Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 644 | 2025-06-20 |
Name
Juliana Daniel Shonza
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. HUSNA J. SEKIBOKO K.n.y. MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza: -
Je, lini kazi ya kuleta maji ya Mto Momba katika Miji ya Tunduma, Mlowo na Vwawa itaanza?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeanza utekelezaji wa Mradi wa Maji Tunduma kwa kutumia maji ya Mto Momba kwa gharama ya shilingi bilioni 119.95 ambao utanufaisha pia Miji ya Vwawa, Mlowo sanjari na vijiji 31 vya Wilaya ya Momba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kazi zinazotekelezwa kupitia mradi huo ni pamoja na ujenzi wa chanzo cha maji katika Mto Momba chenye uwezo wa kuzalisha maji lita milioni 21.5, ujenzi wa mtambo wa kutibu maji (treatment plant) wenye uwezo wa kutibu maji lita milioni 20, ulazaji wa bomba umbali wa kilometa 317, sanjari na ujenzi wa matanki matatu yenye jumla ya ujazo wa lita milioni 10.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa mradi huo upo kwenye hatua za awali za utekelezaji ambapo muda wake wa utekelezaji ni miezi 18 na kukamilika kwake utanufaisha wananchi 1,245,406 wa maeneo hayo, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved