Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 1 Works, Transport and Communication Wizara ya Uchukuzi 10 2026-01-27

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza: -

Je, kwa nini Shirika la Ndege la Tanzania lisianzishe safari za ndege za moja kwa moja toka Zanzibar mpaka Dodoma?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ninaomba nisimame na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuniamini na kuniteua kwa nafasi ya Naibu Waziri wa Uchukuzi. Ahadi yangu kwake ni kuendelea kufanya kazi hii kwa uaminifu, uzalendo na uadilifu mkubwa huku nikiwaahidi Waheshimiwa Wabunge ushirikiano wa dhati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili, kwa kuwa hili ni Bunge letu ni la kwanza tangu nchi yetu ifanye tukio kubwa la kihistoria kule Mwanza, ninatumia nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuzindua rasmi meli ya MV Mwanza, meli kubwa ya kwanza katika nchi yetu ambayo inabeba abiria 1,200, tani 400 na magari makubwa na madogo ya kutosha, itakayokuwa inaunganisha nchi yetu pamoja na nchi jirani. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuzindua meli hii kubwa kihistoria. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri ninaomba kumjibu Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Ndege Tanzania kwa sasa inafanya safari za ndege kutoka Zanzibar mpaka Dodoma kupitia Dar es Salaam. Uamuzi wa kupitia Dar es Salaam ni wa kibiashara ili kuhakikisha ndege inakuwa na ujazo wa kutosha. ATCL inaendelea kuangalia fursa ya kuanzisha safari za Zanzibar na Dodoma punde idadi ya abiria itapoongezeka na kuwezesha ndege kuwa na ujazo wa kutosha angalau wa 80%.