Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 16 | Sitting 1 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 14 | 2024-08-27 | 
 
									Name
Mariamu Nassoro Kisangi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Barabara ya Kongowe hadi Mjimwema?
					
 
									Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
						NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikifanya ukarabati wa maeneo korofi katika Barabara ya Kongowe – Mjimwema – Kivukoni yenye urefu wa kilometa 25.01, hasa yale yaliyoharibika sana katika kipindi cha mvua.  Aidha, katika mwaka wa fedha 2024/2025, Serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 500, kwa ajili ya ukarabati wa maeneo yote yaliyoharibika, ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved