Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Saidi Salim Hamad
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ole
Primary Question
MHE. SAIDI SALIM HAMAD aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukuza na kuhifadhi Miti ya Mikoko ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi?
Supplementary Question 1
MHE. SAIDI SALIM HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Ninaomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza madogo kama ifuatavyo: _
Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali kupitia Waziri iko tayari kuja Jimbo la Ole kuona jitihada ambazo tunazifanya kwenye suala hili la mikoko?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa Jimbo la Ole tumeanzisha vikundi kwa ajili ya kuvikuza na kuitunza mikoko, je, Serikali iko tayari kuviwezesha vikundi hivyo vya akina mama? Ahsante.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, majibu.
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaendelea kumpongeza Mheshimiwa Saidi kwa jitihada zake za kusimamia mazingira, na kama ulivyofahamu, mazingira ni kipaumbele na ni moja kati ya nguzo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi na Vision 2025.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana, na ninakuahidi kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, nitaambatana naye baada ya kukubaliana ni lini ambapo yeye atakuwa na nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nimhakikishie, pwani ambayo ina kilomita zaidi ya 1,424 hivi, inaendelezwa kwa kutumia mpango huu wa kupanda mikoko, na tunatumia sana vikundi kwa ajili ya kupanda mikoko. Hili nimhakikishie, tunaendelea na tutaendelea pamoja na vikundi ambavyo ataviainisha katika Jimbo lako la Ole.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.
Name
Kaspar Kaspar Mmuya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ruangwa
Answer
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaendelea kumpongeza Mheshimiwa Saidi kwa jitihada zake za kusimamia mazingira, na kama ulivyofahamu, mazingira ni kipaumbele na ni moja kati ya nguzo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi na Vision 2025.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana, na ninakuahidi kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nchi, nitaambatana naye baada ya kukubaliana ni lini ambapo yeye atakuwa na nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nimhakikishie, pwani ambayo ina kilomita zaidi ya 1,424 hivi, inaendelezwa kwa kutumia mpango huu wa kupanda mikoko, na tunatumia sana vikundi kwa ajili ya kupanda mikoko. Hili nimhakikishie, tunaendelea na tutaendelea pamoja na vikundi ambavyo ataviainisha katika Jimbo lako la Ole.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kuwasilisha.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved