Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 1 | Union Affairs | Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano | 7 | 2026-01-27 |
Name
Zuberi Yahya Mfaume
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Morogoro Kusini
Primary Question
MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:-
Je, hatua gani zimechukuliwa za uchafuzi wa Mto Mfizigo na Mhuva zitokanazo na shughuli za madini na kubaini kemikali zilizopo na athari zake?
Name
Dr. Festo John Dugange
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwanza ninaomba nitumie fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu, pili kumshukuru sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania, kwa dhamana kubwa aliyonipa kuwa Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira. Ninaomba nimuahidi Mheshimiwa Rais kwamba nitafanya kazi kwa juhudi, maarifa na weledi wa hali ya juu.
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, sasa ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Yahya Mfaume, Mbunge wa Morogoro Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Mito ya Mfizigo na Mhuva iliyopo katika Jimbo la Morogoro Kusini ni moja ya maeneo ambako hufanyika shughuli za uchimbaji mdogo wa madini katika maeneo ya pembezoni mwa mito hiyo.
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha mito hiyo inatunzwa na kuzuia uchafuzi wake kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini, Serikali mwaka 2025 ilichukua sampuli za maji ya mito hiyo kwa ajili ya kupima ikiwa kuna uchafuzi wa kemikali zitokanazo na uchimbaji na uchenjuaji wa madini. Matokeo ya vipimo vya sampuli hizo vilionesha kuwa kuna kemikali za chuma na manganizi. Kemikali zilizobainika kuwepo zinatokana na miamba iliyokuwa inachimbwa na siyo kwamba zinatokana na matumizi ya kemikali za kuchenjua madini kama zebaki.
Mheshimiwa Spika, aidha, Serikali itaendelea kuchukua hatua kulinda vyanzo vya maji na mito ikiwemo Mito ya Mfizigo na Mhuva katika mazingira ya Morogoro Kusini kwa kuzingatia Sheria ya Mazingira ya Mwaka 2004 na Sheria ya Rasilimali za Maji ya Mwaka 2009.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved