Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 1 | Works and Transport | Wizara ya Ujenzi | 12 | 2026-01-27 |
Name
Dotto Jasson Bahemu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngara
Primary Question
MHE. DOTTO J. BAHEMU aliuliza:-
Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Nyakahura – Rulenge – Murugarama kwa kiwango cha lami?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Nyakahura – Rulenge – Murugarama yenye urefu wa kilometa 85.6 unatekelezwa kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Kwa sasa maandalizi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kuanzia Keza yanaendelea, ambapo tayari mkandarasi amepatikana na taratibu za malipo ya awali zinaendelea ili aweze kuanza kazi. Mara baada ya taratibu za malipo ya awali kukamilika kazi za ujenzi zitaanza. Kwa sehemu iliyobaki, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuijenga barabara yote. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved