Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 17 2026-01-27

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:-

Je, lini fidia kwa wananchi wa Kijiji cha Liugai Kata ya Luilo zitalipwa ili wapishe Mradi wa Umeme?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa nami ndio mara yangu ya kwanza kusimama hapa mbele ya Bunge lako Tukufu tokea kuteuliwa kuwa Waziri wa Nishati, ninaomba nitumie nafasi hii kipekee kabisa kumshukuru Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa imani yake kwangu na kuniteua kuweza kumsaidia katika sekta hii ya Nishati na ahadi yangu kwake kwamba sitomwangusha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile niahidi Bunge lako Tukufu na Waheshimiwa Wabunge wote kuwapa ushirikiano wa hali ya juu katika utekelezaji wa majukumu yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharious Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia Desemba, 2025 kazi ya uthamini wa fidia kwa wananchi wa Vijiji vya Lifua, Liugai, Masimavalafu katika Wilaya ya Ludewa, Mkoa wa Njombe imekamilika ikiwa tayari kwa zoezi la uhakiki (verification) pamoja na uwekaji wazi jedwali kwa wafidiwa (disclosure). Aidha, shilingi 6,025,053,947.72 zinatarajiwa kulipwa kwa wananchi 347 waliopisha utekelezaji wa mradi katika Vijiji vya Lifua, Liugai na Masimavalafu na malipo ya fidia kwa wananchi hao yanatarajia kufanyika mwaka wa fedha ujao wa 2026/2027.