Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Abdulhafar Idrissa Juma
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtoni
Primary Question
MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA aliuliza: - Je, ni lini majimbo ya Zanzibar yatapata fedha za Mfuko wa Jimbo kwa wakati?
Supplementary Question 1
MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini ningependa kujua: -
Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na Maafisa Maalum walio chini ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watakaokuwa wanasimamia fedha hizi kwa upande wa Zanzibar badala ya kutegemea Maafisa wa Serikali ya Mapinduzi ambao hawawajibiki moja kwa moja katika Bunge letu?
 
											Name
Hamad Hassan Chande
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kojani
Answer
								NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdul-hafar Idrissa Juma  kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu swali hilo, kwa ruhusa yako naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Abdul-hafar kwa namna anavyopigania Mfuko wa Jimbo kwa Jimbo lake na  majimbo mengine ya Zanzibar.  
Mheshimiwa Spika, Sheikh Abdul-hafar swali lako kama ushauri tumelichukua tunakwenda kushauriana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tuone kama ufanisi utapatikana zaidi kwa kuweka Maafisa kule basi Serikali yako ni sikivu na inaweza ikafanya hivyo. (Makofi)
							
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved