Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:- Je, upi mpango wa Serikali kupunguza gharama za vifurushi kwa Kampuni zote za simu?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru nimepata majibu ya Serikali yamejieleza kwa kina, lakini tunapoongelea uchumi wa kidijiti component mojawapo kubwa ni intanenti ndio kufikia huo uchumi wa kidijiti. Kwa sasa hivi ukiangalia watumiaji wengi wa intanenti ambao inawasaidia kwenye biashara gharama imekuwa ni kubwa sana. Maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; Wizara ya Mawasiliano kwa kushirikiana na Wizara ya Vijana ni upi mkakati wa kuwafikia vijana kwenye makundi mbalimbali ambao wanatumia intanenti mfano vyuo vikuu, watumiaji wa kusafirisha abiria mtandaoni mfano Uber na Bolt, wauza nguo wadogowadogo ambao wanafanya biashara zao kupitia online wakae nao katika hayo makundi waelezee uhalisia na makundi mengineyo namna ambavyo wanapata changamoto kubwa kupitia intanenti na watumiaji wengine?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali inaonaje ikae na taasisi binafsi ambazo zinatoa huduma hizi kwa ajili ya kuwaomba kupunguza gharama za internet, mfano Kampuni ya Vodacom na kampuni nyingine, kwa ajili ya kuwasaidia wananchi kupunguza gharama za vifurushi ili ambao wanajiajiri kupitia sekta hii iweze kuwasaidia? (Makofi)

Name

Switbert Zacharia Mkama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, ninaomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusu ushauri wake wa kukaa na vijana kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Vijana, tumeupokea na tutakutana na vikundi mbalimbali vya vijana ili kujua mahitaji yao na changamoto zao wanazozipata katika upatikanaji wa internet katika shughuli zao. Kwa hiyo, tutawasiliana na wenzetu wa Wizara inayohusika na Maendeleo ya Vijana kwa ajili ya kulishughulikia suala hili.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kukaa na taasisi binafsi kwa ajili ya kupunguza gharama za vifurushi, mwaka jana (2025) Serikali ilikaa na taasisi binafsi na tukapunguza bei za vifurushi vya internet na kwa sasa katika Afrika Mashariki ukiiondoa Rwanda, Tanzania ndiyo nchi yenye vifurushi nafuu kuliko nchi nyingine zote, zaidi ya Rwanda. Kwa hiyo, tutaendelea pia kukaa na hizi taasisi binafsi tuangalie namna gani tunavyoweza kuboresha zaidi gharama za vifurushi ili tuweze kufikia lengo la kuwa na Uchumi wa Kidijiti. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tumepokea ushauri wako na tutaufanyia kazi kwa kadiri inavyowezekana ili tufikie hilo lengo. Ninakushukuru. (Makofi)