Contributions by Hon. Deogratius John Ndejembi (14 total)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema kwa kutujalia zawadi hii ya uhai na kuweza kuiona siku hii ya leo. Pili nitumie nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendela kuwa na imani na mimi kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi yake Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa kumsaidia Mheshimiwa Angellah Jasmine Kairuki hapa TAMISEMI, ni imani kubwa sana, ni imani kubwa sana.
Mheshimiwa Spika, vilevile nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wananchi wa Jimbo la Chamwino hapa Mkoani Dodoma, kwa imani yao ambayo wanayo kwangu mimi kama Mbunge wao na niwaahidi tu wanachamwino kuendelea kuwatumikia kama vile ambavyo wanatarajia kutoka kwa Mbunge wao na tutaendelea kushirikiana kila siku katika changamoto mbalimbali za Jimbo letu la Chamwino.
Mheshimiwa Spika, nikienda moja kwa moja kwenye hoja mbalimbali ambazo Wabunge walizizungumza humu ndani, karibia kila Mbunge aliyesimama humu alizungumzia suala la barabara kupitia TARURA. Waheshimiwa Wabunge, wengi mlisifu sana jitihada ambazo zimefanyika na taasisi ya TARURA nchini ya Engineer Seif, niwatoe mashaka Waheshimiwa Wabunge, ninyi mmekuwa ni mashahidi kwamba ndani ya mwaka mmoja TARURA imefanya kazi kubwa sana kwenye Majimbo yetu, kuhakikisha barabara zinapitika kwa kuhakikisha madaraja yanapitika.
Mheshimiwa Spika, mtakumbuka mwaka mmoja na nusu ama miwili iliyopita kabla ya Serikali hii ya Awamu ya Sita kuingia madarakani, TARURA walikuwa na bajeti ya Bilioni 257 tu, lakini ni utashi wake Rais wetu Dokta Samia Suluhu Hassan, aliona namna ifanyike kuweza kuongezea TARURA fedha. Fedha ile imekwenda kuleta mabadiliko makubwa ambayo huenda tungeyasubiri kwa miaka mingine 10 au 15 kuweza kufikia utengenezaji wa barabara kama tulivyofikia sasa.
Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wote mmesema fedha TARURA haitoshi, niwatoe mashaka katika mwaka huu wa fedha bajeti imeachwa vilevile kama ilivyokuwa mwaka jana na tunakwenda kutekeleza miradi yenye thamani ya Bilioni 838 kwa fedha za ndani na fedha za nje kutoka TARURA. Hii ina maana kila mmoja wetu humu kwenye Jimbo lake na kwenye Mkoa wake anaenda kufikiwa na taasisi yetu ya TARURA.
Mheshimiwa Spika, Watanzania mamilioni na mamilioni wanaenda kufikiwa na TARURA na ninaamini mwakani tukirudi hapa kama ambavyo walikuwa wakimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa TARURA na Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI, Waheshimiwa Wabunge hapa mtazidi kutoa pongezi hizo katika bajeti ambayo inafuata.
Mheshimiwa Spika, kitu ambacho naweza nikasema kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ni kutoa commitment yetu ya usimamizi wa miradi hii. Tutahakikisha hakuna ubadhilifu, tutahakikisha inaenda kukamilika kwa wakati, vilevile tutahakikisha value for money inakuwepo katika miradi hii yote ya barabara ambayo ipo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la elimu, Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumzia, nakumbuka Mheshimiwa Vedastus Manyinyi Mathayo Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini alizungumzia suala la madawati, madarasa yamejengwa mengi
sana, lakini tukumbuke katika mwaka wa 2021/2022 katika madarasa ya UVIKO tayari madawati 794,000 yaliweza kutengenezwa kuendana na madarasa yale yaliyojengwa na UVIKO-19 katika shule za sekondari. Pia madawati 45,000 kwa shule za msingi.
Mheshimiwa Spika, ni commitment ya Serikali, ni commitment ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI, kuhakikisjha kwamba utengenezaji wa madawati unaendana na madarasa yaliyopo. Ninyi ni mashahidi hivi sasa kila eneo la nchi yetu limeguswa na madarasa mapya katika sekondari, katika mradi wa BOOST ambao unaenda kuanza hivi karibuni na Waheshimiwa Wabunge wote, Mheshimiwa Waziri wangu Angellah Jasmine Kairuki amewapa barua ya kuonesha mradi wa BOOST unapoenda kugusa katika Majimbo yenu. Tutahakikisha yale madarasa yanayojengwa vilevile yanaenda kuwa na madawati ya kutosha, kwa hiyo niwatoe mashaka Mheshimiwa Vedastus Manyinyi Mathayo na Waheshimiwa Wabunge wengi mliozungumzia suala zima la madawati.
Mheshimiwa Spika, katika miradi hii ambayo pia imekuwa ikitekelezwa ya madarasa yale ya Milioni 470 katika Majimbo na Wilaya zetu niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge tunaenda kuisimamia kikamilifu ikamilike na watoto walio dhamiriwa kuingia kwenye Shule zile waweze kuingia kwa wakati. Kuna wengi wenu hapa ni mashahidi shule zile zimeshaanza kupokea wanafunzi, kuna zingine ambazo ziko mwishoni kwenye ukamilishaji. Sisi kama timu ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI tutahakikisha shule zile zinaenda kukamilika vizuri, awamu inayokuja vilevile tutahakikisha changamoto zilizojitokeza katika awamu hii ya kwanza basi haziendi kujitokeza zile ambazo zinakuja kwa kila Halmashauri shule za Milioni 470.
Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa ni kwenye shule hizi za wasichana za A-Level ambazo zimeshajengwa 10 za kwanza katika Mikoa Kumi ya mwanzo, awamu ya pili tunaenda kwenye Mikoa Mitano halafu tutakuja kumalizia kwenye Mikoa iliyobaki. Niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, tunakwenda kuhakikisha sasa fedha zinapofika kule zinatumika mara moja hakuna ucheleweshaji kama maeneo mengine ambavyo yalikuwa yamejitokeza, vilevile tunaenda kuhakikisha zile changamoto zilizojitokeza katika awamu ya kwanza ya hizi shule Kumi ambazo Bilioni 30 imekwenda kila Mkoa Bilioni Tatu changamoto zile hazijitokezi tena. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kumaliza kwa kuunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mimi leo ndiyo mara yangu ya kwanza kusimama na kuzungumza mbele ya Bunge lako hili Tukufu tangu kuteuliwa na Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, napenda kutumia nafasi hii mbele ya Bunge lako kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa baraka zake na afya njema ambayo anatujalia sote na kuweza kutekeleza majukumu yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, napenda kutumia nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani yake kubwa aliyoionesha kwangu na kunipandisha kutoka kuwa Naibu Waziri ambapo aliniteua kuwa Naibu Waziri katika Ofisi mbili tofauti, Ofisi ya Rais, Utumishi na Naibu Waziri katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, sasa amenipandisha kumsaidia kazi kama Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee namuahidi Mheshimiwa Rais, wewe Mheshimiwa Spika, Naibu Spika na Wabunge wote hapa ndani kwamba nitajitahidi kadri ya uwezo wangu na alivyonijaalia Mungu kuhakikisha najituma kuweza kufikia malengo ambayo yanategemewa kutoka kwangu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nawashukuru sana Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko, nawaahidi kwamba miongozo yao na maelekezo yao tutayasimamia na kuyatekeleza kama vile ambavyo wanatarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee natumia nafasi hii vilevile kumpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwanza kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Mabunge yote Duniani IPU, Rais wa 31, vilevile kwa kuliongoza Bunge letu hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa viwango vya hali ya juu. Aidha, nakupongeza wewe mwenyewe Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu, Naibu Spika pamoja na Wenyeviti wa Bunge na Wenyeviti wa Kamati kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee vilevile natumia nafasi hii kumpongeza na kumshukuru Mwenyekiti wa Kamati yetu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wote wa Kamati. Bahati nzuri Mwenyekiti wa Kamati hii ni Mbunge mwenzangu kutoka Wilaya ya Chamwino ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Dodoma, Mama yangu Fatma Toufiq. Nakuahidi Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wajumbe wa Kamati na Wabunge wote kuwapa ushirikiano wa hali ya juu na pia maoni yenu, miongozo yenu na ushauri wenu tutauzingatia katika utekelezaji wa majukumu yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ofisi hii ambayo naihudumu kama Waziri wa Nchi, Ofisi ya Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu chini ya Waziri Mkuu ni ofisi ambayo inafanya kazi kwa utatu kwa maana ya Serikali, Waajiri na Wafanyakazi. Natumia fursa hii mbele ya Bunge lako Tukufu kuwaahidi Muungano wa Waajiri (ATE), vilevile Vyama vya Wafanyakazi kupitia Shirikisho lao la TUTCA kwamba tutakuwa pamoja, tutashirikiana katika kuhakikisha utatu wetu unafanya kazi vizuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nijikite kwenye hoja ambazo zimetolewa na Waheshimiwa Wabunge katika michango yao waliyokuwa wanachangia kwenye bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu. Kwanza ni suala ambalo ametoka kumalizia hapa Mheshimiwa Naibu Waziri, suala la ajira, kutafuta fursa za ajira kwa Watanzania. Nawaahidi Waheshimiwa Wabunge kwamba katika hili tutafanya kazi usiku na mchana kwa ajili ya kumsaidia Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kutafuta fursa mbalimbali ambazo zinaweza zikapatikana kwa Watanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, tayari ofisi hii imeshaingia makubaliano na Serikali ya Saudi Arabia na Serikali ya UAE katika kuhakikisha Watanzania wanapata fursa mbalimbali, skilled na unskilled labor katika nchi hizi, vilevile tunaendelea kutafuta fursa mbalimbali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni tumeona Serikali ya Japan imetangaza ajira zaidi 12,900 kwa wageni hasa wanaotokea Afrika. Tutahakikisha tunafanya kazi usiku na mchana kuweza kupata fursa hizo kwa ajili ya Watanzania kwenda kufanya kazi katika mataifa hayo. Tumeshuhudia South Korea ikitangaza ajira mbalimbali kwa ajili ya wageni, tutahakikisha tuna tap-in katika ajira hizo ambazo zimetangazwa ili vijana wetu wa Kitanzania waweze kufanya kazi zote za skilled na unskilled. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile Ofisi yetu hii ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, kazi yetu kubwa ni kuhakikisha tunaratibu fursa mbalimbali zinazotolewa na Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa vijana na watu wenye ulemavu, nawaahidi Waheshimiwa Wabunge kwamba tutafanya kazi kwa karibu sana pamoja na wenzetu wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuhakikihsa 4:4:2 zile fursa ambazo zipo kwa vijana basi zinawafikia na vijana wanaanzisha biashara ambazo zina tija. Tumezoea kuona zile 4:4:2 saa nyingine kila mmoja anakimbilia kwenye trend iliyokuwepo pale wakati huo, hawaangalii fursa nyingine zilizopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, unakuta vijana wa Kagera kule kwa Mheshimiwa Bashungwa, wote wanakimbilia kuwa na bodaboda ilihali ukienda kilomita chache unaweza kukuta kuna Ziwa pale. Tunaweza kuangalia ni namna gani ile 4:4:2 inawasaidia kwa ajili ya kwenda kuwa wavuvi na kuzalisha katika maeneo yale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, unakuta katika maeneo kama ile Mikoa ya big five, vijana wote wanatafuta fursa za mikopo za kwenda kuendesha bodaboda wakati kuna fursa katika mashamba, wana uhakika wa mvua. Serikali hii kupitia Wizara ya Kilimo imejitahidi katika kuhakikisha pembejeo zinawafikia wakulima katika maeneo hayo. Tutakwenda kuratibu ili fursa hizi ziweze kuwafikia vijana kulingana na maeneo ambayo wanatoka ili ile 4:4:2 iweze kuleta tija na ikaonekane. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna nafasi kubwa ya kuweza kunyanyua entrepreneurs kwenda kuwa mamilionea kutokana na fursa mbalimbali ambazo zinatolewa na fedha za Serikali hii ya Dkt. Samia Suluhu Hassan. Ukiacha fedha hizi za 4:4:2 vilevile tumeona wenzetu wa Wizara ya Kilimo wakija na BBT. Tutahakikisha tunatoa fursa nyingi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo kwa vijana wengi zaidi kuweza kuingia katika BBT ya kilimo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi karibuni nimekuwa nikizungumza na Mheshimiwa Waziri wa Madini, Mheshimiwa Antony Peter Mavunde, wanaenda kuanzisha MBT, Mining for a Brighter Tomorrow, ambayo tutahakikisha vilevile tunaratibu vijana wengi zaidi waweze kwenda kwenye fursa hizo. Hizo ndizo kazi ambazo zinaenda kufanywa na Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha fursa hizi zinawafikia vijana wengi zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile hapa Waheshimiwa Wabunge walichangia kuhusu Mifuko yetu ya Hifadhi ya Jamii. Kuna changamoto kubwa ambayo ipo, unakuta michango hukatwa kwa mwajiriwa lakini haifiki katika Mfuko wa Hifadhi ya Jamii. Mwajiriwa pale anapokuwa amestaafu ama ameacha kazi anakwenda kwenye ile Mifuko ya Hifadhi ya Jamii anakuta asilimia yake aliyokatwa yeye ile 10% ilifika, lakini asilimia ya mwajiri haikufika, saa nyingine unakuta zote mbili zile 20% hazijakwenda. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nasema mbele ya Bunge lako Tukufu, tutakuwa wakali kwa waajiri wote ambao hawatapeleka michango ya pensheni kwenye Mifuko yetu ya Hifadhi ya Jamii. Ile ambayo inatakiwa kwenda NSSF na ile ambayo inatakiwa kwenda PSSSF ambayo inatoka kwenye halmashauri zetu na kadhalika, tutahakikisha waajiri wote wanapeleka michango ili wale Watanzania ambao wanafanya kazi waweze kupata fedha yao kwa wakati. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, natumia nafasi hii kuwahakikishia kwamba hoja zote ambazo zimetolewa hapa tumezichukua, tumezipokea na tunakwenda kuzifanyia kazi. Majibu tutaleta kwa niaba ya Mheshimiwa Spika kwenye Kamati yetu inayoongozwa na Mheshimiwa Fatma Toufiq juu ya yale yote ambayo yametolewa na Waheshimiwa Wabunge hapa na namna gani ambavyo tunakwenda kuyafanyia kazi. Nawaahidi ushirikiano wa hali ya juu Waheshimiwa Wabunge wote na Ofisi yetu na sisi ambao tunamsaidia Mheshimiwa Waziri Mkuu tutahakikisha yale malengo ambayo ameyaweka na yale atakayokuja kutuelekeza tunayatekeleza kwa haraka zaidi na kwa ushirikiano mkubwa zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, natumia nafasi hii vilevile kumshukuru sana Mheshimiwa Chief Whip Jenista Joachim Mhagama, Mbunge wa Peramiho kwa ushauri wake. Nimepata bahati ya kuhudumu kama Naibu Waziri wake. Nina imani yale aliyonilea na kunifundisha, ndiyo ambayo yamenisaidia kuweza kufika hapa nilipofika leo. Kwa hiyo namshukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Jenista Joachim Mhagama, kwa ushirikiano mkubwa ambao ameendelea kunipa na hata sasa bado ananipa on the job training huku tunaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile, nawashukuru sana Waheshimiwa Mawaziri wote, Waheshimiwa Naibu Mawaziri wote akiwemo Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mheshimiwa Katambi na Mbunge wa Shinyanga Mjini, kwa ushirikiano na ukaribisho ambao amenipatia kwa muda ambao nimeripoti katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Waziri, mwisho kabisa na si kwa umuhimu, nawashukuru sana wananchi wa Jimbo la Chamwino kwa imani yao kubwa ambayo wanayo kwangu. Mpaka sasa, Jimbo liko salama, liko shwari na naendelea kufanya kazi kwa sababu wamenipa utulivu huo. Kwa hiyo nawashukuru sana Wanachamwino na nawaahidi nitaendelea kuwatumikia kadri ya vile ambavyo Mungu atanijaalia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa, naomba kusema kwamba naunga mkono hoja iliyo mezani ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Naomba kuwasilisha na Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026
WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa ninaomba nichukue nafasi hii kukushukuru wewe mwenyewe kwa kuongoza Bunge hili siku hii ya leo na kuweza kufikia wakati huu wa kuhitimisha hoja ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee ninatumia fursa hii tena kuishukuru Kamati yako ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, chini ya uongozi wake Mheshimiwa Timotheo Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini. Kwa kweli, Kamati hii imekuwa ikitoa miongozo, ambayo imefanya leo tumefikia mafanikio makubwa sana katika utendaji kazi wa Wizara yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ninawashukuru wachangiaji wote waliochangia hoja yetu hii, jumla ya wachangiaji nane wamechangia hoja hii. Nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge, mawazo na ushauri wote walioutoa, sisi kama Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi tunaenda kuufanyia kazi na kuhakikisha kwamba, tunaporejea hapa waone mambo yote waliyoyasema yamefanyiwa kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nigusie baadhi ya hoja ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezizungumzia. Suala la Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita, miaka minne hii ya utawala wa Mheshimiwa Rais wetu kipenzi Dkt. Samia Suluhu Hassan, tume hii imefanya kazi kubwa sana. Kwa sababu, tangu tupate uhuru katika vijiji 12,333 tulivyonavyo, amezungumza hapa Mheshimiwa Mnzava, vijiji vilivyokuwa vimewekewa matumizi bora havizidi 2,600, lakini katika kipindi cha miaka minne tumeona vijiji zaidi ya 4,000 vikiwa vimewekewa matumizi bora ya ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi ninavyozungumza, kwa ushauri wa Kamati yetu ya Kudumu ya Bunge, tumefanikiwa kupokea shilingi bilioni tano kutoka Wizara ya Fedha, kwa ajili ya kwenda kuendeleza upimaji wa vijiji 333 na kuweka matumizi bora. Kazi hiyo imezinduliwa Wilayani Ikungi, Mkoani Singida, wiki kadhaa zilizopita na Kamati yako ya Bunge ilishiriki.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninawahakikishia kwamba, lengo la Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na sisi wasaidizi wake ni kuhakikisha mipango ya matumizi bora ya ardhi inakuwepo kwenye vijiji vyote 12,333. Hii ndiyo itakwenda kuondoa mzizi wa migogoro ya ardhi, hasa kati ya wakulima na wafugaji. Amezungumza hapa Mheshimiwa Lusinde, ipo migogoro kwa sababu ya maeneo kutokupangwa na kuwekwa, kwa ajili ya ufugaji na kilimo, ama maeneo mengine yanakuwa yamepangwa, ambayo hayako suitable, kwa ajili ya kimoja ama kingine. Kwa kupima vijiji vyote hivi, tutahakikisha tunaondokana na changamoto hiyo. Ninalihakikishia Bunge lako kwamba, tunakwenda kutekeleza hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Plot Development Revolving Fund, ambapo ndiyo Mradi wa KKK upo. Tangu Development Fund hii ianzishwe haikuwahi kuwekewa hata senti moja, lakini katika kipindi cha uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameweza kuweka shilingi bilioni 50, ambayo fedha hii imekwenda kupima viwanja zaidi ya 12,303.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia Mheshimiwa Chege, amezungumza changamoto ya halmashauri kutorejesha fedha hizi. Tumekaa na wenzetu wa TAMISEMI, tumekaa na wenzetu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ambayo yeye, Mheshimiwa Chege, ni Makamu Mwenyekiti. Tumekubaliana ya kwamba, kuanzia sasa hakuna maombi yoyote ya halmashauri yataletwa moja kwa moja kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama halmashauri inaona ina uhitaji mkubwa wa kupima viwanja kupitia Mradi huu wa KKK ipitishe maombi yake TAMISEMI; TAMISEMI ione uwezo wa halmashauri ile kurudisha. Kwa sababu, wengine walichukua fedha, walienda kupima katika maeneo ambayo hayauziki na ndiyo maana fedha hii hairejei. Tumeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kwamba, tunalinda fedha hizi shilingi bilioni 50 zilizotolewa na Dkt. Samia Suluhu Hassan na tunahakikisha viwanja zaidi vinaendelea kupimwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumziwa kwa upana wake na Waheshimiwa Wabunge waliochangia; amezungumza Mheshimiwa Mnzava, Mheshimiwa Kunambi, Mheshimiwa Asenga na Waheshimiwa wengine waliopata nafasi ya kuzungumza wamegusia sana suala la Kamisheni ya Ardhi na namna ambavyo inakwenda kutatua changamoto mbalimbali. Ninasema mbele ya Bunge lako Tukufu, tumechelewa sana kuwa na Kamisheni kama hii ya Ardhi na tumechelewa sana kuweka utaratibu madhubuti wa kuhakikisha nchi yetu inakuwa imepimwa na imepangwa vilivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii kuna mwingiliano mkubwa kati ya Mamlaka ya Upimaji na Mamlaka ya Halmashauri, kuna changamoto kubwa. Kwenye master plan unakuta kuna eneo, mfano Jimboni kwako pale Kariakoo, master plan huenda inasema mwisho ni ghorofa kadhaa, tano au sita, ama jengo lilijengwa kama apartment, tumeona changamoto zikijitokeza za maghorofa kudondoka, lakini mabadiliko ya matumizi yanapofanyika Wizara ya Ardhi haihusiki. Mabadiliko ya matumizi kwenda kwenye commercial hayapiti katika entity nyingine za Serikali kuhakikisha ya kwamba, jengo lile linaweza kuhimili mabadiliko hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona kwa Dar es Salaam, Masaki na Oyster Bay, mpango madhubuti wa maeneo yale uliopitishwa na Baraza la Mawaziri unasema ni ground plus five, maximum. Kuna watu wanaojenga ground plus nine, plus ten, ni kwa sababu ya mamlaka kuingiliana. Anapokwenda kuomba kibali cha ujenzi, mtu anaomba cha ghorofa 10 anapewa, hawajui master plan iko vipi! Suluhisho la hili na migongano hii inayojitokeza ni kuhakikisha tunakuwa tuna Land Commission.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninawatoa mashaka Waheshimiwa Wabunge, kuwa na Land Commission hii haimaanishi kwamba, tunakwenda kutoka Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Bado Serikali za Mitaa itakuwa ni kiungo muhimu sana katika utekelezaji wa kazi za Kamisheni hii ya Ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia ndugu yangu, Mheshimiwa Kunambi, amezungumzia suala la Tume na RERA kuwa, chini ya Commission hii. Sasa kwa sababu tuko katika initial stages za kuanzisha tume hii tunachukua mawazo hayo na kwenda kuyafanyia kazi. Nimemsikia Mheshimiwa Mnzava akisema isiathiri D by D; haitoathiri D by D, tutahakikisha tunaboresha yale malengo ya D by D yaweze kuendelea kuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwenye suala la kuanzisha Real Estate Regulator Authority (RERA), kwenye masuala ya miliki, na lenyewe tumechelewa sana. Kumekuwa kuna uholela mwingi katika Sekta ya Real Estate.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii mwananchi wa kawaida anayetaka kununua kiwanja ili aweze kujenga kwa kipato chake anachokipata anaweza akatafuta dalali A akamwonyesha kiwanja, dalali B, akamwonyesha kiwanja kile kile, dalali C, akamwonyesha kile kile; lakini si ajabu hawa watu wote mwenye kiwanja hawafahamu, mwenye kiwanja hawajui, ama hata nyumba ambayo inauzwa; ni kwa sababu kuna uholela mwingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka kuweka utaratibu ambao utamlinda Mtanzania katika kuhakikisha tunawafahamu wenye nyumba, tunawafahamu wanaofanya kazi katika sekta ya milki ili mwananchi awe salama, lakini hata mwenye nyumba na yeye awe salama. Kwa hiyo ni jambo ambalo nalo lilichelewa na niwahakikishie tutalileta hapa Bungeni kwa ajili ya kupitisha sheria zake tuweze kuanza kulitumia.
Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumzwa hapa suala la migogoro ya ardhi. Ni kweli kwamba kuna changamoto kubwa ya migogoro ya ardhi na migogoro hii ipo ya aina mbalimbali. Kuna migogoro ambayo ni administrative ambayo ni jukumu letu kama Wizara, kuna migogoro ambayo ni ya kifamilia, lakini tafsiri ya jamii inaona kama ni wajibu wa sekta ya ardhi kutatua administratively; labda mirathi na kadhalika na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna migogoro ambayo imeshatolewa maamuzi na Mahakama. Katika maamuzi hayo sisi kama administrators hatuwezi kuingilia Mhimili mwingine; wajibu wa ku-counter maamuzi yale ya Mahakamani kukata rufaa katika chombo cha Mahakama ili uamuzi unapotoka, sisi kama administrators tuweze kutekeleza wajibu wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mengine lazima nikiri ni migogoro iliyotengenezwa na watumishi wetu wenyewe katika sekta ya ardhi. Mheshimiwa Msambatavangu amezungumzia kuhusu masuala la double allocation ambayo yamekuwa kinara katika Jiji letu la Dodoma na maeneo mengine. Nitoe maelekezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi hapa leo mbele ya Bunge lako Tukufu; ni marufuku kuendelea kutumia mfumo mwingine zaidi ya e-ardhi katika kutoa au kutoa huduma kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, double allocation ilikuwa inatokeaje; unakuta mtumishi wetu kwa makusudi na kwa kufahamu anakwenda kwenye mfumo ambao hatuutumii tena wa MORIS anatoa hati. Anakuja Mheshimiwa Msambatavangu na yeye anataka hati ya kiwanja hicho hicho anaingia kwenye e-ardhi, kwa sababu mifumo ile ilikuwa haisomani. Kwa hiyo unakuta eneo moja lina hati mbili. Kuanzia leo ni marufuku kuendelea kutumia mfumo wa zamani. Tutahakikisha nchi nzima mpaka ifikapo mwaka 2027 tunaweka mfumo mzima wa e-ardhi ili kuondokana na changamoto hizi za migogoro ya ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Kunambi kuwa nitafika Jimboni kwake. Nimhakikishie Mheshimiwa Asenga kuwa mgogoro ule wa pale kwa Baba Askofu tayari fedha imekwishapelekwa kwa ajili ya kuanza upimaji na kwenda kutatua. Vile vile Mheshimiwa Halima juzi tumekaa na wazee wale; niwaahidi na Mheshimiwa Mbunge wa jimbo rafiki yangu Mheshimiwa Mtemvu, kuwa tutahakikisha kwamba tunafika kuweza kusikiliza pande zote mbili tuone tutatue changamoto ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, si tu kwa Mheshimiwa Mtemvu, hata kwa Mheshimiwa Waziri wa Uwekezaji, Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo ambapo maeneo haya yameingiliwa. Tayari kuna nyumba zaidi ya laki mbili katika eneo hilo; ninaamini tutapata ufumbuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumza Mheshimiwa Naibu Waziri juu ya Shirika letu la Nyumba na wewe mwenyewe uliligusia wakati unamtambulisha DG. Ni kwamba tunaendelea na mradi wa Samia Scheme; na tunatafuta njia bora ya kuhakikisha kuwa tunapata nyumba za bei nafuu ambazo Watanzania wengi wataweza ku-afford kuzinunua.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wanafahamu kuwa ililetwa Bungeni hapa kwa ajili ya kuondoa VAT katika nyumba ambazo zipo chini ya milioni 50; na sasa tunapoelekea ni kutafuta namna ya kuondoa VAT kwenye nyumba amhazo hazizidi milioni 100; na huku tunatafuta teknolojia mpya kwa kuangalia kwa wenzetu nchi mbalimbali wanajenga vipi katika kupunguza gharama ili tupate nyumba ambayo Mtanzania wa kawaida ataweza ku-afford. Hii ndiyo njia pekee pia ya kulinda ardhi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ardhi tuliyokuwanayo wakati wa uhuru wetu mwaka 1961 tukiwa Watanzania milioni tisa ni ardhi ile ile na mipaka ile ile ambayo tunayo leo hii ambayo tuko Watanzania milioni 65. Tukiacha tusambae bila mipango, bila kwenda juu na kujenga nyumba za bei nafuu tutajikuta tunamaliza ardhi yote ambapo vizazi vijavyo vitakosa mahali pa kwenda. Ni lazima tujenge kwenda juu, lakini vile vile tuipendezeshe na miji yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, michango mingine ya Waheshimiwa Wabunge tumeipokea kwa maandishi; niwaahidi tunakwenda kuifanyia kazi. Tutahakikisha kwamba tunaibadili sekta ya ardhi kwa kuweka mifumo madhubuti ya kuhakikisha tunaondokana na migogoro. Niseme tu kwamba Mheshimiwa Rais katika kipindi changu cha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametupa support kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni hivi majuzi tu ametupatia magari zaidi ya 50 ambayo yanakwenda kuongeza kasi ya utekelezaji wa shughuli zetu katika sekta hii ya ardhi. Hata hili land commission ambalo tunalizungumzia ni jambo ambalo yeye mwenyewe Mheshimiwa Rais alielekeza Siku ya Uzinduzi wa Sera ya Ardhi ya Mwaka 1995, Toleo la 2003.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wizara ipo mbioni katika kuandaa sheria mbalimbali zinazotokana na sera ile ili tulete hapa Bungeni; na kanuni mbalimbali, ili tuanze kutekeleza sasa kama vile sera inavyotutaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache, ninaomba sasa nitoe hoja mbele ya Bunge lako ili tuweze kupitishiwa bajeti yetu. Ninashukuru sana. (Makofi)
WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.
(Hoja ilitolewa iamuliwe)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026
WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa ninaomba nichukue nafasi hii kukushukuru wewe mwenyewe kwa kuongoza Bunge hili siku hii ya leo na kuweza kufikia wakati huu wa kuhitimisha hoja ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kipekee ninatumia fursa hii tena kuishukuru Kamati yako ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, chini ya uongozi wake Mheshimiwa Timotheo Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini. Kwa kweli, Kamati hii imekuwa ikitoa miongozo, ambayo imefanya leo tumefikia mafanikio makubwa sana katika utendaji kazi wa Wizara yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile ninawashukuru wachangiaji wote waliochangia hoja yetu hii, jumla ya wachangiaji nane wamechangia hoja hii. Nawahakikishia Waheshimiwa Wabunge, mawazo na ushauri wote walioutoa, sisi kama Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi tunaenda kuufanyia kazi na kuhakikisha kwamba, tunaporejea hapa waone mambo yote waliyoyasema yamefanyiwa kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nigusie baadhi ya hoja ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezizungumzia. Suala la Tume ya Matumizi Bora ya Ardhi:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita, miaka minne hii ya utawala wa Mheshimiwa Rais wetu kipenzi Dkt. Samia Suluhu Hassan, tume hii imefanya kazi kubwa sana. Kwa sababu, tangu tupate uhuru katika vijiji 12,333 tulivyonavyo, amezungumza hapa Mheshimiwa Mnzava, vijiji vilivyokuwa vimewekewa matumizi bora havizidi 2,600, lakini katika kipindi cha miaka minne tumeona vijiji zaidi ya 4,000 vikiwa vimewekewa matumizi bora ya ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi ninavyozungumza, kwa ushauri wa Kamati yetu ya Kudumu ya Bunge, tumefanikiwa kupokea shilingi bilioni tano kutoka Wizara ya Fedha, kwa ajili ya kwenda kuendeleza upimaji wa vijiji 333 na kuweka matumizi bora. Kazi hiyo imezinduliwa Wilayani Ikungi, Mkoani Singida, wiki kadhaa zilizopita na Kamati yako ya Bunge ilishiriki.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninawahakikishia kwamba, lengo la Serikali ya Awamu ya Sita ya Dkt. Samia Suluhu Hassan na sisi wasaidizi wake ni kuhakikisha mipango ya matumizi bora ya ardhi inakuwepo kwenye vijiji vyote 12,333. Hii ndiyo itakwenda kuondoa mzizi wa migogoro ya ardhi, hasa kati ya wakulima na wafugaji. Amezungumza hapa Mheshimiwa Lusinde, ipo migogoro kwa sababu ya maeneo kutokupangwa na kuwekwa, kwa ajili ya ufugaji na kilimo, ama maeneo mengine yanakuwa yamepangwa, ambayo hayako suitable, kwa ajili ya kimoja ama kingine. Kwa kupima vijiji vyote hivi, tutahakikisha tunaondokana na changamoto hiyo. Ninalihakikishia Bunge lako kwamba, tunakwenda kutekeleza hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Plot Development Revolving Fund, ambapo ndiyo Mradi wa KKK upo. Tangu Development Fund hii ianzishwe haikuwahi kuwekewa hata senti moja, lakini katika kipindi cha uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameweza kuweka shilingi bilioni 50, ambayo fedha hii imekwenda kupima viwanja zaidi ya 12,303.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia Mheshimiwa Chege, amezungumza changamoto ya halmashauri kutorejesha fedha hizi. Tumekaa na wenzetu wa TAMISEMI, tumekaa na wenzetu wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ambayo yeye, Mheshimiwa Chege, ni Makamu Mwenyekiti. Tumekubaliana ya kwamba, kuanzia sasa hakuna maombi yoyote ya halmashauri yataletwa moja kwa moja kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama halmashauri inaona ina uhitaji mkubwa wa kupima viwanja kupitia Mradi huu wa KKK ipitishe maombi yake TAMISEMI; TAMISEMI ione uwezo wa halmashauri ile kurudisha. Kwa sababu, wengine walichukua fedha, walienda kupima katika maeneo ambayo hayauziki na ndiyo maana fedha hii hairejei. Tumeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kwamba, tunalinda fedha hizi shilingi bilioni 50 zilizotolewa na Dkt. Samia Suluhu Hassan na tunahakikisha viwanja zaidi vinaendelea kupimwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumziwa kwa upana wake na Waheshimiwa Wabunge waliochangia; amezungumza Mheshimiwa Mnzava, Mheshimiwa Kunambi, Mheshimiwa Asenga na Waheshimiwa wengine waliopata nafasi ya kuzungumza wamegusia sana suala la Kamisheni ya Ardhi na namna ambavyo inakwenda kutatua changamoto mbalimbali. Ninasema mbele ya Bunge lako Tukufu, tumechelewa sana kuwa na Kamisheni kama hii ya Ardhi na tumechelewa sana kuweka utaratibu madhubuti wa kuhakikisha nchi yetu inakuwa imepimwa na imepangwa vilivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii kuna mwingiliano mkubwa kati ya Mamlaka ya Upimaji na Mamlaka ya Halmashauri, kuna changamoto kubwa. Kwenye master plan unakuta kuna eneo, mfano Jimboni kwako pale Kariakoo, master plan huenda inasema mwisho ni ghorofa kadhaa, tano au sita, ama jengo lilijengwa kama apartment, tumeona changamoto zikijitokeza za maghorofa kudondoka, lakini mabadiliko ya matumizi yanapofanyika Wizara ya Ardhi haihusiki. Mabadiliko ya matumizi kwenda kwenye commercial hayapiti katika entity nyingine za Serikali kuhakikisha ya kwamba, jengo lile linaweza kuhimili mabadiliko hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona kwa Dar es Salaam, Masaki na Oyster Bay, mpango madhubuti wa maeneo yale uliopitishwa na Baraza la Mawaziri unasema ni ground plus five, maximum. Kuna watu wanaojenga ground plus nine, plus ten, ni kwa sababu ya mamlaka kuingiliana. Anapokwenda kuomba kibali cha ujenzi, mtu anaomba cha ghorofa 10 anapewa, hawajui master plan iko vipi! Suluhisho la hili na migongano hii inayojitokeza ni kuhakikisha tunakuwa tuna Land Commission.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninawatoa mashaka Waheshimiwa Wabunge, kuwa na Land Commission hii haimaanishi kwamba, tunakwenda kutoka Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Bado Serikali za Mitaa itakuwa ni kiungo muhimu sana katika utekelezaji wa kazi za Kamisheni hii ya Ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimemsikia ndugu yangu, Mheshimiwa Kunambi, amezungumzia suala la Tume na RERA kuwa, chini ya Commission hii. Sasa kwa sababu tuko katika initial stages za kuanzisha tume hii tunachukua mawazo hayo na kwenda kuyafanyia kazi. Nimemsikia Mheshimiwa Mnzava akisema isiathiri D by D; haitoathiri D by D, tutahakikisha tunaboresha yale malengo ya D by D yaweze kuendelea kuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kwenye suala la kuanzisha Real Estate Regulator Authority (RERA), kwenye masuala ya miliki, na lenyewe tumechelewa sana. Kumekuwa kuna uholela mwingi katika Sekta ya Real Estate.
Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii mwananchi wa kawaida anayetaka kununua kiwanja ili aweze kujenga kwa kipato chake anachokipata anaweza akatafuta dalali A akamwonyesha kiwanja, dalali B, akamwonyesha kiwanja kile kile, dalali C, akamwonyesha kile kile; lakini si ajabu hawa watu wote mwenye kiwanja hawafahamu, mwenye kiwanja hawajui, ama hata nyumba ambayo inauzwa; ni kwa sababu kuna uholela mwingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka kuweka utaratibu ambao utamlinda Mtanzania katika kuhakikisha tunawafahamu wenye nyumba, tunawafahamu wanaofanya kazi katika sekta ya milki ili mwananchi awe salama, lakini hata mwenye nyumba na yeye awe salama. Kwa hiyo ni jambo ambalo nalo lilichelewa na niwahakikishie tutalileta hapa Bungeni kwa ajili ya kupitisha sheria zake tuweze kuanza kulitumia.
Mheshimiwa Naibu Spika, limezungumzwa hapa suala la migogoro ya ardhi. Ni kweli kwamba kuna changamoto kubwa ya migogoro ya ardhi na migogoro hii ipo ya aina mbalimbali. Kuna migogoro ambayo ni administrative ambayo ni jukumu letu kama Wizara, kuna migogoro ambayo ni ya kifamilia, lakini tafsiri ya jamii inaona kama ni wajibu wa sekta ya ardhi kutatua administratively; labda mirathi na kadhalika na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna migogoro ambayo imeshatolewa maamuzi na Mahakama. Katika maamuzi hayo sisi kama administrators hatuwezi kuingilia Mhimili mwingine; wajibu wa ku-counter maamuzi yale ya Mahakamani kukata rufaa katika chombo cha Mahakama ili uamuzi unapotoka, sisi kama administrators tuweze kutekeleza wajibu wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mengine lazima nikiri ni migogoro iliyotengenezwa na watumishi wetu wenyewe katika sekta ya ardhi. Mheshimiwa Msambatavangu amezungumzia kuhusu masuala la double allocation ambayo yamekuwa kinara katika Jiji letu la Dodoma na maeneo mengine. Nitoe maelekezo kwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi hapa leo mbele ya Bunge lako Tukufu; ni marufuku kuendelea kutumia mfumo mwingine zaidi ya e-ardhi katika kutoa au kutoa huduma kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, double allocation ilikuwa inatokeaje; unakuta mtumishi wetu kwa makusudi na kwa kufahamu anakwenda kwenye mfumo ambao hatuutumii tena wa MORIS anatoa hati. Anakuja Mheshimiwa Msambatavangu na yeye anataka hati ya kiwanja hicho hicho anaingia kwenye e-ardhi, kwa sababu mifumo ile ilikuwa haisomani. Kwa hiyo unakuta eneo moja lina hati mbili. Kuanzia leo ni marufuku kuendelea kutumia mfumo wa zamani. Tutahakikisha nchi nzima mpaka ifikapo mwaka 2027 tunaweka mfumo mzima wa e-ardhi ili kuondokana na changamoto hizi za migogoro ya ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Kunambi kuwa nitafika Jimboni kwake. Nimhakikishie Mheshimiwa Asenga kuwa mgogoro ule wa pale kwa Baba Askofu tayari fedha imekwishapelekwa kwa ajili ya kuanza upimaji na kwenda kutatua. Vile vile Mheshimiwa Halima juzi tumekaa na wazee wale; niwaahidi na Mheshimiwa Mbunge wa jimbo rafiki yangu Mheshimiwa Mtemvu, kuwa tutahakikisha kwamba tunafika kuweza kusikiliza pande zote mbili tuone tutatue changamoto ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, si tu kwa Mheshimiwa Mtemvu, hata kwa Mheshimiwa Waziri wa Uwekezaji, Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo ambapo maeneo haya yameingiliwa. Tayari kuna nyumba zaidi ya laki mbili katika eneo hilo; ninaamini tutapata ufumbuzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, amezungumza Mheshimiwa Naibu Waziri juu ya Shirika letu la Nyumba na wewe mwenyewe uliligusia wakati unamtambulisha DG. Ni kwamba tunaendelea na mradi wa Samia Scheme; na tunatafuta njia bora ya kuhakikisha kuwa tunapata nyumba za bei nafuu ambazo Watanzania wengi wataweza ku-afford kuzinunua.
Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wanafahamu kuwa ililetwa Bungeni hapa kwa ajili ya kuondoa VAT katika nyumba ambazo zipo chini ya milioni 50; na sasa tunapoelekea ni kutafuta namna ya kuondoa VAT kwenye nyumba amhazo hazizidi milioni 100; na huku tunatafuta teknolojia mpya kwa kuangalia kwa wenzetu nchi mbalimbali wanajenga vipi katika kupunguza gharama ili tupate nyumba ambayo Mtanzania wa kawaida ataweza ku-afford. Hii ndiyo njia pekee pia ya kulinda ardhi yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ardhi tuliyokuwanayo wakati wa uhuru wetu mwaka 1961 tukiwa Watanzania milioni tisa ni ardhi ile ile na mipaka ile ile ambayo tunayo leo hii ambayo tuko Watanzania milioni 65. Tukiacha tusambae bila mipango, bila kwenda juu na kujenga nyumba za bei nafuu tutajikuta tunamaliza ardhi yote ambapo vizazi vijavyo vitakosa mahali pa kwenda. Ni lazima tujenge kwenda juu, lakini vile vile tuipendezeshe na miji yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, michango mingine ya Waheshimiwa Wabunge tumeipokea kwa maandishi; niwaahidi tunakwenda kuifanyia kazi. Tutahakikisha kwamba tunaibadili sekta ya ardhi kwa kuweka mifumo madhubuti ya kuhakikisha tunaondokana na migogoro. Niseme tu kwamba Mheshimiwa Rais katika kipindi changu cha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ametupa support kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni hivi majuzi tu ametupatia magari zaidi ya 50 ambayo yanakwenda kuongeza kasi ya utekelezaji wa shughuli zetu katika sekta hii ya ardhi. Hata hili land commission ambalo tunalizungumzia ni jambo ambalo yeye mwenyewe Mheshimiwa Rais alielekeza Siku ya Uzinduzi wa Sera ya Ardhi ya Mwaka 1995, Toleo la 2003.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Wizara ipo mbioni katika kuandaa sheria mbalimbali zinazotokana na sera ile ili tulete hapa Bungeni; na kanuni mbalimbali, ili tuanze kutekeleza sasa kama vile sera inavyotutaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo machache, ninaomba sasa nitoe hoja mbele ya Bunge lako ili tuweze kupitishiwa bajeti yetu. Ninashukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa Rehema kwa kutujalia zawadi hii ya uhai na kuweza kuiona siku hii ya leo. Pili nitumie nafasi hii mbele ya Bunge lako Tukufu kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendela kuwa na imani na mimi kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri wa Nchi katika Ofisi yake Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa kumsaidia Mheshimiwa Angellah Jasmine Kairuki hapa TAMISEMI, ni imani kubwa sana, ni imani kubwa sana.
Mheshimiwa Spika, vilevile nitumie nafasi hii kuwashukuru sana wananchi wa Jimbo la Chamwino hapa Mkoani Dodoma, kwa imani yao ambayo wanayo kwangu mimi kama Mbunge wao na niwaahidi tu wanachamwino kuendelea kuwatumikia kama vile ambavyo wanatarajia kutoka kwa Mbunge wao na tutaendelea kushirikiana kila siku katika changamoto mbalimbali za Jimbo letu la Chamwino.
Mheshimiwa Spika, nikienda moja kwa moja kwenye hoja mbalimbali ambazo Wabunge walizizungumza humu ndani, karibia kila Mbunge aliyesimama humu alizungumzia suala la barabara kupitia TARURA. Waheshimiwa Wabunge, wengi mlisifu sana jitihada ambazo zimefanyika na taasisi ya TARURA nchini ya Engineer Seif, niwatoe mashaka Waheshimiwa Wabunge, ninyi mmekuwa ni mashahidi kwamba ndani ya mwaka mmoja TARURA imefanya kazi kubwa sana kwenye Majimbo yetu, kuhakikisha barabara zinapitika kwa kuhakikisha madaraja yanapitika.
Mheshimiwa Spika, mtakumbuka mwaka mmoja na nusu ama miwili iliyopita kabla ya Serikali hii ya Awamu ya Sita kuingia madarakani, TARURA walikuwa na bajeti ya Bilioni 257 tu, lakini ni utashi wake Rais wetu Dokta Samia Suluhu Hassan, aliona namna ifanyike kuweza kuongezea TARURA fedha. Fedha ile imekwenda kuleta mabadiliko makubwa ambayo huenda tungeyasubiri kwa miaka mingine 10 au 15 kuweza kufikia utengenezaji wa barabara kama tulivyofikia sasa.
Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge wote mmesema fedha TARURA haitoshi, niwatoe mashaka katika mwaka huu wa fedha bajeti imeachwa vilevile kama ilivyokuwa mwaka jana na tunakwenda kutekeleza miradi yenye thamani ya Bilioni 838 kwa fedha za ndani na fedha za nje kutoka TARURA. Hii ina maana kila mmoja wetu humu kwenye Jimbo lake na kwenye Mkoa wake anaenda kufikiwa na taasisi yetu ya TARURA.
Mheshimiwa Spika, Watanzania mamilioni na mamilioni wanaenda kufikiwa na TARURA na ninaamini mwakani tukirudi hapa kama ambavyo walikuwa wakimpongeza Mkurugenzi Mkuu wa TARURA na Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI, Waheshimiwa Wabunge hapa mtazidi kutoa pongezi hizo katika bajeti ambayo inafuata.
Mheshimiwa Spika, kitu ambacho naweza nikasema kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI ni kutoa commitment yetu ya usimamizi wa miradi hii. Tutahakikisha hakuna ubadhilifu, tutahakikisha inaenda kukamilika kwa wakati, vilevile tutahakikisha value for money inakuwepo katika miradi hii yote ya barabara ambayo ipo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la elimu, Waheshimiwa Wabunge wengi wamezungumzia, nakumbuka Mheshimiwa Vedastus Manyinyi Mathayo Mbunge wa Jimbo la Musoma Mjini alizungumzia suala la madawati, madarasa yamejengwa mengi
sana, lakini tukumbuke katika mwaka wa 2021/2022 katika madarasa ya UVIKO tayari madawati 794,000 yaliweza kutengenezwa kuendana na madarasa yale yaliyojengwa na UVIKO-19 katika shule za sekondari. Pia madawati 45,000 kwa shule za msingi.
Mheshimiwa Spika, ni commitment ya Serikali, ni commitment ya Ofisi ya Rais – TAMISEMI, kuhakikisjha kwamba utengenezaji wa madawati unaendana na madarasa yaliyopo. Ninyi ni mashahidi hivi sasa kila eneo la nchi yetu limeguswa na madarasa mapya katika sekondari, katika mradi wa BOOST ambao unaenda kuanza hivi karibuni na Waheshimiwa Wabunge wote, Mheshimiwa Waziri wangu Angellah Jasmine Kairuki amewapa barua ya kuonesha mradi wa BOOST unapoenda kugusa katika Majimbo yenu. Tutahakikisha yale madarasa yanayojengwa vilevile yanaenda kuwa na madawati ya kutosha, kwa hiyo niwatoe mashaka Mheshimiwa Vedastus Manyinyi Mathayo na Waheshimiwa Wabunge wengi mliozungumzia suala zima la madawati.
Mheshimiwa Spika, katika miradi hii ambayo pia imekuwa ikitekelezwa ya madarasa yale ya Milioni 470 katika Majimbo na Wilaya zetu niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge tunaenda kuisimamia kikamilifu ikamilike na watoto walio dhamiriwa kuingia kwenye Shule zile waweze kuingia kwa wakati. Kuna wengi wenu hapa ni mashahidi shule zile zimeshaanza kupokea wanafunzi, kuna zingine ambazo ziko mwishoni kwenye ukamilishaji. Sisi kama timu ya Ofisi ya Rais - TAMISEMI tutahakikisha shule zile zinaenda kukamilika vizuri, awamu inayokuja vilevile tutahakikisha changamoto zilizojitokeza katika awamu hii ya kwanza basi haziendi kujitokeza zile ambazo zinakuja kwa kila Halmashauri shule za Milioni 470.
Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa ni kwenye shule hizi za wasichana za A-Level ambazo zimeshajengwa 10 za kwanza katika Mikoa Kumi ya mwanzo, awamu ya pili tunaenda kwenye Mikoa Mitano halafu tutakuja kumalizia kwenye Mikoa iliyobaki. Niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge, tunakwenda kuhakikisha sasa fedha zinapofika kule zinatumika mara moja hakuna ucheleweshaji kama maeneo mengine ambavyo yalikuwa yamejitokeza, vilevile tunaenda kuhakikisha zile changamoto zilizojitokeza katika awamu ya kwanza ya hizi shule Kumi ambazo Bilioni 30 imekwenda kila Mkoa Bilioni Tatu changamoto zile hazijitokezi tena. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kumaliza kwa kuunga mkono hoja, ahsante. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema zake nyingi ambazo anaendelea kutujalia sisi waja wake. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie fursa hii kwa sababu ndiyo mara yangu ya kwanza kuzungumza tangu Mheshimiwa Rais, Mama yetu Samia Suluhu Hassan, afanye mabadiliko katika Baraza la Mawaziri na kunibakisha mimi katika nafasi yangu nikiwa nahudumu katika ofisi yake, naomba nitumie nafasi hii kumshukuru sana na kumuahidi sitomuangusha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kushukuru sana wanajimbo wa Jimbo langu la Chamwino ambao wameendelea kuwa na imani nami na tumeendelea kuwa wote pamoja katika kutatua changamoto mbalimbali za Wanachamwino. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho kabisa lakini siyo kwa umuhimu, naomba niwashukuru Wabunge wote 19 ambao wamechangia katika hotuba yetu iliyowasilishwa na Mheshimiwa Waziri hapa ya bajeti yetu ya Ofisi yetu ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja mbalimbali ambazo zimeletwa na Wabunge hapa tumezipokea na nyingi ni hoja ambazo zimejikita katika kuboresha maslahi ya watumishi wetu wa umma ambao ndio engine ya Serikali yetu, watumishi wa umma ndio ambao wanatoa huduma kwa wananchi wetu ambao wengi wao ni maskini katika Taifa letu hili la Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutambua hilo, Serikali katika mwaka wa fedha 2020/2021 imeboresha maslahi ya watumishi wa Serikali kwa kulipa malimbikizo ya madeni ya mishahara kwa watumishi zaidi ya 34,676 ambayo yana jumla ya thamani ya shilingi 69,077,261,014 katika mwaka wa fedha huu 2020/2021. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niliarifu Bunge lako kwamba madeni ya arrears za mishahara yapo ambayo yalifanyiwa uhakiki na yamelipwa mwezi Novemba, 2020 na kuna madeni vilevile ya arrears ambayo yalifanyiwa uhakiki na yamelipwa mwezi uliopita, mwezi Machi, 2021na hivi tunavyozungumza kuna madeni mengine ambayo tayari yanafanyiwa uchambuzi na uhakiki na yatakwenda kulipwa muda si mrefu tayari yakimaliza uhakiki katika Ofisi ya Utumishi na kupelekwa kwa wenzetu kule Hazina yataweza kulipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna hoja ambazo zimeletwa hapa na Waheshimiwa Wabunge ya kuzungumzia masuala ya OPRAS ambayo ni Open Performance Appraisal System ambayo ipo kwa watumishi wa umma. Huu ni mkataba wa ufanyaji kazi baina ya mtumishi na mwajiri wake. Sasa hapa kumekuwa kuna changamoto kidogo, na kama mlivyomsikia Mheshimiwa Rais jana, naye alilizungumzia. Changamoto ni kwamba watumishi wetu wengi wamekuwa wakifanya udanganyifu katika mfumo huu. Kwa maana taarifa za mwaka juzi, mwaka jana, ndizo hizo hizo ata-copy na ku-paste na kubadili tu tarehe bila hata ya kujipima.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukimuuliza mtumishi huyu kwamba hivi wewe kuanzia Januari mwaka jana mpaka Januari, 2021, kuna kipi ulichochangia katika eneo lako la kazi cha kuweza kuleta matokeo chanya ambayo ni faida kwa wananchi wetu wa Tanzania? Ukiuliza swali hilo unaweza ukakuta majibu hayaeleweki.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tunakwenda kubadili mfumo huu na kuweka utaratibu ambao utakuwa ni rahisi sana kwa mtumishi tangu anaingia katika utumishi wa umma na anapoendelea katika ukuaji wake wa utumishi, basi tuweze ku-evaluate performance yake kwa njia rahisi zaidi kwa maana immediate supervisor awe ana uwezo wa kuweka comment, lakini vilevile mwajiri mkuu awe ana uwezo wa kuweka comment katika performance ya mtumishi huyu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuhakikisha ya kwamba hakuna udanganyifu. Kuwe kuna utaratibu wa kuwa na work plan ambayo itatoholewa kutoka kwenye strategic plan ya taasisi yenyewe ili tuweze kujua huyu mtendaji ametusaidia vipi kuweza kufikia malengo yaliyowekwa na taasisi husika, ndipo tutaweza kujua pia kwamba hawa watumishi, je, anastahili kupanda daraja, je, anastahili kupanda mshahara, je, kile anacholipwa na Serikali ni sahihi au amepunjwa au anatakiwa kuongezwa kwa sababu ya tija ya kazi yake anayoifanya?
Mheshimiwa Naibu Spika, hili tunakwenda kulifanyia kazi na kuhakikisha kwamba OPRAS hii inabadilika na kuwa yenye tija katika jamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wabunge wengi pia wamezungumzia suala la kuwawezesha watumishi wetu kwa kuwafanyia training mbalimbali na kuwapa mafunzo kuweza kujua kazi zao ziko vipi na mafunzo mengine ambayo ni ya on the job training.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye hili tumegundua kwamba kuna changamoto moja; tuna Chuo cha Utumishi wa Umma, lakini chuo hiki waajiri wengi wamekuwa hawatengi mafungu au fedha za kuweza kupeleka watumishi wao kuweza kufanyiwa mafunzo ya utumishi wa umma.
Mheshimiwa Naibu Spika, unakuta mtu ametoka chuo fulani lakini akiingia kwenye utumishi wa umma lazima afunzwe apewe etiquette za utumishi wa umma na aweze kuendana nao katika miaka yake yote ya utumishi. Hili ninaamini muda si mrefu Waheshimiwa Wabunge mtaona mabadiliko makubwa sana kwenye hili. Tunataka kuwe na uniformity katika utumishi wa umma, kwamba watu wanavyo- behave akiwa mtaani na akiwa kazini, basi mtu akimuangalia aweze kufahamu kwamba huyu ni mtumishi wa umma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Waheshimiwa Wabunge ambao wamezungumzia suala zima la Uwezeshaji wa Kaya Maskini (TASAF). Mpango huu kiukweli umesadia watu wengi, kaya nyingi ambazo hazikuwa na uhakika wa mlo hata mmoja katika kaya zao, lakini leo hii zimekuwa zina uhakika wa milo mitatu na kaya nyingine zimekwenda hata kuboresha maisha ya kuwa na biashara, kuwa na mifugo, kulima kilimo kilicho bora na kadhalika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini niwahakikishie Wabunge, kaya zilizokuwepo kwenye TASAF III, Phase One zilikuwa ni kaya milioni moja Tanzania nzima. Sasa tunakwenda kuwa na kaya 1,400,000 katika nchi nzima, ambapo vijiji vilivyoachwa mpaka ifikapo mwezi Julai, 2021, vijiji vyote katika nchi yetu vitakuwa vinapokea TASAF. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika suala hili ninaomba sana ushirikishwaji wa Waheshimiwa Wabunge na Waheshimiwa Madiwani, mshiriki sana katika kutoa elimu kwa wnanachi wetu kwamba TASAF si jambo endelevu, TASAF imekuja kwa sababu ya kukuwezesha wewe kukutoa katika hali moja na kukuweka katika hali nyingine ya maisha yako. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kumekuwa na upotoshwaji unaendelea, wanaelezana watu huko kwamba ukiboresha maisha yako watakutoa kwenye Mpango wa TASAF. Lengo la TASAF ndiyo wakutoe, lakini ukiwa umeboresha maisha yako. Kama walikukuta huna mbuzi basi uwe una mbuzi watano, una kuku kumi, una bata ishirini na una nyumba bora, ndilo lengo la Mpango wa TASAF. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu mwisho wa siku ukibaki kwenye mpango huu kwa muda mrefu, siku mpango huu unapokuja kuisha tutakuwa tumetengeneza tatizo kubwa zaidi badala ya mpango huu ulipofika. Mpango huu lazima Waheshimiwa Wabunge twende majimboni mwetu tutoe elimu kwamba umekuja kuwasaidia kuboresha maisha yao na siyo kuwa tegemezi wa mpango huu katika maisha yao yote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mpwapwa, ndugu yangu, kaka yangu, Mheshimiwa Malima, ametoka kumalizia hapa na amezungumzia utaratibu wa kupata kaya hizi maskini. Nilifahamishe Bunge lako Tukufu kuwa utaratibu ni kwamba unakwenda kwenye mkutano wa kijiji na mkutano wa kijiji ndiyo unatambua kaya zile maskini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa changamoto imekuwa kwamba katika wale wananchi wa eneo husika kuna watu ambao wana status fulani katika kijiji. Wale watu wanaogopeka na wanawekwa kwenye mpango na wakiwa kwenye mpango watu wanaogopa kusema kwa kuogopa akisema anaweza akachukuliwa hatua mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja nyingine nyingi tumezichukua na Mheshimiwa Waziri wangu, Mheshimiwa Mchengerwa naye atazizungumzia. Lakini nyingi tulizozichukua tutazitafutia majibu na kuzijibu kwa maandishi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa naomba nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupatia afya njema na amani na furaha katika kipindi chote hiki cha mijadala ya Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora.
Vilevile nitumie nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuniamini na kuniacha katika Ofisi yake yeye kumsaidia. Pia nitumie fursa hii kumshukuru Waziri wangu ambaye amekuwa mlezi, mwalimu na kwa muda mfupi Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama ambaye nimefanya naye kazi kwa kweli nimejifunza mengi sana, namshukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii vile vile kuwashukuru wananchi wa Jimbo langu la Chamwino hapa Mkoani Dodoma kwa kuendelea kuwa na imani na mimi kama Mbunge wao na niendelee kuwaahidi kwamba sito waangusha na nitaendelea kuwatumikia vema siku zote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika shukrani mwisho lakini si kwa umuhimu, kwamba in a particular order pia nimshukuru mke wangu kipenzi Subira na wanangu kwa kuendelea kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho naendelea na shughuli mbalimbali za siasa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile niwashukuru wajumbe wa Kamati ya USEMI wakiongozwa na Mwenyekiti wetu, Mheshimiwa Abdallah Chaurembo; Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa Denis Londo; na wajumbe wote wa Kamati ya USEMI kwa kuendelea kutupa miongozo mbalimbali, ushauri mbalimbali na kufanya nao kazi vizuri siku hadi siku. Mwisho kabisa niwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa ushirikiano wao na kutushauri inapobidi na vile vile kwa michango yao ambayo walikuwa wanaitoa katika kipindi hiki cha bajeti yetu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nikienda kwenye hoja ambazo zimezungumzwa sana humu na Waheshimiwa Wabunge, nitajikita katika kuzungumzia hoja kubwa ambayo imegusa kila Jimbo la Mbunge humu ndani na katika nchi yetu, ni suala zima la TASAF. Katika kuzungumzia TASAF nitaanza kwanza kuelezea ili tupate uelewa wa pamoja wa namna ambavyo walengwa hawa wanapatikana, kwa sababu kwenye michango ya Wabunge nimeona sintofahamu ya walengwa hawa wanavyopatikana. Mfumo ulivyowekwa wa kuwapata walengwa wa kaya hizi ni kwamba wanatambuana wenyewe katika mikutano yao ya Serikali ya Kijiji. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wanapoitana wanaanza utambuzi wa kujua nani anastahili kuwa katika mpango huu wa TASAF na nani ana uwezo wa kutosha wa kutoingia katika mpango huu wa TASAF. Baada ya utambuzi ule, ndipo waratibu wale katika ngazi zile wanachukua majina yale na kuweza kuyaingiza kwenye mfumo na majina yale kisha kwenda Makao Makuu na sasa kuwa authorized na malipo kuanza kufanyika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nipende tu kulitaarifu Bunge lako kwamba mpango huu wa TASAF unaanzia chini kwenda juu na si juu kwenda chini. Kaya hizi tunazozizungumzia ni 1,277,000, nchi nzima, ni kaya ambazo kabla ya mpango huu wa TASAF kuanza zilikuwa hazina uhakika wa milo mitatu kwa siku. Mpango huu umekuja ili kuweza kuwapa safety net ya maisha yao kuweza kuwanyanyua na kuwapa uhakika wa kula yao na uhakika wa kesho yao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ndio maana huwa tunasisitiza na kuwaomba Waheshimiwa Wabunge wawe mabalozi wa mpango huu wa TASAF na kila wanapokwenda Jimboni waweze kuzungumzia mpango huu. Pia kuhimiza wale walengwa yaani kaya zile kuhakikisha kwamba wanazitumia fedha hizi kufuga, fedha hizi kulima ili pale wanapopata uwezo wa kuwa na mifugo mingi, ndipo sasa wataweza kununua bima ya afya na kuweza kukidhi mahitaji mbalimbali ya siku. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango huu umekuwa na mafanikio makubwa sana. Kwa dakika tano sitoweza kuzitaja au sitoweza kutaja mafanikio yote ya mpango huu wa TASAF, lakini mpango huu umekuwa na mafanikio makubwa ambapo ukitembelea maeneo mbalimbali nchini, ukawasikiliza walengwa na kuona vile walivyokuwa wakiishi kabla ya kuingia kwenye mpango na baada ya kuingia kwenye mpango, utaona jambo lililofanywa na Serikali ni jambo kubwa sana. (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa ningependa kuanza kwa kutoa pongezi za dhati kabisa kwa Waziri wa Maliasili na Utalii Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa pamoja na Naibu wake Mheshimiwa Mary Masanja.
Mheshimiwa Spika, kiukweli Mheshimiwa Waziri Mchengerwa anafanya kazi nzuri kama vile Mayele alivyofanya kwa timu ya Dar es Salaam Young Africans. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tumesikiliza hoja mbalimbali za Waheshimiwa Wabunge na wengi walikuwa wakizungumzia maeneo yenye migogoro ya ardhi kati ya hifadhi, vijiji na vitongoji mbalimbali hapa nchini. Vilevile…
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, Taarifa.
SPIKA: Mheshimiwa Deo Ndejembi, kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Esther Matiko.
TAARIFA
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nampa tu taarifa Mheshimiwa Ndejembi kwamba kule Algeria aliyeleta kaushindi kale kagoli moja alikuwa ni Juma sio Mayele. Kwa hiyo, lile goli moja sio la Mayele ni la Juma.
SPIKA: Mheshimiwa Deo Ndejembi, unapokea taaria hiyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, sipokei taarifa hiyo kwa sababu niliposema Mheshimiwa Mchengerwa ni kama Mayele ni kwa sababu Mayele ndio top scorer katika mashindano yale, kwa maana ndio nyota wa mchezo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, zilizungumzwa hoja za Kamati ile ya Mawaziri Nane. Katika maeneo ambapo timu ile ya Mawaziri Nane ilipopita kuna maeneo ambayo hakuna migogoro kabisa na tayari taarifa ile ilikuwa imekwishapelekwa katika Ofisi za Wakuu wa Mikoa. sasa nitumie Bunge lako hili kuwataka Wakuu wa Mikoa wote waliopelekewa taarifa ya migogoro yote ambayo imekwishatatuliwa waweze kwenda site (field). Kwa sababu tumesikia taarifa hapa Wabunge wakisema wanabaki kule mikoani na hawapeleki taarifa hizi kwa wananchi. Basi, hawa Wakuu wa Mikoa waende kule field kwa ajili ya kupeleka taarifa ya utatuzi wa migogoro ile kwa wananchi kwa kushirikiana na Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, eneo la pili ambalo ningependa kulizungumzia jioni hii ya leo ni suala la uanzishaji wa maeneo mapya ya kiutawala. Hili ndilo limekuwa chanzo kikubwa cha migogoro. Kuna vitongoji na vijiji vinaanzishwa katika hifadhi. Sasa sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, safari hii tutahakikisha hatuanzishi maeneo mapya ya utawala bila consultation ya Wizara ya Maji, Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo, Wizara ya Maliasili na Utalii lakini vile vile Wizara ya Ardhi, kuhakikisha kwamba maeneo yanayosajiliwa hayatokuja kuwa na migogoro siku za usoni. (Makofi)
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)
SPIKA: Haya ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tumeona hiyo imekuwa ni changamoto sana. Kwa kusema hayo machache naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kukushukuru wewe pamoja na Bunge lako Tukufu, vilevile nitumie nafasi hii kupongeza sana kazi nzuri ambayo imefanywa na Kamati hizi mbili ambazo hoja zipo Mezani hapa; Kamati ya Utawala, Sheria na Katiba, lakini vilevile Kamati ambayo mimi ni Mjumbe kwa nafasi yangu, Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Niwapongeze Wenyeviti wa Kamati hizi, Dkt. Mhagama pamoja na Mheshimiwa Londo na Wajumbe wa Kamati zote hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu leo utajikita katika sehemu mbili; sehemu ya kwanza ni miundombinu ya barabara ambayo inasimamiwa na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) ambao Waheshimiwa Wabunge wengi pia nao walijikita sana katika michango yao kwenye kuchangia suala zima la barabara zetu za mijini na vijijini hapa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikiri changamoto zipo, changamoto hizo zimetokana na athari kubwa iliyoletwa na mvua za Elnino, mvua ambazo zilitabiriwa kuja nchini kwetu na zimekuja kwa kasi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme kwamba athari tunayoiona leo ni ndogo kulingana na ambavyo ingekuwa endapo TARURA ingekuwa haijafanya kazi yake vizuri katika miaka ya nyuma toka uanzishwaji wake, ni athari ndogo kuliko ambavyo ingekuwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme hapa TARURA ilipoanzishwa mwaka 2017 barabara za lami zilizokuwa chini ya mtandao wao zilikuwa ni kilometa 1,449 hivi sasa tunavyozungumza mwaka huu 2024 mtandao wa lami ni kilometa 3,224 ina maana zimeongezeka, lakini changarawe kutoka kilometa 24,405 hadi kilometa 41,107 lakini vilevile barabara ambazo ni za udongo kutoka kilometa 83,091 kwenda kilometa 100,098.13. Utaona hapa jitihada kubwa ambayo imefanyika na Serikali katika kuhakikisha barabara zetu za mijini na vijijini zinapitika vizuri na kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije katika suala ambalo limezungumziwa sana hapa. Suala zima kuhuzu upatikanaji wa fedha; ni kweli, wakati wa kuwasilisha taarifa katika Kamati ya Utekelezaji wa Bajeti ya nusu mwaka fedha ambayo ilikuwa imefika ilikuwa ni bilioni 82 katika taarifa ile iliyowasilishwa kwenye Kamati ya TAMISEMI. Lakini hadi hivi ninavyozungumza sasa jumla ya fedha ambayo TARURA imepokea kutoka wenzetu wa Wizara ya Fedha ni bilioni 309. Ni kuonesha ni namna gani ambavyo jitihada inafanyika kuhakikisha barabara zetu zinapitika na zinatengenezwa, hasa kipindi hiki ambacho nyingi zimepata madhara kutokana na mvua ambazo zinanyesha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni sawa na asilimia 43 ya bajeti ambayo imetengwa kwa ajili ya TARURA, na tayari jitihada zinaendelea, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa na Waziri wa Fedha Mheshimiwa Mwigulu Mchemba tayari wamekaa vikao mbalimbali vya kukubaliana ni namna gani tunazidi kupokea fedha na kuwapelekea wenzetu wa TARURA, ili barabara zetu ziweze kutengenezwa na kupitika kwa wakati.
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ya dharura ambayo ilitengwa kwenye bajeti ilikuwa bilioni 21.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Salome Makamba.
TAARIFA
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachojaribu kukisema Mheshimiwa Waziri, anataka kuonesha kwamba, Wabunge au Wajumbe wa Kamati ni waongo au yeye ni muongo, kwa sababu Taarifa ambazo kamati inazo na mimi ni Mjumbe, mpaka tunaingia kwenye Bunge hili, pesa zilizopelekwa ni bilioni 89 tu na zile fedha za dharura. Hiyo bilioni mia tatu na ngapi ni taarifa ambayo anaisema hapa ambayo hakuna Mbunge yeyote katika Bunge hili anaweza kuthibitisha jambo hilo. Yaani anaijua yeye na most of the time kama pesa imeingia leo kuna hatihati ikawa ni exchequer hiyo, sio hela ambayo…
MWENYEKTI: Ahsante Mheshimiwa.
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi naomba tu yaani anachokisema hakuna anayeweza kukithibitisha, yaani ni fallacy, anatuletea hadithi ambayo sisi hatuwezi kukubaliana nayo.
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Salome. Mheshimiwa Naibu Waziri Taarifa unaipokea?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa hiyo siipokei kwa sababu nilishasema kwamba Taarifa tuliyowasilisha kwenye Kamati ya nusu mwaka ya utekelezaji wa bajeti, Mheshimiwa Makamba amezungumza, ni sahihi ilikuwa ni bilioni 89, lakini nikikwambia kwamba, exchequer ikitolewa na Hazina wenzetu ni sawasawa na fedha ambayo imelipwa kwetu sisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naendelea kukupa taarifa ya kwamba, ukiachilia exchequer ambayo ni bilioni 309 fedha iliyolipwa ni bilioni 262 hadi siku hii ya leo ambayo ni asilimia 85 ya fedha yote ambayo ilikuwa imetolewa exchequer, na bado tunavyozungumza Serikali ipo kazini ni kwamba, fedha hiyo inaendelea kulipwa. Ndio maana nasema taarifa ninazozitoa ni mpaka hivi sasa katika uchangiaji wangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ambayo ilikuwa imetengwa kwa ajili ya dharura nchi nzima, ilikuwa bilioni 21, na mpaka sasa fedha yote hiyo imepokelewa, lakini baada ya tathmini kwa kumalizia, baada ya tathmini kufanyika iligundulika inahitajika bilioni 65 kwa ajili ya dharura ya hizi mvua ambazo zimeendelea sasa. Hivi sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wizara ya Fedha na Mipango wanakaa katika kuona ni namna gani tunapata hiyo deficit ya bilioni 44 katika kipindi hiki kwa ajili ya kutengeneza barabara ambazo zimeathirika sana. Ahsante sana.
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kwa kukushukuru wewe pamoja na Bunge lako Tukufu, vilevile nitumie nafasi hii kupongeza sana kazi nzuri ambayo imefanywa na Kamati hizi mbili ambazo hoja zipo Mezani hapa; Kamati ya Utawala, Sheria na Katiba, lakini vilevile Kamati ambayo mimi ni Mjumbe kwa nafasi yangu, Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Niwapongeze Wenyeviti wa Kamati hizi, Dkt. Mhagama pamoja na Mheshimiwa Londo na Wajumbe wa Kamati zote hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu leo utajikita katika sehemu mbili; sehemu ya kwanza ni miundombinu ya barabara ambayo inasimamiwa na Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) ambao Waheshimiwa Wabunge wengi pia nao walijikita sana katika michango yao kwenye kuchangia suala zima la barabara zetu za mijini na vijijini hapa nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikiri changamoto zipo, changamoto hizo zimetokana na athari kubwa iliyoletwa na mvua za Elnino, mvua ambazo zilitabiriwa kuja nchini kwetu na zimekuja kwa kasi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme kwamba athari tunayoiona leo ni ndogo kulingana na ambavyo ingekuwa endapo TARURA ingekuwa haijafanya kazi yake vizuri katika miaka ya nyuma toka uanzishwaji wake, ni athari ndogo kuliko ambavyo ingekuwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme hapa TARURA ilipoanzishwa mwaka 2017 barabara za lami zilizokuwa chini ya mtandao wao zilikuwa ni kilometa 1,449 hivi sasa tunavyozungumza mwaka huu 2024 mtandao wa lami ni kilometa 3,224 ina maana zimeongezeka, lakini changarawe kutoka kilometa 24,405 hadi kilometa 41,107 lakini vilevile barabara ambazo ni za udongo kutoka kilometa 83,091 kwenda kilometa 100,098.13. Utaona hapa jitihada kubwa ambayo imefanyika na Serikali katika kuhakikisha barabara zetu za mijini na vijijini zinapitika vizuri na kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije katika suala ambalo limezungumziwa sana hapa. Suala zima kuhuzu upatikanaji wa fedha; ni kweli, wakati wa kuwasilisha taarifa katika Kamati ya Utekelezaji wa Bajeti ya nusu mwaka fedha ambayo ilikuwa imefika ilikuwa ni bilioni 82 katika taarifa ile iliyowasilishwa kwenye Kamati ya TAMISEMI. Lakini hadi hivi ninavyozungumza sasa jumla ya fedha ambayo TARURA imepokea kutoka wenzetu wa Wizara ya Fedha ni bilioni 309. Ni kuonesha ni namna gani ambavyo jitihada inafanyika kuhakikisha barabara zetu zinapitika na zinatengenezwa, hasa kipindi hiki ambacho nyingi zimepata madhara kutokana na mvua ambazo zinanyesha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni sawa na asilimia 43 ya bajeti ambayo imetengwa kwa ajili ya TARURA, na tayari jitihada zinaendelea, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, Mheshimiwa Mohamed Mchengerwa na Waziri wa Fedha Mheshimiwa Mwigulu Mchemba tayari wamekaa vikao mbalimbali vya kukubaliana ni namna gani tunazidi kupokea fedha na kuwapelekea wenzetu wa TARURA, ili barabara zetu ziweze kutengenezwa na kupitika kwa wakati.
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ya dharura ambayo ilitengwa kwenye bajeti ilikuwa bilioni 21.
MWENYEKITI: Mheshimiwa Naibu Waziri, kuna Taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Salome Makamba.
TAARIFA
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachojaribu kukisema Mheshimiwa Waziri, anataka kuonesha kwamba, Wabunge au Wajumbe wa Kamati ni waongo au yeye ni muongo, kwa sababu Taarifa ambazo kamati inazo na mimi ni Mjumbe, mpaka tunaingia kwenye Bunge hili, pesa zilizopelekwa ni bilioni 89 tu na zile fedha za dharura. Hiyo bilioni mia tatu na ngapi ni taarifa ambayo anaisema hapa ambayo hakuna Mbunge yeyote katika Bunge hili anaweza kuthibitisha jambo hilo. Yaani anaijua yeye na most of the time kama pesa imeingia leo kuna hatihati ikawa ni exchequer hiyo, sio hela ambayo…
MWENYEKTI: Ahsante Mheshimiwa.
MHE. SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi naomba tu yaani anachokisema hakuna anayeweza kukithibitisha, yaani ni fallacy, anatuletea hadithi ambayo sisi hatuwezi kukubaliana nayo.
MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Salome. Mheshimiwa Naibu Waziri Taarifa unaipokea?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa hiyo siipokei kwa sababu nilishasema kwamba Taarifa tuliyowasilisha kwenye Kamati ya nusu mwaka ya utekelezaji wa bajeti, Mheshimiwa Makamba amezungumza, ni sahihi ilikuwa ni bilioni 89, lakini nikikwambia kwamba, exchequer ikitolewa na Hazina wenzetu ni sawasawa na fedha ambayo imelipwa kwetu sisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naendelea kukupa taarifa ya kwamba, ukiachilia exchequer ambayo ni bilioni 309 fedha iliyolipwa ni bilioni 262 hadi siku hii ya leo ambayo ni asilimia 85 ya fedha yote ambayo ilikuwa imetolewa exchequer, na bado tunavyozungumza Serikali ipo kazini ni kwamba, fedha hiyo inaendelea kulipwa. Ndio maana nasema taarifa ninazozitoa ni mpaka hivi sasa katika uchangiaji wangu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha ambayo ilikuwa imetengwa kwa ajili ya dharura nchi nzima, ilikuwa bilioni 21, na mpaka sasa fedha yote hiyo imepokelewa, lakini baada ya tathmini kwa kumalizia, baada ya tathmini kufanyika iligundulika inahitajika bilioni 65 kwa ajili ya dharura ya hizi mvua ambazo zimeendelea sasa. Hivi sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wizara ya Fedha na Mipango wanakaa katika kuona ni namna gani tunapata hiyo deficit ya bilioni 44 katika kipindi hiki kwa ajili ya kutengeneza barabara ambazo zimeathirika sana. Ahsante sana.
Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue nafasi hii kushukuru kwa nafasi hii ya kuchangia taarifa ya Kamati hizi mbili ambazo zimewasilishwa siku hii ya leo. Pia, nichukue nafasi hii kupongeza Kamati hizi mbili kwa kazi nzuri ambayo wamekuwa wakifanya.
Mheshimiwa Spika, mchango wangu utajikita katika Kamati ya LAAC ambapo pia nachukua nafasi hii kumpongeza Mwenyekiti wa Kamati hii Mheshimiwa Halima James Mdee, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hii Mheshimiwa Stanslaus Mabula na Wajumbe wa Kamati hii ya LAAC kwa kazi nzuri ambayo wanaifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sisi kama Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tuko tayari kupokea miongozo, maelekezo na maazimio ya Bunge lako Tukufu yatakayo toka hapa na tutakwenda kutekeleza kama vile ambavyo Kamati na Bunge lako Tukufu litaazimia hapa mbele. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tumesikia hapa Waheshimiwa Wabunge wengi wakichangia hoja juu ya Force Account, jambo hili ni zuri kwa maana nilinaokoa gharama kubwa. Ndio, kuna changamoto nyingi juu ya usimamizi wa miradi kupitia Force Account, na katika utatuzi wa changamoto hizi tayari Serikali imeajiri Wahandisi zaidi ya 362 kote nchini na katika hao kila halmashauri nchini walau ilipata mhandisi mmoja. Mwaka jana wa fedha Serikali iliajiri ma-quantity Surveyor 100 kwa ajili ya kuhakikisha kwamba mfumo mzima wa Force Account unafanya kazi bila kuwa na changamoto yoyote. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Force Account, natoa mfano; katika majengo yanayojengwa sasa ya shule za mikoa kuna mikoa ambayo ilitekeleza Force Account to the T kama ilivyotakiwa kwa mujibu wa sheria na wamefanikiwa vizuri sana na mpaka sasa shule hizo zimefika zidi ya asilimia 90 ya ujenzi wake katika zile shilingi bilioni tatu ambazo zilikuwa zimepelekwa. Hapo hapo kuna wengine ambao Mikoa mingine ilitangaza tender kupata wakandarasi na BOQ za Wakandarasi zilikuwa mara mbili ya gharama ile ambayo ilikuwa imepelekwa na Serikali katika Mikoa hiyo, kwa hiyo utaona ni namna gani ambavyo Force Account inaokoa fedha nyingi ya Serikali katika ujenzi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hapa cha kusimamia ni ubora wa kile ambacho kinapatikana kama ambavyo kamati imewasilisha mbele ya Bunge lako. Nirejee tena kusema tuko tayari kwa ajili ya utekelezaji wa maelekezo ya Kamati yaliyotolewa na maazimio ya Bunge yatakayotolewa.
Mheshimiwa Spika, vilevile kuna michango ilikuja kwa ajili ya shule zile ambazo zilipelekewa shilingi milioni 470, tayari tathmini inafanyika na Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuona ni wapi ambapo kuna mapungufu ili fedha iweze kutafutwa kujazilizia lakini wakati huo huo kuna ambao waliomba vibali maalum baada ya kupokea shilingi milioni 470 kuweza kujenga majengo ya ghorofa. Mfano, Tunduma TC walipopokea shilingi milioni 470 walikuwa na uhaba wa maeneo waliomba kibali cha kujenga ghorofa kwa kuongeza na mapato yao ya ndani, thamani nzima ya majengo yale itakuwa ni shilingi milioni 800. Liwiti, Shule ya Sekondari Liwiti, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala waliomba kibali cha shilingi milioni 470 waweze kujenga ghorofa na wanaongeza kwenye mapato yao ya ndani, vilevile Nzega waliomba kibali kwa ajili ya kuweza kujenga ghorofa kwa mapato yao ya ndani.
Mheshimiwa Spika, tutaendelea kusimamia changamoto, narudia tena hatutamvumilia yeyote, kama ambavyo Kamati imependekeza, hatutamvumilia yeyote ambaye atazembea katika usimamizi wa fedha ya umma na tutachukua hatua mara moja. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tayari Serikali hii ya Awamu ya Sita imeanza kuchukua hatua kali dhidi ya wale wote ambao wameonekana kuzembea usimamizi wa miradi ya Serikali. Kuna wakurugenzi ambao wamepoteza teuzi zao kwa kutenguliwa, kuna wakuu wa idara za ujenzi ambao wametenguliwa teuzi zao, kuna wale wasimamizi wa miradi hii tayari wamechukuliwa hatua mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, nirejee tena nchi hii ni yetu sote na hapa mapendekezo ambayo yanatolewa ni kwa ajili ya kuboresha, katika kuhakikisha tunapata value for money katika fedha ya Serikali na Ofisi ya Rais, TAMISEMI italisimamia hilo chini ya uongozi mahili wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa na kwa msaada mkubwa wa Kamati hii ya LAAC ambayo inatupa mapendekezo mazuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba niseme naunga mkono hoja ya Kamati zote mbili zilizokuwa mbele yetu. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2024 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2024
WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwanza nami naomba niungane na Waheshimiwa Wabunge, Mawaziri wenzangu, kutoa pongeza kwa Kamati za Kudumu za Bunge ambazo zimefanya mawasilisho ya taarifa zake leo.
Mheshimiwa Spika, kipekee, napenda kutoa pongezi kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mheshimiwa Timotheo Mnzava, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hii, Mheshimiwa Najma Giga pamoja na Wajumbe wote wa Kamati hii ambao wanafanya kazi kubwa ya kukuwakilisha wewe katika kuisimamia Serikali na kusimamia sekta yetu hii ya ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi.
Mheshimiwa Spika, niseme kwamba tunapokea maoni yote yaliyotolewa na Kamati. Tunapokea michango yote iliyotolewa na Waheshimiwa Wabunge leo humu ndani katika kuchangia Taarifa hii ya Kamati. Nami niseme kwamba, naunga mkono Taarifa hiyo ya Kamati. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sisi kama Serikali tutakwenda kuhakikisha tunatekeleza maazimio yote yaliyotolewa kwenye Taarifa hii ya Kamati na kuhakikisha kwamba tunaleta Taarifa ya Utekelezaji wa Maazimio hayo. Kama ulivyojionea wewe mwenyewe, jitihada kubwa imekuwa ikifanyika katika kuhakikisha kwamba katika Sekta ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi tunatekeleza maazimio yanayotolewa na Bunge lako.
Mheshimiwa Spika, Maazimio hayo ya Bunge maana yake ni sauti za wananchi ambao wanaishauri Serikali nini kifanyike katika sekta hii. Tutaweka mkazo katika kuhakikisha mifumo inakuwa inasomana. Tunaenda kuweka mkazo katika kuhakikisha halmashauri zote 184 zinaenda kupata Mfumo wa Ardhi. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, vilevile, ni kilio cha muda mrefu cha kuhakikisha kwamba vijiji vyetu vyote nchini vinapimwa. Tutahakikisha tunaweka nguvu kama ambavyo Kamati imeshauri na imeelekeza.
Mheshimiwa Spika, tutaweka nguvu kupima vijiji zaidi ya 330 mara moja, kwa sababu juzi tu tumefanya kikao cha Wizara ya Fedha, sisi Wizara ya Ardhi pamoja na Kamati hii ya Kudumu ya Bunge na kuna commitment hiyo ya kuhakikisha kwamba tunaenda kupima vijiji hivi mara moja. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, mengine tutaendelea kupeana miongozo na maelekezo mbalimbali kupitia vikao mbalimbali vya Bunge na kupitia Kamati yako, nasi tuko tayari kuendelea kutekeleza maelekezo na maazimio yoyote yale ya Bunge. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, nashukuru sana kwa kupewa nafasi hii. (Makofi)
Taarifa ya Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2023 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutuwezesha kufika siku hii ya leo tukiwa wazima na wenye afya. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwako kwa kuweza kunipatia nafasi ya kuweza kuchangia bajeti hii na ninasema tu kwamba, naunga mkono hoja iliyo mbele yetu hapa. Vilevile naomba nitumie nafasi hii kupongeza Wizara hizi mbili, Wizara ya Fedha na Wizara ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji kwa kazi nzuri ambayo wameifanya na wasilisho zuri ambalo lipo mbele yetu hapa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, napenda kuchangia eneo la kikokotoo, ambalo limejadiliwa humu ndani na Waheshimiwa Wabunge wengi, lakini limekuwa pia, likijadiliwa na wabunge humu ndani katika vikao mbalimbali vya Bunge. Bajeti hii ambayo tunaenda kuipitisha ni bajeti ambayo inaonesha ni namna gani Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anaguswa na maisha ya wafanyakazi wa nchi hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tangu aingie madarakani Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan, tumeona mwaka wake wa kwanza tu katika uongozi wake alipandisha madaraja yaliyokuwa yamekwama miaka mingi. Kuna Watumishi wa Umma waliokuwa hawajapandishwa madaraja kwa zaidi ya miaka tisa, aliwapandisha zaidi ya watumishi 222,000 katika mwaka wake wa kwanza wa utumishi. Mheshimiwa Rais, vilevile aliguswa sana na madeni ya arrears kwa Watumishi wa Umma na alitoa fedha kwa ajili ya kulipa madeni hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sasa hili ambalo nataka nilizungumzie, la kikokotoo, nalo linaonesha ni namna gani Mheshimiwa Rais wetu anawajali wafanyakazi wa Taifa lake. Julai, 2022 kuna mabadiliko ya kikokotoo yalifanyika ambapo wale ambao ni Watumishi wa Umma walilipwa kwa mkupuo wa asilimia 50 na kushuka kwenda asilimia 33 na wale waliyokuwa asilimia 25 walipanda kwenda asilimia 33. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ilikuwa ni kilio kwa watumishi wengi ambao mishahara yao ni ya chini na mara nyingine husubiria mkupuo wa fedha hizi, kwa ajili ya kuanza maisha yao pale wanapokuwa wamestaafu. Mheshimiwa Rais wetu, kama alivyosikia kilio cha madaraja, kama ambavyo alisikia kilio cha madeni ya watumishi, Mheshimiwa Rais, alielekeza kikokotoo hiki kiweze kuangaliwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naishukuru na kuipongeza Wizara ya Fedha, Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Naibu Waziri na timu nzima ya Wizara ya Fedha. Baada ya kukaa nao waliangalia ni namna gani bora tunaweza kupunguza kilio hiki na kuweka katika bajeti hii tunayoenda kuipitisha shilingi bilioni 155, kwa ajili ya kulipa kikokotoo, kunyanyua kutoka asilimia 33 kwa wale waliokuwa asilimia 50 kabla ya Julai 22 kwenda asilimia 40 na wale ambao walikuwa asilimia 25 vile vile hawakuachwa, mpaka Julai 22 nao wamepandishiwa kwenda asilimia 35. Hii inaonesha ni namna gani Serikali hii ya Awamu ya Sita inajali watumishi wake. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, tumesikia Waheshimiwa Wabunge wengi mmezungumzia suala la kuangalia kiwango hiki kiendelee kunyanyuka kurejea pale kilipokuwa, asilimia 50. Tumesikia utatu huu wa vyama vya wafanyakazi na waajiri; vyama vya wafanyakazi vimezungumzia namna ambavyo wanashukuru asilimia hii 40, lakini nakuomba asilimia iweze kurudi asilimia 50 lakini huu ni mwanzo mzuri, kilio hiki kimesikika na ndiyo maana asilimia saba hii imewekwa. Kadiri tunavyokwenda na kutengemaa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii inavyokuwa inaendelea, ile actual evaluation itakavyofanyika. Serikali itazidi kuangalia ni namna gani inarudi katika asilimia 50, lakini mwanzo huu ni mzuri.
Mheshimiwa Spika, niwatoe mashaka Waheshimiwa Wabunge, hawa wanaokwenda kulipwa siyo tu wale ambao wanastaafu kuanzia Julai mosi mwaka huu 2024, wanaenda kulipwa wote hata wale waliostaafu kuanzia Julai Mwaka 2022. Katika bajeti hii inayoenda kupitishwa watumishi waliostaafu kuanzia Julai 22 mpaka Juni. Hivi tunavyozungumza 2024 jumla ya 17,068 wanaenda kulipwa mapunjo yao, yale ya asilimia saba ambayo walistahili kupata na wale ambao walikuwa wanapata asilimia 33 kwenda asilimia 35 watalipwa mapunjo yao ya asilimia mbili. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunatarajia kuona wengi wakija kudai mapunjo ya mafao yao. Tutaendelea kukiangalia kikokotoo hiKi kadiri actual evaluation itakavyofanyika kwenye mifuko yetu ya hifadhi ya jamii. Ninawahakikishia Serikali hii ni Sikivu na itaendelea kuliangalia na kuona ni namna gani bora tunazidi kusogea katika kiwango kinachozidi zaidi ya hapa asilimia 40.
Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja tena. Ahsante sana kwa nafasi hii. (Makofi)
Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Shirika la Nyumba la Taifa wa Mwaka 2025
WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaomba nichukue nafasi hii tena kukushukuru wewe pamoja na Bunge lako Tukufu kwa kuweza kusimama hapa leo na kuleta Muswada huu mbele ya Bunge hili. Nichukue nafasi hii kuwashukuru wachangiaji Mheshimiwa Festo Sanga na Mheshimiwa Asha Mshua ambao ninawahakikishia kwamba yale waliyoyasema tutayazingatia katika utekelezaji wa majukumu yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaishukuru pia tena kipekee Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kwa maoni waliyoyatoa, ushauri hasa katika kipindi ambacho tulikuwa tunapitia huu Muswada wa Sheria na ninakushukuru wewe kama Makamu Mwenyekiti vilevile wa hii Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, maboresho haya ambayo yanaenda kufanyika yanakwenda kurahisisha decision-making process katika utendaji wa day to day wa Shirika la Nyumba la Taifa. Katika kufanya hivyo maana yake mlaji wa mwisho ambaye ni mwananchi anakwenda kupata huduma iliyobora. Maamuzi ya uwekezaji, maamuzi ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu, maamuzi ya kuhakikisha ya kwamba tunaweka miji yetu kwa ujenzi wa kwenda juu kupitia Shirika letu la Nyumba la Taifa yote yanakwenda kufanyika kwa haraka zaidi kwa mabadiliko ya sheria hizi. Kwa hiyo, ninawashukuru sana na ningeomba Wabunge waridhie baadaye tunapopitisha, basi sheria hii iweze kupita ili tuweze kwenda kutekeleza wajibu wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, ninaomba kutoa hoja. (Makofi)