Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Energy and Minerals | Wizara ya Madini | 641 | 2025-06-20 |
Name
Lucy John Sabu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. CHARLES M. KAJEGE K.n.y. MHE. LUCY J. SABU aliuliza: -
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwa na Sera rafiki ya nishati ya umeme kwa Vijana wanaojihusisha na Uzalishaji kwenye Viwanda vidogo vidogo?
Name
Doto Mashaka Biteko
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Bukombe
Answer
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII K.n.y. NAIBU WAZIRI MKUU NA WAZIRI WA NISHATI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Sera ya Taifa ya Nishati ya Mwaka 2015, imelenga kuwezesha upatikanaji wa Nishati ya Umeme nchini kwa ajili ya kuchochea maendeleo ya kiuchumi pamoja na kijamii kwa watu wote wakiwemo vijana.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza sera hii, Serikali kupitia REA, imekamilisha kupeleka umeme katika vijiji vyote vya Tanzania Bara na sasa kazi ya kusambaza umeme katika vitongoji inaendelea. Aidha, REA inaendelea kutoa elimu na kuhamasisha wananchi wakiwemo vijana kuhusu matumizi ya umeme kwenye uzalishaji mali hususan viwanda vidogo vidogo.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved