Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 15 | Sitting 33 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 429 | 2024-05-24 | 
 
									Name
Florent Laurent Kyombo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nkenge
Primary Question
						MHE. FLORENT L. KYOMBO aliuliza: -
Je, lini Serikali italipa fidia kwa wananchi waliopisha Mradi wa Umeme Kakono – Misenyi?
					
 
									Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: - 
Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la tathmini ya fidia kwa wananchi wanaopisha mradi wa njia ya kusafirisha umeme Msongo wa kilovoti 220 kutoka Kakono – Kyaka umekamilika na gharama za fidia kwa wananchi wanaopisha mradi huu ni fedha za Kitanzania shillingi billioni 1.543. Malipo haya yanategemewa kuanza kulipwa hivi karibuni, ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved