Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 3 | Sitting 15 | Works, Transport and Communication | Wizara ya Ujenzi | 176 | 2026-04-23 |
Name
William Kafiti Kafiti
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ilemela
Primary Question
MHE. KAFITI W. KAFITI aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa barabara ya Airport – Kayenze kilometa 34?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Kafiti William Kafiti Mbunge wa Ilemela kama ifuatavyo:
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara ya Airport – Kayenze – Nyanguge yenye urefu wa kilometa 46 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Awamu ya kwanza inahusisha ujenzi kwa kiwango cha lami kuanzia maeneo ya Airport hadi Kibangaja (kilometa 10) ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia sita. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved