Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Esther Lukago Midimu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kujenga miundombinu ya maji shuleni ili kuepuka milipuko ya magonjwa?
Supplementary Question 1
MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini sasa Serikali itapeleka hiyo miundombinu ya maji katika shule zilizobaki? (Makofi)
 
											Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na zoezi hili ni endelevu la kuboresha miundombinu ya maji katika shule zetu katika Mkoa wa Simiyu na katika mikoa yote kote nchini. Kwa hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba tutaendelea katika kila bajeti ya mwaka kutenga fedha kutoka vyanzo mbalimbali kwa ajili ya kuboresha huduma za maji katika shule zetu. (Makofi)
 
											Name
Grace Victor Tendega
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTHER L. MIDIMU K.n.y. MHE. MINZA S. MJIKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kujenga miundombinu ya maji shuleni ili kuepuka milipuko ya magonjwa?
Supplementary Question 2
MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba shule zinazojengwa sasa zinawekewa miundombinu ya uvunaji wa maji ya mvua ili kuzisaidia ziweze kupata maji safi na salama? (Makofi)
 
											Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Mkakati wa Serikali ni kwamba tumetoa maelekezo na mwongozo rasmi kwamba shule zote zinazojengwa, lakini pia vituo vya huduma za afya lazima kwanza viwe na miundombinu ya kuvuna maji ya mvua ikiwemo kufunga gata kwenye majengo yote, lakini kuchimba visima kwa ajili ya kuhifadhi maji ya mvua. Kwa hiyo, zoezi hilo linafanyika na shule zote, kwa mfano za mikoa 26 za wasichana zote zina miundombinu hiyo mahususi kwa ajili ya kuvuna maji, lakini shule ambazo zimejegwa hivi sasa za SEQUIP zimeendelea pia kuwekewa miundombinu ya maji. Zoezi hili ni endelevu, tutaendelea kulisimamia kuhakikisha watoto wetu wanapata maji ya uhakika katika shule zao. Ahsante sana.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved