Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Khamis Yussuf Mussa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kwahani
Primary Question
MHE. KHAMIS YUSSUF MUSSA aliuliza:- Je, lini Serikali itainufaisha Zanzibar katika matumizi ya nishati ya gesi kutumika katika magari?
Supplementary Question 1
MHE. KHAMIS YUSSUF MUSSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Pamoja na majibu hayo mazuri nina swali moja la nyongeza pamoja na ushauri. 
Mheshimiwa Spika, swali langu lipo hivi, je, Serikali imejipangaje katika kutoa elimu juu ya matumizi ya gesi katika magari Visiwani Zanzibar?
Mheshimiwa Spika, ushauri wangu ni kwamba mafunzo yatakapotolewa yawalenge hasa watumishi wa Serikali pamoja na Wizara na Mashirika ili wao ndiyo wawe changamoto kubwa sana katika kuwashajihisha watumiaji wengine binafsi.
 
											Name
Judith Salvio Kapinga
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa swali la Mheshimiwa Mbunge. Kama ambavyo nimetangulia kusema tutaendelea kushirikiana na wenzetu wa ZPDC kwa sababu tayari tuna ushirikiano basi na hilo la lenyewe tutalichukua kwa ajili ya kufanya kazi kwa pamoja na wao waweze kulichukua na kulifanyia kazi kwa upande wa Zanzibar. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved