Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 642 | 2025-06-20 |
Name
Innocent Sebba Bilakwate
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kyerwa
Primary Question
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE K.n.y. MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza: -
Je, lini Serikali itaanza kujenga mradi wa maji wa Kyerwa, Nyakatuntu na Kamuli – Kyerwa?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026 imepanga kuanza utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji wa kimkakati katika Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Kazi zinazotarajiwa kufanyika kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji katika Mto Kagera, ujenzi wa matanki yenye jumla ya ujazo wa lita 3,300,000, ulazaji wa bomba mbalimbali zenye urefu wa kilometa 225, sanjari na ujenzi wa vituo 75 vya kuchotea maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miezi 18 ambapo unalenga kunufaisha zaidi ya wananchi 168,670 waishio kwenye vijiji 37 vilivyopo kwenye Kata Saba za Kyerwa, Nyakatuntu, Nyaruzumbura, Kitwe, Businde, Bugala, na Kamuli, ninakushukuru.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved