Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 1 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 6 | 2026-01-27 |
Name
Latifa Khamis Juwakali
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuliza:-
Je, kipi kipaumbele cha Wizara ya Vijana kwa vijana wa Tanzania?
Name
Joel Arthur Nanauka
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mtwara Mjini
Answer
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MAENDELEO YA VIJANA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwanza ninapenda kuchukua fursa hii kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuniteua kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Maendeleo ya Vijana. Pia kwa namna ya kipekee kwa kuunda Wizara mpya inayoshughulikia maendeleo ya vijana ikiwa ni dhamira yake ya kuwaweka vijana katikati ya maendeleo ya Taifa letu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sasa ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kipaumbele kikuu cha Wizara ya Maendeleo ya Vijana kwa vijana wa Tanzania ni kuwawezesha vijana kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa lengo la kuboresha ustawi wao na kuchangia kwa tija katika maendeleo endelevu ya Taifa. Katika kutekeleza kipaumbele hicho, Wizara inajielekeza katika maeneo makuu yafuatayo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza, Wizara inaendelea kuimarisha uwezeshaji wa vijana kiuchumi kwa kuweka mazingira rafiki ya upatikanaji wa mitaji, mafunzo ya ujasiriamali, ukuzaji wa biashara na ajira. Pili, Wizara inaweka mkazo katika uendelezaji wa ujuzi kwa vijana ili kuwaandaa kukabiliana na mahitaji ya soko la ajira na kujiajiri.
Mheshimiwa Spika, pia Wizara inaendelea kuimarisha ushiriki wa vijana katika maamuzi na masuala ya utawala bora, kwa kuanzisha na kusimamia majukwaa rasmi ya ushiriki wa vijana. Mwisho, Wizara inatekeleza afua za ustawi, malezi na ulinzi wa vijana, ikijumuisha masuala ya afya ya akili, maadili, uzalendo, amani na mshikamano wa kitaifa, kwa kushirikiana na Wizara, taasisi pamoja na wadau mbalimbali.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved