Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Edefonce Joackim Canoni
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kalambo
Primary Question
MHE. EDIFONSI J. KANONI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza ardhi ya kilimo kwa wananchi wa Kata ya Mkoe na Mbuluma kutoka katika eneo la NARCO?
Supplementary Question 1
MHE. EDIFONSI J. KANONI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, ninapongeza sana kwa majibu ya Serikali, lakini pia ninasema katika Wilaya ya Kalambo, Kata za Mbuluma na Mkoe Wananchi wa Kijiji cha Lolesha, Kalemasha, Mbuluma, Mao, Katapulo, Mkoe pamoja na Ilimba wana changamoto kubwa sana ya shughuli za kiuchumi ikiwa ni pamoja na kuomba Serikali iwasaidie hiyo ardhi kwa ajili ya mifugo. Je, ni utaratibu upi unaotumika ili kuweza kukodi hayo maeneo na hasa kipaumbele katika hayo maeneo ambayo nimeyataja katika vijiji hivyo ambavyo nimevitaja? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Mheshimiwa Waziri, upo tayari kuambatana na mimi Mbunge kwenda mpaka kwenye eneo hilo katika Wilaya ya Kalambo, Kata ya Mbuluma na Mkoe ili wananchi waweze kuwasilisha kero mbele ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi? (Makofi)
Name
Ng'wasi Damas Kamani
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana na ninampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuendelea kupambania maslahi ya wananchi wake.
Mheshimiwa Spika, ninaomba niyajibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kwa pamoja. Mheshimiwa Mbunge amehitaji kujua ni utaratibu gani unaotumika kukodi maeneo hayo? Swali lake la awali lilikuwa linahitaji kujua ni namna gani tunaweza tukatenga maeneo hayo ambayo yamepimwa mahususi kwa ajili ya mifugo ili yatumike kwa ajili ya kilimo?
Mheshimiwa Spika, ninarudia tena kumwambia Mheshimiwa Mbunge kwamba katika vijiji hivi tayari kuna maeneo 31 ya ranchi ambayo yameshatengwa na kutolewa kwa wananchi. Katika Kijiji cha Mbuluma tumetenga hekta 3,167 na Kijiji cha Lolesha hekta 2,107 ambazo tayari wameshapewa wananchi na wanaendelea kwa shughuli za mifugo.
Mheshimiwa Spika, kwa vile tayari Serikali ina commitment ya kuongeza maeneo ya ufugaji kutoka hekta milioni 3.4 mpaka hekta milioni sita, maana yake tayari katika maeneo yetu hatuna maeneo ya ziada kwa ajili ya kilimo.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge amehitaji kujua kama tuko tayari kuambatana naye kwa ajili ya kwenda kusikiliza kero za wananchi wake. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, hilo ndiyo hasa jukumu letu kubwa. Kwa hiyo, muda na wakati ambao tutapanga kwa pamoja tutaambatana na kwenda kuwasikiliza wananchi wetu hasa wafugaji katika kata hizi ili tuweze kutatua changamoto zao. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved