Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 7 | Sitting 35 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 312 | 2022-06-01 | 
 
									Name
Dunstan Luka Kitandula
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mkinga
Primary Question
						MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- 
Je, ni lini Wananchi wa Kata ya Bosha na Mhinduro watapata maji salama?
					
 
									Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:- 
Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Jimbo la Mkinga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imekamilisha usanifu wa Mradi wa Maji wa Mhinduro utakaohudumia Kata za Bosha na Mhinduro na ujenzi utaanza mwezi Juni, 2022 na kukamilika katika mwaka wa fedha 2022/2023.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved