Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 1 2026-01-27

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza kutekeleza Mradi wa TACTIC katika Jimbo la Mbinga Mjini?

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ninamshukuru sana Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuniteua kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Jonas William Mbunda.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa ufadhili wa Benki ya Dunia imeanza utekelezaji wa Mradi wa TACTIC katika Jimbo la Mbinga Mjini, ambapo sasa Mradi huu upo hatua ya usanifu chini ya Mhandisi Mshauri aitwaye Bosphorus Technical Consulting Corporation ikishirikiana na Building Design Authority Limited pamoja na Masterpiece Consult Limited. Mara baada ya kukamilika usanifu huo ujenzi utaanza mara moja. (Makofi)