Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
 
											Name
Hussein Nassor Amar
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nyang'hwale
Primary Question
MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari la Zimamoto Wilaya ya Nyang’hwale?
Supplementary Question 1
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kuipongeza Serikali kwa kutupatia gari la Zimamoto Wilaya ya Nyang’hwale, lakini pia niwapongeze Jeshi la Zimamoto Wilaya ya Nyang’hwale wanafanya kazi kwa kujituma pamoja na kwamba wapo wachache naomba niwatambue tu wa kwanza kiongozi wa Sajini Abdalah Mwinyimvua, Konstabo Fadhili Kipilipili, Konstabo Bichi Philemoni wanafanya kazi kubwa sana kipindi hasa cha masika yanapotokea mafuriko. 
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, Serikali ipo tayari kutupatia gari kwa ajili ya Maafisa hawa waweze kufanya kazi ya kuzunguka na kutoa elimu kwenye taasisi mbalimbali?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Serikali ipo tayari kusambaza au kutengeneza miundombinu kwa ajili ya maji ya dharura ya zimamoto katika Makao Makuu ya Wilaya ya Nyang’hwale?
 
											Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
								NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa pongezi alizotoa kwa Askari ambao wanafanya kazi nzuri sana katika Wilaya ya Nyang’hwale.
 
Mheshimiwa Spika, kuhusu maswali mawili ya nyongeza, swali la kwanza, kwa sasa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limesambaza magari katika mikoa yote nchini, hatua inayofuata ni kusambaza magari kwenye wilaya zote ikiwepo Wilaya ya Nyang’hwale.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, tayari Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limeshafanya vikao vitatu na mamlaka za maji ili kuhakikisha kwamba wilaya zote za Mkoa wa Geita zinapata fire hydrants ikiwepo Wilaya ya Nyang’hwale. 
							
 
											Name
Oliver Daniel Semuguruka
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari la Zimamoto Wilaya ya Nyang’hwale?
Supplementary Question 2
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Ngara hatuna gari la zimamoto ningependa kujua ni lini Serikali itatupatia gari la zimamoto na hili swali nimeuliza mara ya tatu katika Bunge lako Tukufu? Ahsante sana. (Makofi)
 
											Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
								NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Oliver, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu na msingi tayari Serikali imeshaagiza magari 150 kwa ajili ya kupatia Zimamoto Wilaya zote nchini, ikiwemo Wilaya ya Ngara. Ahsante sana. (Makofi)  
							
 
											Name
Robert Chacha Maboto
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bunda Mjini
Primary Question
MHE. HUSSEIN N. AMAR aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari la Zimamoto Wilaya ya Nyang’hwale?
Supplementary Question 3
MHE. ROBERT C. MABOTO: Mheshimiwa Spika, je, ni lini Serikali italeta gari ya zimamoto katika Halmashauri ya Mji wa Bunda? Ninakushukuru.
 
											Name
Daniel Baran Sillo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Babati Vijijini
Answer
								NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Robert Maboto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali tayari imeshaagiza haya magari 150 kwa ajili ya Wilaya zote ikiwepo Wilaya ya Bunda pia. Ahsante sana. 
							
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved