Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 1 Works and Transport Wizara ya Ujenzi 11 2026-01-27

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:-

Je, upi mpango wa Serikali wa kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Kibaoni – Dabaga na Dabaga hadi Idete?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ni mara yangu ya kwanza kusimama mbele ya Bunge lako ninaomba kutumia nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuendelea kuniamini na kuniteua kumsaidia kwenye nafasi hii ya Naibu Waziri wa Ujenzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ninakuhakikishia na Waheshimiwa Wabunge hawa kwamba nitatoa ushirikiano kwa 100%. Baada ya kusema hayo ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge wa Kilolo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Kibaoni – Dabaga na Dabaga hadi Idete ni sehemu ya Barabara ya Ipogolo – Idete yenye urefu wa kilometa 67.47. Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii umeanza kwa sehemu ya Ipogolo – Kilolo yenye urefu wa kilometa 33.61 chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia kupitia Programu ya RISE ambapo utekelezaji wake umefikia 98%. Sehemu iliyobaki ya kutoka Kilolo – Idete yenye urefu wa kilometa 33.86, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.