosha.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niipongeze Serikali kwa uwekezaji mkubwa sana uliowekezwa kwenye eneo la Mkoa wa Katavi hasa uwanja wa ndege pamoja na jengo la abiria na mengine ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyaeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kwambauuliza Serikali ilikuwa imeahidi kufanya miruko ya ndege kutoka Dar es Salaam, Mpanda hadi Lubumbashi. Ni lini Serikali itatekeleza ahadi ambayo ilikuwa imetoa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kumjibu Mheshimiwa Mwenyekiti wetu wa Kamati ya Miundombinu na Mbunge wa Kalema Mheshimiwa Kakoso kwamba, hoja yake tumeipokea na tunaendelea kuichakata Serikalini ili kutazama fursa zilizopo na uwezekano wa kuanza. Pia, Mheshimiwa Kakoso ninajua kuna suala ambalo amesahau kwa sababu tu pengine ni swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimjulishe pamoja na Wabunge wengine wa Mikoa mitatu Rukwa, Kigoma na Katavi kwamba, jana meli yetu ya MT-Sangara ilisimama kwa muda mrefu imeanza kufanya safari zake rasmi kutoka Kigoma kwenda Mpurungu kwenda Kalemii na kwenda Bujumbura. Hii ikiwa inamaanisha nini? Utekelezaji wa yale ambayo wanayaagiza Waheshimiwa Wabunge lakini Serikali ikiahidi.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Wizara, ninaipongeza kwa kufanya usafi katika Uwanja wa Urambo, ambapo sasa Uwanja unapendeza kwa kuwa upo katikati ya Mji. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:
Swali la kwanza, kwa kuwa uwanja huo upo katikati ya mji. Je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kuweka utaratibu maalum wa kudumu wa usafi ili tusiwe tunangojea mpaka hali iwe mbaya ndiyo tuombe? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa uwanja upo katikati ya Mji kwa ajili ya usalama na kupendezesha Mji pia. Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kuweka taa angalau za solar katika uwanja huo wa ndege? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, kwanza, kwa niaba ya Serikali kupitia Waziri wetu Mheshimiwa Prof. Mbarawa, tunapokea shukurani zake kwa sababu wachache ambao wakitendewa wema huwa wanashukuru. Wiki mbili zilizopita Mheshimiwa Sitta, alisimama hapa na akatoa ushauri wake na Serikali ikachukua jambo lake kwa uzito unaostahili, ikatekeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pili, nimpongeze kwa jinsi ambavyo amekuwa mfuatiliaji makini wa maendeleo kwenye eneo lake. Amekuwa ni mmoja wa Wabunge wa kuigwa ambaye kila wakati anafuatilia maendeleo ya eneo lake. Ameleta maswali mawili la pili ni kama ushauri.
Swali lake la kwanza, nimhakikishie sisi kama Serikali tunajipanga kufanya jambo alilolieleza la usafi kuwa endelevu. Kwa hiyo, kila wakati tutajitahidi kuhakikisha kwamba usafi unafanyika katika Kiwanja hiki cha Ndege cha Urambo. (Makofi)
Swali lake la pili, Mheshimiwa Mbunge anaulizia kuhusiana na taa. Nimhakikishie kwamba Serikali imelipokea jambo hili kama ushauri, ninailekeza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini iende kwenye eneo hilo ikatazame gharama zilizopo na kisha tutazame tunachoweza kukifanya ili kama alivyosema moja tuimalize ulinzi na usalama lakini pili tupendezeshe Mji wake wa Urambo, lakini tatu tuweze kuondoa vibaka pengine na wavamizi katika eneo hilo ambao wangeweza kuwa changamoto katika uendeshaji wa shughuli za wananchi za kila siku. (Makofi)
MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa, kupande hiki cha Mroyo – Ndungu kimetandazwa kokoto ambazo magari mengine yakipita, haya yaliyopo nyuma yanavuviwa vioo, kwa ajili ya zile kokoto zinarukaruka sana, na Kwa kuwa, pembezoni mwa hii barabara kwa mwaka wa nne huu kumewekwa udongo ambao naamini ulikuwa ni mchanga na umeota majani, je, Serikali ina mpango gani wa kuchukua hatua za dharura kusaidia kuondoa huu udongo kwa sababu hata gari lililopo nyuma ambapo kokoto zinarukaruka, haliwezi hata kukwepa zile kokoto?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa, Serikali imeshatoa malipo ya awali kwa kipande hiki cha Ndungu – Mkomazi kwa mkandarasi, na kwa kuwa, mkandarasi huyu ameshaweka kambi ile, je, Serikali inamsimamia mkandarasi kwamba, aanze hiyo kazi ya kuweka lami wakati gani au kipindi kipi kinachokuja? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza Mheshimiwa Kaboyoka kwa jinsi ambavyo anasimamia eneo lake na kuhakikisha kwamba, tunatekeleza vizuri majukumu yetu. Natumia nafasi hii pia kumkumbusha Mheshimiwa Kaboyoka kwamba, awali wananchi wa Kilimanjaro, hususan Same, walikuwa wanaiomba Serikali ikamilishe au ianze ujenzi wa mradi huu, lakini huko nyuma hatukuweza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Awamu ya Sita imeamua rasmi kuijenga barabara hiyo kwa maslahi ya Taifa letu, lakini kwa sasa hivi mkandarasi hajalipwa, hivyo kazi imesimama kidogo kwa kuwa ni muhimu pale tunapokuwa na miradi, barabara hizo zipitike bila kuleta usumbufu kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninamwelekeza Mkurugenzi Mkuu au Mtendaji wa TANROADS, kupitia Meneja wa Mkoa husika wa Kilimanjaro, aende katika eneo husika atazame changamoto inayozungumzwa na Mheshimiwa Mbunge. Kama kutakuwa na changamoto hiyo kwa ukubwa huo, waifanyie kazi, ili wananchi wapite bila changamoto yoyote katika eneo hilo kwa sababu, katika maeneo yote ambayo tunatekeleza miradi ya barabara au miradi mingine, barabara inapaswa kuwa passable, yaani iendelee kupitika wakati huo mradi unaendelea kutekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumza pia kuhusu uendelezaji wa barabara hiyo. Namkumbusha Mheshimiwa Kaboyoka kwamba, barabara hii yenye kilomita 98 Serikali imekamilisha usanifu mwaka 2018/2019 na ilifanya maamuzi ya kuanza kuijenga 2021 kwa awamu ya kwanza, ambapo zilikuwa ni kilomita 5.2.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi ninavyozungumza tunategemea mwishoni mwa mwaka huu, 2025, ikamilike awamu ya pili ya Ndungu – Mkomazi kilomita 36. Tumeshampata mkandarasi ambaye ameanza kufanya kazi na kipande cha tatu cha Same – Mahore, kilomita 56, tupo kwenye hatua ya manunuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia mara tu wakandarasi wanapolipwa advance payment au fedha za malipo ya awali wanaelekezwa waanze kufanya kazi. Hivyo basi, kwa maeneo yote ambayo wameshalipwa nawaelekeza wakandarasi waanze kufanya kazi mara moja, ili tuweze kuhakikisha miradi hiyo inakamilika.
MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Naibu Waziri, nina maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, hali ilivyo sasa hivi, Kampuni za CCECC na YAPI MARKEZI ambazo zinajenga Reli ya SGR na wana kambi pale Bukene, wana jumla ya vibarua (wafanyakazi wasio na ujuzi) kama 300; lakini kati ya hawa 300, wanaotoka katika Jimbo la Bukene hawazidi 12. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuongozana nami ili twende kwenye kambi hii ili akahakiki ukweli?
Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ulivyo ni kwamba, hawa CCECC pamoja na YAPI MARKEZI hata kwa kazi za vibarua wanaleta vijana kutoka Morogoro na Dar es Salaam na vijana wa eneo la pale wanakosa ajira.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, namshukuru Mheshimiwa Zedi kwa jinsi anavyofuatilia Vijana wa Bukene waweze kupata ajira katika mradi ambao kimsingi unapita katika eneo ambalo yeye ni mwakilishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Zedi kwamba ni maelekezo ya Serikali, wakandarasi mbalimbali wanaotekeleza miradi mbalimbali katika maeneo mbalimbali katika nchi yetu, wahakikishe kwamba wanatoa kipaumbele kwa vijana wa eneo husika hususan wanapokuwa wanatekeleza miradi mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, inaielekeza TRC iende katika eneo husika ikatazame, kama, ambavyo Mheshimiwa Mbunge amekuwa akizungumza, kwamba kuna watu wengi wametoka eneo lile.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, baada ya Bunge hili pengine tutapanga mimi na yeye twende tukajiridhishe; na ninawataka wakandarasi hao sasa waendelee kuhakikisha kwamba wanachukua vijana katika maeneo ambayo miradi hiyo inapita.
MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Changamoto ya vijana wa maeneo husika katika mradi huu siyo Bukene peke yake, hata katika Jimbo la Tabora Mjini, vijana wengi wanaoletwa pale hawatoki Tabora Mjini, wanakuja kutoka mikoa mingine mbalimbali. Nini changamoto hiyo ambayo hata vijana wetu wanaweza kufanya hizo shughuli ambazo wengine wanakuja kutoka mikoa mingine?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukisoma takwimu za jumla ya ajira zote katika mradi wetu huu wa SGR kutoka Dar es Salaam mpaka Tabora kwenda mpaka Mwanza na kwenda mpaka Kigoma, tuna vijana au watu walioajiriwa takribani 1,730 na ajira za kati ni 5,659 wakati ajira za chini ni 5,694. Hawa wa ajira za chini wote kwa sehemu kubwa wanatoka nchini mwetu sehemu tofauti tofauti.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi, ninawaelekeza wakandarasi hao kuhakikisha kuwa wanapokuwa wanachagua vijana hao wa ajira za chini wahakikishe kwamba wanatoa msukumo zaidi au kipaumbele zaidi kwenye eneo ambalo mradi huo unapita.
MHE. KILUMBE S. NG'ENDA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ambayo nayapongeza, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, moja, Serikali imefanya kazi nzuri sana ya usafiri kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma wa SGR na wananchi wote Tanzania sasa wanatamani hatua hiyo wafikie. Nini hatua ya Serikali katika kutekeleza mradi wa SGR kwenye maeneo yote nchini ikiwemo kufika Kigoma? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ni kwamba, reli ya kati kipande cha kutoka Kigoma kwenda Tabora kina changamoto kubwa na kimeanza ukarabati. Nataka kujua ni lini ukarabati huo utakamilika na kuwawezesha wananchi kuendelea kutumia reli hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda kwa maelezo yake ya awali ya kuipongeza Serikali yetu pendwa kwa kazi kubwa ambayo imefanywa katika miaka hii minne kwenye sekta ya reli.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumwarifu Mheshimiwa Kilumbe pamoja na Waheshimiwa Wabunge juu ya hatua mbalimbali ambazo Serikali imefanya katika kipindi kifupi cha miaka hii minne. Tukianza na kutoka Dar es Salaam - Morogoro mpaka Dodoma, hili halihitaji hata kulifafanua kwa sababu kila mtu anaona; tunapanda reli, tunafurahia usafiri salama na ulio mzuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumshukuru Mheshimiwa Rais wetu mpendwa ambaye ndiye anasimamia utekelezaji wa Ilani ya CCM ambayo iliahidi kuhakikisha kwamba itaboresha usafirishaji katika Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi ninavyozungumza, naomba kumwarifu Mheshimiwa Mbunge, kutoka Makutupora – Tabora, Kilometa 368 mkandarasi yuko site tayari, na tuko asilimia 14.5, kutoka Tabora mpaka Isaka, Dkt. Samia Suluhu Hassan pia aliidhinisha na tulishasaini mkataba na mkandarasi ameshaanza kazi kilometa 165, tuko asilimia sita. Aidha, kutoka Mwanza mpaka Isaka kilometa 341, tuko 60%. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama haitoshi, hivi karibuni mwaka jana pia Mheshimiwa Rais alikubali, tumeanza ujenzi wa reli ya kisasa, kilometa 506 na tuko asilimia sita. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka huu mwezi wa Tatu, tumesaini mkataba unaounganisha nchi yetu kutoka Uvinza kwenda Msongati kwenye madini ya Nickel ambapo ni kilometa 240. Hii ni hatua kubwa ambayo tumeshaifanya kama Serikali kwa upande wa SGR. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hilo, tupo kwenye maandalizi kwa sababu tunao mpango kama Serikali kuhakikisha tunajenga SGR (reli ya kisasa) kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay inayounganisha pamoja na matawi la Liganga na Mchuchuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, tunao mpango wa kujenga reli tena kutoka Tanga mpaka Musoma ili kuunganisha na maeneo yenye machimbo au madini ikiwemo na Engaruka ambako tuna Magadi Soda, pale Minjingu tuna Phosphates na kule Dutwa tuna Nickel. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili anataka kufahamu hatua ambayo Serikali imefanya katika ujenzi wa Meter gauge kutoka Tabora kwenda mpaka Kigoma. Kwanza, nimwambie Mheshimiwa Mbunge, Serikali tayari imeshasaini mkataba na mjenzi ameanza kazi kutoka Kaliua mpaka Mpanda kilometa 210, ambapo zaidi ya bilioni 379 zimeidhinishwa na Mheshimiwa Rais wetu mpendwa ili kuhakikisha kwamba ukanda huo unakwenda kuboreshwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, ninavyozungumza hapa, tumeshasaini mkataba wa reli kutoka Tabora mpaka Kigoma na tunasubiri mkandarasi aweze kuanza kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ninamwomba Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine wa Kigoma wawe na subira, siyo muda mrefu neema inaendelea kuja kwao. (Makofi)
MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Katika Reli ya MGR, Station ya Goweko ilikuwa ina njia tatu, lakini mlitoa njia ya pili na ya tatu mkaacha njia moja, na pale tuna mizigo mingi. Ni lini mtarudisha reli ile ili wananchi wa Goweko wapate fursa ya kupakia mizigo yao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba nikae na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kufuatilia jambo analolizungumza niweze kulifanyia kazi kwa ufasaha zaidi.
MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali madogo wawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza. Je, kuna ufuatiliaji au tathmini ya mafanikio haya yanayotolewa na Wizara kwa wanawake hawa wajasiliamali? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kufuatia ufinyu na idadi ndogo ya wanawake wajasiriamali katika fursa zinazotokana na uchukuzi, je, Wizara inachukua hatua gani kukabiliana na changamoto hii hasa katika upatikanaji wa taarifa na mitandao ya biashara? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi kwa kutambua umuhimu mkubwa wa nafasi ya mwanamke katika jamii, imeendelea kufuatilia na kuratibu kuhakikisha kwamba mwanamke kama kiongozi, kama mwanamama anakuwa sehemu muhimu ya kushiriki katika uendeshaji wa shughuli za usafirishaji katika nchi yetu. Hivi ninavyozungumza tayari kozi mbalimbali kama nilivyozungumza zinaendelea kutolewa na tathmini imefanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya ajira milioni 16.3, wanawake ni takribani 3,200,000. Ninawahakikishia Waheshimiwa Wabunge, tutaendelea kuhamasisha na kuhakikisha kwamba wanawake wanashirikishwa kikamilifu katika shughuli mbalimbali za usafirishaji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, Mheshimiwa Mbunge ameuliza swali la pili kuhusiana na jinsi Wizara ilivyojipanga. Kwanza, tumejipanga kuhakikisha kwamba Ilani ya CCM, Toleo la 2025 ambayo imeelezea vilivyo katika Ibara ya 231, Kifungu cha (g) na (h), nafasi ya mwanamke na kuimarisha vituo vya mafunzo. Tutaendelea kukisimamia kifungu hicho kuhakikisha kwamba wanawake wanapata fursa hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia, kwenye upande wa Kanuni za Manunuzi ya Umma, imeeleza vizuri sana kwenye Kanuni Namba 35, jinsi mwanamke anavyopaswa kupewa fursa, ambapo imeelezwa kwamba takribani 30% ya kazi au bidhaa au shughuli zitolewe kwa wanawake.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, ninamhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kufanya kazi kubwa ya kuhakikisha kwamba mwanamke anashiriki ipasavyo katika kujenga uchumi wa Taifa lake kupitia sekta yetu ya usafirishaji. (Makofi)
MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza. Kwa kuwa Serikali imeanza utafutaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa reli hii, je, haioni upo umuhimu wa kupata wabia ili kuharakisha ujenzi wa reli hii?
MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu. Ah, okay, kuna swali la pili.
MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kwa kuwa Magufuli City ni eneo ambalo Wizara mbalimbali za Serikali pamoja na Idara za Serikali zipo kule na ufikaji wake nao umekuwa ni wa kusuasua, je, Serikali haioni kwamba miongoni mwa vipaumbele vya maeneo ya viunga vya Dodoma kujengewa reli kama hii ni pamoja na Magufuli City? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru Mheshimiwa Fatma Hassan Toufiq kwa jinsi anavyofuatilia kwa ukaribu mapinduzi ya reli nchini na kipekee reli ya maeneo ya mijini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ameuliza maswali mawili; la kwanza ni umuhimu wa kupata wabia. Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuwa na wabia wa Sekta Binafsi katika ujenzi wa miundombinu ya reli na miundombinu mingine, mwaka 2023 ilifanya maboresho ya Sheria Na. 10 ya 2017 ambapo sasa tumeruhusu wawekezaji binafsi au wabia kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa reli yetu. Hivi ninavyozungumza, tumekwishaanza taratibu kwa ajili ya kupata wabia kwa ajili ya ujenzi wa reli hiyo katika Jiji la Dar es Salaam na Jiji la Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hiyo pia kuendelea kutangaza kwa yeyote mwenye mbia yeyote ambaye anapenda kushiriki katika maeneo haya mawili, nafasi na fursa ipo wazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, amezungumzia kwenye upande wa Magufuli City. Sote ni mashahidi kwamba huu ni mji mzuri na mkubwa ambao Serikali imetenga fedha nyingi kuuendeleza. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Magufuli City ni sehemu ya mradi wa Commuter train wa hapa Dodoma, hivyo basi, tumeshakamilisha usanifu, na sasa tunatafuta fedha. Tutakapopata fedha, hatua itakayofuata ni utekelezaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimpe habari njema Mama yangu Mheshimiwa Toufiq, anakumbuka juzi tarehe 30 mwezi wa Tano hapa Dodoma, CCM ilizindua Ilani yake ya Miaka Mitano ijayo. Ukienda katika ukurasa wa 25 mpaka 31 imeainisha kwa kina miradi itakayokwenda kutekelezwa. Katika miradi hiyo ukisoma ukurasa wa 29, mradi huu umetaja kwa kina wa kujenga reli ya kisasa katika Miji ya Dar es Salaam na Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo basi, tumwombee Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aweze kuendelea kuongoza nchi yetu kwa kipindi cha pili kwa maana ya kwamba atakapochaguliwa itadhihirisha na kumaanisha tunakwenda kutekeleza miradi hii miwili ambayo nimeshaielezea hapo awali.
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwa kuwa, Bandari yetu ya Dar es Salaam inafanya vizuri, na magari ya mizigo ikiwemo ya mafuta yameongezeka sana kwenye barabara hiyo ambayo inapita katikati ya jiji, je, sasa ni lini wananchi waliopisha ujenzi wa hiyo barabara wakiwemo wa Kata ya Inyala, Kata ya Ijombe, Kata ya Swaya, Kata ya Igale, Kata ya Lwindi na Kata ya Bonde la Songwe watalipwa fidia?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kipande cha kilomita 22 wa barabara ya Isyonje – Kikondo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru Mheshimiwa Oran Njeza kwa maswali yake ya nyongeza mawili ambayo ameyauliza ambayo kimsingi yanasadiki umuhimu wa barabara yetu hii kubwa katika kusaidia Bandari yetu ya Dar es Salaam na kuinua sekta ya uchukuzi nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumza kuhusiana na upande wa fidia. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hiyo, uthamini umekamilika kwenye barabara ya Mbeya bypass na tayari tumeshaanza kulipa fidia. Tumelipa shilingi bilioni 10 kwa ajili ya wananchi wa maeneo hayo. Hivyo, nawaomba wananchi wote wanaonisikiliza wa Kata alizozitaja ikiwemo Kata ya Ijombe, Swaya, Igale, Lwindi na Songwe kwamba Serikali inaendelea kutafuta fedha na inao mpango wa dhati wa kuwalipa fidia ili wapishe eneo hilo au eneo hilo liende kutumika kwa ajili ya barabara yetu ambayo tumeizungumza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia amezungumza kuhusu jambo la pili barabara ya Isyonje – Kikondo kilomita 22 hadi Makete kwamba ni lini pengine ujenzi wake utakamilika? Nimpe uhakika Mheshimiwa Mbunge pamoja na Waheshimiwa Wabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama tunavyofahamu mpaka sasa Serikali imekamilisha ujenzi wa kilomita za lami zaidi ya 12,000 na katika Awamu ya Sita peke yake; miaka minne zaidi ya asilimia 10, zaidi ya kilometa 1,300 barabara za lami zimejengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi, kutokana na umuhimu mkubwa wa barabara hii aliyoizungumza, inayounganisha Mikoa miwili katika Mkoa wa Njombe pamoja na Mkoa wa Mbeya, tayari usanifu wa kina umeshakamilika na ujenzi umeshaanza kuanzia kwenye Mkoa wa Njombe.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwape matumaini wananchi wa Mbeya na watu wa mikoa yote hii miwili na maeneo mengine kwamba tunakwenda kujenga barabara hiyo kama ambavyo tumekuwa tukiwaeleza, kwa sababu tayari kazi imeshaanza.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, awali ya yote ninaomba kukupongeza na kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa na nzuri ambazo amezifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa leo tuko kwenye Wizara ya Kilimo, Mheshimiwa Rais wetu amejipambanua vyema kabisa katika eneo la kilimo kuhakikisha kwamba anaongeza bajeti kubwa na ya kutosha ili Tanzania iweze kujilisha yenyewe hatimaye Afrika na tuweze kuilisha dunia.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba tunazungumzia suala la pembejeo, pembejeo hizi ni muhimu sana kwa kuwa bila pembejeo uzalishaji unakuwa ni chini. Sasa swali langu ni kwamba, Wizara tuliomba na walitupangia kutupatia pesa shilingi bilioni 31.3 kwa ajili ya bonde letu la Kinyope. Je, Serikali lini mtatupatia hizi pesa shilingi bilioni 31.3 ili tuendeleze kilimo na kilimo hiki kitaleta manufaa kwa vijana pamoja na wanawake?
Mheshimiwa Spika, ninaomba jibu la Serikali. Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ninampongeza sana Mheshimiwa Mbunge mama Salma Kikwete, Mbunge wa Mchinga, anafanya kazi nzuri sana katika jimbo lake.
Mheshimiwa Spika, ninamthibitishia tu kwamba maelekezo ambayo Serikali imeshatoa katika hili bonde ambalo ameliainisha na maombi ya fedha ya shilingi bilioni 31.3, tayari Wizara ya Kilimo tumeshayapeleka Wizara ya Fedha na tunasubiri tu taratibu zikamilike ili tuhakikishe bonde lile linakamilishwa na linaanza utekelezaji wake kama tulivyoainisha. Ahsante sana.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu haya ya Serikali, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kama Serikali ilivyokiri, kwamba mradi huu ni wa muhimu, lakini ni wa muhimu kwa nchi yetu kuliko ilivyo wa muhimu kwa nchi nyingine za Afrika Mashariki, ikiwemo kuongeza thamani na utekelezaji wa haraka wa Mradi wa LNG wa Lindi ambao ni mradi mkubwa kuliko yote katika historia ya nchi yetu. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kuuchukuwa mradi huu kutoka kwenye miradi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na kuufanya mradi wa Serikali yetu ili tuutekeleze utupe advantage kwa nchi za Afrika Mashariki?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; je, Serikali ipo tayari kushirikiana na wabia wanaotekeleza Mradi wa LNG wa Gesi wa Lindi katika kutafuta rasilimali za ujenzi wa reli hii kwa sababu nao ni wanufaika wakubwa wa kusafirisha mizigo na wananchi watakaokwenda kutekeleza mradi huu wa gesi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Nape Nnauye kwa swali lake la msingi na maswali ya nyongeza ambayo ameyaongezea. Ninakubaliana naye kwamba mradi huu ni muhimu kwa uchumi wa Taifa letu. Serikali ilipoamua kuuingiza kwenye Master Plan ya East Africa msingi wake ni nini? Ni kutaka uingizwe katika vipaumbele vya Kanda ya Afrika Mashariki; lakini mbili ni kutaka tushirikiane katika utafutaji wa pamoja wa rasilimali fedha kwa miradi yote iliyopo katika kanda hii; na tatu ni kutaka mradi huu usomane na miradi mingine inayotekelezwa katika jumuiya hii; kwa hiyo ndiyo hoja ya kwanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na kwamba ni muhimu na kwamba tuiingize kwenye kipaumbele chetu, hilo tumelipokea na tunakubali kwamba ni muhimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili ambapo kimsingi ni dhana ya PPP; kwamba je, Serikali haioni sasa ni muhimu kushirikiana na wawezekaji wanaofanya Mradi wa LNG. Pengine labda uniruhusu niseme kwa ufupi sana kuhusu concept ya PPP.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali zote duniani zinatambua na kuthamini mchango wa sekta binafsi katika kukuza uchumi wa mataifa yao; na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameendelea kuweka mazingira mazuri na rahisi ili wawekezaji, ama sekta binafsi iweze kunawiri na kustawi katika nchi yetu ili ishiriki katika kujenga uchumi wa nchi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa, kwenye upande wa reli ukitazama miradi ambayo inatekelezwa, ukiangalia kuanzia kipindi cha uhuru mpaka miaka 2020 tulikuwa na reli ya mita gauge ambayo ni kama 2700 pamoja na TAZARA ambayo ni kilomita kama 975, ukijumlisha kwa pamoja ni kilomita 3,600. Mipango ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na Serikali yake ni nini? Ni kujenga reli ya SGR peke yake yenye urefu takriban 4,700. Tayari hivi ninavyozungumza miradi yenye urefu wa kilometa 2,100 imekwishaanza kutekelezwa; na ipo kwenye mpango wa kujenga reli ya kusini kilomita 1,000 kaskazini, kilometa 1,000 pamoja na reli ya mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukichukua miradi hii peke yake fedha inayohitajika kwa ujenzi ni matrilioni. Hapo ndipo unakubali kwamba ni lazima uzishirikishe sekta binafsi katika kujenga miundombinu hiyo. Ukishamaliza kuijenga bado utahitaji vitendea kazi, vichwa na mabehewa. Ndiyo maana kwa kutambua hilo sekta ya uchukuzi kama Serikali ilibadilisha Sheria Namba 10 ya Mwaka 2017 ili kuruhusu sekta binafsi kuingia katika ujenzi wa miundombinu ya reli.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo basi, nimhakikishie Mheshimiwa Nape Nnauye pamoja na Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali inatambua umuhimu huo na kwa kweli inakaribisha wadau wote, wale wa LNG pamoja na wadau wengine waje tushirikiane kujenga uchumi. Hii ni kwa sababu tulipoanza kujaribisha tumeona faida yake. Kule TAZARA kama tunavyofahamu tuliporuhusu open access, yaani watu walete mabehewa na vichwa vyao, takriban nusu ya mzigo imeongezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, kule Bandarini vilevile tuliporuhusu sekta binafsi washiriki katika ujenzi wa nchi yetu tumeona meli zimeongezeka kutoka 4,200 zipo 4,800, mzigo umeongezeka kutoka tani milioni 17 zilizokuwepo mwaka 2020 leo zipo tani milioni 32. Kwa hiyo sekta binafsi ni muhimu sana na Serikali inawakaribisha katika kushiriki kwenye nchi yetu.
MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa nafasi. Hitaji la Uwanja wa Ndege wa Njombe ni kubwa sana kutokana na uchumi wa Njombe, lakini ni mradi wa kimkakati, pia ni ahadi Rais, ni lini sasa ujenzi wa uwanja huu utaanza?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mwanyika kwa ufuatiliaji wake wa karibu sana juu ya Uwanja wa Ndege wa Njombe. Yeye na Wabunge wenzake wa Mkoa wa Njombe wanafanya kazi nzuri. Serikali imetambua na kuthamini umuhimu wa uwanja wa Njombe kama nilivyosema kwenye kubebea mazao kama vile parachichi na kadhalika na kwa sababu hiyo, Serikali inakwenda kujenga uwanja mkubwa. Ni hatua gani tuko mpaka sasa hivi?
Mheshimiwa Spika, tayari tulikuwa kwenye hatua ya kwanza ya kutafuta eneo, kwa sababu eneo la pale mjini halitoshi. Tayari viongozi wa mkoa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege wanashirikiana. Hatua ya pili tunayokwenda sasa ni kwa ajili ya kufanya usanifu ili tuweze kujua kiasi gani kinachohitajika uwanja utakaojengwa uweze kwenda sawasawa na hadhi ya Mkoa wa Njombe.
MHE. KAFITI W. KAFITI: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, bado sisi kama Mwanza na kama wakazi wa Jimbo la Ilemela, tunahitaji kujua huo upembuzi yakinifu utakamilika lini?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, ukamilishwaji wa uwanja huu...
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Kafiti Mbunge wa Ilemela alikuwa anajaribu kukazia hoja ile ile ya uwanja wa ndege na kimsingi yeye pale kwake hoja kubwa ambayo anaizungumzia ni upande wa fidia au namna ya kuweza kuondoa wananchi wa pale. Serikali ina dhamira ya kuufanya Uwanja wa Ndege wa Mwanza kuwa wa kimataifa. Ili uweze kuwa na sifa hizo, lazima kama kuna wavamizi waondolewe. Kwa hiyo, nimwombe tu awe na subira, tutamilisha muda siyo mrefu tutaanza kufanya kazi.
MHE. BONNAH L. KAMOLI: Mheshimiwa Spika, pamoja na kazi nzuri ambayo inafanywa, Mkoa wa Dar es Salaam especially Kipunguni ambako Serikali imefanya kazi kubwa kuwalipa wananchi wa pale, lakini bado kuna wananchi ambao wanahitaji kulipwa ili waondoke. Je, ni lini Serikali itawamalizia hawa wananchi wa Kipunguni pesa zao ili waweze kuondoka maana hapo kuna mateso makubwa? Ninashukuru.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi ya kujibu tena swali lingine la Mheshimiwa Bonnah, Mbunge wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kazi ambayo alishaianza huko mwanzoni kwa ajili ya wananchi wa Kipunguni. Kama tunavyofahamu wananchi hawa wamekuwa wakidai fidia zao kwa miaka mingi sana, lakini ni Dkt. Samia Suluhu Hassan, mara baada ya kuingia na mpaka mwaka jana kati ya fedha walizokuwa wanazidai amekwishalipa bilioni 66 kwa wananchi karibu 717 kati ya 1,147. Nimwombe Mheshimiwa Bonnah na Wabunge wote wa Mkoa wa Dar es Salaam wavumilie, wale waliobakia watakwenda kulipwa kadri ya upatikanaji wa fedha Serikalini.
MHE. MASANJA K. KADOGOSA: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa hii fursa. Serikali ilifanya tathmini ya uwanja wetu wa Simiyu eneo la lgegu na hiyo tathmini ilifanyika kwa takribani miaka minne iliyopita. Je, ni lini sasa Serikali itatoa fidia lakini vilevile kuanza ujenzi wa uwanja ule?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mshimwa Spika, ninampongeza Mshimiwa Kadogosa kwa kufuatilia Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Simiyu kwa sababu pia ni sera za Serikali kuhakikisha kwamba angalau kila mkoa unaweza kupata uwanja wa ndege.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Serikali imeshakamilisha usanifu wa uwanja huo na tumebaini kwamba tunahitaji eka karibu 3,386 na wananchi 700 kama na 92 ambao tumewatambua pale kiasi wanachodai ni shilingi bilioni 6.2. Nimwombe avumilie. Mara baada ya upatikanaji wa fedha tutaweza kwenda kulipa eneo hilo. (Makofi)
MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Kadogosa ameuliza ila ninataka kukazia hapo. Ni muda mrefu tunauliza kuhusu ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mkoa wa Simiyu na Uwanja ule ukikamilika watalii watakua wanashuka. Pale ni karibu kwenda Serengeti na Ngorongoro. Ni lini sasa uwanja huo utakamilika? Tunataka kauli ya Serikali kwa sababu ni muda mrefu eneo limeshatengwa. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa swali la nyongeza la Mheshimiwa Midimu ambaye anasisitiza umuhimu wa Uwanja wa Ndege wa Simiyu. Kama nilivyokwishakujibu pale mwanzoni kwamba tayari tumekwishaainisha kiasi cha fidia kinachohitajika shilingi bilioni sita pamoja na wananchi ambao tunatakiwa tuwafidie na eneo lenyewe.
Mheshimiwa Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge, mpango wa Serikali ni mzuri. Ukiangalia miaka mitano nyuma na sasa ni tofauti. Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imekwenda kujenga viwanja karibu vyote nchini. Ni maeneo machache sana ambayo hatujayafikia. Ukiangalia Kanda ya Ziwa peke yake ambapo Waheshimiwa wako huko: Shinyanga, Musoma, Serengeti (tunakwenda kuanza kujenga), Kyabajwa na Mwanza yenyewe. Ninaomba Ndugu zangu wavumilie, tunakwenda kufikia eneo hilo. (Makofi)
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, ningependa kumwuliza swali la nyongeza Mheshimiwa Waziri. Mheshimiwa Naibu Waziri amesema lile jengo la Mwanza litabaki kama jengo la general aviation na lina mkataba wake na yeye amefanya upembuzi yakinifu kwa ajili kujenga jengo la international. Kama halivunjwi kwa nini mkandarasi anaondoka asimalizie lile jengo? Ninakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, tunaendelea na mazungumzo katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza ikiwezekana kujenga kwa kupitia mwekezaji binafsi (Sekta ya PPP) tushirikiane na mjenzi. Kwa hiyo, nimwombe awe na subira tukikamilisha taratibu atapata taarifa nzuri zaidi.
MHE. AMINA ALI MZEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, pia ninaipongeza Serikali yetu inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uendelezaji bora wa Bandari ya Dar es Salaam. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Ni yapi manufaa ambayo yamepatikana katika uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam hasa kutokana na uwekezaji ambao umefanyika mwaka 2023?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni ipi mikakati ya Serikali katika kuboresha Bandari ya Dar es Salaam katika kukuza biashara na kuweka ushindani katika East Africa na SADC?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza sana Mheshimiwa Amina Ali Mzee, Mbunge wa Viti Maalum ambaye anawakilisha kundi la vijana, kwa sababu kupitia maelezo yake na ufuatiliaji wake anathibitisha umuhimu na namna ambavyo vijana wa CCM walivyo makini kufuatilia maendeleo ya vijana wenzao katika Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kazi kubwa imefanyika na ninashukuru kwa pongezi zake ambazo amezielekeza moja kwa moja kwa Serikali hii ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa maono makubwa na mapana ya namna ya kutumia bandari zetu kugeuza kuwa uchumi kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ushirikishwaji wa sekta binafsi katika uendeshaji wa bandari kwenye Taifa letu, upo kwa mujibu wa sheria. Hivyo basi, baada kuona umuhimu mkubwa, ndiyo maana Serikali ikaamua kufanya hivyo. Ninapenda sasa kumjibu kwenye hoja yake aliyozungumza kuhusu manufaa ambayo tumeyapata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, ifahamike kwa Watanzania na Wabunge wote kwamba tuliposhirikisha sekta binafsi, especially DP World kwa ajili ya kuendesha kitengo namba moja, mwaka 2024 haikuwa mara ya kwanza. Mara ya kwanza, kazi hii iliwahi kufanyika mwaka 2000 ambapo wenzetu wa TICTS walipewa mkataba wa zaidi ya miaka 20 kuendesha sehemu ya makasha pale Dar es Salaam. Mwaka 2024 tulishirikisha wenzetu wa TICTS pamoja na wenzetu wa DP World kitengo cha kwanza, pamoja na East Africa Gateway Terminal Limited kitengo cha pili ili watusaidie katika kuendesha. Manufaa ambayo tumeyapata ni mengi na makubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, ni kwenye utoaji wa huduma ya meli. Hapo zamani, kuna kitu kilikuwa kinaitwa ship turnaround time, yaani muda ambao meli inatumia kuanzia inapofika, inakwenda kuhudumiwa na inaondoka. Zamani zilikuwa zinatumika takribani siku 30. Zimeshuka mpaka kuwa siku nne kutokana na kazi kubwa ambayo wanafanya wenzetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, kuna kitu kinaitwa Ship turn at berth, yaani muda ambao meli inahudumiwa ikiwa kwenye eneo la gati. Zamani tulikuwa tukitumia kuhudumia mpaka siku 10, lakini imeshuka mpaka siku tatu. Hii yote inaongeza ushindani wa bandari yetu. Ndiyo maana ukienda kwenye ranking leo za bandari unakuta bandari yetu imekuwa ya 373 wakati ya wenzetu majirani zetu pale Mombasa imekuwa ya 393. Kwa hiyo, tuko mbele yao kiufanisi. Tembeeni kifua mbele Watanzania, kwa sababu kazi hii ni nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, manufaa makubwa ambayo tunaweza kuyazungumza, mengine ni kwenye upande wa makasha. Makasha yaliyokuwa yanahudumiwa wakati huo kwa Bandari ya Dar es Salaam peke yake ilikuwa 728,000, leo imefika 1,080,000. Hivyo, kuifanya Bandari ya Dar es Salaam kuwa miongoni mwa Bandari kubwa katika Bara la Afrika. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni shehena kwa maana ya mzigo. Wakati huo tulikuwa tunahudumia tani 16,000,000 kwa maana ya Bandari ya Dar es Salaam. Leo imefika tani 27,000,000 ndani ya muda mfupi ya muda miaka michache. Hii yote ni kwa sababu ya uwekezaji ya ambao tumeufanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni kwenye idadi ya meli. Meli zilizokuwa zinahudumiwa kwenye Bandari ya Dar Salaam peke yake ilikuwa ni meli 880 zimeongezeka mpaka kufika meli 1,245, wakati meli zote Kitaifa zimeongezeka kutoka meli 4,241 mpaka meli 4,888. Hii yote ni kwa sababu ya maono ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuamua kushirikisha wawekezaji katika bandari yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, magari yaliyokuwa yanahudumiwa mwaka 2021/2022 mpaka 2023, yalikuwa ni machache, takribani magari 100,047. Mara baada ya kufanya maamuzi hayo, magari yanayohudumiwa yamefika 216,000. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, hata mapato ya TPA yalikuwa shilingi bilioni 896 kwa mwaka. Mara baada ya kufanya maamuzi haya, mapato yakaongezeka mpaka yakafika takribani shilingi trilioni mbili, ya TPA 1.3, na yanayobaki ya wawekezaji. Pesa hiyo ndiyo imekwenda sasa kwenda kujenga na bandari nyingine kwenye nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, hata wenzetu wa TRA wameongeza fedha zao maradufu zaidi. Fedha kwenye Mfuko wa Serikali zimeongezeka, ndiyo maana hata wanafunzi wa elimu ya juu sasa wamekuwa wengi zaidi takribani 235,000 kutoka 170,000. Kwa sababu gani? Mheshimiwa Dkt. Samia ameongeza fedha kwenye mfuko wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, shehena ya nchi yetu inayokwenda kwenye nchi jirani ilikuwa ni tani 5,600,000. Kutokana na ufanisi na mzigo kuongezeka, shehena imeongezeka na kufikia milioni 12.6. Hata Wabunge wenyewe wanakubali na kusema kwamba kweli Mheshimiwa Dkt. Samia ameamua kuibadilisha nchi yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge ameuliza je, ni ipi mikakati ambayo Serikali hii ya Awamu ya Sita imejiwekea kuifanya Bandari yetu ya Dar es Salaam kuwa shindani? Ninataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na Mheshimiwa Amina Ali Mzee ambaye anatoa sauti kwa niaba ya vijana wa nchi hii wanaopenda kuona nchi yetu ikinufaika na uchumi wetu. Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anayo mikakati mingi, ninaomba nitaje michache:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, kama nilivyosema kwenye swali la msingi, ni kuhakikisha kwamba tunaongeza gati kwenye Bandari Dar es Salaam na tayari Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi ameshaanza vikao, na ameielekeza Mamlaka ya Bandari Tanzania iharakishe mchakato huo ili tupate gati nyingi zaidi.
Muheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo haitoshi, tunaboresha reli yetu kama ulivyoona ule mradi ambao tunaufanya na mzigo tunaobeba unafanyika wakati Reli ya TAZARA ambayo Mheshimiwa Dkt. Samia anaihubiri haijaanza kufanya kazi vizuri. Reli ya SGR haijaanza kutekeleza kazi yake vizuri. Je, tukikamilisha SGR, na kukamilisha TAZARA, hali itakuwaje? Maana yake ufanisi wetu utaongezeka zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi wote ni mashahidi, kila akisimama hapa Waziri wetu Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa Mnyaa anaelezea kwa kina na uchungu mkubwa umuhimu wa ushirikishwaji wa sekta binafsi. Moja ya mkakati wetu ni kuendelea kuwaalika Watanzania na wasio Watanzania, maadamu ni wawekezaji, waje kuwekeza kwenye sekta yetu. Walete meli, wajenge SGR, walete matreni na vitu vingine. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo ni nini? Kuiongezea uwezo mamlaka yetu. Hapa asubuhi mmesikia ninyi wenyewe kwamba tunakwenda kushirikisha sekta binafsi kwenye kujenga barabara kuondoa msongamano kutoka maeneo ya Kibaha mpaka Chalinze, kutoka Chalinze mpaka Morogoro na maeneo mengine. Yote hii sasa ili mzigo unaotoka Bandari ya Dar es Salaam uweze kufika maeneo husika katika muda ambao umepangwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
MHE. JANETH E. MAHAWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, ni kwa namna gani Serikali imeandaa programu maalumu au mafunzo ya uwezeshaji ili kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika miradi hii? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, Serikali imeweka mikakati gani kuhakikisha wanawake hawabaki nyuma katika fursa za zabuni na uwezeshwaji kiuchumi katika miradi mikubwa ya Serikali? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Janeth, kama ambavyo ameongezea. La kwanza, ametaka kufahamu programu na mafunzo mbalimbali, ambazo kimsingi Serikali hii inafanya katika kuimarisha wanawake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza kabisa, kama nilivyosema kwenye swali la msingi, msingi namba moja ni uwepo wa sheria na miongozo mbalimbali. Kwa hiyo, cha kwanza Serikali inahakikisha kwamba, sheria, miongozo na kanuni mbalimbali ambazo zinawapa fursa wanawake zinapewa msukumo wa kipekee, lakini pia ziko programu mbalimbali kama vile mafunzo ambayo kwa mfano wenzetu wa TanTrade wanayo, wenzetu wa Bodi ya Wakandarasi wanayo na kadhalika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mafunzo ya elimu kwa vitendo (internship) hapa yameongelewa mara kadhaa. Yote hiyo ni kuwajengea uwezo wanawake kuhakikisha kwamba, wanapata uwezo wa kushiriki katika ujenzi wa uchumi wa nchi yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, tumeweka mafunzo muhimu ya kiufundi, kama vile kupitia vyuo vyetu vya VETA, ambapo tunawajengea uwezo wanawake, wakimaliza, wakipata ufundi huo, waweze kwenda kwenye shughuli za uzalishaji mali na hivyo kuweza kushiriki kikamilifu kuwa na nguvu ya kifedha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, vipaumbele mbalimbali katika utoaji wa ajira, yote haya pamoja na mengine, imekuwa ni mambo muhimu ambayo tunayafanya, kama sekta, ikiwa ni pamoja na kutoa elimu mbalimbali katika masuala ya fidia, kwamba, fedha mtakazopata zitumikaje, ili isije ikatokea mtu amepata compensation halafu tena zile fedha amezitumia vibaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, kama tulivyozungumza, mikakati mbalimbali inatolewa kuhakikisha kwamba, wanapata nafasi kama vile kwenye zabuni na kadhalika. Hii ni pamoja na fursa za kielimu. Hapa kwenye elimu, nchi yetu imetoa nafasi kubwa kwa mwanamke kuhakikisha kwamba, kila mtoto wa kike anayetaka kusoma shule au anayetaka kwenda shule kuanzia elimu ya awali mpaka chuo kikuu, anashiriki kikamilifu bila ubaguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia inatoa fursa maalum kama vile ambavyo Mheshimiwa Rais kwa ubunifu wake amekujanavyo, kama vile Samia Scholarship Award, ambayo kimsingi inawasaidia watoto wa kike waliofanya vizuri kwenye masomo mbalimbali, kama vile sayansi, waweze kupata msukumo wa kipekee na kuwajengea uwezo waweze kufikia ndoto zao ambazo kimsingi wanazihitaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, financial institution zetu (taasisi za kifedha) zimekuwa ni maeneo mengine inapotokea mwanamke ana bidii katika shughuli za uzalishaji mali, wanatoa msukumo wa kipekee katika kumpa mikopo, ili kuhakikisha kwamba, wanawake kwenye nchi yetu wanafanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye Sheria zetu za Manunuzi, imetoa fursa na upendeleo maalumu, kwamba 30% ya kandarasi zetu au tender zetu, basi msukumo utolewe kwa wananchi, kwa wanawake, na pia, upande wa udhibiti vitendo vya kikatili ni moja kati ya mikakati ambayo Serikali inafanya, ili kumfanya mwanamke asijisikie mnyonge kwenye jamii, ashiriki kwenye uzalishaji kama kiumbe mwingine kwenye jamii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, kabla sijahitimisha ikiwa ni pamoja na kwenye uongozi, tayari unaweza kuona jinsi ambavyo wanawake wanashirikishwa katika masuala ya uongozi. Pamoja na kuwapa nafasi ya kushiriki kama watu wengine, bado wanapewa dawati la pekee kama vile kwenye Viti Maalumu ama katika uteuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo ni kwamba, washiriki katika maamuzi wanapotunga sera au kanuni au sheria na wao waweze kuwa sehemu ya kuwasemea wanawake wenzao nchi nzima. Ninaomba kuwasilisha.
MHE. EDIFONSI J. KANONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Wilaya ya Kalambo ina bandari ambayo ni muhimu sana katika uchumi wa nchi, uchumi wa Wilaya ya Kalambo na wananchi kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii bandari Serikali imewekeza shilingi 7,200,000,000 lakini kutokana na mabadiliko ya tabianchi, imezama toka mwaka 2023. Nini mpango wa Serikali kuboresha bandari hii ili ianze kufanya kazi iwanufaishe wananchi wa eneo lile pamoja na Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaweza kufafanua kidogo. Kwanza ninamshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa kuweza kutambua kazi ambayo Serikali imefanya kwenye upande wa Bandari yetu ya Kalambo, Mkoani Rukwa, ambapo ni moja ya bandari ambazo zilirasimishwa, lakini pamoja na kurasimishwa Serikali iliona umuhimu ikaiendeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa, pamoja na dhamira njema ya Serikali kuiendeleza tulipata changamoto kubwa ya maji. Kwa hiyo, maji yalijaa na yale maji hayakujaa kwenye Bandari ya Kalambo peke yake, ni karibu maziwa makuu yote. Tayari Serikali inaandaa mkakati, tumetafuta mkandarasi au mshauri mwelekezi, ambaye anatusaidia kutuambia nini tukifanye.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ni katika kutatua changamoto ya maji yaliyojaa kwa sasa hivi. Mbili, in long run, ni tufanye nini, ili tatizo kama hili likijitokeza, basi lisiweze kuathiri bandari zetu na hivyo, wananchi wa Kalambo na maeneo mengine wanufaike na bandari ambazo zipo kwenye maeneo yao.
MHE. MWINYI JAMAL RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa heshima hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa bandari hii ni bandari tegemezi kwa wafanyabiashara wetu kutoka visiwani na bara na inaleta tija sana kwa uchumi wa nchi yetu, swali langu lipo hapa, ni mara ngapi tangu nchi yetu imepata uhuru bandari hii imefanyiwa utanuzi ama ujenzi wa kuongezwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la nyongeza, katika jitihada za Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukuza uchumi wetu wa nchi na kuweka mkazo katika eneo hili, hatuoni sasa suluhisho la kuongeza uchumi wa nchi yetu ni kwa kutengeneza Bandari ya Bagamoyo? Sambamba na hilo, tujue, je, Bandari ya Bagamoyo kwa sasa imefikia wapi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Jamal Ramadhan kwa uzalendo wake mkubwa wa kufuatilia miundombinu ya kimkakati katika Taifa letu hususan roho ya nchi ambayo ni bandari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzia uhuru kwa kweli takwimu specific nitashindwa kuzisema hapa lakini ni mara ngapi Serikali imefanya maboresho? Ni mara nyingi katika kuhakikisha na kuona kwamba bandari hii inaongezewa uwezo. Pamoja na mambo ambayo yamefanyika huko nyuma, bado inaendelea kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano, tumeboresha gati namba sifuri mpaka namba saba ambapo imeongeza uwezo wa bandari yetu kuhudumia. Pia tumeongeza kina cha bandari yetu ili iweze pengine kuwa na urefu zaidi kwenda chini pamoja na kuongeza upana wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, tuna miradi mingine inayoendelea bandarini, kama vile kuunganisha reli kwenye bandari yetu, kuhakikisha kwamba tunajenga Gati Namba 12 mpaka 15, kama nilivyozungumza kuhakikisha kwamba, tunawezesha Kituo chetu cha Kurasini kinakuwa na uwezo mkubwa wa kuhudumia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, tayari kuna mradi mkubwa ambao uko 32%, mradi wa kujenga matenki 15 yenye uwezo wa kuhifadhi mita za ujazo wa mafuta 378. Maboresho yote hayo yana lengo moja tu la kuhakikisha kwamba, bandari yetu inazidi kuimarisha uwezo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, swali lake la pili la nyongeza ametaka kufahamu kuhusiana na ujenzi wa bandari yetu ya Bagamoyo ya Mbegani. Ni kweli kabisa ukiangalia uwezo wa mahitaji yetu sasa ya mzigo kutokana na diplomasia nzuri ya Rais wetu, na jinsi anavyosimamia Uchumi, unaona kabisa Bandari ya Dar es Salaam hata ungeifanyia maboresho kiasi gani inazidi kuzidiwa. Hivyo basi, Serikali imefanya maamuzi ya kuboresha au kuanza ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, Mbegani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ninavyozungumza, tumeshamaliza usanifu. Tayari tumeanza taratibu kwa ajili ya kuanza ujenzi, ili tuanze na kilomita moja, kwa ajili ya kupata kilomita 1.3, kupata gati ambayo itawezesha sasa meli kubwa ambazo kwa sasa haziwezi kutua kwenye Bandari ya Dar es Salaam, ambayo itakuwa inaweza kufika pale. Kwa kweli, bandari ile ikianza kufanya kazi itakuwa ndiyo bandari kubwa kuliko zote kwa ukanda wetu wa Afrika.
MHE. DKT. REGINA C. MALIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Nina swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri kuhusiana na Bandari ya Nansio katika Kisiwa cha Ukerewe. Bandari hii pia, imechakaa, imechoka, haijawahi kufanyiwa ukarabati tangu uhuru. Wakati mwingine hali ya hewa ikiwa ni mbaya meli pia zinapata shida kuweza kupaki. Kwa hiyo, ninaomba kujua, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa Bandari hii ya Nansio katika Kisiwa cha Ukerewe? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka anapoingia madarakani Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwaka 2021, takribani bandari 80 zilikuwa zinatambuliwa na kurasimishwa. Kutokana na umuhimnu wa sekta ya bandari, Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo maalumu na mahususi kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Wizara ya Uchukuzi kwanza, tufanye urasimishaji. Tumekamilisha urasimishaji na bandari zimeongezeka mpaka 142.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua ya pili ni kuanza kutafuta fedha, kuboresha bandari moja baada ya nyingine. Namwomba Mheshimiwa Malima awe na Subira, Bandari ya Nansio ni moja kati ya bandari muhimu kwenye Taifa letu. Tutakwenda kuifikia pindi fedha zitakapokuwa zimepatikana.
MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari ya Ujiji na Kibirizi zina mahusiano ya moja kwa moja na Bandari Ndogo ya Kagunga, ambayo iko mpakani mwa Burundi na Tanzania. Sasa nataka kupata majibu ya Serikali, ni lini mtakamilisha miradi fungamanishi, kama Barabara ya Mwandiga - Bubango - Chankere mpaka Kagunga, ambayo itakuwa kitovu cha kuweza kuunganisha nchi ya Burundi na Kongo na kuweza kuongeza uchumi katika Jimbo la Kigoma Kaskazini, Kigoma na Tanzania kwa ujumla?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Serikali imekuwa ikihusisha sekta binafsi katika uwekezaji wa bandari, kwa mfano Kigoma, Dar es Salaam na maeneo mengine. Taifa limenufaika na nini katika kushirikisha sekta binafsi? Ninataka majibu ya Waziri, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Mayeye kwa maswali yake na uzalendo kwa Taifa lake, jinsi anavyosimamia miundombinu na kuunga mkono kazi ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ni Wabunge wachache wanaweza kuelewa mchango ambao Mheshimiwa Rais anautoa katika Taifa letu. Kwa muda mrefu Wabunge kutoka Mkoa wa Katavi, Rukwa na Kigoma wamepiga kelele kutaka Serikali zote kuanzia ya kwanza mpaka sasa ziboreshe Ziwa Tanganyika kwa sababu ni uchumi, ni maisha, ni ulinzi na ni ajira kwa vijana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kumtaarifu Mheshimiwa Mayeye, na yeye ni shahidi kwamba Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ana miaka minne tu, lakini mambo aliyoyafanya kwenye eneo hilo ni ya kipekee. Ukiacha SGR anayojenga kuipeleka mpaka Kigoma ili kuhakikisha kwamba Kigoma inafunguka; ukiacha meli anazokarabati ikiwemo MV Liemba ambayo inakaribia 40%, MV Mwongozo ambayo ipo kwenye mpango wa Manunuzi, MT Sangara na meli ya mafuta inayofanya kazi; ukiacha kiwanda cha meli kinachojengwa pale Katabe, Kigoma, bado Mheshimiwa Dkt. Samia hajawaacha Wanakigoma pamoja na Ziwa Tanganyika kwa ujumla kwa sababu, ni yeye ameidhinisha mradi mkubwa wa maboresho wa Bandari tatu za Kibirizi, Kigoma na Ujiji na akapeleka fedha, shilingi bilioni 32.5 ambazo zimeboresha maeneo yale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi, Serikali hii kwa kutambua umuhimu wa Bandari hiyo ya Kagunga ilipeleka fedha shilingi bilioni tatu na kidogo, na tayari tumekamilisha pale gati ya mita 50. Kama nakubaliana naye, ni kweli kabisa, ili Mradi wa Bandari ya Kagunga uweze kuwa na tija kwa Taifa letu, na wananchi wa Kigoma ambao ninaamini wanafuatilia, ni lazima ufungamanishwe na miradi ya soko pamoja na barabara aliyoitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kulitambua hilo, tayari imeanza kwa upande wa soko. Wenzetu wa TAMISEMI wametenga shilingi bilioni 2.3 na wamemlipa mkandarasi shilingi milioni 222 kuhakikisha kwamba, soko linajengwa na faida ya soko lile inakwenda kufungua bandari. Watakuja wenzetu wa Congo, watakuja watu wa Burundi, watakuja eneo lile kwenye bandari na baadaye tutafanya kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, barabara hii aliyoitaja ya Mwandiga Chankere, Mwamgongo pamoja na Kagunga yenye urefu wa kilomita takribani 65, Serikali imeanza kufanya kazi, imejenga kilomita 18, ili bandari ile iweze kufunguka. Namwahidi Mheshimiwa Mbunge awe na subira na Wabunge wote wa Kigoma. Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anakwenda kuimarisha na kuendelea kuleta mapinduzi makubwa kwenye Mkoa wa Kigoma.
MHE. FLORENT L. KYOMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Naishukuru Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa kampeni yake aliwaahidi wananchi wa Misenyi na Mkoa wa Kagera kwamba ndani ya siku 100 ataanza utakelezaji wa mradi huo, na sasa ni ushuhuda, kutokana na majibu ya Serikali ndani ya siku 100 mtaalamu mwelekezi amefika site na kuanza upembuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa hatua hiyo, chini ya Wizara ya Uchukuzi, chini ya Waziri, Mheshimiwa Prof. Mbarawa na Naibu Waziri, Mheshimiwa David Kihenzile, kwa kazi nzuri wanayoifanya. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, uwanja huo ni wa Kimataifa, na utainua uchumi mkubwa Mkoa wa Kagera na Jimbo la Misenyi kwa ujumla, je, ni mkakati gani ambao Wizara ya Uchukuzi inaweza kuuratibu pamoja na halmashauri kupima na kupanga maeneo yote yanayozunguka eneo la uwanja huo, ili kuweza kuleta taswira nzuri na kuwainua wananchi hao kiuchumi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kwa kuwa, uwanja huo utakuwa wa kimkakati ukihudumia nchi za Maziwa Makuu, ni mwongozo upi ambao Serikali inautoa ili tuweze kujiandaa kwa shughuli za kiuchumi, ili uwanja huo sasa ukianza uwe na tija kubwa kwa wananchi wa Misenyi, Mkoa wa Kagera na Taifa kwa ujumla? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Kyombo kwa kutambua kazi nzuri ya Mheshimiwa Rais Samia, ambaye ndani ya siku 100 aliahidi na ameanza kutekeleza kwa ajili ya kujenga uwanja mkubwa wa Kyabajwa. Ninakubaliana naye, Serikali iko tayari kushirikiana na halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninawaomba halmashauri waweke mkakati huo na yeye mwenyewe Mbunge akiwa ni sehemu ya halmashauri, ili tupime maeneo yale yawe vizuri, wananchi wasivamie kwa sababu, uvamizi unatokea pale ambapo halmashauri ilikuwa inajua kwamba kuna jambo zuri linakuja, lakini haikuweka mkakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawaomba waanze kuweka mpango huo mzuri. Sisi kama sekta, kwa maana ya Wizara ya Uchukuzi, chini ya Mheshimiwa Prof. Makame Mbarawa, pamoja na TAA, tuko tayari kushirikiana na nyie kuhakikisha kwamba, tunaweka jambo hili vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, amezungumza kuhusiana na tija ya uwanja huo. Natoa wito na rai kwa wananchi pamoja na viongozi Mkoa wa Kagera kwamba, mradi huu ni mkubwa sana, utakwenda kuunganisha nchi yetu na mikoa ya jirani, utakwenda kuunganisha nchi yetu na mikoa ya jirani, utakwenda kuunganisha nchi yetu na nchi jirani. Ni vyema wakaanza kuchangamkia fursa za kiuwekezaji na tuwaombe wananchi wetu walinde ardhi yao, wasiuzeuze tu, maana hii inayokuja sasa ni neema.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Dkt. Samia anawaletea neema. Itakuwa ni jambo la kusikitisha baadaye ardhi yote imechukuliwa na watu wa nje, wao hawana ardhi. Hivyo basi, tuchangamkie fursa, tutazame cha kufanya kuhakikisha kwamba, uwanja huu unakwenda kuwa na tija kubwa kwa wananchi na Taifa letu.
MHE. YAGI M. KIARATU: Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Singida wana hamu sana ya kupata usafiri wa anga. Pamoja na kuchagiza shughuli za kiuchumi, usafiri na usafirishaji Singida ni katikati ya nchi. Singida ni jirani na Dodoma, ikitokea rubani akashindwa kutua Dodoma, mji wa karibu kutua ni Singida; lakini kwa sababu, Singida ni Katikati, itakuwa kiungo kizuri cha usafirishaji ndani ya nchi. Ninaomba kauli ya Serikali, ni lini sasa Singida watajengewa uwanja wa ndege? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge wa Singida Mjini na Mheshimiwa Mstahiki Meya Mstaafu kwa ufuatiliaji wake wa uwanja huu mzuri na muhimu kwa Taifa letu. Kama alivyoeleza yeye mwenyewe, uwanja huu ulijengwa miaka ya 1950 na Serikali imekuwa ikiutumia, lakini kwa kweli, kiwango chake kiko chini ni wa changarawe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na maombi ya Waheshimiwa Wabunge na wakati mwingine viongozi, Serikali imepokea kilio hicho na imeanza kufanya usanifu. Ninamhakikishia, tunakwenda kujenga Uwanja wa Singida na mwaka wa fedha 2026/2027 tunaingiza kwenye bajeti. Tunaenda kuongeza runway kutoka 1,000 mpaka 2,000, tunaweka lami pamoja na kuhakikisha kwamba, tunaweka taa, ili uwanja utumike mchana na usiku.
MHE. MARY F. MASANJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Uwanja wa Kimataifa wa Mwanza ni muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu, hususan Mkoa wa Mwanza. Uwanja huu mpaka sasa haujakamilika na ukizingatia ni wa muhimu kwa kuwa, tuko karibu sana na hifadhi ya Serengeti, ni kilomita 130 tu. Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha uwanja huu, ili angalau wananchi wa Mkoa wa Mwanza waanze kufaidika na uchumi unaotokana na masuala ya utalii?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nitakwenda kujibu kwa kifupi kama ulivyonielekeza. Ninampongeza Mheshimiwa Mary Masanja kwa kutambua umuhimu wa uwanja huu ambao kimsingi ndiyo kitovu cha Kanda ya Ziwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kulitambua hilo, moja, imeanza mchakato, kwa ajili ya kuboresha jengo la abiria; na pili, imeanza na documentation ili kuufanya kuwa wa Kimataifa pamoja na mambo mengine, kama vile kumaliza mgogoro wa wananchi ambao walivamia eneo la pembeni ili uweze kuwa na ulinzi. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inalitambua hilo na itaongeza kasi kuhakikisha kwamba, inauboresha na kuufanya uwanja huu kitovu ndani na nje ya nchi yetu.
MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka nijue ni lini Uwanja wa Ndege wa Musoma, kama kielelezo cha Mkoa wa Mara, utakamilika?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kwa kutambua umuhimu wa Mkoa wa Mara, ilianza ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mara. Pale Serikali inajenga runway, kwa maana ya njia ya kuruka na kutua ndege, pia inajenga na majengo mbalimbali. Tayari runway imekamilika, tunakwenda kumalizia majengo yaliyobaki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilisema ninaomba kurejea kauli yangu niliyoitoa siku tano au sita kwamba, kuanzia mwezi ujao au unaofuatia, Serikali ina mpango wa kuanza kufanya testing ya ndege za Shirika letu la Ndege ATCL kwenye viwanja vitatu; Uwanja wa Musoma, Shinyanga na Sumbawanga. Hii ni kuthibitisha dhamira ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba, ameamua kuitendea haki nchi hii kwenye sekta ya anga.
MHE. SIGRADA W. MLIGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nina maswali ya nyongeza kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa SGR mpaka Kigoma?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa uwanja wa ndege Mkoa wa Njombe ambapo ni Serikali hii tangu mwaka 2005 imeweka mkakati wa kuijenga lakini mpaka leo haijaanza? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Sigrada Mligo, kwa maswali yake ya nyongeza ambayo ameuliza kwa niaba ya Mheshimiwa Kiza Mayeye, Mbunge wa Kigoma Kaskazini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imejidhatiti na imekwishaanza ujenzi wa miradi ya SGR kutoka Dar es Salaam mpaka Dodoma ambapo takribani kilometa 722 zimekamilika kwa zaidi ya 99% na sisi sote ni wanufaika tumeshanza kuona matunda yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kutoka pale Makutopora mpaka Tabora kwenye kilometa 368 mkandarasi yuko site na yuko 14.5% na kutoka Tabora mpaka Isaka kilometa 165 mkandarasi yuko anafanya kazi yake vizuri na tunakabiria asilimia tisa. Vilevile, Isaka mpaka Mwanza karibu kilometa 341 napo mkandarasi anafanya kazi kwa zaidi ya 68%. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, pia kutoka Tabora mpaka Kigoma ambapo ni kilometa 506 mkandarasi ameshaanza kazi tayari yuko site na ukipita utamuona na tuko 10.3%. Kama haitoshi kutoka pale Uvinza kwenda mpaka Malagarasi na kutoka Malagarasi mpaka Msongati kwenda nchi ya pili tayari mkandarasi ameshapatikana, ameshasaini mkataba na kazi inaanza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Kiza Mayeye, kupitia Mheshimiwa Sigrada Mligo ambaye ameuliza swali hili, Serikali hii imedhamiria kukamilisha miradi hiyo haraka iwezekanavyo ili wananchi siyo tu wa Kigoma na Watanzania kwa ujumla wanufaike na uwepo wa kimkakati wa nchi yao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ambalo ameuliza kuhusiana na uwanja wa ndege wa Njombe, ninafahamu kwamba wananchi wa Mkoa wa Njombe na mikoa ya jirani ya Mbeya, Iringa, Songea kwa maana ya Ruvuma na Kusini kwa ujumla wamepaza sauti kwa muda mrefu ili kuhakikisha ujenzi wa uwanja wa ndege wa Njombe unakamilika. Kwa nini?
(i) Kwa sababu ya kusafirisha mazao ya mboga mboga kama horticulture na kadhalika;
(ii) Tunao mradi mkubwa wa Liganga na Mchuchuma katika Mkoa wa Njombe; na
(iii) Tunayo madini na vitu vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba aondoe mashaka. Serikali tumeshakubaliana, tumeshamkabidhi site mkandarasi ili akamilishe usanifu wa kina na pengine kabla ya mwezi wa sita mwaka huu atakuwa ameshakamilisha. Baada ya kukamilisha usanifu wa kina, taratibu za ujenzi zitaanza.
MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaishukuru Serikali kwa majibu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kutokana na umuhimu wa mradi huu, nini sasa mkakati wa Serikali kuhakikisha wanapata mwekezaji haraka iwezekanavyo na huu mradi uweze kutekelezwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa sekta ya uchukuzi ndio inachochea kwa kiasi kikubwa katika sekta ya utalii. Ni namna gani sasa sekta hii inaweza kufanya kazi kwa haraka na kuhakikisha kwamba inapata wawekezaji wa ndani ili mradi huu uweze kutekelezwa kwa haraka? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninampongeza Mheshimiwa Esther Malleko, kwa uzalendo wake na jinsi anavyofuatilia kwa ukaribu miradi ya uchukuzi lakini hasa pia uwanja wa ndege kule Kilimanjaro na Kaskazini kwa ujumla. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekwishamjibu kwamba usanifu unaendelea. Nimhakikishie mara tutakapokamilisha, tumeshamaliza usanifu sasa tupo kwenye hatua ya kupata mkandarasi. Atupe muda, ninajua anatamani kuona kazi hiyo inaanza hata kesho. Tukishapata mwekezaji ambaye yuko tayari, tukishaelewana naye tutakuwa tayari kwa ajili ya kuanza kazi hii. Na nitoe rai, kwamba wawekezaji wa ndani na nje wachangamkie fursa hizi za kujenga hoteli kwenye viwanja vya ndege ili kuhakikisha sekta yetu inaboreka zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Mbunge ametaka kufahamu jinsi ambavyo tumejipanga kama sekta katika kuhakikisha kwamba tunashirikisha wawekezaji wa ndani katika uboreshaji wa miundombinu ya uchukuzi kwenye Taifa letu. Sote tunakumbuka mwaka jana tarehe 17 Julai, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Dira ya 2050. Katika dira hiyo ambayo kimsingi itaanza kutekelezwa tarehe 1 Julai, 2026 inasema tunataka tujenge Taifa kubwa la Tanzania ambalo litakuwa mfano katika ukanda wa Afrika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunataka tujenge Taifa kubwa ambalo uchumi wake kama ambavyo mnakumbuka Mheshimiwa Profesa Kitila mara kwa mara amekuwa akirudia ambayo itakuwa na uchumi wa dola trilioni moja, sasa hivi tunazungumzia uchumi wa karibu dola bilioni kama 87. Anasema tunataka tujenge Taifa ambalo wananchi kipato chao kitakuwa ni dola 7,000 sasa hivi unazungumzia kipato cha kama dola 1,200 au 1,300.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ili tufikie azma hiyo, lazima sekta binafsi ipewe fursa ya kushika uchumi kwa sekta 70% kwa sababu hiyo, kama mnataka mjenge Taifa kubwa la namna hiyo ambalo 70% mmetoa kwenye sekta binafsi haukwepi kushirikisha wawekezaji binafsi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kama mnakumbuka wakati Mheshimiwa Rais anazindua dira yetu, alisema anataka mapitio ya sheria zetu za uwekezaji ambazo zinakwenda kulinda na kuhamasisha wawekezaji mbalimbali duniani, lakini mkazo ikiwa ni wawekezaji wa ndani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Esther Malleko kwamba Serikali inajipanga na nitumie nafasi hii kuwasihi wawekezaji wote wa ndani wachangamkie fursa katika miradi ya uwekezaji kwenye reli, kwenye viwanja vya ndege, kwenye SGR kuweka treni, kwenye bandari ili uchumi wa Taifa letu ushikwe na wazawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitoe rai kwa wawekezaji wa nje kwamba yapo manufaa makubwa wanayoyapata endapo wakija wakashirikiana na wawekezaji wa ndani ya nchi yetu. Kuna baadhi ya vitu ambavyo kimsingi wanapewa kupitia wenzetu wa PPP.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba kuwasilisha. (Makofi)
MHE. KASSIMU A. MBARAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, shukrani, nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, kwa kuwa hii ndiyo reli ya kwanza kujengwa, ndani ya Taifa hili la Tanzania wakati huo ikiitwa Tanganyika. Je, Serikali ina mpango gani sasa kuimarisha na kuiboresha reli ya meter gauge yaani MGR, kuweza kutoa shehena nyingi, kubwa na kutosha kutoka pale Tanga, Kilimanjaro hadi Arusha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la nyongeza, je, ni upi mpango wa Serikali kukifanya sasa Kituo cha Pugu, Pugu Station kwenye reli yetu ya mwendokasi inayoenda speed ili ya express, kuweza kukifanya kuwa sasa ni kituo kama kituo kingine cha kushukia, tuseme cha tatu kutokea Dodoma na pia kutokea Dar es Salaam kiweze kutumika effectively, kwa reli ya mwendokasi inayoenda speed. Ni lini Serikali itakifanya kile kituo ni cha muhimu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Kassimu Amari Mbaraka kwa maswali yake ya nyongeza na nampongeza jinsi anavyofuatia maendeleo ya Mkoa wa Tanga na Kaskazini kwa ujumla.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, Serikali inasimamia Reli ya meter gauge yenye urefu wa kilometa 2,707 ambayo ilipokuwa inajengwa ufanisi wake ilikuwa ni kubeba mzigo wa takribani tani milioni tano. Kutokana na changamoto mbalimbali, reli ya Kati pamoja na Kaskazini uwezo umeshuka mpaka umefika takribani 290,000 sawa na 5.8%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tayari maboresho yameshaanza kwa upande wa reli ya kati na tayari ninavyozungumza Serikali imeshaagiza material kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunapata vitendea kazi vya kuanza ujenzi wa kutoka Ruvu kuelekea Dar es Salaam na hatua ya pili itakuwa kutoka Ruvu - Tanga mpaka Kilimanjaro, ili kuhakikisha kwamba tunaijengea uwezo kutoka kwenye speed ya ratili 20 mpaka 15 iliyopo sasa iweze kwenye uwezo wake wa 80 mpaka 70.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yake ya pili kuhusu Kituo cha Pugu ili tuweze kuongeza. Msingi wa reli ya kisasa ni kufupisha safari. Tunayo treni yetu ya kawaida inayofanya safari zake za kawaida kutoka Dar es Salaam mpaka Dodoma, na kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro na Morogoro mpaka Dar es Salaam na kadhalika ambayo kutoka Dar es Salaam mpaka hapa tuna vituo karibu 10. Serikali iliamua kuweka treni nyingine ya express ambayo inatoka Dar es Salaam mpaka Morogoro, ikitoka Morogoro kituo kinachofuatia ni hapa. Tumepokea maombi yake, lakini msingi tulidhani kwamba, tuendeleze ratiba hii kwanza, ikionekana kuna uhitaji sana baada ya uchambuzi wa kina tutafanya hivyo, kwa muda huu tunawashauri abiria wa pale Ruvu waweze kupanda treni ya kawaida ya kisasa ambayo na yenyewe inatumia masaa kama manne tu, na hii nyingine ni kama karibu masaa matatu na robo. Ahsante.
MHE. MGORE M. KIGERA: Mheshimiwa Spika, nashukuru, kwanza napenda kutoa pongezi na shukrani za dhati kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa majibu mazuri ya kuonesha dhamira ya dhati ya kuweza kufufua ya New Musoma Hotel. Nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeonesha nia ya kuanzisha Tourism Corridor between Serengeti National Park na Lake Victoria. Je, haioni sasa umuhimu wa kuharakisha mchakato huu ili kuweza kupata mwekezaji huyo kwa uharaka. Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Mipango na Uwekezaji aliwaahidi wananchi wa Jimbo la Musoma Mjini kufikia Julai, mwekezaji huyu atakuwa amekabidhiwa hoteli hiyo. Ni lini sasa Serikali itaona umuhimu wa kulifanya hili kwa uharaka?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kupitia hoteli ya New Musoma, itaweza kuleta watalii pamoja na wawekezaji kwa uharaka. Tuna uwanja wetu wa ndege wa Musoma, mpaka sasa haujaweza kuanza kufanya kazi. Je, Serikali inatuambia nini Wananchi wa Musoma na Mkoa wa Mara, uwanja huo lini utaanza kufanya kazi rasmi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mgore Kigera, kwa jinsi ambavyo anafuatilia maendeleo ya wananchi wa Musoma, wilaya au mkoa ambao ni muhimu kwa Taifa letu.
Mheshimiwa Spika, kwanza, tunatambua umuhimu huo ndiyo maana tumeshaanza mchakato Serikalini kuifufua hoteli hiyo, kushirikisha sekta binafsi, kwa sababu tunatambua kwamba pale Musoma kuna ziwa, kuna shughuli za uvuvi na usafirishaji majini, pale Musoma kuna hifadhi kwa maana ya kwamba watalii wanahitaji kupata hoteli nzuri ambayo ni ya kisasa, pale Musoma kuna madini, lakini pale Musoma kwenye Mkoa huo ndipo anapotoka baba wa taifa. Kwa hiyo, watu wengi sana wangependa kwenda katika mkoa huo.
Mheshimiwa Spika, tayari tumeshaanza mchakato huo na mhusika mmojawapo mwekezaji binafsi ambaye ameonesha nia ameshapatikana. Tutakwenda kwa ushauri wake alioutoa, ambao ndio wa Kibunge, kuongeza kasi ya majadiliano ili tufike hatima nzuri, hatimaye hoteli hii muhimu iweze kuanza kufanya kazi.
Mheshimiwa Spika, swali la pili; ameuliza kwamba hoteli hii itategemea pia iweze kupokea wateja au watu wanaokuja kwenye shughuli mbalimbali ambao kimsingi tunakusudia moja ya usafiri utakaotumika ni uwanja wa ndege, anataka kufahamu ni lini utakamilika.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeonesha kutambua na kuthamini umuhimu wa kuboresha Uwanja wa Ndege wa Musoma ndio maana imeidhinisha shilingi bilioni 36 na ujenzi uko 67%.
Mheshimiwa Spika, wiki iliyopita Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa Profesa Mbarawa, alinituma hapa nitoe route mpya ya ndege zetu na miongoni mwa maeneo ambayo aliyatolea maelekezo ni pamoja na Uwanja wa Ndege wa Musoma pamoja na Shinyanga ambapo mwezi huu tunakusudia kuanza majaribio ya ndege kwenye viwanja viwili, Musoma pamoja na Shinyanga. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimsihi Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wengine kuendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Dkt. Samia, kwa sababu anazidi kuleta tabasamu kwa wananchi wake. (Makofi)
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuweza kunipatia fursa na mimi kuuliza swali.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Tanzania tunatarajia kunufaika na uwepo wa AFCON na ukuaji wa utalii, na kwa kuwa wageni ambao watakuja kipindi cha AFCON watahitaji hoteli zenye hadhi ya nyota nne mpaka tano wengine.
Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuweza kufufua au kutafuta wawekezaji kwenye hoteli za umma ambazo zimetelekezwa kwa muda mrefu kama vile Motel Agip na Embassy ili ziweze kuongeza malazi, ajira na mapato ya taifa kuliko kuendelea kuwa liability kwa Taifa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, aliyeuliza kwa ujumla hoteli mbalimbali za Serikali.
Mheshimiwa Spika, mimi kimsingi, kwa niaba ya Waziri wa Uchukuzi, nitajikita kwenye miradi iliyopo kwenye sekta yetu. Kama ambavyo nimeshaanza kumjibu Mheshimiwa Mgore, tunatambua maeneo mbalimbali, kwanza, kwa ajili ya kuongeza ajira, ukifufua hoteli unaongeza ajira kwa wananchi, lakini pili, unaimarisha utalii. Kwa maeneo ambayo ni ya kimkakati ambapo AFCON inakwenda kutumika maana yake pia inasaidia kuongeza accommodation, wananchi waweze kupata mahali au washiriki kwenye kombe hilo, waweze kushiriki.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ametuongezea msukumo mkubwa zaidi ya kutushauri na kutukumbusha Serikalini ili tuendelee kuona umuhimu wa kuweza kufufua maeneo hayo kwa maslahi ya Watanzania wote.
MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kumekuwa na utaratibu mara nyingi wa kufanya usanifu kwa ajili ya mabwawa, lakini baada ya kukamilika usanifu wa mabwawa ndiyo kazi ya ujenzi wa skimu inafuata na jambo hili huwa linachelewesha kazi hizi. Je, Serikali haioni sasa iko haja ya usanifu wa skimu za umwagiliaji na mabwawa haya uende kwa pamoja?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na kazi nzuri ambayo Serikali inafanya, lakini iko ahadi ya muda mrefu ambayo ilitolewa na Serikali kupitia kwa Waziri Mkuu ya ujenzi wa bwawa kwa ajili ya Skimu ya Mombo pamoja na ujenzi wa eneo la Skimu ya Kwamkumbo. Ni lini ahadi hii ya Serikali itatekelezwa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Kilimo, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Timotheo Mnzava, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, la kwanza, napenda kumpongeza Mheshimiwa Mnzava ni mfuatiliaji mzuri sana wa miradi ya umwagiliaji kwenye jimbo lake, lakini na kwa nchi nzima. Kwa kweli amethibitisha jinsi ambavyo vijana wakiaminiwa wana uwezo wa kufuatilia mambo makubwa kwenye majimbo na kwenye nchi hii, ili Taifa letu liweze kusonga.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na ushauri wake ambao amesema kwamba kwa nini isiende pamoja mambo yote mawili, kwanza nipende kupokea, lakini pili, kupitia Waziri wa Kilimo, nimwombe Mkurugenzi wa Tume ya Umwagiliaji wapokee ushauri huu, uchakatwe na kama utaonekana pengine unaweza kuwa na tija, tuanze kuufanyia kazi kwa sababu lengo letu wote ni kujenga.
Mheshimiwa Spika, la pili, kuhusiana na kufufua Mto Soni, moja nipende kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imekwisha kamilisha usanifu wa miundombinu ya umwagiliaji kwa maana ya Skimu za Mombo pamoja na bwawa. Kwa kuwa tumeshakamilisha, hatua inayofuata ni kuanza manunuzi kwa ajili ya kumpata mkandarasi huyo.
Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya kumpata mkandarasi huyu, tutakwenda kuanza utekelezaji ili wananchi wake wa Korogwe ambao kimsingi anawapenda sana, waweze kunufaika na miradi hii. Naomba kuwasilisha.
MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Spika, ahsante, katika Jimbo la Nanyumbu, Kata ya Masuguru, kuna Skimu ya Umwagiliaji katika Bwawa la pale Lukula na Kijiji cha Masuguru. Upembuzi yakinifu umefanyika na umekamilika na usanifu wa kina umekwisha. Ni lini sasa ujenzi wa skimu hii utaanza ili wananchi wa kata ile waweze kunufaika na mradi huu?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mhata, Mbunge wa Nanyumbu kwa swali lake la nyongeza alilouliza kuhusiana na skimu ya wananchi wake.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii imetambua umuhimu mkubwa sana kwa maana ya kuboresha skimu za umwagiliaji nchini na ndiyo maana, siyo tu imeongeza bajeti ya kilimo kutoka shilingi bilioni 294 mpaka shilingi trilioni 1.1, lakini pia imeongeza bajeti nzima ya miradi yote inayotekelezwa nchini kama ambavyo kimsingi Mheshimiwa Waziri alizungumza ambapo miradi zaidi ya 886 nchi nzima ipo kwenye hatua mbalimbali, ikiwemo na ile miradi 146 ambayo naamini na ya kwake ni mmojawapo.
Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira. Iko miradi ambayo inatekelezwa na kukamilishwa, ipo mingine ambayo tunategemea kwenda kuanza, na ipo mingine tunakwenda kusaini, wakandarasi wanakwenda kusaini, lakini na mingine tunakwenda kuanza hatua za usanifu. Awe na subira, Serikali itakwenda kufikia miradi yote ikiwepo na wa kwake kulingana na upatikanaji wa fedha za Serikali.
MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Skimu ya maji ya umwagiliaji ya Kata ya Endagaw, ina zaidi ya miaka 15. Imetumia fedha za Serikali shilingi bilioni 1.5 na mara ya mwisho mkandarasi ana miaka miwili toka aondoke.
Je, ni lini Serikali itaenda kukamilisha Skimu ya Miradi ya Maji ya Endagaw, na je, Mheshimiwa Waziri uko tayari twende tukakague fedha hizi nyingi za Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ambazo ametuletea lakini bado hazijaleta matokeo chanya kwa wananchi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga ambaye anawapigania wananchi wake kuhakikisha kwamba skimu ya umwagiliaji ambayo Serikali imeshaianza inakamilika.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunayo miradi takribani 71 ambayo ipo kwenye hatua mbalimbali, kuanzia asilimia moja mpaka 99% kuelekea 100%. Naamini mradi huu ni mmojawapo. Hapa nyuma nchi hii imekuwa na mambo mengi ya kufanya na wewe ni shahidi. Tumekuwa na fedha nyingi tumepeleka kwenye SGR ambayo leo Watanzania wananufaika, tumepeleka kwenye Bwawa la Mwalimu Nyerere. Nina uhakika, baada ya kukamilisha miradi hii mikubwa, kasi ya maendeleo kwenye miradi mbalimbali ikiwemo ya maji, ukiwemo huu wa kwako itakwenda kukamilika. Naomba uwe na subira.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na ombi la kuambatana na mimi Mheshimiwa Mbunge kama Mheshimiwa Waziri wa Kilimo asipokuwa na nafasi, yeye au Naibu wake, akanituma mimi nimwakilishi, sitaweza kukataa maelekezo ya Serikali. (Makofi)
MHE. JASMINE C. NG’UMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, swali langu ni kuwa; je, ni nini mpango wa Serikali kuhakikisha skimu za umwagiliaji zinafika katika Mkoa wa Iringa, hususani katika majimbo yote saba, ili kuweza kuwasaidia vijana wa Mkoa wa Iringa kujiajiri, lakini pia kulima kilimo cha kisasa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mbunge wa Vijana, Mheshimiwa Jasmine Ng'umbi kwa jinsi ambavyo anawapigania vijana wa nchi hii. Yeye na Wabunge wenzake ambao wanawakilisha vijana hapa Bungeni wamethibitisha umuhimu wa kuwa na vijana makini wanaofuatilia masuala ya maendeleo ya vijana, kwa maslahi ya Taifa leo na kesho.
Mheshimiwa Spika, kwa swali lake ambalo kimsingi anauliza kwa upande wa Mkoa wa Iringa kwamba ni lini skimu hizi zitakamilika.
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa katika mkoa wetu wa Iringa, Wizara ya Kilimo inatekeleza miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na uchimbaji wa visima virefu karibu kwenye majimbo yote saba katika mkoa wetu. Pili, tuna miradi takribani 24 ambayo ipo kwenye hatua mbalimbali ya usanifu, lakini tatu, tunayo miradi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Mradi wa Ruaha Mbuyuni, Mradi wa Mgololo, Mradi wa Mkombozi na Miradi mingine, ambayo kimsingi inatekelezwa. Serikali inampa uhakika Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote ambao wanataka kufahamu kuhusiana na Mkoa wa Iringa na maeneo mengine, itakwenda kuongeza kasi kuhakikisha kwamba maeneo hayo, au wananchi wa Mkoa wa Iringa hususani vijana ambao yeye anawawakilisha, wanakwenda kunufaika ili washiriki kwenye uzalishaji, wapate ajira, wajenge uchumi na waweze kusaidia shughuli mbalimbali katika familia zao.
MHE. EMMANUEL J. KHAMBAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali itakamilisha zoezi la upembuzi yakinifu juu ya ujenzi wa bwawa la umwagiliaji katika Kata ya Bagara, hususani eneo la Kijiji cha Nakwa ili wananchi wa eneo hilo waweze kunufaika na kilimo cha umwagiliaji?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, napenda kujibu swali la nyongeza kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameweza kuuliza kwamba kama nilivyosema hapo awali, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge. Kasi ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha kwamba, wananchi wake wananufaika na nchi hii na ameamua kukifanya kilimo kuwa uti wa mgongo.
Mheshimiwa Spika, ili kukamilisha hoja hiyo, eneo la umwagiliaji, ambalo wakati anaingia yeye madarakani lilikuwa ni eneo dogo sana la kumwagilia, takribani eneo la hekta laki sita, wakati Mungu ametupa fursa ya eneo lenye ukubwa zaidi ya hekta milioni 40. Ninakuhakikishia Mheshimiwa Mbunge na ukawaambie na wananchi, Waziri wa Kilimo anawaambia, atakwenda kuwafikia maeneo yote ambayo ni ya kimkakati ili wananchi waweze kuzalisha na tuweze kuuza nje ya nchi na ndani ya nchi chakula pamoja na mazao mbalimbali.
MHE. MOSES C. BUJAGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, barabara hii ya Fulo - Nyambiti – Malya ilitakiwa kukamilika huo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kufikia mwezi wa Aprili, 2026. Ningependa kufahamu ni kwa nini kazi hiyo haijakamilika mpaka sasa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, barabara hii kwa sasa iko katika hali mbaya sana na ndiyo inayobeba uchumi wa Jimbo la Sumve, minada ya Bungulwa, usafirishaji wa mazao kama dengu na pamba ambayo ndiyo msimu wa sasa hivi utakuwa ni changamoto. Serikali ina mpango gani kuhakikisha barabara hii inapitika, ili kurahisisha usafirishaji wa mazao na usafiri wa wananchi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Moses Charles Bujaga, Mbunge wa Sumve, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, awali napenda kumpongeza kwa jinsi ambavyo amekuwa ni mtu wa shukrani ya kutambua kazi nzuri ambayo inafanywa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye eneo lake, lakini pili, amekuwa ni mfuatiliaji makini, kwa huu muda mfupi wote tunashuhudia, anavyopigania barabara za jimbo lake na hata za mkoa wake kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika, ameuliza kwa nini haijakamilika katika muda uliokuwa umepangwa; moja, mhandisi mshauri alikuwa ameshakamilisha ile kazi, lakini kama unavyofahamu, mahitaji yanazidi kuongezeka. Timu ya wataalam ikapitia na kubaini kwamba kuna mambo mengine ambayo yakiongezwa, yatakuwa na maslahi mapana zaidi kuliko walivyofikiria pale awali na kimsingi jambo hili ni jambo jema kwa sababu pengine barabara ya awali ilikuwa inakusudiwa, ilitazamiwa kwa mahitaji ya pale mwanzoni.
Kwa hiyo, wataalamu wakaona iko haja kufanya maboresho, ili barabara itakayofikiwa kuamuliwa kujengwa, iendane na ndoto na matamanio ya yeye Mbunge, wananchi na Taifa letu kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika, nimwombe awe na subira, kwa sababu baada ya hatua hii sasa, tumemwongezea mkandarasi muda, angalau mpaka kabla ya mwezi wa Agosti au kabla ya mwaka huu haujaisha ili kazi hii iwe imekamilika.
Mheshimiwa Spika, la pili; ameuliza kwamba barabara hii imekuwa ni mbovu ambayo kimsingi sisi Serikali tunakubaliana na yeye na tunampa pole kwa changamoto hiyo, kawaida barabara hii itakiwa ifanyiwe ukarabati mara mbili kwa maana mwezi wa 10 pamoja na mwezi Mei mpaka Juni. Mwaka jana mwezi wa 10 ukarabati mzuri ulifanyika, sasa kipindi kama hiki ambacho wakulima na wananchi wanakusudiwa kusafirisha mazao mbalimbali kama vile pamba, dengu na mazao mengine barabara hiyo kweli ni mbovu.
Mheshimiwa Spika, tayari taratibu zimeshaanza kufanyika ili mkandarasi huyu sasa aingie kazini hivi karibuni na namwelekeza kwa Niaba ya Waziri wa Ujenzi amenituma nimwelekeze Meneja wa TANROADS ili alisimamie jambo hili mkandarasi huyo aingie kazini, aanze kufanya kazi na aboreshe barabara hii ili wananchi wa Sumbe na Mkoa wa Mwanza na maeneo jirani kwa ujumla waweze kunufaika na barabara hii na kujenga uchumi wao.
MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Rungwe kuna barabara ya muhimu sana inayotoka Kiwila, Kinyala inapita Isangati inatokea Mbalizi. Barabara hiyo wananchi wanateseka sana namna ya kusafirisha mazao yao na kusafiri wao wenyewe hasa wanawake.
Mheshimiwa Spika, je, ni lini barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Suma Fyandomo, Mbunge kutoka Mkoani Mbeya anayewakilisha kina mama kwa jinsi anavyowapigania Wananchi wa Mkoa wa Mbeya wakiwemo wa Rungwe, wakiwemo wa Kyela, Mbozi, Chunya na maeneo mengine yote na kimsingi barabara hii sisi kama Serikali tunatambua umuhimu wake.
Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Suma Fyandomo pamoja na Wabunge wa majimbo wa maeneo hayo na wananchi kwa ujumla wawe na subira, Serikali inatambua umuhimu wa barabara hii na maeneo mengine ni muhimu yakajengwa kiwango cha lami, lakini kwa sasa sungura ni mdogo tujipe muda wakati utafika itajengwa na watafurahia.
MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Tunayo barabara ya kutoka pale Nyashimo kwenda Dutwa Wilaya ya Bariadi kupitia pale Maliri, Shigala, Ngasamo pamoja na Dutwa yenyewe inayounganisha wilaya mbili na tumekuwa tukiahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami.
Je, ni lini Serikali sasa itaanza ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami kwa ajili ya uchumi wa hizi wilaya mbili?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi swali la Mheshimiwa Songe ambaye anaielezea barabara hiyo yake muhimu na nipende kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge pamoja na Wabunge wengine wote kwa sababu naamini eneo hili ni eneo nyeti sana Serikali inatambua umuhimu wa barabara katika uchumi wa Taifa lake na kwa sasa kama ambavyo Waziri wa Ujenzi amesimama mara kadhaa tupo kwenye mchakato Serikalini, kwanza ya kutambua wakandarasi ambao walikwishaanza kazi wamesimama, wakandarasi ambao walikwishaanza kazi walisimama na ambao pengine mikataba yao hawajisainiwa lakini pia maeneo mengine ambayo bado hayajasainiwa na yanayotakiwa kutangazwa.
Mheshimiwa Spika, niwahakikishieni mlimsikia mwenyewe Mheshimiwa Waziri Mkuu akizungumza hapa na naomba tuwe na subira Waheshimiwa Wabunge. Barabara hizi baada ya kuwa tumeshafanya kazi nzuri ya kusimamia uchaguzi wenyewe kwa hela zetu kujenga Daraja la Busisi, kujenga SGR, kujenga Bwawa la Mwalimu Nyerere na kufanya mambo mengine mengi makubwa ninayo hakika Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anakwenda kujenga barabara mbalimbali kwenye nchi hii zikiwemo hata zile za kule Mufindi ambazo tunazipigania kila wakati.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Barabara ya Mlima Magara katika Jimbo la Mbulu Mjini barabara yenye jiografia ngumu sana, na kwa kuwa mkandarasi aliyekuwa anajenga zege katika Mlima Magara amesimama kwa muda wa zaidi ya mwaka moja; ni lini mkandarasi atarudi site ili akamilishe zege katika Mlima Magara?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia barabara yake muhimu ambayo kimsingi mkandarasi alikuwa site kama alivyoeleza amesimama.
Mheshimiwa Spika, mara tutakapokamilisha taratibu za fedha tukishamlipa mkandarasi huyo atarejea kufanya kazi na wewe Mheshimiwa Mbunge na wananchi tunaomba muwe na subira kwa kipindi hiki.
MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, barabara inayotoka Kahama kupitia Nyang'hwale mpaka Busisi ni barabara muhimu sana kwa biashara na uchumi wa Mkoa wa Geita. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, Serikali inayo dhamira ya kuhakikisha wananchi wanaopita kwenye barabara hiyo inayotokea Kahama wanaboreshewa barabara hiyo, lakini kwa sasa kwa kuwa fedha hazipo tunaomba wananchi wavumilie, tunaendelea na mchakato Serikalini pale itakapokuwa tayari Serikali itakwenda kujenga kwa kiwango cha lami.
MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Bariadi kwenda Lamadi ina hali mbaya sana, ina mashimo na mabonde imebomoka bomoka. Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa barabara hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi namwelekeza Meneja wa TANROADS wa Mkoa huo wa Simiyu aende atazame barabara ambayo imelalamikiwa na Mheshimiwa Mbunge ili atazame kiwango cha uharibifu na kisha kuweza kuweka mpango wa namna bora ya kuweza kuikarabati ili Serikali na wananchi waendelee kunufaika.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Barabara yetu ya Milola - Kiwawa, Milola - Kutwa itajengwa kwa kiwango, mimi sihitaji lami mimi nahitaji changarawe na hizi barabara ni muhimu sana na hizi barabara umuhimu wake mkubwa ni sehemu ambayo inazalisha ufuta kwa kiwango kikubwa sana na ukubwa wa barabara hii ni kilometa sita tu. Je, lini Serikali itatupatia pesa kujenga barabara hizi?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi ninamwelekeza Meneja wa TANROADS aende akaone eneo hilo la kilometa sita ambalo limelalamikiwa au limeombewa na Mheshimiwa Mbunge kwamba lina usumbufu na hivyo linahatarisha biashara ya ufuta pamoja na wananchi kupita kwenye maeneo hayo na kwa msingi Mbunge anatimiza jukumu la msingi la Kibunge la kuishauri na kuisimamia Serikali na sisi Serikali hii ya Mheshimiwa Dkt. Samia wakati wote tumesisitizwa kuwa wasikivu kwa sauti za Wabunge na mara baada ya kujua mahitaji halisi basi Serikali itachakata na kuwa namna bora kuweza kufanyia kazi ombi la Mheshimiwa Salma Kikwete, Mbunge kama alivyoomba.
MHE. SALUM K. SALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini tu kumkumbusha kwamba barabara hiyo imewekwa kwenye ilani safari ya tatu hii ilani tatu na siku zote inakosa fedha. Sasa ni muhimu mkajua umuhimu wa barabara hiyo kusudi bajeti hii itengewe fedha na mkandarasi aanze.
Mheshimiwa Spika, pili, barabara hiyo inakutukutanisha sisi Mkoa wa Simiyu pamoja na Mkoa wa Singida kwa Daraja kubwa la Mto Sibiti, Daraja la Sibiti lilivyojengwa lilikuwa lina kilometa 24 za lami ambazo contractor CHICO alishapewa mkataba huo, kwa hiyo, tunaiomba tena Wizara impe fedha mkandarasi CHICO kusudi ajenge kilometa 24 ambazo kilometa zingine zitakuwa kwa Mkoa wa Singida na zingine Mkoa wa Simiyu.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi nampongeza Mheshimiwa Salum Khamis Salum kwa kuendelea kufuatilia miradi ya kimkakati ikiwemo barabara hii muhimu sana kwa uchumi na maisha ya wananchi wake.
Mheshimiwa Spika, kimsingi kama alivyosema barabara hii imekuwa ikiahidiwa mara kadhaa kwenye Ilani ya CCM, lakini pamoja na kuahidiwa mara kadhaa kwenye ilani za huko nyuma ni wajibu wetu yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote kuweza kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua sasa kwanza kuijenga, kitendo cha kusaini mkataba na kampuni ya CCECC ni dhamira ya dhati kwamba Serikali sasa imeamua inaenda kuijenga.
Mheshimiwa Spika, na kwa sasa kama ambavyo tumesema kwenye majibu ya msingi Serikali baada ya kuwa imeshasini mkataba inafanya taratibu za kutafuta fedha Serikalini.
Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi kwa ujumla wawe na subira dhamira ya Serikali ya kuijenga barabara hii kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge mara kwa mara anakumbushia iko pale pale, subira yavuta kheri, tutaifikia barabara hiyo kuijenga vizuri na wao watafurahia.
MHE. KANGI A. LUGOLA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya kutoka Busambara hadi Mugara - Iramba zaidi ya miaka 10 tuliomba iingizwe kwenye huduma ya TANROADS na tunaambiwa mchakato unaendelea zaidi ya miaka 10.
Sasa je, ni lini mchakato huu utakamilika kwa sababu barabara hii inaendelea kuharibika sana na mpaka sasa magari hayapiti? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y. WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Kangi Lugola kwa kukumbushia ombi lake muhimu, ninaomba awe na Subira, wakati Serikali inaendelea na mchakato wa kina wa kuona namna bora ya kuweza kuihudumia barabara hiyo, na mara baada taratibu zitakapokamilika Serikalini basi ombi la Mheshimiwa Kangi Lugola litakwenda kukamilika.
MHE. RAMADHANI H. SINGANO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara ya Mombo – Soni - Lushoto ni barabara ya kimkakati kwa majimbo matatu. Ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuipanua barabara hii ili kukidhi haja katika eneo hili?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge pia kwa kufuatilia barabara yake ambayo ni muhimu kwa sababu barabara ndiyo mishipa ya uchumi wa nchi yetu, lakini muombe awe na subira. Tutaendelea na mchakato Serikalini itakapokuwa tayari tutakwenda kuikamilisha na hivi ndivyo tunakwenda Serikalini kwa vipaumbele, baada ya kumaliza hatua moja tunakwenda hatua nyingine barabara moja tunakwenda barabara nyingine.
MHE. MORRIS J. MAKOI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Barabara ya Kagongwa – Igusule - Mwamara mpaka Nzega imeshajengwa mpaka tabaka la tatu kutoka Kagongwa kwenda Igusule kilometa 18.3 kilichobaki ni kuwekwa lami kipande hicho cha kilometa 18.3. tukikiacha kitaharibika.
Mheshimiwa Spika, sasa Serikali ina mpango gani wa kukamilisha uwekaji wa lami kilometa 18.3 kutoka Igusule kwenda Kagongwa ili kuokoa thamani ya fedha iliyotumika hadi sasa?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Morris kwa kukumbushia barabara yake muhimu kama ambavyo nimesema kwenye majibu ya msingi, Serikali inayo dhamira ya dhati na inawahakikishia Wabunge wote ikiwemo Mheshimiwa Mbunge huyu miradi yote ambayo tumekwisha kuianza tutakwenda kuikamilisha na ile ambayo tunakusudia kuianza Serikali inakwenda kuikamilisha.
Mheshimiwa Spika, naomba awe na subira kwa kuwa tumeshaonesha nia, Serikali imekwisha anza ujenzi hata kipande hicho Serikali itakwenda kukikukamilisha ili kuwaweza kusikiliza kilio na maombi ya wananchi wa eneo hilo kama ambavyo imewasilishwa na Mheshimiwa Mbunge leo.
MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante, barabara inayotoka Mkunze inaenda Iponyang’olo - Ilamba, Igwamanoni inapakana na wenzetu wa Masumbwe ni barabara ambayo imepanda kwenda TANROADS leo miaka minne, lakini haijawahi kutengewa fedha na wala hawajafika hata kuikagua. Ni nini mkakati wa Serikali juu ya barabara hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa uvumilivu wake pamoja na kwamba anasema barabara yake haikutengewa fedha na kwa kweli anafuatilia sana maendeleo ya jimbo lake, wilaya yake na sekta zote.
Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Cherehani vuta subira. Serikali hii imefanya mambo mengi na makubwa zaidi haitashindwa kujenga barabara za nchi hii ikiwemo ya kwako. Tujipe muda hatua kwa hatua, tutaifikia barabara yake na yeye atafurahi pamoja na wananchi kama ambavyo tumekwisha fanya kwenye maeneo mengine ya maji, umeme pamoja na sekta zingine ndani ya jimbo lako.
MHE. IBRAHIM M. SHAYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri umekuwa ukiniambia kila siku tarehe 01 Juni, mkandarasi ataingia site kuhusu barabara ya Mailisita kuelekea Kiboroloni ya njia nne. Je, ni lini unawaambia wananchi wa Moshi Mjini mkandarasi ataingia site?
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI K.n.y WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Shayo kwa jinsi ambavyo anakumbushia barabara hii. Endelea kuvuta subira Mheshimiwa Shayo, tunakamilisha taratibu za kifedha ndani ya Serikali kama ambavyo Serikali hii imefanya mengi kwenye Jimbo la Moshi na wewe unafahamu kwenye uwanja wa ndege tumepeleka mabilioni pale, nataka nikuhakikishie hata hii vuta subira tutakwenda kufika na wananchi wa Moshi watafurahia.