Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2015-2020 | Session 18 | Sitting 9 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 116 | 2020-02-07 | 
 
									Name
David Ernest Silinde
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Tunduma
Primary Question
						MHE. DAVID E. SILINDE aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani kwa sasa kutatua kero ya maji kwa uhakikia katika Jimbo la Momba?
					
 
									Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa David Ernest Silinde, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika juhudi za kutatua tatizo la maji katika Jimbo la Momba, Serikali inaendelea kutekekeza miradi mitatu katika Vijiji vya Ndalambo ambapo ujenzi umekamilika  kwa  asilimia  95,  Kijiji  cha  Chitete  ujenzi  umekamilika  kwa  asilimia 12 na Tindingomba ujenzi umekamilika kwa asilimia 80. Miradi hii ikikamilika, itahudumia jumla ya watu wapatao 23,397 na kuongeza upatikanaji wa huduma ya maji safi, salama kwa wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali imeanza kutekeleza miradi ya vijiji vitano kupitia Programu ya Malipo kwa Matokeo (PfR) katika Vijiji vya Mkulwe, Chiwanda, Kasinde, Ikana na Namsinde II kwa gharama ya Sh.805,885,340. Kukamilika kwa miradi hii, kutawezesha jumla ya watu 31,984 kupata huduma ya maji.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved