Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Rashid Abdallah Shangazi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mlalo
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. AZIZA S. ALLY aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa maboma ya zahanati na shule yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi Nzega?
Supplementary Question 1
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri kabisa ya Serikali, nina swali moja tu la nyongeza. 
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa maboma haya mengi yana muda mrefu sana, Serikali haioni umuhimu sasa wa kufanya tathmini ya kina na kuweza kubaini maboma yote nchi nzima ili iweze kutenga bajeti kwa wakati mmoja na kumaliza changamoto ya umaliziaji wa haya maboma?  Ahsante. (Makofi)
 
											Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
								NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wananchi wameitikia wito wa Serikali na kuchangia nguvu zao kwa ajili ya ujenzi wa maboma ya zahanati na madarasa na tayari Serikali ilishafanya tathmini na kuyatambua na kuyaorodhesha maboma yote ya zahanati na madarasa yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi na kila mwaka wa fedha Serikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya kwenda kuyakamilisha maboma hayo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ninaomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kutenga fedha kwa awamu ili kukamilisha maboma ambayo yamejengwa kwa nguvu za wananchi.  Ahsante sana.
							
 
											Name
Yahaya Omary Massare
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Manyoni Magharibi
Primary Question
MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. AZIZA S. ALLY aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa maboma ya zahanati na shule yaliyojengwa kwa nguvu za wananchi Nzega?
Supplementary Question 2
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, katika Halmashauri ya Itigi yapo maboma mengi ya shule katika kata karibu zote, lakini na maboma ya zahanati. Je, Serikali ipo tayari sasa kupeleka fedha katika Halmashauri ya Itigi kumalizia maboma haya ambayo wananchi walijitolea? Ahsante sana.
 
											Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali ipo tayari kupeleka fedha kwa ajili ya kumalizia maboma ya zahanati na madarasa katika Halmashauri ya Itigi na imekuwa ikifanya hivyo kila mwaka wa fedha na zahanati kadhaa zimekamilishwa, lakini madarasa yamekamilishwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Massare kwamba tutaendelea kuweka kwenye bajeti ya kila mwaka ili kukamilisha maboma hayo ya zahanati na shule katika Halmashauri ya Itigi. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved