Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 2 | Sitting 5 | Natural Resources and Tourism | Wizara ya Maliasili na Utalii | 63 | 2021-02-08 | 
 
									Name
Mrisho Mashaka Gambo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Arusha Mjini
Primary Question
						MHE. MRISHO M. GAMBO Aliuliza: -
Serikali imeongeza viwango vya tozo za utalii kwa Hifadhi zilizo chini ya TANAPA kuanzia mwezi Julai, 2021.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kusitisha tozo hizo ili kutoa fursa kwa Sekta ya Utalii nchini ambayo imeathirika sana na ugonjwa wa Corona?
					
 
									Name
Mary Francis Masanja
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
						NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII Alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mrisho Mashaka Gambo, Mbunge wa Arusha Mjini, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, ongezeko la tozo limelenga Hifadhi za Taifa nne ambazo ni Ziwa Manyara, Serengeti, Tarangire na Arusha. Kiwango cha tozo kilichoongezeka kwa hifadhi husika ikilinganishwa na viwango vya sasa ni kama ifuatavyo: -
HIFADHI	ENTRYFEE	SEASONAL ANDSPECIALCAMPING FEE	CONCESSIONFEE
	Tozoya sasa	Tozokuanzia 1/7/2021	Tozoyasasa	Tozo kuanzia 1/7/2021	Tozoya sasa	Tozo kuanzia 1/7/2021
Serengeti	60USD	70USD	50USD	60USD	50USD	60USD
Manyara	45USD	50USD	50USD	60USD	40USD	40USD
Tarangire	45USD	50USD	50USD	60USD	40USD	40USD
Arusha	45USD	50USD	50USD	60USD	40USD	40USD
Mheshimiwa Spika, wakati wafanyabiashara ya utalii wakiishinikiza Serikali kuacha tozo zikiwa za chini sana, wenyewe wamekua wakiwatoza watalii tozo za juu ambazo hawataki kuziweka wazi kwa Serikali. Usiri wa tozo za makampuni binafsi unainyima Serikali taarifa za msingi za kuweza kuona uzito wa hoja yao.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa rai kwamba suala la COVID-19 lisitumike kuinyima Serikali mapato ambayo yanasaidia kukuza uchumi wa nchi. Pia, nisisitize kwamba pamoja na shinikizo la kupunguza tozo, sekta binafsi haijawasilisha takwimu zozote Serikalini za kuthibitisha ongezeko la idadi ya wageni waliofuta safari zao kuja nchini kutokana na ongezeko la tozo.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved