Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2025-2030 Session 2 Sitting 5 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) 69 2026-02-02

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:-

Je, lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Masama pamoja na nyumba za watumishi wa Kituo hicho?

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, TAMISEMI, ninaomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Saashisha kutoka Jimbo la Hai.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Masama kilijengwa Mwaka 1979, hali inayosababisha kuwa na miundombinu michache na chakavu. Kituo hicho kinahitaji miundombinu muhimu, ikiwa ni pamoja na jengo la huduma za wagonjwa wa nje (OPD), maabara, jengo la huduma za uzazi, jengo la upasuaji, jengo la kufulia, kichomea taka, vyoo vya nje na nyumba za watumishi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imefanya tathmini na kuainisha vituo vya afya kongwe 532 kote nchini, ambavyo vinahitaji kuongezewa na kukarabatiwa miundombinu yake. Aidha, jumla ya shilingi bilioni 102.08 zinahitajika, kwa ajili ya uboreshaji wa vituo hivyo. Serikali itaendelea kutenga fedha, kwa ajili ya ukarabati wa vituo vya afya kongwe kote nchini, kikiwemo Kituo cha Afya Masama. (Makofi)