Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Masama pamoja na nyumba za watumishi wa Kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na nini maswali mawili ya nyongeza: swali la kwanza; wakati tukisubiri Serikali ilete fedha, kwa ajili ya ukarabati, je, Serikali haioni ipo haja sasa ya kuanzisha huduma ya upasuaji kwenye kituo hiki, ambayo ni huduma muhimu sana kwa watu wa Masama?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; Hospitali ya Wilaya ya Hai iko katikati na inapokea wagonjwa wengi sana wanaotokana na ajali kwenye maeneo mbalimbali kwenye Barabara yetu ya Arusha kwenda Moshi, lakini mpaka sasa hivi hatuna theatre, kwa ajili upasuaji. Je, Serikali ni lini italeta fedha ya kujenga theatre, kwa ajili ya upasuaji katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Hai? [MANENO HAYA SIYO SEHEMU YA TAARIFA RASMI ZA BUNGE]

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Saashisha, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Kituo chetu cha Afya cha Masama, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kuuliza maswali ya msingi. Pili, ninamwelekeza Mkurugenzi kuendelea kutenga fedha za ndani na kuanza ujenzi wa jengo la upasuaji katika Kituo chetu cha Afya cha Masama.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; tayari halmashauri ilijenga jengo la upasuaji katika Hospitali ya Hai na tayari kazi za upasuaji zinafanyika pale, wataalam wangu wameni-brief. Ninamhakikishia tu Mheshimiwa Mbunge, kama taarifa hazijafika kwa wakati, ninamwomba DMO aweze kumpa taarifa Mheshimiwa Mbunge, lakini pia, Mkurugenzi anifikishie taarifa sahihi kwa Mheshimiwa Mbunge kwa maana ya kwamba, Hospitali ya Hai imeshaanza matibabu hayo ya upasuaji hadi upasuaji wa mifupa. (Makofi) [MANENO HAYA SIYO SEHEMU YA TAARIFA RASMI ZA BUNGE]

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Masama pamoja na nyumba za watumishi wa Kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Serikali iliahidi kujenga vituo vya afya vya kimkakati, ili wananchi wasiendelee kufuata huduma katika umbali mrefu sana. Katika Wilaya yetu ya Kilolo kuna Kata za Kimara, Idete, Ukwega, Kwiugumu na Image, wananchi wanapata mateso sana kufuata huduma za afya na barabara hazipitiki. Mpaka sasa hivi madaraja hayapo…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa uliza swali.
MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, je ni lini sasa hivi vituo vya kimkakati vitajengwa, ili wananchi wasiendelee kupata mateso makubwa? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ilimetenga bajeti ya zaidi ya vituo 120 katika majimbo 120 vya kimkakati, zaidi ya shilingi bilioni 30. Tayari tumeomba fedha zingine, kwa ajili ya majimbo 94 pamoja na yale majimbo ambayo ni mapya, yote yataingia katika mpango huo na tutakwenda kujenga hivi vituo vya afya vya kimkakati. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Masama pamoja na nyumba za watumishi wa Kituo hicho?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Hunyari kimejengwa ni miaka mitatu sasa hakina jengo la upasuaji. Wananchi wenyewe wakaamua kujenga jengo na Serikali ikasema itakwenda kuwasaidia kulimalizia. Sasa ni lini jengo hili litakwenda kumaliziwa kwenye Kituo cha Afya cha Hunyari? Ninakushukuru

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere. Kwanza tunawapongeza wananchi kwa hatua waliyochukua na kuanza kujenga majengo hayo katika hospitali aliyoiainisha. Ninamwelekeza Mkurugenzi aweze kutenga fedha na kuanza ujenzi wa majengo yanayopelea katika hospitali hiyo.

Name

Charles Mhando Njama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Masama pamoja na nyumba za watumishi wa Kituo hicho?

Supplementary Question 4

MHE. CHARLES M. NJAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi. Kwanza naanza kwa kumshukuru Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametuletea pesa wiki iliyopita shilingi bilioni 1.4, kwa ajili ya ukarabati wa Hospitali yetu ya Magunga. Hospitali ya Magunga imezeeka sana, imechakaa na ina umri karibu miaka 73 sasa. Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari twende pamoja katika hospitali ile, kwa ajili ya kufanya tathmini, ili ikiwezekana tufikirie kujenga majengo mapya badala ya kuendelea kuweka viraka katika hospitali ile, ambayo inakuwa ni gharama kubwa zaidi kwa Serikali? (Makofi)

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Charles, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi pamoja na timu ya wataalam tutaongozana pamoja na Mheshimiwa Mbunge kwenda kwenye hospitali hiyo kufanya tathmini na kuendelea kuboresha miundombinu ya hospitali hiyo. (Makofi)

Name

Moshi Selemani Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tanganyika

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati Kituo cha Afya Masama pamoja na nyumba za watumishi wa Kituo hicho?

Supplementary Question 5

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Karema, Kituo cha Afya cha Kasekese na Kituo cha Afya cha Mwese kuna tatizo kubwa la ukosefu wa Jengo la Mama na Mtoto, Maabara na nyumba za watumishi. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha,ili iweze kukamilisha hivyo vituo vya afya? Ahsante.

Name

Dr. Jafar Rajab Seif

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. JAFAR R. SEIF): Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema awali kwamba, zaidi ya vituo 532 vimeishatengewa bajeti ya shilingi bilioni 102.08. Kwa hiyo, pamoja na vituo ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameviainisha vimo katika ukarabati huu mkubwa na kuweza kujenga majengo mengine ambayo yanahitaji, kama maabara, ili kuendelea kupata huduma kwa wananchi wetu.