Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dotto Jasson Bahemu
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ngara
Primary Question
MHE. DOTTO J. BAHEMU aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Nyakahura – Rulenge – Murugarama kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 1
MHE. DOTTO J. BAHEMU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Vile vile, ninamshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini majibu kama haya si mara ya kwanza kuyasikia hapa Bungeni kwa sababu mwaka jana mwezi Aprili wakati Mheshimiwa Waziri akijibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ngara aliyepita, alisema kwamba Serikali tayari ilikuwa katika hatua za mwisho za kumlipa mkandarasi ili kazi ianze kufanyika. Sasa leo, majibu ni kama yale yale ya mwaka jana. Sasa ningependa kupata kauli ya Serikali katika maswali yangu mawili.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; je, ni lini sasa kazi rasmi ya ujenzi itaanza?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, katika eneo la Keza ambalo amesema ndiyo ujenzi utaanza; wanaanza kutoka Keza kwenda Nyakahura au Keza kwenda Murugarama kwa sababu Keza ni katikati?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninaomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge maswali yake mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, miradi yetu inachukua muda mrefu na ndiyo maana bado hatujasimamisha, tunaendelea na utaratibu wa kuijenga. Pia, kama nilivyosema kwamba barabara hiyo itajengwa, itaendelea kujengwa na bajeti yake imeshakamilika na ndiyo maana tayari tumeshapata mkandarasi.
Mheshimiwa Spika, barabara hiyo tutajenga kuanzia Keza – Nyakahura kwa hatua ya kwanza wakati tunasubiri lot ya pili kutoka Keza – Rulenge – Murugarama. Ahsante.
Name
Eng. Ezra John Chiwelesa
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Biharamulo Magharibi
Primary Question
MHE. DOTTO J. BAHEMU aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Nyakahura – Rulenge – Murugarama kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 2
MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, barabara hii inayoongelewa na Mbunge wa Ngara, inaunganisha Jimbo la Biharamulo na Jimbo la Ngara. Kwa hiyo Nyakahura iko kwangu lakini baadhi ya wananchi waliosimamisha shughuli zao kupisha ujenzi wa barabara hii hawajalipwa fidia mpaka sasa.
Mheshimiwa Spika, sasa ninataka kujua kauli ya Serikali, wana mpango wa kujenga bila kulipa fidia au plan ya fidia ni miongoni mwa hiyo process ya kujenga ili wananchi wangu wanaofuatilia hapa waweze kujua ni lini wananchi waache shughuli zao za maendeleo waweze kuwapisha wajenge hiyo barabara? Ahsante sana.
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, Serikali ya Awamu ya Sita haiwezi ikabomoa nyumba za wananchi kabla ya kuifidia. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, pale tutakapoanza kuijenga ni pale ambapo tumelipa fidia kwa wananchi ambao wanastahili fidia kwa mujibu wa sheria. Ahsante.
Name
Kija Limbu Ntemi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katoro
Primary Question
MHE. DOTTO J. BAHEMU aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Nyakahura – Rulenge – Murugarama kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 3
MHE. KIJA L. NTEMI: Mheshimiwa Spika, ahsante na nina swali moja kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Ni lini Barabara ya STAMICO – CCM – Ushirombo itajengwa kwa kiwango cha lami ili kuondoa adha ya wananchi kwa sababu barabara ilishaandaliwa katika mfumo wa kuwekewa lami, lakini sasa hadi leo haijawahi kujengewa lami na watu walibomolewa nyumba kusogea ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami? Ni lini Serikali itaamua kujenga kutoka STAMICO – CCM – Ushirombo kwa kiwango cha lami ili kuondoa vumbi na kero inayowapata wananchi wa Jimbo la Katoro?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ninaomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutashirikiana na wenzetu wa TARURA kama Serikali kuhakikisha kwamba kama tayari wameshabomolewa watu, basi mpango upo. Hata hivyo, tutashirikiana na wenzetu wa TARURA kuhakikisha kwamba hiyo barabara inajengwa. Kwa sisi TANROADS, barabara yetu ni kutokea Ushirombo kuja Katoro (ile barabara kubwa ambayo ndiyo tunashughulikia).
Mheshimiwa Spika, hiyo barabara nyingine, tutaongea na wenzetu wa TAMISEMI kupitia TARURA tuone wamefikia hatua gani ama baada ya hapa nimwombe Mheshimiwa Mbunge tuje tukae tuone ni barabara ipi hasa anayoisemea.
Name
Juliana Daniel Shonza
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DOTTO J. BAHEMU aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Nyakahura – Rulenge – Murugarama kwa kiwango cha lami?
Supplementary Question 4
MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, ninashukuru. Ninaomba kufahamu ni lini Serikali itakamilisha rasmi taratibu za awali ambazo zimesuasua kwa muda mrefu ili ujenzi wa Barabara ya Mlowo – Kamsamba uweze kuendelea?
Name
Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Ileje
Answer
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, Barabara aliyoitaja tulishapata mkandarasi na bahati nzuri siku za karibuni Mheshimiwa Waziri Mkuu alitembelea na alitoa maelekezo mahsusi kwa Wizara ya Ujenzi kuhakikisha kwamba mkandarasi yule ambaye anatakiwa kulipwa shilingi bilioni 3.7 ziweze kutafutwa. Tayari Wizara imeshaanza kutafuta hizo fedha kama yalivyokuwa maelekezo mahususi ili barabara hiyo ianze kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved