Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 1 | Works, Transport and Communication | Wizara ya Uchukuzi | 10 | 2026-01-27 |
Name
Mattar Ali Salum
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Shaurimoyo
Primary Question
MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza: -
Je, kwa nini Shirika la Ndege la Tanzania lisianzishe safari za ndege za moja kwa moja toka Zanzibar mpaka Dodoma?
Name
David Mwakiposa Kihenzile
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mufindi Kusini
Answer
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwanza ninaomba nisimame na kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa kuniamini na kuniteua kwa nafasi ya Naibu Waziri wa Uchukuzi. Ahadi yangu kwake ni kuendelea kufanya kazi hii kwa uaminifu, uzalendo na uadilifu mkubwa huku nikiwaahidi Waheshimiwa Wabunge ushirikiano wa dhati. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, pili, kwa kuwa hili ni Bunge letu ni la kwanza tangu nchi yetu ifanye tukio kubwa la kihistoria kule Mwanza, ninatumia nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa kuzindua rasmi meli ya MV Mwanza, meli kubwa ya kwanza katika nchi yetu ambayo inabeba abiria 1,200, tani 400 na magari makubwa na madogo ya kutosha, itakayokuwa inaunganisha nchi yetu pamoja na nchi jirani. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kuzindua meli hii kubwa kihistoria. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri ninaomba kumjibu Mheshimiwa Mattar Ali Salum, Mbunge wa Shaurimoyo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Kampuni ya Ndege Tanzania kwa sasa inafanya safari za ndege kutoka Zanzibar mpaka Dodoma kupitia Dar es Salaam. Uamuzi wa kupitia Dar es Salaam ni wa kibiashara ili kuhakikisha ndege inakuwa na ujazo wa kutosha. ATCL inaendelea kuangalia fursa ya kuanzisha safari za Zanzibar na Dodoma punde idadi ya abiria itapoongezeka na kuwezesha ndege kuwa na ujazo wa kutosha angalau wa 80%.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved