Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 3 Sitting 15 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi 176 2026-04-23

Name

William Kafiti Kafiti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. KAFITI W. KAFITI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Airport – Kayenze kilometa 34?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Kafiti William Kafiti Mbunge wa Ilemela kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara ya Airport – Kayenze – Nyanguge yenye urefu wa kilometa 46 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Awamu ya kwanza inahusisha ujenzi kwa kiwango cha lami kuanzia maeneo ya Airport hadi Kibangaja (kilometa 10) ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia sita. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.