Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 645 | 2025-06-20 |
Name
Abdallah Jafari Chaurembo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbagala
Primary Question
MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO K.n.y. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: -
Je, lini maji ya DAWASA yatasambazwa Jimbo la Mbagala Mitaa ya Majimatitu, Machinjioni, Serenge, Changanyikeni, Vikunai, Kongowe na Masaki?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAJI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Mitaa ya Jimbo la Mbagala inapata huduma ya majisafi na salama isiyo toshelevu kupitia mtambo wa mtoni, sanjari na visima virefu 29 vya maji vilivyopo Mianzini, Nzasa I, Nzasa II, Machinjioni, Kongowe I, Kongowe II, Goroka I, Goroka II na Serenge.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mpango wa muda mfupi wa kuboresha huduma ya maji katika jimbo hilo, Serikali katika mwaka wa fedha 2025/2026, itafanya usanifu wa mradi wa kutoa maji kutoka Kisarawe II kwa lengo la kunufaisha mitaa ya Kongowe, Vikunai na Changanyikeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa muda mrefu wa Serikali ni kutumia maji ya Mto Rufiji kwa ajili ya kunufaisha mikoa ya Pwani, Lindi, na Dar es Salaam. Mradi huo upo kwenye hatua ya usanifu ambapo unatarajiwa kukamilika mwezi Agosti, 2025 na kunufaisha mikoa tajwa ikiwemo Jimbo la Mbagala, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved