Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Energy and Minerals | Wizara ya Nishati | 640 | 2025-06-20 |
Name
Masache Njelu Kasaka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Lupa
Primary Question
MHE. FESTO R. SANGA K.n.y. MHE. MASACHE N. KASAKA aliuliza: -
Je, lini Serikali itafanya juhudi za makusudi kupeleka umeme kwenye maeneo ya Wachimbaji Wadogo Wilayani Chunya?
Name
Doto Mashaka Biteko
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukombe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini inatekeleza mradi wa kupeleka umeme katika migodi midogo nchini ambapo katika Wilaya ya Chunya, Serikali imepeleka umeme katika maeneo ya migodi ya wachimbaji wadogo 16 kati ya migodi 18 iliyopo Wilayani hapo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maeneo mawili ya migodi yaliyobaki, Mkandarasi aitwaye OK Electrical and Electronics anaendelea na kazi, na anatarajia kukamilisha kupeleka umeme hivi karibuni.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved