Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 9 | Sitting 10 | Works, Transport and Communication | Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi | 148 | 2022-11-11 | 
 
									Name
Kabula Enock Shitobela
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
						MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA K.n.y. MHE. KABULA E. SHITOBELO aliuliza: -
Je, ni sheria gani inayotumika kwenye tozo za bandari nchini?
					
 
									Name
Atupele Fredy Mwakibete
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Busokelo
Answer
						NAIBU WAZIRI	WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu: -
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kabula Enock Shitobela, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, tozo za bandari zinatozwa kwa mujibu wa Sheria ya Bandari Namba 17 ya mwaka 2004. Kwa mujibu wa sheria hiyo, kitabu cha viwango vya tozo (tariff book) huidhinishwa na mdhibiti ambaye ni Shirika la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC).
Mheshimiwa Spika, Sheria ya Bandari Namba 17 ya mwaka 2004 imeeleza vyanzo  vya mapato vya TPA ambavyo vinajumuisha tozo za bandari (kifungu Na. 67). Aidha, sheria hiyo inaelekeza TPA kuandaa tariff  book inayoainisha viwango vya tozo za bandari kwa kila huduma, ahsante.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved