Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Yahya Mfaume

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:- Je, hatua gani zimechukuliwa za uchafuzi wa Mto Mfizigo na Mhuva zitokanazo na shughuli za madini na kubaini kemikali zilizopo na athari zake?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI Y. MFAUME: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, shughuli hizi za madini ni shughuli zinazowaendeshea maisha wananchi wenzetu. Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa sasa elimu ya utunzaji wa mazingira ili wananchi wenzetu waendelee na shughuli zao za kujipatia kipato?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba shughuli za madini ni shughuli muhimu kwa uchumi wa nchi yetu na wananchi na sisi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira kwa kushirikiana na Wizara ya Madini na Wizara zote zenye nasaba na masuala ya mazingira na madini tutaendelea, kwanza kuhakikisha kwamba tunatoa elimu kwa wananchi na wachimbaji wote wa madini kuzingatia sheria na taratibu za uhifadhi wa mazingira ili kuwa na uchimbaji wa madini na uhifadhi wa mazingira endelevu. Ahsante sana.

Name

Alan Thomas Mvano

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kakonko

Primary Question

MHE. ZUBERI Y. MFAUME aliuliza:- Je, hatua gani zimechukuliwa za uchafuzi wa Mto Mfizigo na Mhuva zitokanazo na shughuli za madini na kubaini kemikali zilizopo na athari zake?

Supplementary Question 2

MHE. ALAN T. MVANO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika Wilaya ya Kakonko Mkoa wa Kigoma tunao uchimbaji wa madini ya dhahabu Kata ya Nyamtukuza, Vijiji vya Nyamtukuza maeneo ya Nyamwilonge. Tarehe 10 Disemba tulikwenda na Mkuu wa Mkoa pale na akazuia shughuli za uchimbaji kwa sababu zilikuwa zinakiuka sheria za mazingira na zinaathiri wananchi wa Vijiji zaidi ya saba vya Kihomoka, Kumwiyando na Vijiji vingine vya Bwera mpaka Nyamwilonge. Je, ni hatua gani zimechukuliwa na Serikali ili kunusuru maisha ya wananchi hao kwa sababu mto ule haufai kabisa kwa matumizi ya binadamu. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba suala la uchimbaji wa madini linaendeshwa kwa mujibu wa sheria na suala la uhifadhi wa mazingira linasimamiwa kwa mujibu wa Sheria, Sura ya 191.

Mheshimiwa Spika, ninaomba nitumie nafasi hii kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kakonko kwamba kipaumbele cha kwanza ni kutunza mazingira, lakini Serikali itaendelea kuhakikisha inaweka mazingira wezeshi kwa wachimbaji wa madini ili kunufaika na rasilimali za madini vilevile kutunza mazingira katika maeneo hayo. Tutawasiliana na Ofisi ya Wizara ya Madini ili tuweze kuliweka sawa na wananchi waweze kuendelea kuchimba madini.