Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date | 
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 11 | Sitting 20 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 263 | 2023-05-08 | 
 
									Name
Condester Michael Sichalwe
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Momba
Primary Question
						MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -
Je, ni lini changamoto ya maji ndani	ya Jimbo la Momba litatatuliwa?
					
 
									Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
						WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua adha ya maji wanayopata Wananchi wa Wilaya ya Momba na tayari hatua zimeanza kuchukuliwa. Katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 miradi ya maji ya Msangano-Naming’ongo, Isanga - Kakozi na Tindingoma - Mlomba inaendelea kutekelezwa na itahudumia vijiji 11 vya Msangano, Nkala, Makamba, Naming'ongo, Yala, Ipata, Ntinga, Chindi, Isanga, Kakozi na Mlomba.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya maji kupitia chanzo cha maji cha Mto Momba ili kuhakikisha wananchi katika vijiji vilivyobaki Wilayani Momba wanapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza.
					
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved