Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. John Danielson Pallangyo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Arumeru-Mashariki
Primary Question
MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO K.n.y. MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO aliuliza: - Je, lini maji ya DAWASA yatasambazwa Jimbo la Mbagala Mitaa ya Majimatitu, Machinjioni, Serenge, Changanyikeni, Vikunai, Kongowe na Masaki?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Je, ni lini mradi wa maji wa Kata za Imbaseni, Maji ya Chai, Kikatiti mpaka Maroroni kule Arumeru Mashariki utamalizika?
Name
Khamis Hamza Khamis
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Uzini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, tayari tumeshaeleza katika majibu mengi ya msingi ambayo tumeyajibu hapa kwamba bahati nzuri sana bajeti yetu imeshakamilika na Waheshimiwa Wabunge mmepitisha hapa fedha kupitia Wizara hii ya Maji takribani shilingi trilioni 1.06 mmeziidhinisha hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaambie Waheshimiwa Wabunge, wananchi na Watanzania wote, kupitia fedha zile zitakwenda kukamilisha miradi, zitakwenda kufikisha maji, zitakwenda kuondoa changamoto yote ya upatikanaji wa majisafi na salama katika nchi yetu, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved