Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Enviroment | Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano | 638 | 2025-06-20 |
Name
Nusrat Shaaban Hanje
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ASYA MWADINI MOHAMMED K.n.y. MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza:-
Je, Serikali ina Mikakati gani ya kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi Nchini? (Makofi)
Name
Khamis Hamza Khamis
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uzini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA) alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inashirikiana kikamilifu na Jumuiya za Kimataifa katika kubuni mikakati na hatua madhubuti za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi katika ngazi zote. Baadhi ya Mikakati inayochukuliwa na nchi katika kukabiliana na athari hizo ni pamoja na kuridhia Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Itifaki ya Kyoto ya makubaliano ya Paris, kuandaa na kutekeleza nyenzo za kisera zitakazosaidia kutoa dira na kuibua programu na kutekeleza miradi inayosaidia jamii katika maeneo mbalimbali ya kuhimili mabadiliko ya tabianchi, hii inajumuisha mikakati wa Taifa wa Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (2021), Mpango Kabambe wa Taifa wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032) na Mchango wa Taifa katika kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi (2021).
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali imeendelea kutekeleza miradi ya kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi katika maeneo mbalimbali nchini. Miradi hii inajumuisha upandaji wa miti, usambazaji wa majisafi kwa matumizi ya majumbani na mifugo, ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji, matumizi ya nishati mbadala ikiwemo nishati safi ya kupikia ili kupunguza kasi ya ukataji wa misitu, ujenzi wa kuta katika maeneo ya fukwe za bahari yanayokabiliwa na mmomonyoko wa ardhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, Serikali itaendelea na ujenzi wa matuta na mabwawa kudhibiti mafuriko, kuwezesha jamii kubuni miradi mbadala ya kuongeza kipato na iliyo rafiki kwa mazingira na kurejesha maeneo ya ardhi yaliyoharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved