Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 643 | 2025-06-20 |
Name
Constantine John Kanyasu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Geita Mjini
Primary Question
MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza: -
Je, lini mradi wa maji katika Mji wa Geita uliosainiwa Mwaka 2022 utakamilika na kuanza kutoa huduma ikizingatiwa kuwa mradi huu ni wa muda mrefu?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Maji wa Miji 28 katika Mji wa Geita unaohusisha ujenzi wa dakio katika Ziwa Victoria, ujenzi wa mtambo wa kutibu maji, ulazaji wa bomba umbali wa kilometa 109 pamoja na ujenzi wa matanki matano yenye jumla ya ujazo wa lita 8,900,000. Utekelezaji wa mradi huo umefikia wastani wa 54% ambapo unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2025 na kunufaisha zaidi ya wananchi 361,000 wa Mji wa Geita.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved