Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2020-2025 | Session 19 | Sitting 50 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Waziri wa Mifugo na Uvuvi | 646 | 2025-06-20 |
Name
Noah Lemburis Saputi Mollel
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Arumeru-Magharibi
Primary Question
MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO K.n.y. MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: -
Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha Maziwa Kijiji cha Likiushin Mnadani - Arumeru Magharibi?
Name
Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Kondoa
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI K.n.y. WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu: -
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ina wajibu wa kuhakikisha kuwa inaweka mazingira mazuri ya upatikanaji wa maziwa kwa kuweka miundombinu muhimu ya ukusanyaji ili kurahisisha upatikanaji wa maziwa nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kufanikisha hilo, Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mwaka 2022/2023 ilitenga kiasi cha shilingi bilioni moja kwa ajili ya kujenga vituo 10 vya kukusanyia maziwa ikiwa ni pamoja na Kituo cha Maziwa cha Likiushin, Arumeru Magharibi ambapo kwa sasa ujenzi wa kituo hicho umekamilika kwa 100% na Mkandarasi ameshakabidhi kituo hicho kwa Serikali kwa ajili ya kuanza kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, katika kukamilisha miundombinu ya utunzaji wa maziwa taratibu za ununuzi na usimikaji wa tenki la kupozea maziwa na generator zinaendelea, ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved