Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
| Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
|---|---|---|---|---|---|---|
| 2025-2030 | Session 2 | Sitting 5 | Regional Administration and Local Government Authorities | Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) | 69 | 2026-02-02 |
Name
Ester Amos Bulaya
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ESTER A. BULAYA aliuliza:-
Je, lini Mradi wa TACTIC Awamu ya Tatu utaanza kutekelezwa katika Jimbo la Bunda Mjini?
Name
Kwagilwa Reuben Nhamanilo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Handeni Mjini
Answer
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Ester Amos Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa TACTIC kwa Halmashauri ya Bunda Mjini utatekeleza miradi mitatu ambayo ni Ujenzi wa Soko Kuu, Ujenzi wa Stendi ya Mabasi na Ujenzi wa Barabara zenye urefu wa kilometa 4.5. Miji yote ya kundi la tatu, ukiwemo Mji wa Bunda, utekelezaji upo hatua ya usanifu. Baada ya hapo taratibu za kutangaza zabuni zitafuata. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2026. All Rights Reserved