Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 1 Information, Communication and Information Technology Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari 19 2026-01-27

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:-

Je, upi mpango wa Serikali kupunguza gharama za vifurushi kwa Kampuni zote za simu?

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa vile nami ni mara yangu ya kwanza, nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Rais kwa imani yake kwangu na kuniteua kuwa msaidizi wake kama Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari. Ninapenda niahidi kwamba nitafanya kazi hii kwa uaminifu mkubwa kwa weledi kwa nguvu zangu zote na akili yangu yote.

Mheshimiwa Spika, baada ya utangulizi huo, kwa niaba ya Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, ninaomba nijibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa upatikanaji wa huduma za mawasiliano kwa gharama nafuu kwa wananchi. Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari pamoja na taasisi zake za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF) na Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) imeendelea kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha huduma za simu, intaneti na data zinakuwa rafiki kwa wananchi.

Mheshimiwa Spka, hatua zilizochukuliwa ni pamoja na:-

(i) Kusimamia ushindani wa haki miongoni mwa Kampuni za simu ili kuchochea ubunifu na upatikanaji wa vifurushi vya gharama nafuu vinavyokidhi uwezo wa wananchi;
(ii) Kufanya mapitio ya gharama na tozo mbalimbali ili kuhakikisha utozaji unazingatia gharama halisi za huduma na kumlinda mlaji wa mwisho;

(iii) Kuhimiza matumizi ya miundombinu ya pamoja ili kupunguza gharama za uendeshaji;

(iv) Kuendelea na Ujenzi wa miundombinu ya Mawasiliano ikiwemo Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano, minara ya mawasiliano maeneo ya vijijini na yasiyo na mvuto wa kibiashara pamoja na ujenzi wa vituo vya kuhifadhi data. Hatua hii inachangia kushuka kwa gharama za huduma, hususan intaneti ya faiba majumbani na maofisini.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kufuatilia mwenendo wa soko na kuchukua hatua stahiki za kisera na kikanuni ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za mawasiliano kwa gharama nafuu na sekta inaendelea kuchangia maendeleo ya uchumi wa kidijiti nchini.