Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 7 | Sitting 52 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi | 456 | 2022-06-27 | 
 
									Name
Fatma Hassan Toufiq
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. FATMA H. TOUFIQ K.n.y. MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa treni ya mwendokasi kutoka Kaliua-Mpanda hadi Karema?
					
 
									Name
Atupele Fredy Mwakibete
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busokelo
Answer
						NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TRC imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa awali wa ujenzi wa njia ya reli ya Kaliua – Mpanda – Karema kwa kiwango cha Standard Gauge. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga fedha kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi wa reli hii.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved